Monday, September 30, 2013

TANROADS Singida yatumia shilling 6.4 bilioni kugharamia matengenezo ya barabara.

 Mkuu wa mkoa wa Singida na mwenyekiti wa bodi ya barabara mkoa wa Singida, Dk.Parseko Kone akifungua kikao cha 35 cha bodi ya barabara kilichofanyika kwenye ukumbi wa ofisi ya mkuu wa mkoa mjini Singida.Wa kwanza kulia ni mwenyekiti wa CCM mkoa wa Singida, Mgana Izumbe Msindai na kushoto ni mbunge wa jimbo la Singida Magharibi Mohammed Missanga.
 Kaimu meneja wa TANROADS mkoa wa Singida, Eng.Yohannes Mbegalo (wa kwanza kushoto) akifuatilia kwa makini taarifa mbalimbali zilizokuwa zikijadiliwa kwenye kikao cha 35 cha bodi ya barabara mkoa wa Singida.
Baadhi ya wakuu wa wilaya za mkoa wa Singida waliohudhuria kikao cha 35 cha bodi ya barabara mkoa wa Singida kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano ofisi ya mkuu wa mkoa Singida.

WAKALA wa barabara (TANROADS) Mkoa wa Singida umetumia zaidi ya shilingi 6.4 bilioni katika kugharamia matengenezo mbalimbali ya barabara kuu za mkoa na madaraja katika kipindi cha kuanzia Januari hadi Juni mwaka huu.

Hayo yamesemwa na Kaimu Meneja wa TANROADS, Mkoa wa Singida Eng.Yohannes Mbegalo wakati akitoa taarifa yake ya utekelezaji mbele ya kikao cha 35 cha bodi ya barabara mkoa kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa ofisi ya mkuu  wa mkoa mjini hapa.

Amesema fedha hizo zimetumika kugharamia matengenezo ya kawaida kwa upande wa barabara za lami na changarawe.

“Pia zimetumika kugharamia matengenezo ya sehemu korofi,matengenezo ya vipindi maalum.Matengenezo yote hayo yamefanyika kwenye barabara za lami na zile za changarawe Shilingi 1.5 bilioni zimetumika katika matengenezo ya madaraja mbalimbali”,amesema Kaimu Meneja huyo.

 Kwa upande wa miradi mikubwa, Mbegalo amesema barabara ya Manyoni-Itigi-Chaya mkoani Tabora inayojengwa kwa kiwango cha lami na mkandarasi Sinohydro Corporation kutoka China yenye urefu wa kilomita 89.3,ujenzi wake hadi Juni mwaka huu,ulikuwa asilimia 43.9 kulingana na mkataba,wakati kazi ilitakiwa iwe imefikia asilimia 89.

 “Mradi mwingine mkubwa wa ujenzi wa daraja la

Sunday, September 29, 2013

Mtoto auawa na Bibi yake kwa kuchelewa kuleta Mwiko wa Ugali

 Mwenyekiti wa mtaa wa Lulumba New Kiomboi mjini wilaya ya Iramba, Abel Seit akitoa taarifa kwa waandishi wa habari (hawapo kwenye picha) juu ya tukio la mtoto wa kike Zuhura (6) kumwagiwa maji ya moto na bibi yake Magreth Sombi (55) na kusababisha kifo chake.
 Mwenyekiti wa mtaa wa Lulumba New Kiomboi mjini wilaya ya Iramba,Abel Seit akifungua mlango wa nyumba ya Magreth Sombi ambaye kwa sasa anashikiliwa na polisi kwa tuhuma ya kumuuguza mjukuu wake Zuhura na kusababisha kifo chake.
 Sehemu ya ndani ya nyumba ya mtuhumiwa Magreth Sombi anayedaiwa kumuuguza mjukuu wake maji ya moto na kusababisha kifo chake.
 Mtoto wa mtuhumiwa Magreth Sombi,Naomi ambaye hivi karibuni amehitimu mafunzo ya ualimu mkoani Tabora na alikuwa anasubiri kupangwa kazi.Kwa sasa Naomi na mama yake Magreth Sombi wanashikiliwa na jeshi la polisi wilaya ya Iramba kuhusiana na mauaji ya Zuhura.
Picha ya mtuhumiwa Magreth Sombi anayetuhumiwa kumuua mjukuu wake Zuhura kwa kumumwagia maji ya moto ambayo yaliyokuwa yatumike kupikia ugali wa jioni.

Mtoto wa kike aliyetambulika kwa jina moja la Zuhura (6) mkazi wa mtaa wa Lulumba New Kiomboi mjini, wilayani Iramba,amefariki dunia baada ya kudaiwa kuuguzwa kwa maji ya moto na bibi yake Magreth Sombi (55).

Imedaiwa kwamba Zuhura alimwagiwa maji ya moto ambayo yalikuwa yatumike kupikia ugali,kwa kile kilichodaiwa kuwa ni kitendo cha mtoto huyo kuchelewa kukabidhi mwiko aliotumwa na bibi yake.

Akisimulia mkasa huo wa aina yake,Mwenyekiti wa mtaa wa Lulumba,Abel Seit,amesema tukio hilo limetokea Septemba 24 mwaka huu majira ya jioni huko mtaa wa Lulumba katika mji wa New Kiomboi.

Amesema siku ya tukio,Zuhura alitumwa na bibi yake Magreth akalete mwiko wa kusoga ugali wa jioni na inadaiwa kwamba mtoto huyo alichelewa kuukabidhi mwiko huo.

Seit amesema baada ya kuleta mwiko huo,alimwagiwa mwilini maji yaliyokuwa yamechemka tayari kwa kutumika kupikia ugali wa jioni.

“Kama vile adhabu hiyo haikutosha,Magreth kwa ushirikiano na mtoto wake Naomi,walimkamata kwa nguvu Zuhura na kisha kuingiza viganja

Friday, September 27, 2013

Wanahabari wa Singida watahadharishwa kuhusu Ukimwi.


 Baadhi ya wananchama wa klabu ya waandishi wa habari (Singpress) mkoa wa Singida wakijifunza uandishi wa habari kupitia mtandao. Mafunzo hayo ya siku nne yamefanyikia katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya mkuu wa wilaya Iramba. Mwenye fulana ya misitari ni mkufunzi wa mafunzo hayo ya uandishi kupitia mtandao (on line journalism),John Mnubi akiwaelekeza wanachama wa Singpress namna ya kufungua blog.

Wanachama wa Klabu ya Waandishi wa Habari (Singpress) Mkoa wa Singida, wametahadharishwa na vitendo vya ngono zembe vinavyochochea maambukizi mapya ya virusi  Ukimwi kwa madai kwamba baadhi ya wanawake wa mjini Kiomboi Wilaya ya Iramba hawajui kusema ‘hapana’ pindi wanapoombwa kuwa na mahusiano ya kimapenzi.

Mwenyekiti wa Singpress,Seif Takaza ambaye ni mkazi wa mjini New Kiomboi,ametoa tahadhari hiyo wakati akiwakaribisha wanachama 15 wa Singpress wanaohudhuria mafunzo ya siku nne ya uandishi bora wa habari kupitia mtandao (on line Journalism).

Mafunzo hayo yanayosimamiwa na Mwezeshaji John Mnubi kutoka mkoa wa Iringa,yanaendelea kwenye ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Iramba mkoani  Singida.

Akifafanua,Takaza alisema baadhi ya wanawake na wasichana wa mjini hapa,wana tabia ya kuchangamkia wageni hususani wanaokuja kuhudhuria

Wednesday, September 25, 2013

Halmashauri za Wilaya na Manispaa waaswa kutotoza ushuru kwa ‘Lumbesa’

 Mkuu wa wilaya ya Singida, mwalimu Queen Mlozi akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi msaada  mizani za vipimoaina mbalimbali  iliyotolewa na wakala wa vipimo uliopo chini ya wiraza ya viwanda na biashara kwa lengo la kupiga vita magunia maarufu kwa jina la Lumbesa.Wa pili kulia ni kamishina msaidizi wa wakala wa vipimo,Peter Samwel Masinga na wa kwanza kulia ni makamu mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Singida, Elia Digha.
 Kamishina msaidizi wa wakala wa vipimo,Peter Samwel Masingida akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi msaada wa mizani ya aina mbalimbali iliyotolewa msaada na wakala wa vipimo kwa ajili ya kukabiliana na tatizo sugu la gunia maarufu kwa jina la Lumbesa.Wa kwanza kushoto ni mkuu wa wilaya ya Singida,mwalimu Queen Mlozi na kulia ni makamu mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Singida na diwani wa kata ya Msange, Elia Didha.
 Kamishina msaidizi wa wakala wa vipimo Peter Samwel  Masinga (kulia)akimkabidhi mkuu wa wilaya ya Singida,mwalimu Queen Mlozi moja ya mizani iliyotolewa na wakala wa vipimo kwa ajili ya kukabiliana na gunia aina ya lumbesa linalodaiwa kuwadhulumu wakulima jasho lao.
 Mkuu wa wilaya ya Singida,mwalimu Queen Mlozi (kushoto) akimkabidhi mstahiki meya wa manispaa ya Singida moja ya mzani uliotolewa na wakala wa vipimo kwa lengo la kutokomeza gunia maarufu kwa jina la lumbesa linalodaiwa kuwapunja mapato wakulima.
Mkuu wa wilaya ya Singida, mwalimu Queen Mlozi (kushoto) akimkabidhi makamu mwenyekiti wa halmashauri ya Singida na diwani wa kata ya Msange,Elia Digha moja ya mzani uliotolewa msaada na wakala wa vipimo kwa lengo la kutokomeza gunia aina ya Lumbesa.

Halmashauri za Wilaya na Manispaa Mkoa wa Singida, zimeaswa kutotoza ushuru kwa kutumia kipimo cha ‘gunia’ ambacho kimedaiwa kushawishi wafanyabiashara na wasafirishaji kutumia kitendo hicho cha kujaza gunia maarufu kama ‘Lumbesa’ kwa lengo la kulipa ushuru kidogo.

Hayo yamesemwa hivi karibuni na Kamishina Msaidizi wa Wakala wa Vipimo Ndugu Peter Samwel Masinga,wakati akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi mizani za viwango mbalimbali ambazo zimetolewa  kwa msaada na Wizara ya Viwanda na Biashara.

Msaada huo umetolewa kwa halmashauri ya wilaya na manispaa ya  Singida Ndugu Masinga  amesema matumizi ya kipimo cha kutumia gunia kutoza ushuru yalibainika juni mwaka huu wakati afisa mtendaji mkuu wa wakala wa vipimo, Magdalena Chuwa alipotembelea mkoa wa Singida.

Masinga alisema halmashauri kuendelea kutoza ushuru kwa kutumia kipimo cha

Friday, September 20, 2013

Serikali ya Mkoani Tabora imewaagiza madiwani kusimamia kikamilifu fedha za umma

 Katibu tawala mkoa wa Tabora, Kudra Mwinyijuma akizungumza kwenye hafla ya kumuaga aliyekuwa mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Igunga Protace Magayane Kwa sasa Magayane ni mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Ikungi mkoa wa Singida. Pia katika hafla hiyo iliyofanyika Igunga mjini,mkurugenzi mpya wa halmashauri ya Igunga, mwalimu Rustika Turuka alikaribishwa rasmi.Wa kwanza kulia (walioketi) ni mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Ikungi,Protace Mgayane na anayefuatia ni mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Igunga, Abubakari Shaban.
 Katibu tawala mkoa wa Tabora, Kudra Mwinyijuma (kulia) akimkabidhi mweka hazina wa halmashauri ya wilaya ya Igunga,Gordon Julius Dinga,cheti maalum baada kuiwezesha halmashauri hiyo kupata hati safa ya mahesabu kwa kipindi cha mwaka wa fedha wa 2010/2011 na 2011/2012.
 Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Igunga mkoani Tabora, Abubakari Shaban akitoa nasaha zake kwenye halfla iliyofana ya kumuaga aliyekuwa mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Igunga, Protace Magayane aliyehamia wilaya ya Ikungi mkoa wa Singida. Pia kumkaribisha mkurugenzi mpya wa halmashauri ya Igunga, mwalimu Rustika Taruka.Wa pili kushoto ni mkurugenzi Protace Magayane na wa kwanza kushoto ni mke wake mkurugenzi Magayane.
 Aliyekuwa mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Igunga,Protace Magayane akitoa nasaha zake wakati akizungumza kwenye hafla ya yeye kuagwa na viongozi na wananchi wa halmashauri ya wilaya ya Igunga.
 Mkurugenzi wa halmashauri mpya ya Ikungi mkoa wa Singida, Protace Magayane (kushoto) akijadiliana mambo ya Afisa wake wa Kilimo Ayubu Sengo wakati wa hafla ya kuagwa (Magayane) iliyofanyika Igunga mjini.
 Baadhi ya viongozi na wananchi wa halmashauri ya wilaya ya Igunga mkoa wa Tabora, wakipata msosi kwenye hafla ya kumuaga aliyekuwa mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Igunga, Protace Magayane na kumkaribisha mkurugenzi mpya wa halmashauri ya wilaya ya Igunga, mwalimu Rustika Turuka.Hafla hiyo ilifanyika  Igunga mjini.
Mtaalam wa kufungua champeni wa wilaya ya Igunga ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja akifungua Shampeni  kwenye hafla ya kumuaga aliyekuwa mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Igunga, Protace Magayane na kumkaribisha mkurugenzi mpya mwalimu Rustika Turuka.

SERIKALI mkoa wa Tabora,imewaagiza madiwani wa Halmashauri ya Wilaya na Manispaa,kusimamia kikamilifu matumizi ya mali za umma ikiwemo fedha, kwa kuzingatia kanuni,taratibu na sheria za nchi.

 Hatua hiyo itasaidia pamoja na mambo mengine,Halmashauri kupata hati safi za mahesabu ya fedha za umma.

 Changamoto hiyo imetolewa juzi na Katibu Tawala Mkoa wa Tabora,Kudra Mwinyimvua,wakati akizungumza kwenye sherehe ya kupongezana watumishi wa Halmashauri ya Igunga kwa kupata hati safi kwa miaka miwili mfululizo (2010/2011 na 2011/2012).

 Alisema dawa pekee ya kuwa na uhakika wa halmashauri kupata hati safi,ni kuimarisha usimamizi wa ndani wa matumizi ya mali za umma ikiwemo fedha za umma.

 Mwinyimvua alisema usimamizi huo pia utasaidia utoaji huduma bora zitakazokidhi matarajio ya wananchi na utekelezaji  wa miradi mbalimbali ya wananchi kuwa ubora unaofanana na fedha za umma zilizotumika.

 “Kwa halmashauri ya Igunga,nitumie jioni hii kuwapongeza kwa dhati kabisa madiwani na watendaji kwa juhudi zao zilizofanikisha halmashauri kupata

Tuesday, September 17, 2013

MEZA YA MAGAZETI LEO JUMANNE TAREHE 17 - 09 - 2013





Wafanyakazi wa Wakala Jiolojia wajeruhiwa wakidhaniwa ni Majambazi na wanyonyaji Damu

 Mfanyakazi wa muda wa wakala waJiolojia mkoani Dodoma na mwanafunzi wa mwaka wa pili katika chuo kikuu Dodoma anayesomea masomo ya Jiolojia, Edwin Rwekiza (25) akipatiwa matibabu katika hospitali ya mkoa baada ya kupigwa vibaya na baadhi ya wananchi wa kijiji cha Irisya wilaya ya Ikungi kwa kuhisiwa kuwa ni Jambazi na mnyonya damu za Binadamu. Edwin amesafirishwa kupelekwa hospitali ya KCMC Moshi mkoani Kilimanjaro kwa matibabu zaidi.
 Mfanyakazi wa wakala wa Jiolojia  Dodoma mjini,Peter Lucas akiwa katika hospitali ya mkoa mjini Singida kutibiwa majeraha yaliyotokana na kupigwa vibaya na wananchi wa kijiji cha Irisya. Wananchi hao pamoja na kuonyeshwa vitambulisho na wafanyakazi hao,hawakuwaamini na kuendelea na imani yao kuwa ni Majambazi na wanyonya Damu za Binadamu.
 Mganga wa zamu katika hospitali ya mkoa, Dk.Reginald Pweleza akizungumzia hali za majeruhi (wafanyakazi wa wakala wa Jiolojia kutoka Dodoma) waliopigwa na wananchi wa kijiji cha Irisya baada ya kuwahisi kuwa ni majambazi na wanyonya Damu za Binadamu.
 Kamishna msaidizi wa madini kanda ya kati Singida,Manase Mbasha,akitoa taarifa kwa waandishi wa habari (hawapo kwenye picha) juu ya wafanyakazi wa wakala wa Jiolojia  kutoka Dodoma,kupigwa na wananchi wa kijiji cha Irisya wilaya ya Ikungi.
    Jengo la ofisi ya madini mkoani Singida.
WAFANYAKAZI wawili wa Wakala wa Jiolojia kutoka Dodoma mjini,wamepigwa na kujeruhiwa vibaya wakiwa kazini na baadhi ya wananchi wa kijiji cha Irisya tarafa ya Sepuka wilaya ya Ikungi,kwa madai ya kuhisiwa kuwa ni majambazi na wanyonyaji damu.

Wananchi hao waliwavamia Peter Lucas (30) na Edwin Rwekiza (25), wakiwa kazini na kuwapiga kwa kutumia silaha za jadi ikiwemo marungu.

Wafanyakazi hao wameumizwa vibaya vichwani na Edwin ambaye ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu Dodoma mwaka wa pili akichukua masomo ya Jiolojia,amevunjika mifupa ya kichwani na hali yake ni mbaya.

Juzi jioni Edwin amesafirishwa kwa ndege kupelekwa hospitali ya KCMC Moshi mkoani Kilimanjaro,kwa matibabu zaidi.Kwa upande wake Peter,yeye anaendelea na matibabu katika hospitali ya mkoa mjini hapa.

Wakala huo ambao unafanya kazi chini ya Wizara ya Madini na Nishati,wafanyakazi wake hao wako mkoani Singida kwa kazi ya kuchora ramani za kijolojia.

Shughuli zingine ni uchunguzi kwa kutumia kemikali,ili kubaini madini na kwa ujumla walikuwa

Monday, September 16, 2013

MEZA YA MAGAZETI LEO JUMATATU TAREHE 16 - 09 - 2013





Watahiniwa wa darasa la saba wamebambwa wakiwa hawajui kusoma na kuandika

JUMLA ya wanafunzi 22 wa shule tatu za msingi wilaya ya Ikungi mkoani Singida,’wamebambwa’ wakiwa kwenye vyumba vya kufanyia mtihani wa taifa darasa la saba,huku wakiwa hawajui kusoma wala kuandika.

 Wanafunzi hao na idadi yao kwenye mabano walikuwa kwenye shule ya msingi Muhintiri (2),Iglansoni (16) na Kinyampee (4) tarafa ya Ihanja wilaya ya Ikungi.

 Wakati kwenye shule ya msingi Mnyange tarafa hiyo hiyo ya Ihanja mwanafunzi mmoja wa kike hakufika kufanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi hakuhudhuria kufanya mtihani huo kwa kile kilichodaiwa tayari ameishaozwa.

 Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Ikungi Protace Magayane,aliyekuwa akikagua maendeleo ya zoezi la kufanya mtihani huo katika siku yake ya mwisho juzi, aliagiza wazazi wa mwanafunzi huyo wa kike ambaye hakufanya mtihani,wachukuliwe hatua stahiki za kisheria haraka iwezekanavyo.

 Baadhi ya wasimamizi akiwemo Ernest Mahendeka wa shule ya Kinyampembee, Rebeca Julius wa Muhintiri na Salum Jafari wa Iglanson wamesema ilibidi wajaze fomu maalumu kulingana na maelekezo kabla ya kuwaacha waendelee na mtihani kulingana na jinsi wanavyoelewa.

 Kwa upande wao  wahitimu akiwemo Perpetua Msengi na John Martin, wamesema wana matumaini makubwa ya kufaulu mtihihani huo, ingawa somo la hisabati lilionekana kuwa gumu kwa upande wao.

 Katika hatua nyingine,Mkurugenzi Magayane amesema wamejipanga vizuri kuhakikisha mwakani

Mkuu wa mkoa wa Singida Amtembelea Hospitalini Mwandishi wa Mwananchi na The Citizen aliyekatwa Mapanga na Jambazi

 Mkuu wa mkoa wa Singida, Dk.Parseko Vicent Kone akimjulia hali Mwandishi wa Habari wa Magazeti ya Mwananchi na The Citizen mkoa wa Singida, Awila Silla anayeendelea na matibabu katika hospitali ya mkoa mjini Singida, akitibiwa majeraha baada ya kukatwa katwa kichwani kwa Panga na kijana anayedaiwa kuwa ni Jambazi.


Mwandishi wa Habari wa Mwananchi na The Citizen Ajeruhiwa kwa Mapanga.


Mwandishi wa habari wa gazeti la The Citizen na mwananchi mkoani Singida, Awila Silla amenusurika kuuawa na mtu anadhaniwa kuwa Jambazi baada ya kukatwa katwa kichwani na kusababisha kuzirai. Tukio hilo limetokea juzi saa mbili usiku jirani na mahakama ya mwanzo ya Utemini mjini Singida. Awila ambaye amelazwa wodi 2  hospitali ya mkoa amedai baada ya kukutana na kijana huyo aliamuriwa

Thursday, September 12, 2013

KIJANA ADAIWA KUKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA MJINI SINGIDA.



Vyandarua vyatumika kuezeka vyoo.

Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mkoani Singida Edward Ole Lenga akizungumza na wananchi wa kijiji cha Kinampundu mara baada ya kukabidhiwa Zahanati na nyumba mbili za mganga na shirika moja lisilo la kiserikali la HAPA,hafla hiyo ilifanyikajuzi kijijini hapo.
 Ni Mwakilishi wa shirika la SIMAVI kutoka nchini Uholanzi Lieke Ongering akizungumza katika hafla ya kukabidhi mradi wake kwa ushirikiano na shirika la HAPA Singida kukamilisha mradi wa ujenzi wa Zahanati na nyumba mbili za mganga kijiji cha Kinampundu takribani umbali wa kilomita 70 kutoka mjini Singida.
Ni mmoja wa kinamama wajawazito akipimwa uzito na mkuu wa Wilaya ya Mkalama Ole Lenga mara baada ya kukabidhiwa vifaa vya zahanati hiyo, anayeshuhudia kipimo hicho ni mhasibu mkuu wa shirika hilo Noel Makyao.
Mkurugenzi wa HAPA Davd Mkanje  (Kulia) kimkabidhi DC wa Mkalama Ole Lenga baadhi ya vifaa vya kutolea huduma kwenye Zahanati hiyo wakati wa hafla fupi ya makabidhiano ya mradi huo.
Ni baadhi ya wageni kutoka Mataifa mbalimbali nje ya nchi wakicheza muziki na wananchi wa kijiji cha Kinampundu mara baada ya kukabidhiwa mradi huo wa afya ya uzazi wa mama na mtoto.
Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Ole Lenga, kushoto mwenye suti, mwakilishi wa SIMAVI, Lieke, MMkurugenzi wa shirika la HAPA, Davd Mkanje na mhasibu mkuu wa shirika hilo Noel Makyao wakifurahia pamoja na wananchi mara baada ya kukabidhi mradi huo.

Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mkoani Singida ameonya tabia ya baadhi wananchi kuezekea kwenye vyoo vyandarua vya kujikinga na mbu wa malaria.

Onyo hilo limetolewa mwishoni mwa wiki iliyopita na Mkuu huyo wa Wilaya, Edward ole Lenga wakati akizungumza na wananchi wa kijiji cha Kinampundu muda mfupi baada ya kukabidhiwa Zahanti ya kijiji na shirika la HAPA.

Alisema imezuka tabia ya wananchi kutumia vyandarua hivyo kwa matumizi yasiyo rasmi ikiwa na pamoja na wengine kuvifanya kama mabanda ya kuhifadhi vifaranga vya kuku.

“Hii ni aibu, wenzetu wanatupatia vyandarua  ili tusipate malaria, nyie mnatumia kuezeka vyoo kwa kweli hii ni aibu kubwa sana na mimi nimetembea vijijini na kujionea hili, na kwa kweli atakayekamatwa atakiona cha moto.” Alisema Dc Lenga kwa masikitiko.

Aidha alisema serikali inatumia fedha nyingi kwa ajili ya kuagizi

Monday, September 9, 2013

Shirika lisilo la kiserikali lakabidhi Zahanati na Nyumba zenye thamani ya Tsh 115.9 mkoani Singida

 Mkurugenzi wa shirika la HAPA, David Mkanje akizungumza kwenye hafla ya makabidhiano ya Zahanati na nyumba ya watumishi ya kijiji cha Kinampundu wilaya ya Mkalama. Kulia wa nne ni mkuu wa wilaya ya Mkalama na wa kwanza kushoto ni katibu tarafa Nduguti wilaya ya Mkalama, Nyalandu.
 Mkurugenzi wa shirika la HAPA,David Mkanje (kushoto) akimkabidhi mkuu wa wilaya ya Mkalama, funguo za zahanati ya kijiji cha Kinampundu. HAPA imejenga zahanati hiyo na nyumba ya watumishi kwa gharama ya zaidi ya shilingi 115.9.
 Mkuu wa wilaya ya Mkalama,Edward Ole Lenga akifungua rasmi Zahanati ya kijiji cha Kinampundu.
Mkuu wa wilaya ya Mkalama mkoa wa Singida,Edward Ole Lenga akizungumza kwenye hafla ya kukabidhiwa zahanati ya kijiji cha Kinampundu.Wa kwanza kushoto ni mkurugenzi wa shirika la HAPA lililojenga zahanati hiyo kwa zaidi ya shilingi 115.9. Siku za nyuma wakazi zaidi ya 7,000 wa kijiji hicho, walikuwa wakitembea umbali wa zaidi ya kilomita 12 kufuata huduma ya afya.
Baadhi ya wageni kutoka Uholanzi, Amerika, Uingereza na Ireland waliohudhuria hafla ya makabidhiano ya zahanati na nyumba ya watumishi wa katika kijiji cha Kinampundu wilaya ya Mkalama.
Mkuu wa wilaya ya Mkalama Edward Ole Lenga akiwa na mwakilishi wa shirika la SIMAVI la nchini Uholanzi, Ljeke muda mfupi baada ya kuzindua nyumba ya watumishi wa zahanati ya kijiji cha Kinampundu.Wa pili kulia ni mkurugenzi wa shirika la HAPA, David Mkanje.

Shirika lisilo la kiserikali la Health Action Promotion Association (HAPA) la Mkoa wa Singida limetumia zaidi ya shilingi 115.9 milioni kugharamia ujenzi wa jengo la Zahanati na nyumba ya watumishi katika kijiji cha Kinampundu wilaya ya Mkalama.

Fedha hizo, pia zimetumika kununulia kitanda cha kuzalishia,vifaa vya kuzalishia, mizani ya watu wazima, mizani ya watoto wachanga, stendi ya drip na kitoroli cha kugawia dawa.

Hayo yamesemwa mwishoni mwa juma na Mkurugenzi wa HAPA, David Mkanje wakati akizungumza kwenye makabidhiano ya majengo hayo kwa uongozi wa wilaya ya Mkalama.

Alisema ujenzi wa jengo la zahanati pamoja na vyoo vyake, HAPA imetumia shilingi