Wednesday, December 18, 2013

MAJAMBAZI MAWILI YAUWAWA (Samahani Kwa Picha Hizi)


WATU wawili wakazi wa manispaa ya Singida ambao majina yao bado hayajajulikana,wakiwa kwenye Jokofu la kuhifadhia maiti baada ya kuuawa wakati wa majibishano ya risasi na polisi.
Kamanda wa polisi mkoa wa Singida,SACP Geofrey Kamwela,akionyesha bunduki ya kijeshi aina ya SMG no.34555  iliyokuwa ikitumiwa na watu wawili wanaodhaniwa kuwa majamabazi katika kijiji cha Manga manispaa ya Singida.

JESHI  la Polisi mkoani Singida limewauwa watu wawili wanaodhaniwa kuwa ni majambazi wakati wa kurushiana rasasi.
Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Singida, SACP, Geofrey Kamwela amesema tukio hilo limetokea desemba tisa mwaka huu saa 12:00 jioni, huko katika kijiji cha Manga nje kidogo ya mji wa Singida.
Amesema watu watatu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi wakiwa na bunduki moja ya kijeshi aina ya SMG, walifika kijijini hapo kwa lengo la kufanya uhalifu.
Kamanda Kamwela, amesema watu hao ambao miili yao imehifadhi kwenye chumba cha mochwari katika hospitali ya mkoa, majina na makazi yao bado hayajajulikana.
Akifafanua, amesema taarifa za siri kutoka kwa raia wema zilifikia jeshi la polisi na ndipo askari polisi walipofika kwenye eneo la tukio.
“Baada ya polisi kufika kijijini hapo watu hao walistuka kuwa wanafuatilwa na askari polisi na hivyo kuanza kukimbia kuelekea kijiji cha Uhamaka kwa kutumia pikipiki yenye namba za usajili T. 634 BTW aina ya Sanlag yenye rangi nyeusi”,amesema Kamwela.
Amesema walipoona Polisi wanawakaribia waliamua kutelekeza pikipiki yao hiyo na kuanza kukimbilia porini kwa miguu.
“Hali ilipokuwa ngumu zaidi, walianza kuwarushia polisi risasi, hivyo polisi nao ikwabidi kujibu mapigo.  Katika majibizao hayo ya risasi, majambazi mawili yaliweza kujeruhiwa huku mmoja akifanikiwa kutoroka”
Amesema majambazi hayo yaliyojeruhiwa yalifariki dunia wakati yanakimbizwa katika hospitali ya mkoa kwa matibabu,lakini yakafia njiani.
Amesema katika eneo la tukio, ilipatikana
bunduki moja aina ya SMG yenye namba 34555 ikiwa na risasi saba kwenye magazine.  Pia pikipiki iliyokuwa iantumiwa na majambazi hayo, iliwezea kupatikana.
Kamwela alitoa wito kwamba wananchi waendelee na moyo huo huo wa kuwafichua watu wanaowatilia shaka ili waweze kudhibitiwa mapema kabla ya kufanya uhalifu.

No comments:

Post a Comment