Tuesday, November 13, 2012

WATU SITA WASHIKILIWA NA POLISI MKOANI SINGIDA KWA KUKUTWA POMBE BANDIA AINA YA VIROBA VYA JOGOO NA KONYAGI.

Kamanda wa polisi mkoa wa Singida ACP Linus Sinzumwa. 
 
Jumla ya watu sita wakiwemo wakazi wawili wa jijini Dar-es-salaam, wanashikiliwa na jeshi la polisi mkoani Singida kwa tuhuma ya kupatikana na kiasi kikubwa cha pombe kali aina ya viroba vya jogoo/konyagi inayosadikika kuwa ni bandia.
Watuhumiwa hao ni Hagai Mwalumile (38), Yusuph George (28), Geofrey Mushi (45) na mmoja mwenye umri wa miaka 17 ambaye bado hajatambuliwa jina lake.
Watuhumiwa hao wote ni wakazi wa Mitunduruni mjini Singida.
Watuhumiwa ambao ni wakazi wa jijini Dar-es-salaam ni Mohammed Rashid (42) na Richard Leonard (32).
Kamanda wa polisi mkoa wa Singida ACP Linus Sinzumwa, amesema watuhumiwa hao kwa pamoja wamekamatwa Septemba 22 mwaka huu eneo la Unyankindi kata ya Mitunduruni mjini Singida, kwenye nyumba ya mtuhumiwa Godfrey Mushi.
Kamanda Sinzumwa amesema nyumba ya mtuhumiwa Godfrey Mushi, inasadikika kuwa iligeuzwa na kuwa kiwanda maalum kwa ajili ya kutengeneza pombe kwa njia ya kienyeji.
Amesema kuwa ndani ya nyumba hiyo, kumesimikwa mtambo wa kutengeneza kienyeji viroba vya pombe aina ya jogoo na konyagi bandia, ambayo ni hatari kwa maisha ya binadamu.
Kamanda huyo ametaja bidaa iliyokamatwa kuwa ni katoni 49 za viroba, katoni 6 za konyagi kila moja ikiwa na pakiti na majiko ya manne ya mchina 4.
Ametaja bidhaa zingine kuwa ni sprit lita tatu na nusu, vyuma vya ku-sealed 11, soletape 4, marker  pen 6, mkasi moja, outer tupu za konyagi 1,561, outer tupu za viroba 235, katoni tupu za konyagi 12 na pamba bunda tatu.
Kamanda huyo amesema kuwa watuhumiwa hao wanatarajiwa kufikishwa mahakamani wakati wo wote upelelezi utakapokamilika.

No comments:

Post a Comment