Thursday, November 15, 2012

WATU WATATU WA FAMILIA MOJA WAFARIKI DUNIA BAADA YA KUANGUKIWA NA NYUMBA.



WATU watatu wa familia moja wamefariki duniani mkoani Singida baada ya kuangukiwa na nyumba.
Kamanda wa polisi mkoa wa Singida kamishina msaidizi Linus Sinzumwa amesema tukio  hilo limetokea jana majira  ya saa 10 alfajiri wakati  wanafamialia hao wakiwa wamelala.
Amewataja waliokufa kuwa ni baba wa familia hiyo Ramadhani   Amrani  (25) mkewe  Mariam Kondo  (23) na mtoto wao  Amrani Ramadhani  mwenye  umri wa miezi  saba wote wakazi wa eneo la Tambuka-Reli katika halshauri ya wilaya ya Manyoni mkoani Singida.
Kamanda Sinzumwa amesema siku ya tukio wanafamilia  hao walikuwa wamelala kwenye nyumba yao waliyojenga kwa tofali mbili na kuezeeka kwa miti na udogo mwezi mmoja uliopita.
Hata  hivyo amesema kutokana na  kile kinachosadikiwa kuwa kuzidishwa udogo juu,  miti iliyotumika kujengea nyumba hiyo ilivunjika, hali iliyosababisha udogo na kuta kuporomoka.
Kamanda Sinzumwa amesema  hali hiyo  ilisababisha wanafamilia hao watatu kukandamizwa na  kupondwa na miti, tofali na udogo hadi wakapoteza maisha yao  papo hapo.
Kufuatia  vifo hivyo jeshi la polisi mkoani Singida  limetoa wito kwa wananchi husani  wanaoishi kwenye nyumba za kienyeji maarufu kama tembe kuzifanyika ukarabati kabla ya mvua za masika.

No comments:

Post a Comment