Sunday, June 2, 2013

Watoto wawili wa familia moja wauawa kikatili mkoani Singida baada ya kulawitiwa na watu wasiojulikana.

 Afisa mtendaji wa kata ya Iguguno Josia Pangani akizungumzia tukio la kulawitiwa na kisha kunyongwa hadi kufa wanafunzi wawili wa familia moja wa shule ya msingi Lukomo wilaya ya Mkalama.
 Mama mzazi wa watoto waliobakwa na kisha kunyongwa hadi kufa Veronica Nuru mkazi wa kijiji cha Lukomo wilaya ya Mkalama, akizungumzia tukio la kuuawa kikatili watoto wake.
Makaburi walikozikwa wanafunzi wawili waliolawitiwa na kisha kunyongwa hadi kufa.

Watoto wawili wa familia moja wameuawa kikatili  mkoani Singida baada ya kulawitiwa na  watu wasiojulikana,  kisha  kunyongwa kabla ya milii yao  kwenda kufungwa kwenye mti porini.

Watoto hao wametajwa kuwa ni Esta Daudi  (14)  na  Anita Shila (9)  wote wanafunzi wa darasa la saba na  tatu katika shule ya msingi Lukomo kata ya Iguguno wilaya ya Mkalama mkoani Singida.

Afisa mtendaji wa kata hiyo Josia  Pangani, amesema tukio hilo limetokea majira ya saa  12 jioni wakati watoto hao  wa kike wakiwa wanachunga mifugo kwenye pori jirani na nyumbani kwao.

Pangani amesema  baada ya  muda  wa kurejesha  mifugo  zizini kufika, wazazi wa watoto hao  walishangaa kutowaona watoto wala mifugo, hali iliyosababisha kuanza juhudi za kuwatafuta.

Amesema juhudi hizo hazikuweza kuzaa matunda siku hiyo hadi kesho yake walipoikuta miili ya watoto hao ikiwa imefungwa kwenye mti.

Baada ya uchunguzi  wa kitaalamu kufanyika, ilibainika kuwa walibakwa, kunyongwa shingo, kisha kufungwa vitambaa usoni na watu wasiojulikana.

Habari za kipolisi zinasema  kuwa watu wawili akiwemo baba mzazi wa watoto waliouawa
wanahojiwa kuhusiana na tukio hilo.


Tukio hilo limekuja mwezi mmoja tu baada ya mvulana mmoja mkazi wa kijiji hicho kulawitiwa, kuvunjwa mkono na kutobolewa  macho kisha kuuawa, hali inayozua hofu kubwa kwa wakazi wa eneo hilo.

3 comments:

  1. AnonymousJune 14, 2013

    Wow, this aгtіcle is fastiԁіous, my sister is analyzing these kinԁs of things,
    thus I am going to сonvey her.

    My web sіtе; Lodgings pertaining to Visitors along with People to Morocco mole

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 14, 2013

    You ѕhould be a part of a соntest for
    one of the best blogs online. I'm going to highly recommend this web site!

    Visit my web site - airline

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 15, 2013

    Please let me κnоw if уou're looking for a article writer for your blog. You have some really good articles and I think I would be a good asset. If you ever want to take some of the load off, I'd lоvе to write somе content
    fοr уour blog in exchange foг а linκ back tο mine.
    Plеase blast me аn e-mаіl if interestеd.
    Mаnу thanks!

    my ωеbpage: Street. Mark's Basilica Venice Italy

    ReplyDelete