Tuesday, December 11, 2012

Wahandishi wa habari mkoa wa Singida wagawanyika, mkutano mkuu wautaka uongozi wa zamani kukabidhi ofisi ndani ya wiki mbili.

Katibu wa klabu ya waandishi wa habari (Singpress) mkoa wa Singida Bw. Abby Nkungu akitoa taarifa yake ya utekelezaji kwa kipindi cha mwaka uliopita.


Mkutano Mkuu wa mwaka wa Klabu ya Waandishi wa habari (Singpress) Mkoani Singida, umeagiza uongozi wa zamani wa Klabu hiyo, kukabidhi ofisi katika kipindi cha wiki mbili, vinginevyo uchukuliwe hatua kali zikiwemo za kisheria.
Mkutano huo uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri ya Wilaya ya Manyoni mjini, Umeagiza uongozi huo uandikiwe barua rasmi ya kuupa muda wa wiki mbili kuanzia
tarehe ya barua husika.
Akitoa pendekezo hilo mbele ya mkutano huo mkuu, Shabanj Msangi, amesema pamoja na muungano wa jumuiya ya vilabu vya waandishi wa habari nchini (UTPC), kuridhia uongozi wa sasa kuingia ofisini bila makabidhiano, uamuzi huo ni kinyumbe na katiba ya Singpress.
Baada ya mvutano mkali kwa upande uliokuwa unapendekeza juu ya hatua ya kukabidhi rasmi ofisi na upande uliokuwa ukidai kwamba hatua hiyo haina mashiko au tija, zilipingwa kura na upande uliokuwa unataka uongozi wa zamani uliokuwa  chini ya uenyekiti wa mchungaji Emmanuel Barnaba ukabidhi ofisi, ulishinda.
Katika hatua nyingine, mkutano huo katika hali isiyokuwa ya kawaida, uliamua kusamehe deni la shilingi milioni 2,217, 600 ambalo walikuwa wanadaiwa wanachama waliokodisha vifaa vya klabu ikiwemo kamera.
Baadhi ya wanachama walidai kwamba kutokana na udhaifu mkubwa ulionyeshwa na uongozi uliopita, basi madeni hayo ambayo yameacha  vifaa vilivyokodishwa  kuharibika  na kupelekea visitumike  tena, basi madeni yafutwe na wasidaiwe wanachama hao.
Wanachama hao waliokodisha vifaa hivyo,walikodishwa vikiwa vipya havijatumika kabisa na vimekaa mikononi mwao hadi vikaharibika na havitegenezeki tena.
Baada ya mvutano huo mkali kudumu zaidi ya nusu saa, upande uliopendekeza madeni hayo yafutwe na yasionekane kwenye kumbukumbu za Klabu, ulishinda.
Mapendekezo hayo yawaligawa wananchama wa Singpress katika vipande viwili na baadhi walidai kuwa kitendo cha kusamehe madeni hayo ni sawa na kuifanya Singpress kuwa ni shamba la bibi.
Uamuzi huo uliendelea kulaumiwa kwa madai kwamba msamaha wa aina hiyo usiokuwa na tija, utakuwa endelevu kwa vile wakopaji au watumiaji wa mali ya Klabu watakuwa wanautumia katika kuihujumu Klabu kiuchumi.
Wadaiwa hao na madeni yao kwenye mabano ni  Doris Mehgji, (90,000/=), Elisante Mkumbo (25,000/=), Jumbe Ismail (1,431,600), Hillary Shoo (615,000) na Evarist Thomas (56,000).
Hata hivyo Hillary Shoo kwa sasa sio mwanachama wa Singpress.

No comments:

Post a Comment