Thursday, April 11, 2013

Mkuu wa wilaya ya Singida afanya ziara ya kukagua usafi kwenye soko la Vitunguu Misuna.

 Mkuu wa wilaya ya Singida, mwalimu Queen Mlozi (wa pili kulia) akizungumza na katibu wa soko la vitunguu Misuna, Jonathan Gunda Mtumba (kushoto aliyeshika vitunguu). Kitunguu chekundu  alichoshika DC Mlozi, ndivyo vyenye bei kubwa kuliko alivyoshika katibu Jonathan vyenye rangi ya kijivu.
 Baadhi ya wanawake wa manispaa ya Singida wamepata ajira ya muda ya kuchambua vitunguu na kuvijaza kwenye magunia kama wanavyoonekana kwenye picha.
Baadhi ya wafanyabishara makuli na vibarua wengine wa soko la vitunguu la Misuna walivyokutwa na mpiga picha wetu.
Mkuu wa wilaya ya Singida,mwalimu Queen Mlozi, akiwahimiza mama lishe wa soko la vitunguu la Misuna kudumisha usafi wakati wote ili kuondoa uwezekano wa kulipuka kwa magonjwa ya mlipuko ukiwemo kipindupindu.

No comments:

Post a Comment