Thursday, October 24, 2013

WALIOSACHI MAITI NA KUPORA ZAIDI YA MILLION 19 KORTINI KWA HUKUMU.

 Gari aina ya Land cruiser mali ya chuo cha SUA cha mjini Morogoro kama linavyoonekana baada ya kupigwa mawe na watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi  nje kidogo ya mji wa Singida.
 Kesi inayowakabili washitakiwa watano walioteka gari la chuo cha SUA mjini Morogoro na kunyang’anya zaidi ya shilingi 19.8 milioni, hukumu yake inatarajiwa kutolewa kesho na mahakama ya wilaya ya Singida. Utekaji huo ulifanyika Desemba sita mwaka jana saa saba na nusu usiku kwenye barabara kuu ya Dodoma – Singida eneo la Kisaki manispaa ya Singida.
Hudumu wa chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali ya mkoa mjini Singida ambaye jina lake halikuweza kutambuliwa mara moja,akiliweka sawa baada ya kufanyiwa ukarabati baada ya kubomolewa na majambazi na kulisachi.

KESI inayowakabili washitakiwa watano ya utekaji wa gari la chuo cha SUA Morogoro mjini na kisha kunyang’anya zaidi ya shilingi 19.8 milioni hukumu yake inatarajiwa kutolewa kesho na Mahakama ya Wilaya ya Singida.

Hukumu hiyo inayovutia hisia za wakazi wengi wa Manispaa ya Singida na vitongoji vyake inatarajiwa kusomwa na hakimu wa Wilaya ya Singida Flora Ndale.

Washitakliwa hao inadaiwa baada ya kufanikiwa azma yao ya unyang’anyi wa kutumia silaha za jadi waliweza kufungua jeneza lililokuwa linasafirisha mwili wa mwanafunzi wa SUA Munchari Lyoba na kulisachi kwa imani kwamba kuliwekwa mali.

Washitakiwa hao vijana ni Idd Omari (37),Khalid Hamisi (20), Abubakari Jumanne (25) wote wakazi wa kijiji cha Kisaki Manispaa ya Singida Wengine ni Hamisi Issa (32) mkazi wa kijiji cha Unyamikumbi na Amosi Ally (22) mkazi wa kijiji cha Mtakuja.

Washitakiwa hao wanatuhumiwa kuteka gari linalomilikiwa na SUA lenye namba za usajili SU 37012 ambalo siku ya tukio lilikuwa linaendeshwa na Kalistus Malipula.

Washitakiwa hao waliteka gari hilo desemba sita mwaka jana saa saba na nusu eneo la kijiji cha Kisaki Gari hilo lilikuwa linasafirisha mwili wa mwanafunzi Lyoba kwenda kuzikwa mkoani Mara.


Inadaiwa washitakiwa hao walitumia silaha za jadi ikiwemo
fimbo na mawe kufanikisha azma yao hiyo Waliweka mawe makubwa barabarani kwa lengo la kuzuia magari kupita.

HABARI KUHUSIANA NA TUKIO LA KUIPORA MAITI BOFYA HAPA

No comments:

Post a Comment