Wednesday, December 18, 2013

Wilaya ya Ikungi kuvuna tani 144,826 ya mazao ya chakula.

Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Ikungi, Bw.Protace Magayaye, akitoa taarifa yake kwa waandishi wa habari (hawapo kwenye picha)  ya utekelezaji wa shughuli za kilimo msimu wa 2013/2014 ambapo wanatarajia kuvuna tani 144,826 mazao ya chakula na hivyo kuwa na ziada tani 83,090.Mahitaji ya wakazi wa wilaya hiyo 225,521,ni tani 61,736 kwa mwaka.
Afisa kilimo halmashauri ya wilaya ya Ikungi mkoa wa Singida, Ayubu Sengo.

HALMASHAURI ya Wilaya ya Ikungi mkoani Singida inatarajia kulima hekta 84,014 za mazao ya chakula msimu huu wa 2013/2014 na wanatarajia kuvuna tani 144,826.

Halmashauri hiyo ya Ikungi yenye jumla ya wakazi 225,521 ambao mahitaji yao ya chakula kwa mwaka ni tani 61,736, kwa matarajio ya mavuno ya msimu huu ya tani 144,826, halmashauri hiyo mpya itakuwa na ziada ya tani 83,090 ya mazao ya chakula.

Hayo yamesemwa hivi karibuni na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Protace Magayane wakati akitoa taarifa yake ya utekelezaji wa shughuli za kilimo msimu wa 2013/2014.

Alitaja mazao hayo na hekta zake kwenye mabano kuwa ni mtama (34,498), uwele (35,629), mounga (3,012), mhogo (1,500) na viazi vitamu (4,500).

Magayane alitaja mazao mengine ya chakula kuwa ni maharage (2,875), kunde (1,500) na njugumawe (500).

Mkurugenzi huyo amesema mafaniko hayo yatatokana na upatikanaji wa mvua yenye mtawanyiko mzuri kanuni bora za kilimo ikiwemo matumizi ya mbolea na mbegu bora.

Kwa upande wa mazao ya biashara, Magayane amesema wamejiwekea lengo la kulima hekta 22,097 na matarajio ni kuvuna tani 45,431.3.


Wakati huo huo, Mkurugenzi huyo, amesema wamesambaza

MAJAMBAZI MAWILI YAUWAWA (Samahani Kwa Picha Hizi)


WATU wawili wakazi wa manispaa ya Singida ambao majina yao bado hayajajulikana,wakiwa kwenye Jokofu la kuhifadhia maiti baada ya kuuawa wakati wa majibishano ya risasi na polisi.
Kamanda wa polisi mkoa wa Singida,SACP Geofrey Kamwela,akionyesha bunduki ya kijeshi aina ya SMG no.34555  iliyokuwa ikitumiwa na watu wawili wanaodhaniwa kuwa majamabazi katika kijiji cha Manga manispaa ya Singida.

JESHI  la Polisi mkoani Singida limewauwa watu wawili wanaodhaniwa kuwa ni majambazi wakati wa kurushiana rasasi.
Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Singida, SACP, Geofrey Kamwela amesema tukio hilo limetokea desemba tisa mwaka huu saa 12:00 jioni, huko katika kijiji cha Manga nje kidogo ya mji wa Singida.
Amesema watu watatu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi wakiwa na bunduki moja ya kijeshi aina ya SMG, walifika kijijini hapo kwa lengo la kufanya uhalifu.
Kamanda Kamwela, amesema watu hao ambao miili yao imehifadhi kwenye chumba cha mochwari katika hospitali ya mkoa, majina na makazi yao bado hayajajulikana.
Akifafanua, amesema taarifa za siri kutoka kwa raia wema zilifikia jeshi la polisi na ndipo askari polisi walipofika kwenye eneo la tukio.
“Baada ya polisi kufika kijijini hapo watu hao walistuka kuwa wanafuatilwa na askari polisi na hivyo kuanza kukimbia kuelekea kijiji cha Uhamaka kwa kutumia pikipiki yenye namba za usajili T. 634 BTW aina ya Sanlag yenye rangi nyeusi”,amesema Kamwela.
Amesema walipoona Polisi wanawakaribia waliamua kutelekeza pikipiki yao hiyo na kuanza kukimbilia porini kwa miguu.
“Hali ilipokuwa ngumu zaidi, walianza kuwarushia polisi risasi, hivyo polisi nao ikwabidi kujibu mapigo.  Katika majibizao hayo ya risasi, majambazi mawili yaliweza kujeruhiwa huku mmoja akifanikiwa kutoroka”
Amesema majambazi hayo yaliyojeruhiwa yalifariki dunia wakati yanakimbizwa katika hospitali ya mkoa kwa matibabu,lakini yakafia njiani.
Amesema katika eneo la tukio, ilipatikana

Wednesday, December 11, 2013

Unyanyapaa bado ni tatizo mkoani Singida.

Meneja mradi wa Global Fund uliopo chini ya AMREF Tanzania, Andulile Kanza, akitoa maelezo juu ya mradi wao wa uhamasiahaji wa upimaji wa afya wenye lengo la ifikapo mwaka 2015 maambukizi mpya ya Virusi vinavyosababisha UKIMWI,kiwango kifikie 0, vifo vitokanavyo na UKIMWI, 0 na unyanyampaa ufikie kiwango cha 0. Andulile alikuwa akitoa maelezo hayo  kwenye kituo kikuu cha mabasi mjini Singida.
Mkazi wa Singida mjini, akishikiriki kupima Afya yake kwenye zoezi lililokuwa likiendeshwa na shirika la AMREF lililofanyika katika kituo kikuu cha mabasi mjini Singida.
Mwanakikundi maarufu cha ‘Mtaa wa saba’ cha Majengo mjini Singida, akitoa burudani katika hafla ya zoezi la upimaji wa afya lililoendeshwa na AMREF kwenye kituo cha mabasi cha mjini Singida.
Kikundi cha sarakasi kutoka jijini Dar-es-salaam, kikitoa burudani wakati wa kampeni ya uhamasishaji upimaji wa afya iliyokuwa ikiendeshwa na shirika la AMREF katika kituo cha mabasi mjini Singida.

UNYANYAPAA na woga wa baadhi ya watu unachangia watu wengi zaidi kupima afya zao nyakati za usiku wakati wa kampeni za upimaji afya zinazofanyika nyakati hizo, imeelezwa.

 Hayo yamesemwa na Meneja Mradi wa Global Fund uliopo chini ya AMREF Tanzania, Andulile Kanza, wakati akizungumza na waandishi wa habari juu ya kauli mbiu ya ‘Getting zero’ katika masuala ya UKIMWI.

 Amesema kuwa watu wengi wamekuwa wakiogopa kupima afya zao asubuhi au mchana kwa hofu kwamba watu watawaona na hivyo wataanza kuwanyanyapaa na kuwatenga.

 “Ndio maana sisi AMREF kwenye kampeni hii ya kuhakikisha Tanzania ifikapo 2015, kiwango cha maambukizi mapya ya Ukimwi kitakuwa sifuri vifo vitokanavyo na ukimwi vitafikia sifuri  tunapima afya hadi saa tatu usiku na malengo yetu yanaenda vizuri”,alifafanua Andulile.

 Katika hatua nyingine, Maria Edward aliyepima afya yake baada ya kuhamasishwa na AMREF, ametoa wito kwamba  watu na hasa wanawake wajitokeze kwa wingi kupima afya zao ili waweze kujitambua endapo wameambukizwa au laa virusi vinavyosababisha ugonjwa wa UKIMWI.

“Natoa wito kwa wanawake wenzangu kwanza waelewe kwamba baadhi ya wanaume wetu wana mitandao ya ngono tofauti na wanawake Hivyo tunalazimika kupima afya zetu mara kwa mara ili kujua kama tumeathirika au la”,amesema.

 Amesema faida ya kutambua afya yako zipo nyingi ikiwemo endapo utagundulika una maambukizi uweze kupata ushauri nasaha utakaokuwezesha kuishi maisha marefu.


 Kwa upande wake Bakari Ramadhani, amesema kazi yake ya kusafiri sehemu nyingi hapa Tanzania , imechangia awe na  mtandao mingi ya hatari ya ngono lakini baada ya kupima na kugundulika

Tuesday, December 3, 2013

BREAKING NEWS....! MWENYEKITI WA CHADEMA MKOA WA SINGIDA KAJIUZULU.

                                                                                                                 
                                                                                                                    WILFRED NOEL KITUNDU
MWENYEKITI CHADEMA MKOA SINGIDA
S.L.P 260
3.12.2013
KATIBU WA CHADEMA MKOA
S.L.P 260
SINGIDA
YAH: - KUJIUZURU UENYEKITI MKOA SINGIDA
Somo hapo lahusika,
Ninapenda kukuarifu kuwa nimeamua kujiuuzuru nafasi yangu ya uenyekiti wa mkoa ambayo nimekuwa nikiitumikia kwa kipindi kirefu sasa kama kielelezo cha kuamini na kudai demokrasia ya kweli ndani ya chama.

Ikumbukwe kwamba mimi ndio mwanachama wa kwanza kujiunga na CHADEMA mkoa wa SINGIDA na ni mwanachama wa 300 kitaifa, hiyo ni heshima kubwa sana kwangu na sipo tayari kuipoteza kwa kukubali kuwa sehemu ya udharirishaji huu wa demokrasia uliopitiliza

Maamuzi na vitendo vinavyoendelea ndani ya chama chetu kwa sasa ni ubakaji na udharirishaji wa demokrasia ya kweli tunayoihubiri mbele ya umma.

Kwa barua hii basi, nimeonelea bora upate ufahamu huo kuwa si vema mimi kuendelea kupingana na dhamira yangu inayonituma kuwa mwanademokrasia wa kweli.

Kwa kipindi hiki kifupi mnaweza mkaendelea kuitumia anuani yangu ya posta mpaka hapo mtakapopata anuani yenu tayari.

Ninatanguliza shukrani zangu za dhati kwa wanachadema wote wanaopinga upuuzi huu uliofanywa na kamati kuu ya chama.

Kusimamia haki, katiba na misingi ya chama ni wajibu wangu, hivyo kwa namna yoyote ile sitaweza kuwa tayari kufumba macho pindi ujinga wa namna hii unapoendelea kutekelezwa kwa uwoga wa uchaguzi.


Nakutakia kila la heri kwenye majukumu yako.

………………………………………………….
Wilfred N. Kitundu
0764619335/0786215181

MSIMAMO WA MWENYEKITI CHADEMA MKOA WA SINGIDA DHIDI YA UAMUZI WA KAMATI KUU YA CHAMA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


 UTANGULIZI
Ikumbukwe kwamba mimi ndio mwanachama wa kwanza kujiunga na CHADEMA mkoa wa SINGIDA na ni mtu wa  300 kitaifa kujiunga na Chama hiki. Nimejiunga mwaka 1992 siku ya mkutano mkuu kwanza wa uzinduzi chama uliofanyika mnazi mmoja.

Nimekuwa nikijitolea vya kutosha nguvu, muda na akili zangu nyingi kukijenga na kukilinda chama hiki mpaka sasa mkoa wetu wa singida umepata wabunge watatu mmoja wa kuchaguliwa na wawili wa viti maalum.

Tangu mwaka 1992 mpaka 2011, chadema imekuwa ikitumia nyumba yangu kama

Klabu ya Waandishi wa Habari waaswa kuacha makundi.

Katibu mtendaji  wa klabu ya waandishi wa habari (Singpress) mkoa wa Singida, Abby Nkungu akitoa taarifa yake juu ya baadhi ya wanachama na viongozi wa klabu hiyo waliosimamishwa Uanachama kutokana na tuhuma mbalimbali.
Mkurugenzi mtendaji wa Umoja wa vilabu vya waandishi wa habari (UTPC) Tanzania, Abubakari Karsan akitoa nasaha zake mbele ya mkutano mkuu maalum wa klabu ya waandishi wa habari (Singpress) mkoa wa Singida.Mkutano huo uliitishwa kwa ajili ya kuwajadili baadhi ya wananchama ambao hawajishughulishi kikamilifu na kazi ya uandishi wa habari.
Baadhi ya wananchama wa klabu ya waandishi wa habari (Singpress) mkoa wa Singida, wakifuatilia kwa makini taarifa zilizokuwa zikitolewa kwenye mkutano mkuu maalum wa klabu hiyo.
WANACHAMA wa Klabu ya Waandishi wa Habari (Singpress) Mkoa wa Singida wameaswa kuacha kuendeleza makundi kwa madai kwamba yatadumaza ustawi wa klabu hiyo.

Wito huo umetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Umoja wa Vilabu vya Waandishi wa Habari (UTPC) Tanzania, Abubakar Karsan wakati akizungumza kwenye Mkutano Mkuu maalum wa klabu hiyo ya Singpress.

Amesema makundi kwenye chama au kikundi chochote cha watu ni sumu ya maendeleo kwa umoja wa wahusika.

Karsan amesema kuwa maendeleo endelevu ya kikundi au chama cho chote yataletwa na ushirikiano wa dhati baina ya wahusika wa chama au kikundi.

“Mimi niwaombe tu muepuke kuwa na makundi imarisheni ushirikiano upendo na kuvumiliana kwa lengo la kuendeleza klabu yenu Pia viongozi watumikieni kikamilifu wanachama wenu kwa kuwapa fursa kwanza”,amesema.

Katika hatua nyingine, Karsan amesema UTPC imesikitishwa sana na kitendo cha baadhi askari polisi wa Mkoa wa Singida kuwanyanyasa na kuwazuia waandishi wa habari kutekeleza majukumu yao.

“Hata hivyo niwaombeni mfahamu kwamba kitendo hicho hakijafanywa na Jeshi la Polisi isipokuwa kimefanywa na wahuni wachache walioko katika Jeshi la Polisi, Polisi kwa ushirikiano na UTPC itawachukulia hatu stahiki wahuni hao”,alifafanua Karsan.

Mkutano huo maalum, umemchagua Jenifrida Hongoa kuwa Mweka Hazina wa klabu hiyo baada ya kuzoa kura 11 za ndio kati za 15 zilizopigwa.

Hongoa ameziba nafasi hiyo baada ya aliyekuwa Mweka Hazina Awila Silla, kuvuliwa wadhifa huo kwa madai kuwa sio mwanachama halali na pia hana uwezo wa  kumudu nafasi hiyo.

Aidha, Mkutano huo umemchagua Damiano Mkumbo kuwa Makamu Mwenyekiti na Hudson Kazonta kuwa mjumbe wa Kamati ya Utendaji.

Wakati huo huo, Mkutano huo umewaagiza Doris Meghji na Daudi Nkuki kuwasilisha kwa kamati ya utendaji vielelezo vya

Monday, December 2, 2013

Dk. Kone afunga semina ya siku mbili ya soko la kukuza Ujasiriamali (EGM).

Mkuu wa mkoa wa Singida,Dk.Parseko Vicent Kone, akifungua semina ya siku mbili iliyohusu soko la kukuza ujasiriamali (EGM) iliyoandaliwa na soko la hisa la Dar-es-salaam (DSE) na kufadhiliwa na Financial Sector Deepening trust (FSDT).Semina hiyo imefanyika kwenye ukumbi wa Aque Vitae hotel mjini Singida. Kushoto ni Afisa Mahusiano na mshauri wa masula ya Kisheria wa soko la Hisa  Dar-es-salaam, Bi.Mary Mniwasa na kulia ni mwenyekiti  wa TCCIA mkoa wa Singida,Francis Mashuda.
Baadhi ya wajasiriamali na wafanyabiashara mjini Singida,waliohudhuria semina ya siku mbili iliyohusu soko la kukuza Ujasiriamali (EGM) iliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Aqua Vitae hoteli mjini Singida.
Mkuu wa mkoa wa Singida,Dk.Parseko Vicent Kone (wa pili kushoto) akijadiliana jambo na Afisa Mahusiano na mshauri wa masuala ya Kisheria wa soko la Hisa la Dar-es-salaam,Bi. Mary Mniwasa,(wa pili kulia) muda mfupi baada ya kufungua semina ya siku mbili iliyohusu soko la kukuza Ujasiriamali (EGM).
Mkuu wa mkoa wa Singida,Dk.Parseko Vicent Kone,(wa pili kulia walioketi) akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wajasiriamali na wafanyabiashara wa mjini Singida waliohudhuria semina ya siku mbili ya soko la kukuza Ujasiriamali (EGM).Wa kwanza kulia (walioketi) ni afisa mahusiano na mshauri wa masuala la kisheria wa soko la hisa la Dar-es-salaam (DSE) Mary Mniwasa na kushoto ni mwenyekiti wa TCCIA mkoa wa Singida,Francis Mashuda.

WAJASIRIAMALI na wafanyabiashara mkoani Singida wametakiwa kuchangamkia fursa zilizopo Soko la Hisa la Dar es Salaam ili kuboresha na kuendeleza biashara zao.
Mwito huo umetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk Parseko Kone wakati akifungua semina ya siku mbili juu ya Soko la kukuza ujasiriamali iliyofanyika ukumbi wa Aqua Vitae mjini hapa.

Dk Kone alisema kuwa Soko la Hisa la Dar es Salaam kupitia kitengo chake kipya kijulikanacho kama “Soko la Kukuza Ujasiriamali”, ni suluhisho la upatikanaji wa mitaji kwa wajasiriamali kote nchini.
Alisema kuwa soko hilo litatoa suluhisho kwa changamoto zinazowakabili wajasiriamali katika upatikanaji wa uhakika wa mitaji ya muda mrefu kwa ajili ya kuendeleza biashara zao, jambo ambalo limekuwa likiwasumbua wajasiriamali na wafanyabiashara.

“Kwa hiyo basi, soko la kukuza ujasiriamali litasaidia kuleta msukumo wa utekelezaji sera mbalimbali za serikali zinazolenga kuondoa changamoto hizo na kuleta urahisi wa upatikanaji wa mitaji kwa ajili ya kukuza biashara zao,” Dk Kone alisema.
Aidha, alieleza kuwa soko hilo linatarajiwa kulichangamsha soko kwa ujumla kupitia ongezeko la utoaji na uorodheshaji wa hisa, kupanua wigo na fursa za kuwekeza mitaji na kuongeza

Enock Rajabu kutoka Singida aibuka mshindi kwenye droo ya “Chomoka na Mwananchi"


Mwalimu wa shule ya msingi Mwanzi ya Manyoni mjini, mkoani Singida, Enock Rajabu (kulia) akikabidhiwa hundi yenye thamani ya shilingi milioni moja baada ya kushinda droo ya  ’Chomoka na Mwananchi’ na meneja mauzo wa kampuni ya Mwananchi mikoa ya Singida na Tabora, Bw. Aretas Mroso. Shindano hilo la kuwania shilingi milioni moja,bado linaendelea katika droo ya kila siku na inamwezesha mhusika kuingia kwenye droo kubwa ya kujishindia gari kubwa jipya kabisa aina ya TATA safari.

Sunday, December 1, 2013

AMPIGA FIMBO YA KICHWA MAMA MKWE NA KUMSABABISHIA MAUTI, KISA KACHOKA KUMLEA.

Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Singida, ACP. Geofrey Kamwela akitoa taarifa kwa waandishi wa habari (hawapo kwenye picha) juu ya matukio ya kuuawa watu wawili mkoani Singida, likiwemo la Egila Petro kumpiga kwa fimbo mama mkwe wake mwenye umri wa miaka 80 na kusababisha kifo chake.

WATU wawili mkoani Singida wamefariki dunia kwenye matukio tofauti likiwemo la kikongwe mmoja mwenye umri wa miaka 80, kupigwa fimbo kichwani na mkwewe kwa kile kilichodaiwa kuwa mkwewe huyo, amechoka kumlea.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida SACP,Geofrey Kamwela, amesema Egila Petro (42) mkazi wa kijiji cha Mpora kata ya Iseke tarafa ya Nkoko wilayani Manyoni amempiga fimbo kichwani mama mkwe wake Doris Chiwiche na kumsababishia kifo chake siku tisa baadaye.

Amesema kikongwe huyo Doris alipigwa fimbo kichwani na Egila Novemba 18 mwaka huu saa nane mchana na alifariki Novemba 27 mwaka huu saa 12 asubuhi.

Kamwela amesema chanzo cha mauaji hayo ni mgogoro wa chini kwa chini kati ya Egila na mama mkwe wake Doris huku ikidaiwa kuwa Egila amekuwa akimshinikiza mumewe Benard Mdemu amwondoe mama yake huyo na kumpeleka kwa ndugu zake wengine kwa vile yeye amechoka kumlea.

Katika tukio jingine Kamanda Kamwela amesema John Liongo (37) mkazi wa Misuna Singida mjini amefariki dunia baada ya kupigwa risasi kichwani na tumboni na watu wasiojulikana.

Amesema tukio hilo limetokea Novemba 27 mwaka huu saa 6.10 mchana huko katika kijiji cha Mnang’ana kata na tarafa ya Sepuka wilayani Ikungi.

“Uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa marehemu akiwa na watu wasiojulikana siku ya tukio aliondoka Singida mjini kwa gari ambalo bado halijajulikana namba zake za usajili Walipofika katika kijiji cha Mnang’ana waliingia porini na huko ndiko walipomuulia John”,alifafanua Kamwela.

Kamanda huyo amesema katika eneo hilo la mauaji waliokota

Wakulima Singida wahimizwa kulima Mihogo.

Diwani wa kata ya Ikungi wilaya ya Ikungi, Haji Mukhandi akitoa nasaha zake kwenye mkutano wa uchaguzi wa kamati ya shule ya msingi Ikungi mchanganyiko uliofanyika kwenye viwanja wa shule hiyo kongwe iliyojengwa mwaka 1944.Wa kwanza kulia waliokaa,ni mwalimu mkuu wa shule hiyo,Olivary Kamilly na anayefuata ni mwenyekiti wa kamati ya shule inayomaliza muda wake, Naftali Gukwi.
Mwenyekiti wa kamati ya shule ya msingi Ikungi mchanganyiko anayemaliza muda wake, Naftali Gukwi (ata tetea nafasi yake hiyo), akifungua mkutano wa uchaguzi wa kamati ya shule hiyo uliyofanyika shuleni hapo.Wa kwanza kulia ni mwalimu mkuu Olivarry Kamilly na kushoto ni diwani wa kata ya Ikungi, Haji Mukhandi.
Baadhi ya wazazi/walezi wakipiga kura kuchangua kamati ya shule ya msingi Ikungi mchanganyiko wilaya ya Ikungi katika uchaguzi uliofanyika shuleni hapo.
Baadhi ya wazazi/walezi wakifutatlia kwa makini mkutano wa uchaguzi wa kamati ya shule ya msingi Ikungi mchanganyiko.

DIWANI (CCM) Kata ya Ikungi wilayani Ikungi Haji Mukhandi amewaagiza wakulima kulima mashamba ya kutosha ya muhogo, ili pamoja na mambo mengine, kupunguza makali ya uhaba wa chakula.

 Haji ametoa agizo hilo wakati akizungumza kwenye mkutano wa uchaguzi wa kamati ya shule ya msingi Ikungi mchanganyiko, uliofanyika kwenye viwanja vya shule hiyo iliyojengwa mwaka 1944.

Amesema zao la muhogo ni zao ambalo limepewa kipaumbele na mkoa kwa vile linastahimili ukame na ni kwa ajili ya kinga ya njaa.

 Aidha, amesema zao la muhogo lina soko kubwa kutokana na matumizi yake ambayo ni pamoja na kuliwa kama ugali, vitafunwa mbalimbali na majani yake hutengenezwa mboga (Kisamvu).

 “Matumizi mengine ni kutengeneza vinywaji vya aina ya togwa na pombe. Viwandani muhogo hutumika kutengeneza biskuti, wanga na huchanganywa na mazo mengine kupata chakula cha mifugo”,alifafanua zaidi diwani huyo.

 Amesema kutokana na matumizi hayo, muhogo una soko kubwa ambalo lina mkubwa wa kumwezesha mkulima kuinua kipato chake.

 Mkutano huo wa uchaguzi uliosimamiwa na Mwenyekiti wa Kamati inayemaliza muda wake,Naftal Gukwi, ulimchagua mwalimu mstaafu Rashidi Msaru kutoka kijiji cha Ikungi kuwa mjumbe wa kamati ya shule hiyo kwa kipindi cha miaka mitatu ijayo kuanzia januari mwakani.

 Kwa mujibu wa mwalimu mkuu wa shule hiyo Olivary Kamilly, Msaru anaugana na wajumbe wengine  waliochaguliwa kutoka vijiji vya Muungano na Mbwajiki, ambao ni Selemani Ng’amo na Yoel Isingo.

 Wajumbe wengine wa kamati hiyo ni Hamisi Mdachi, Mwajuma Sambe na Deodatus Mtaturu ambao wamechaguliwa na serikali ya kijiji cha Ikungi.

 “Pia kwenye kamati hiyo watakuwepo

Saturday, November 30, 2013

MWENYEKITI WA KIJIJI MBARONO KWA KUCHOMA MOTO NYUMBA MBILI (2).

Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Singida, ACP. Geofrey Kamwela akitoa taarifa kwa waandishi wa habari (hawapo kwenye picha) juu ya kuwashikilia wanakijiji 25 wakazi wa kijiji cha Makunda tarafa ya Kinampanda wilaya ya Iramba,kwa tuhuma ya kuchoma nyumba mbili kutokana na ugomvi wa kugombea ekari 284 za ardhi.

JESHI LA POLISI Mkoa wa Singida linawashikilia watu 25 wakazi wa kijiji cha Makunda Kata ya Kyengenge tarafa ya Kinampanda Mkoa wa Singida kwa kosa la kuchoma moto nyumba mbili kwa kile kinachodaiwa kuwa ni kutokana na ugomvi wa kugombea ekari 284 za ardhi.

Kati ya watuhumiwa hao mmoja ni Mwenyekiti wa Kijiji cha Makunda, Bw Godfrey Ayubu.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, ACP Geofrey Kamwela amesema tukio hilo limetokea Novemba 26 saa mbili asubuhi huko katika Kijiji cha Makunda.

Amesema siku ya tukio, watu wapatao 50 wakazi wa Kijiji cha Makunda wakiwa wanaongozwa na Mwenyekiti wa Kijiji Bw, Godfrey huku wakiwa wamebeba silaha za jadi walichoma moto nyumba ya Esau Talanzia (47) na kuteketeza mali yote iliyokuwemo ndani.

“Vitu vilivyoteketea kwa moto huo ni magunia sita ya mahindi, gunia mbili za alizeti, godoro moja, fedha taslimu 450,000 pamoja na mali zingine vyote vikiwa na thamani ya zaidi ya Tsh 18 milioni”,amesema Kamwela.

Amesema nyumba nyingine iliyochomwa moto na kuteketeza mali ya zaidi ya shilingi laki saba ni ya Matayo Kizaberga mali ya Matayo iliyoteketea ni gunia nne za mahindi, debe moja la dengu na fedha taslimu laki tano.

“Chanzo cha tukio hilo ni mgogoro wa mashamba ambapo wanakijiji cha Makunda wanapinga Esau na Matayo kumilikishwa ekari 284 wakati sio wazawa wa kijiji hicho”,amesema Kamanda Kamwela.

Kamwela amesema uchunguzi zaidi bado unaendelea na mara baada ya kukamilika watuhumiwa watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili.

Katika tukio jingine, Kamwela amesema mjasiriamali mkazi wa Mwenge mjini hapa, Richard  Williamu (33) Novemba 26 mwaka huu saa 1.45 jioni alipigwa risasi tumboni na paja la kulia na watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi.

“Watu watatu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi walifika kwenye duka la Richard na kuomba wauze vocha na walipoambiwa kuwa dukani hapo hakuna vocha walichomoa bunduki inayodhaniwa ni SMG na

Wachimbaji wadogo wa madini watakiwa kuwa na nidhamu ya matumizi fedha.

Rais wa shirikisho la wachimbaji madini Tanzania (FEMATA), John Bina akifungua kikao cha kwanza cha kamati ya dhahabu ya FEMATA Taifa, kilichofanyikia mjini Singida.Wa kwanza kulia na mwenyekiti wa FEMATA Ahmed Adamu na kushoto ni Golden Hainga, katibu wa FEMATA.
Katibu wa chama cha wachimbaji madini mkoa wa Singida,Farijala Kiunsi akitoa taarifa yake ya utekelezaji katika kikao cha FEMATA.
Baadhi wa wajumbe wa mkutano wa FEMATA wakifuatilia kwa makini mada zilizokuwa zikitolewa kwenye kikao cha wachimbaji Dhahabu mkoani Singida.
Rais wa FEMATA Taifa, John Bina (wa pili kulia walioketi) akiwa kwenye picha ya pomoja na viongozi wa kitaifa wa FEMATA taifa waliohudhuria kikao mjini Singida.Wa kwanza kulia ni mwenyekiti wa FEMATA, Ahmed Adamu na kushoto ni katibu wa FEMATA,Golden Hainga.

RAIS wa Shirikisho la wachimbaji madini Tanzania (FEMATA), John Bina, amewataka wachimbaji madini kujenga utamaduni wa kuwa na nidhamu ya matumizi ya fedha ili fedha wanazozipata ziweze kuwaletea maendeleo endelevu.

 Bina amesema hayo wakati akifungua kikao cha kamati ya dhahabu ya FEMATA taifa, kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa ofisi ya madini kanda ya kati mjini hapa.

 Amesema wachimbaji madini wamekuwa na sifa mbaya kwa madai kwamba, wengi hutumia fedha vibaya na kupelekea shughuli ya madini kutokuwanufaisha kimaisha.

 Bina amesema matumizi  hayo mabaya ya fedha, yana madhara mengi ikiwemo mhusika kufilisika mapema.

 “Uzoefu unaonyesha kwamba mchimbaji akipata kwa mfano shilingi milioni 10,kipaumbele chake kinakuwa ni  kuoga mwili kwa  pombe (bia), ataacha kuchimba madini na kutumbukia kwenye anasa hadi hapo fedha zitakapomwishia”,alifafanua Rais huyo.

 Kwa hali hiyo,Bina aliwataka wabadilike na kuwa na nidhamu nzuri ya matumizi ya fedha, ili fedha wanazozipata ziwasaidie kujiletea maendeleo wao binafsi,familia zao,mkoa wao na taifa kwa ujumla.

 Katika hatua nyingine, Rais Bina aliwataka wachimbaji madini kujiepusha na uchimbaji haramu na pia wajenge utamaduni wa

Friday, November 29, 2013

WANANCHI ZAIDI YA 1,000 SINGIDA WACHOMEWA NYUMBA ZAO MOTO.

Baadhi ya wananchi wakiwa wamehamishia makazi yao chini ya mti uliopo kwenye korongo kijiji cha Handa mpakani mwa Wilaya ya Chemba na Singida Vijijini mara baada ya nyumba zao kuchomwa moto na askari polisi na wale wa kikosi cha kupambana na ujangili kwa madai ya kuvamia hifadhi ya msitu wa mgori 
Huyu ni mmoja wa watoto walionashwa na kamera yetu akiwa amelala hoi kwa kukosa chakula na huduma zingine, baada ya nyumba zao kuchomwa moto wakati wa operesheni ya kuwahamisha katika kitongoji cha Kazamoyo kwa madai ya kuvamia hifadhi, hata hivyo wananchi hao wameisha katika eneo hilo kwa zaidi ya miaka nane toka mwaka 2005 , lakini sheria ya kuingiza eneo hilo kwenye msitu wa hifadhi ya mgori ilifanyika mwaka 2007.

KITUO cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) wametakiwa kufika katika kitongoji cha Kazamoyo kijiji cha Nguamuhanga tarafa ya Mgori Wilayani Singida vijijini na kujionea unyanyasaji dhidi ya wananchi wakati wa zoezi la kuwaondoa katika hifadhi ya msitu wa mgori.

Hayo yamesemwa juzi katika kitongoji hicho na baadhi ya wananchi walioamua kuhamia kwenye korongo na kuishi chini ya miti kama digidigi kunusuru maisha yao kutokana na vipigo kutoka kwa wa kikosi cha kupambana na ujangili Wilaya ya Singida na askari polisi.

Wamesema ni vyema kituo hicho wakafika mapema ili kuona jinsi ambavyo binadamu wanavyoishi maisha ya shida na taabu kwenye eneo hilo kufuatia amri ya mkuu wa Wilaya ya kuhamishwa kwa muda mfupi.

Wamesema eneo hilo wameishi zaidi ya miaka nane na kujenga makazi bora bila matatizo yoyote, lakini jambo la ajabu ni baada ya Wilaya ya Chemba na Singida kuwekeana mipaka na kuonekana kuwa wako Singida.

“Wakati tuko kijiji cha Handa Wilaya ya Chemba, tuliishi bila matatizo lakini baada ya kuhamia singida ndipo mambo yalianza kubadilika na kuambiwa kuwa tuko eneo la hifadhi, hii ni ajabu sana , Wilaya moja tuliishi vizuri hii nyingine haitutaki sasa tuende wapi.” Alihoji mmoja wa kina mama.

Licha ya kukosa huduma muhimu kama vile maji, mahema, vyoo baadhi ya kina mama na watoto walionekana wakiwa katika huzuni kubwa huku wengine wakiangua vilio baada ya kuwaona waandishi wa habari wakidhani kuwa ni

Monday, November 25, 2013

Singida na mkakati wa kuibuka kiriadha.



                             Picha zote kutoka maktaba ya Singida Yetu Blog

SINGIDA ni moja kati ya mikoa ambayo ilikuwa inafanya vizuri katika mchezo wa riadha miaka ya 1980 na kutoa wanariadha mahiri ambao waliiwakilisha Tanzania katika mashindano mbalimbali ya kimataifa.
Mkoa huo ni wenye mandhari nzuri yenye mawe mawe pamoja na mto upande wa kushoto na kulia hususan pale unapofika mkoani hapo.
Hakika mkoa huu ni wenye vitu vingi, lakini kikubwa zaidi ni wakimbiaji wa riadha hususan maeneo ya Singida Vijijini ambako kama wakimbiaji hao wataweza kupewa vifaa maalumu kwa ajili ya kukimbia na wadau wa riadha wakajitokeza na kuchangia zaidi katika riadha, Tanzania itakuwa na medali nyingi na kupata heshima katika nchi mbalimbali duniani.
Nasema hivyo kwa sababu hivi karibuni Mbunge wa Singida Vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu aliandaa mashindano ya riadha hususan vijijini kwa ajili ya kuibua vipaji kwa kushirikiana na Mkurugenzi wa Shrika la African Wildlife Trust (AWT), Pratic Patel.

Mbio hizo zilizojulikana kwa jina la Singida Marathon za kilometa 21, zilianza rasmi Novemba 9, mwaka huu kwa kushirikisha wakimbiaji zaidi ya 400 kutoka Singida Mjini na Singida Vijijini na zilianzia Kijiji cha Mitula, Kata ya Kinyagigi na kuishia Viwanja vya Shule ya Msingu Ntunduu (W) Singida Vijijini.
Mbio hizo zilikuwa za kilometa 21 ambazo ni nusu marathoni na kilometa 5 na mwisho kabisa ni kilometa 2.5 ambazo ziliwashirikisha watoto wa kiume na wa kike. Wakimbiaji walikuwa wamejiandaa wenyewe na walijiandikisha, lakini baadhi yao pamoja na kukabiliwa na ukosefu wa viatu, lakini waliweza kumudu hali hiyo kutokana na mazingira waliyokua nayo na kuonesha vipaji vyao vilivyowashangaza wengi.

Inawezekana kukimbia bila viatu ni jambo lisiloruhusiwa, lakini kutokana na mazingira yenyewe ya vijijini hali hiyo haikuwa kikwazo kwa wakimbiaji hao kukimbia bila viatu ila walionesha kuwa wana moyo na nia ya dhati kuonesha vipaji vyao hakika ilikuwa faraja kubwa kwao kwani mwisho wa siku waliweza kuibuka washindi na wengine wakapata kifuta jasho.

Washindi hao ni Paulo Itambi ambaye aliibuka mshindi wa kwanza kwa upande wa wanaume ambaye alipewa zawadi ya Sh 300,000, Emmanuel Samson wa pili (Sh 200,000) na Samwel Ikungi wa tatu (Sh 100,000). Kwa upande wa wanawake, mshindi wa kwanza Fabiola William (Sh 300,000), Zakia Abdallah (Sh 200,000) na Winfrida Hassani (Sh 100,000).
Mbio za kilometa tano, washindi ni Gabriel Garado (Sh 200,000), Deo Lazaro (Sh 100,000) na Jonas John (Sh 50,000) huku wanawake ni Neema Kisuda (Sh 200,000), Pascalina Silvesta (Sh 100,000) na Christina Yuda (Sh 50,000) ambao washindi wa kilometa 2.5 wakiwa ni Julita Antony (Sh 100,000), Editha Gabriel (Sh 50,000) na Magreth Bernado (Sh 25,000).
Wanaume walikuwa ni Petro Pascal mshindi wa kwanza na kupewa Sh 100,000, Baraka Sebastian (Sh 50,000), Haji Swalehe (Sh 25,000) huku washindi wengine 400 kila mmoja akipewa Sh 10,000. Baada ya washindi hao kukabidhiwa zawadi zao, Patel ambaye alikuwa mgeni rasmi kwa niaba ya Naibu Waziri Nyalandu, alikabidhi pia medali mbalimbali kwa washindi hao.

Aidha, alitoa changamoto kwa

Friday, November 22, 2013

WAHAMASISHWA KUTUMIA VYOO BORA ILI KUZUIA MAGONJWA YA MILIPUKO.



BAADHI YA VYOO BORA MKOANI SINGIDA.
Kata ya Mtamaa Manispaa ya Singida inakabiliwa na tatizo la ukosefu wa vyoo bora hali inayoweza kusababisha kutokea kwa magonjwa ya miripuko ikiwemo kipindupindu.

Uchunguzi uliofanywa na Singida Yetu Blog katani hapo umebaini kuwa kati ya kaya tano hadi kumi ni kaya moja tu ndiyo yenye choo bora huku kaya nyingine zikiwa zinatumia vyoo visivyo bora na nyingine kutumia vyoo vya majirani au vya taasisi za elimu kama vile shule.

Baadhi ya wakazi walihojiwa na standard radio wamesema kukosekana kwa vyoo bora kumesababishwa na kukosekana kwa elimu huku wengine wakisema vyoo vingi vilibomolewa na mvua zilizonyesha mwanzoni mwa mwaka huu

Akizungumzia tatizo hilo Diwani wa kata hiyo Bw. Gwae Mbua amesema kuwa kwa kuanza wameanza kuweka msisitizo katika shule kuwa na vyoo bora na baada ya kukamilika mpango huo utahamia katika

KATA YA MTAMAA MANISPAA YA SINGIDA YAPATA NEEMA YA UMEME.


Mjumbe wa halmashauri kuu ya taifa CCM Bw. Hassan Mazala (Picha Kutoka Maktaba Yetu)

Kata ya mtamaa manispaa ya Singida inatarajiwa kuunganishiwa nishati ya umeme wa grid wa taifa kupitia mradi wa umeme vijijini REA ili kukabiliana na umasikini wa kipato kwa wananchi wa kata hiyo.

Mjumbe wa halmashauri kuu ya taifa CCM Bw. Hassan Mazala wakati akizungumza na wananchama wa CCM katika kata hiyo ambapo amesema upembuzi yakinifu juu ya mradi huo unatarajiwa kuanza mwezi huu.


Amesema kuwa endapo umeme ukiunganishwa katika kata hiyo kutasaidia wananchi kujishughulisha na shughuli za kiuchumi ambazo zinategemea nishati hiyo na hatimaye kuondokana na umasikini wa kipato unaowakabili wakazi wa kata hiyo


Aidha Bw Mazala ametoa wito kwa wananchi wa kata hiyo kuwa tayari kuonyesha nia ya kuhitaji huduma hiyo kwa kujiandikisha hali ambayo itaongeza juhudi za mradi huo wa REA kwenda kasi kutokana na mahitaji ya

Wednesday, November 20, 2013

Chuo Cha Utumishi wa Umma kuongeza matawi zaidi.

Mtendaji mkuu wa chuo cha utumishi wa umma Tanzania, Said Nassor kitoa taarifa yake kwenye mahafali ya 16 ya chuo hicho yaliyofanyika mjini Singida. Jumla ya wahitimu 1,909 kutoka chuo cha Tabora na Singida walihitimu katika ngazi mbalimbali.
Mkuu wa mkoa wa Singida,Dk.Parseko Kone akitoa nasaha zake kwenye mahafali ya 16 ya chuo cha utumishi wa umma Tanzania yaliyofanyika mjini Singida.Kulia aliyekaa,ni Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais Menenjimenti ya Utumishi wa Umma Tanzania, Mh.Celina Kombani ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mahafali hayo.
Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma Tanzania,Celina Kombani akizungumza kwenye mahafali ya 16 ya chuo cha Utumishi wa Umma Tannzania mjini Singida.
Baadhi ya wahitimu wa chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania,waliohitimu mafunzo yao.

WAHITIMU wa Chuo Cha Utumishi wa Umma Tanzania wameagizwa kutumia elimu walioipata kufanya kazi kwa ufanisi ili kuleta tija kwa lengo la kukuza na kuendeleza uchumi wa nchi.

 Agizo hilo limetolewa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Tanzania, Celina Kombani, wakati akizungumza kwenye sherehe ya mahafali ya 16 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, mjini hapa.

 Aliwaasa kuwa wawe watendaji wazuri mara watakapoanza kazi,na hiyo iende sambamba na kuzingatia kanuni , sheria na taratibu za utumishi wa umma.

 “Tekelezeni majukumu yenu kwa ufanisi kwa kuonyesha uwezo wa kumudu majukumu,uadilifu  na kutoa huduma bora kwa wananchi na sio kufanya kazi kwa mazoea, ili kukamilisha lengo la serikali la kupata matokeo makubwa sasa” amesema Kombani

 Awali Mtendaji Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania Said Nassor, amesema wana mkakati wa kupanua vyuo vyake ambapo mwakani wanaanzisha tawi jipya mkoani mbeya.

 Aidha, amesema pia mwakani wanatarajia kuongeza madasa katika tawi la tabora na wataanza ujenzi wa Tawi la chuo cha mkoa wa singida.

 “kwa ujenzi wa tawi la mkoa wa singida, tayari tumekamilisha zoezi la la kulipa fidia kiasi cha shilingi

SEMA yagharamia ujenzi wa Vyoo kwa Tsh 155m shule tano za Manispaa ya Singida.

Meneja wa shrika la SEMA, Ivo Manyanku,(wa kwanza kulia) akitoa taarifa yake ya ujenzi wa vyoo bora katika shule tano za msingi manispaa ya Singida kwa Naibu Waziri TAMISEMI (Elimu), Mh. Kassim Majaliwa (mwenye miwani).Vyoo hivyo vimegharimu zaidi ya shilingi 155 milioni.
Naibu Waziri TAMISEMI (Elimu) Mh. Kassim Majaliwa (aliyeipa kisongo kamera) akizindua rasmi ujenzi wa vyoo bora katika shule ya msingi Unyankindi.Vyoo hivyo bora vimejengwa kwa gharama ya shilingi 155 milioni na shirika la SEMA.Kushoto ni meneja wa SEMA. Ivo Manyanku.
Naibu Waziri wa TAMISEMI (Elimu),Kassim Majaliwa akikata utepe kuashiria ufunguzi wa matumizi ya vyoo bora vya shule ya msingi Unyankindi mjini Singida.Vyoo hivyo vimejengwa na shirika la SEMA kwa gharama ya shilingi 155 milioni.
Moja ya vyoo bora vya shule ya msingi Unyankindi manispaa ya Singida vilivyojengwa na shirika la SEMA la mkoa wa Singida.

Shirika lisilo la kiserikali la Sustainable Environment Management Action (SEMA) la mkoani Singida limetumia zaidi ya shilingi 155 milioni kugharamia ujenzi wa vyoo bora katika shule tano za manispaa ya Singida.

 Shule zilizonufaika na mradi huo ni,Unyankindi,Singidani,Manguamitogho,Mtamaa na Mtisi.

 Hayo yamesemwa juzi na Meneja wa SEMA, Ivo Manyanku wakati akizungumza kwenye hafla iliyofana ya uzinduzi wa vyoo hivyo uliofanyika katika shule ya msingi Unyankindi Singida mjini.

 Amesema fedha hizo zilizotumika katika ujenzi huo zimetolewa ufadhili na shirika la WaterAid Tanzania kwa ajili ya kutekeleza mradi wa maji na usafi shuleni katika halmashauri ya manispaa ya Singida.

 “Vyoo hivi vina matundu 48 ambayo yana uwezo wa kuhudumia wanafunzi 2,903 kati yao wavulana ni 1,446 na wasichana ni 1,457.Idadi hiyo inajumuisha na walemavu 38 ambao 25 ni wavulana na 13 ni wasichana”,amesema Meneja huyo.

 Kwa upande wake mgeni rasmi katika uzinduzi huo,naibu waziri TAMISEMI (elimu),Kassimu Majaliwa,alitumia fursa hiyo kulipongeza shirika la SEMA kwa ujezi bora wa vyoo hivyo ambavyo vimekidhi vigezo vyote vinavyohitajika.

 Amesema serikali na wadau wengine wa maendeleo hawana budi kuliunga mkono shirika la SEMA kwa madai linatelekeza miradi yake kulingana na thamani ya fedha zilizotumika.

 “SEMA binafsi nawapongezeni sana ujenzi huu mtakuwa mmeisaidia serikali katika kupunguza

Tuesday, November 19, 2013

Waislamu Singia wamuenzi mjukuu wa Mtume Al – Imamul – Hussein (A.S)




Baadhi ya waumini wa Dhehebu la Shia mkoani Singida wakiwa kwenye matembezi ya kuadhimisha kumbukumbu za kifo cha mjukuu wa Mtume Al-Imamul Hussein (AS).