Saturday, October 22, 2011

Ujenzi Wa Barabara Ya Singida-Katesh(Manyara), Wakamilika

Mkuu wa mkoa Dk.Kone, (kushoto) ba mhandisi Kkangolle(kulia),na wakandarasi wa wa ujenzi wa barabara hiyo iliyoigharimu serikali zaidi ya Sh.Bilioni 51.6, ambao umekamilika na magari yataruhusiwa kuanza kupita katika kipindi cha siku saba kuanzia leo.

Mkuu wa mkoa Dk.Kone, akipewa maelekezo na mhandisi Kangole, juu ya mawe mawili katika barabara hiyo, ambayo ni lango la kuingia na kutoka katika mji wa Singida

Mkuu wa mkoa Singida Dk.Parseko Kone(katikati), meneja wa wakala wa barabara Singida,mhandisi Yustak Kangole, wakiwa kwenye picha ya pamoja na wataalamu wa kampuni ya Sinohydro Corporation Ltd ya China, baada ya kukagua ujenzi wa barabara ya Singida-Kateshi(Manyara) kilomita 65.1

Mkuu wa mkoa Singida Dk.Parseko Kone baada ya kukagua mradi wa barabara ya Manyoni-Chaya, jana aliendelea na kazi hiyo, kwa kufanya ukaguzi barabara ya Singida-Kateshi(Manyara) inayojengwa na kampuni ya Sinohydro Corporation Ltd, kwa zaidi ya Sh.Bilioni 51.6.

No comments:

Post a Comment