Saturday, November 30, 2013

MWENYEKITI WA KIJIJI MBARONO KWA KUCHOMA MOTO NYUMBA MBILI (2).

Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Singida, ACP. Geofrey Kamwela akitoa taarifa kwa waandishi wa habari (hawapo kwenye picha) juu ya kuwashikilia wanakijiji 25 wakazi wa kijiji cha Makunda tarafa ya Kinampanda wilaya ya Iramba,kwa tuhuma ya kuchoma nyumba mbili kutokana na ugomvi wa kugombea ekari 284 za ardhi.

JESHI LA POLISI Mkoa wa Singida linawashikilia watu 25 wakazi wa kijiji cha Makunda Kata ya Kyengenge tarafa ya Kinampanda Mkoa wa Singida kwa kosa la kuchoma moto nyumba mbili kwa kile kinachodaiwa kuwa ni kutokana na ugomvi wa kugombea ekari 284 za ardhi.

Kati ya watuhumiwa hao mmoja ni Mwenyekiti wa Kijiji cha Makunda, Bw Godfrey Ayubu.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, ACP Geofrey Kamwela amesema tukio hilo limetokea Novemba 26 saa mbili asubuhi huko katika Kijiji cha Makunda.

Amesema siku ya tukio, watu wapatao 50 wakazi wa Kijiji cha Makunda wakiwa wanaongozwa na Mwenyekiti wa Kijiji Bw, Godfrey huku wakiwa wamebeba silaha za jadi walichoma moto nyumba ya Esau Talanzia (47) na kuteketeza mali yote iliyokuwemo ndani.

“Vitu vilivyoteketea kwa moto huo ni magunia sita ya mahindi, gunia mbili za alizeti, godoro moja, fedha taslimu 450,000 pamoja na mali zingine vyote vikiwa na thamani ya zaidi ya Tsh 18 milioni”,amesema Kamwela.

Amesema nyumba nyingine iliyochomwa moto na kuteketeza mali ya zaidi ya shilingi laki saba ni ya Matayo Kizaberga mali ya Matayo iliyoteketea ni gunia nne za mahindi, debe moja la dengu na fedha taslimu laki tano.

“Chanzo cha tukio hilo ni mgogoro wa mashamba ambapo wanakijiji cha Makunda wanapinga Esau na Matayo kumilikishwa ekari 284 wakati sio wazawa wa kijiji hicho”,amesema Kamanda Kamwela.

Kamwela amesema uchunguzi zaidi bado unaendelea na mara baada ya kukamilika watuhumiwa watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili.

Katika tukio jingine, Kamwela amesema mjasiriamali mkazi wa Mwenge mjini hapa, Richard  Williamu (33) Novemba 26 mwaka huu saa 1.45 jioni alipigwa risasi tumboni na paja la kulia na watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi.

“Watu watatu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi walifika kwenye duka la Richard na kuomba wauze vocha na walipoambiwa kuwa dukani hapo hakuna vocha walichomoa bunduki inayodhaniwa ni SMG na

Wachimbaji wadogo wa madini watakiwa kuwa na nidhamu ya matumizi fedha.

Rais wa shirikisho la wachimbaji madini Tanzania (FEMATA), John Bina akifungua kikao cha kwanza cha kamati ya dhahabu ya FEMATA Taifa, kilichofanyikia mjini Singida.Wa kwanza kulia na mwenyekiti wa FEMATA Ahmed Adamu na kushoto ni Golden Hainga, katibu wa FEMATA.
Katibu wa chama cha wachimbaji madini mkoa wa Singida,Farijala Kiunsi akitoa taarifa yake ya utekelezaji katika kikao cha FEMATA.
Baadhi wa wajumbe wa mkutano wa FEMATA wakifuatilia kwa makini mada zilizokuwa zikitolewa kwenye kikao cha wachimbaji Dhahabu mkoani Singida.
Rais wa FEMATA Taifa, John Bina (wa pili kulia walioketi) akiwa kwenye picha ya pomoja na viongozi wa kitaifa wa FEMATA taifa waliohudhuria kikao mjini Singida.Wa kwanza kulia ni mwenyekiti wa FEMATA, Ahmed Adamu na kushoto ni katibu wa FEMATA,Golden Hainga.

RAIS wa Shirikisho la wachimbaji madini Tanzania (FEMATA), John Bina, amewataka wachimbaji madini kujenga utamaduni wa kuwa na nidhamu ya matumizi ya fedha ili fedha wanazozipata ziweze kuwaletea maendeleo endelevu.

 Bina amesema hayo wakati akifungua kikao cha kamati ya dhahabu ya FEMATA taifa, kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa ofisi ya madini kanda ya kati mjini hapa.

 Amesema wachimbaji madini wamekuwa na sifa mbaya kwa madai kwamba, wengi hutumia fedha vibaya na kupelekea shughuli ya madini kutokuwanufaisha kimaisha.

 Bina amesema matumizi  hayo mabaya ya fedha, yana madhara mengi ikiwemo mhusika kufilisika mapema.

 “Uzoefu unaonyesha kwamba mchimbaji akipata kwa mfano shilingi milioni 10,kipaumbele chake kinakuwa ni  kuoga mwili kwa  pombe (bia), ataacha kuchimba madini na kutumbukia kwenye anasa hadi hapo fedha zitakapomwishia”,alifafanua Rais huyo.

 Kwa hali hiyo,Bina aliwataka wabadilike na kuwa na nidhamu nzuri ya matumizi ya fedha, ili fedha wanazozipata ziwasaidie kujiletea maendeleo wao binafsi,familia zao,mkoa wao na taifa kwa ujumla.

 Katika hatua nyingine, Rais Bina aliwataka wachimbaji madini kujiepusha na uchimbaji haramu na pia wajenge utamaduni wa

Friday, November 29, 2013

WANANCHI ZAIDI YA 1,000 SINGIDA WACHOMEWA NYUMBA ZAO MOTO.

Baadhi ya wananchi wakiwa wamehamishia makazi yao chini ya mti uliopo kwenye korongo kijiji cha Handa mpakani mwa Wilaya ya Chemba na Singida Vijijini mara baada ya nyumba zao kuchomwa moto na askari polisi na wale wa kikosi cha kupambana na ujangili kwa madai ya kuvamia hifadhi ya msitu wa mgori 
Huyu ni mmoja wa watoto walionashwa na kamera yetu akiwa amelala hoi kwa kukosa chakula na huduma zingine, baada ya nyumba zao kuchomwa moto wakati wa operesheni ya kuwahamisha katika kitongoji cha Kazamoyo kwa madai ya kuvamia hifadhi, hata hivyo wananchi hao wameisha katika eneo hilo kwa zaidi ya miaka nane toka mwaka 2005 , lakini sheria ya kuingiza eneo hilo kwenye msitu wa hifadhi ya mgori ilifanyika mwaka 2007.

KITUO cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) wametakiwa kufika katika kitongoji cha Kazamoyo kijiji cha Nguamuhanga tarafa ya Mgori Wilayani Singida vijijini na kujionea unyanyasaji dhidi ya wananchi wakati wa zoezi la kuwaondoa katika hifadhi ya msitu wa mgori.

Hayo yamesemwa juzi katika kitongoji hicho na baadhi ya wananchi walioamua kuhamia kwenye korongo na kuishi chini ya miti kama digidigi kunusuru maisha yao kutokana na vipigo kutoka kwa wa kikosi cha kupambana na ujangili Wilaya ya Singida na askari polisi.

Wamesema ni vyema kituo hicho wakafika mapema ili kuona jinsi ambavyo binadamu wanavyoishi maisha ya shida na taabu kwenye eneo hilo kufuatia amri ya mkuu wa Wilaya ya kuhamishwa kwa muda mfupi.

Wamesema eneo hilo wameishi zaidi ya miaka nane na kujenga makazi bora bila matatizo yoyote, lakini jambo la ajabu ni baada ya Wilaya ya Chemba na Singida kuwekeana mipaka na kuonekana kuwa wako Singida.

“Wakati tuko kijiji cha Handa Wilaya ya Chemba, tuliishi bila matatizo lakini baada ya kuhamia singida ndipo mambo yalianza kubadilika na kuambiwa kuwa tuko eneo la hifadhi, hii ni ajabu sana , Wilaya moja tuliishi vizuri hii nyingine haitutaki sasa tuende wapi.” Alihoji mmoja wa kina mama.

Licha ya kukosa huduma muhimu kama vile maji, mahema, vyoo baadhi ya kina mama na watoto walionekana wakiwa katika huzuni kubwa huku wengine wakiangua vilio baada ya kuwaona waandishi wa habari wakidhani kuwa ni

Monday, November 25, 2013

Singida na mkakati wa kuibuka kiriadha.



                             Picha zote kutoka maktaba ya Singida Yetu Blog

SINGIDA ni moja kati ya mikoa ambayo ilikuwa inafanya vizuri katika mchezo wa riadha miaka ya 1980 na kutoa wanariadha mahiri ambao waliiwakilisha Tanzania katika mashindano mbalimbali ya kimataifa.
Mkoa huo ni wenye mandhari nzuri yenye mawe mawe pamoja na mto upande wa kushoto na kulia hususan pale unapofika mkoani hapo.
Hakika mkoa huu ni wenye vitu vingi, lakini kikubwa zaidi ni wakimbiaji wa riadha hususan maeneo ya Singida Vijijini ambako kama wakimbiaji hao wataweza kupewa vifaa maalumu kwa ajili ya kukimbia na wadau wa riadha wakajitokeza na kuchangia zaidi katika riadha, Tanzania itakuwa na medali nyingi na kupata heshima katika nchi mbalimbali duniani.
Nasema hivyo kwa sababu hivi karibuni Mbunge wa Singida Vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu aliandaa mashindano ya riadha hususan vijijini kwa ajili ya kuibua vipaji kwa kushirikiana na Mkurugenzi wa Shrika la African Wildlife Trust (AWT), Pratic Patel.

Mbio hizo zilizojulikana kwa jina la Singida Marathon za kilometa 21, zilianza rasmi Novemba 9, mwaka huu kwa kushirikisha wakimbiaji zaidi ya 400 kutoka Singida Mjini na Singida Vijijini na zilianzia Kijiji cha Mitula, Kata ya Kinyagigi na kuishia Viwanja vya Shule ya Msingu Ntunduu (W) Singida Vijijini.
Mbio hizo zilikuwa za kilometa 21 ambazo ni nusu marathoni na kilometa 5 na mwisho kabisa ni kilometa 2.5 ambazo ziliwashirikisha watoto wa kiume na wa kike. Wakimbiaji walikuwa wamejiandaa wenyewe na walijiandikisha, lakini baadhi yao pamoja na kukabiliwa na ukosefu wa viatu, lakini waliweza kumudu hali hiyo kutokana na mazingira waliyokua nayo na kuonesha vipaji vyao vilivyowashangaza wengi.

Inawezekana kukimbia bila viatu ni jambo lisiloruhusiwa, lakini kutokana na mazingira yenyewe ya vijijini hali hiyo haikuwa kikwazo kwa wakimbiaji hao kukimbia bila viatu ila walionesha kuwa wana moyo na nia ya dhati kuonesha vipaji vyao hakika ilikuwa faraja kubwa kwao kwani mwisho wa siku waliweza kuibuka washindi na wengine wakapata kifuta jasho.

Washindi hao ni Paulo Itambi ambaye aliibuka mshindi wa kwanza kwa upande wa wanaume ambaye alipewa zawadi ya Sh 300,000, Emmanuel Samson wa pili (Sh 200,000) na Samwel Ikungi wa tatu (Sh 100,000). Kwa upande wa wanawake, mshindi wa kwanza Fabiola William (Sh 300,000), Zakia Abdallah (Sh 200,000) na Winfrida Hassani (Sh 100,000).
Mbio za kilometa tano, washindi ni Gabriel Garado (Sh 200,000), Deo Lazaro (Sh 100,000) na Jonas John (Sh 50,000) huku wanawake ni Neema Kisuda (Sh 200,000), Pascalina Silvesta (Sh 100,000) na Christina Yuda (Sh 50,000) ambao washindi wa kilometa 2.5 wakiwa ni Julita Antony (Sh 100,000), Editha Gabriel (Sh 50,000) na Magreth Bernado (Sh 25,000).
Wanaume walikuwa ni Petro Pascal mshindi wa kwanza na kupewa Sh 100,000, Baraka Sebastian (Sh 50,000), Haji Swalehe (Sh 25,000) huku washindi wengine 400 kila mmoja akipewa Sh 10,000. Baada ya washindi hao kukabidhiwa zawadi zao, Patel ambaye alikuwa mgeni rasmi kwa niaba ya Naibu Waziri Nyalandu, alikabidhi pia medali mbalimbali kwa washindi hao.

Aidha, alitoa changamoto kwa

Friday, November 22, 2013

WAHAMASISHWA KUTUMIA VYOO BORA ILI KUZUIA MAGONJWA YA MILIPUKO.



BAADHI YA VYOO BORA MKOANI SINGIDA.
Kata ya Mtamaa Manispaa ya Singida inakabiliwa na tatizo la ukosefu wa vyoo bora hali inayoweza kusababisha kutokea kwa magonjwa ya miripuko ikiwemo kipindupindu.

Uchunguzi uliofanywa na Singida Yetu Blog katani hapo umebaini kuwa kati ya kaya tano hadi kumi ni kaya moja tu ndiyo yenye choo bora huku kaya nyingine zikiwa zinatumia vyoo visivyo bora na nyingine kutumia vyoo vya majirani au vya taasisi za elimu kama vile shule.

Baadhi ya wakazi walihojiwa na standard radio wamesema kukosekana kwa vyoo bora kumesababishwa na kukosekana kwa elimu huku wengine wakisema vyoo vingi vilibomolewa na mvua zilizonyesha mwanzoni mwa mwaka huu

Akizungumzia tatizo hilo Diwani wa kata hiyo Bw. Gwae Mbua amesema kuwa kwa kuanza wameanza kuweka msisitizo katika shule kuwa na vyoo bora na baada ya kukamilika mpango huo utahamia katika

KATA YA MTAMAA MANISPAA YA SINGIDA YAPATA NEEMA YA UMEME.


Mjumbe wa halmashauri kuu ya taifa CCM Bw. Hassan Mazala (Picha Kutoka Maktaba Yetu)

Kata ya mtamaa manispaa ya Singida inatarajiwa kuunganishiwa nishati ya umeme wa grid wa taifa kupitia mradi wa umeme vijijini REA ili kukabiliana na umasikini wa kipato kwa wananchi wa kata hiyo.

Mjumbe wa halmashauri kuu ya taifa CCM Bw. Hassan Mazala wakati akizungumza na wananchama wa CCM katika kata hiyo ambapo amesema upembuzi yakinifu juu ya mradi huo unatarajiwa kuanza mwezi huu.


Amesema kuwa endapo umeme ukiunganishwa katika kata hiyo kutasaidia wananchi kujishughulisha na shughuli za kiuchumi ambazo zinategemea nishati hiyo na hatimaye kuondokana na umasikini wa kipato unaowakabili wakazi wa kata hiyo


Aidha Bw Mazala ametoa wito kwa wananchi wa kata hiyo kuwa tayari kuonyesha nia ya kuhitaji huduma hiyo kwa kujiandikisha hali ambayo itaongeza juhudi za mradi huo wa REA kwenda kasi kutokana na mahitaji ya

Wednesday, November 20, 2013

Chuo Cha Utumishi wa Umma kuongeza matawi zaidi.

Mtendaji mkuu wa chuo cha utumishi wa umma Tanzania, Said Nassor kitoa taarifa yake kwenye mahafali ya 16 ya chuo hicho yaliyofanyika mjini Singida. Jumla ya wahitimu 1,909 kutoka chuo cha Tabora na Singida walihitimu katika ngazi mbalimbali.
Mkuu wa mkoa wa Singida,Dk.Parseko Kone akitoa nasaha zake kwenye mahafali ya 16 ya chuo cha utumishi wa umma Tanzania yaliyofanyika mjini Singida.Kulia aliyekaa,ni Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais Menenjimenti ya Utumishi wa Umma Tanzania, Mh.Celina Kombani ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mahafali hayo.
Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma Tanzania,Celina Kombani akizungumza kwenye mahafali ya 16 ya chuo cha Utumishi wa Umma Tannzania mjini Singida.
Baadhi ya wahitimu wa chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania,waliohitimu mafunzo yao.

WAHITIMU wa Chuo Cha Utumishi wa Umma Tanzania wameagizwa kutumia elimu walioipata kufanya kazi kwa ufanisi ili kuleta tija kwa lengo la kukuza na kuendeleza uchumi wa nchi.

 Agizo hilo limetolewa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Tanzania, Celina Kombani, wakati akizungumza kwenye sherehe ya mahafali ya 16 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, mjini hapa.

 Aliwaasa kuwa wawe watendaji wazuri mara watakapoanza kazi,na hiyo iende sambamba na kuzingatia kanuni , sheria na taratibu za utumishi wa umma.

 “Tekelezeni majukumu yenu kwa ufanisi kwa kuonyesha uwezo wa kumudu majukumu,uadilifu  na kutoa huduma bora kwa wananchi na sio kufanya kazi kwa mazoea, ili kukamilisha lengo la serikali la kupata matokeo makubwa sasa” amesema Kombani

 Awali Mtendaji Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania Said Nassor, amesema wana mkakati wa kupanua vyuo vyake ambapo mwakani wanaanzisha tawi jipya mkoani mbeya.

 Aidha, amesema pia mwakani wanatarajia kuongeza madasa katika tawi la tabora na wataanza ujenzi wa Tawi la chuo cha mkoa wa singida.

 “kwa ujenzi wa tawi la mkoa wa singida, tayari tumekamilisha zoezi la la kulipa fidia kiasi cha shilingi

SEMA yagharamia ujenzi wa Vyoo kwa Tsh 155m shule tano za Manispaa ya Singida.

Meneja wa shrika la SEMA, Ivo Manyanku,(wa kwanza kulia) akitoa taarifa yake ya ujenzi wa vyoo bora katika shule tano za msingi manispaa ya Singida kwa Naibu Waziri TAMISEMI (Elimu), Mh. Kassim Majaliwa (mwenye miwani).Vyoo hivyo vimegharimu zaidi ya shilingi 155 milioni.
Naibu Waziri TAMISEMI (Elimu) Mh. Kassim Majaliwa (aliyeipa kisongo kamera) akizindua rasmi ujenzi wa vyoo bora katika shule ya msingi Unyankindi.Vyoo hivyo bora vimejengwa kwa gharama ya shilingi 155 milioni na shirika la SEMA.Kushoto ni meneja wa SEMA. Ivo Manyanku.
Naibu Waziri wa TAMISEMI (Elimu),Kassim Majaliwa akikata utepe kuashiria ufunguzi wa matumizi ya vyoo bora vya shule ya msingi Unyankindi mjini Singida.Vyoo hivyo vimejengwa na shirika la SEMA kwa gharama ya shilingi 155 milioni.
Moja ya vyoo bora vya shule ya msingi Unyankindi manispaa ya Singida vilivyojengwa na shirika la SEMA la mkoa wa Singida.

Shirika lisilo la kiserikali la Sustainable Environment Management Action (SEMA) la mkoani Singida limetumia zaidi ya shilingi 155 milioni kugharamia ujenzi wa vyoo bora katika shule tano za manispaa ya Singida.

 Shule zilizonufaika na mradi huo ni,Unyankindi,Singidani,Manguamitogho,Mtamaa na Mtisi.

 Hayo yamesemwa juzi na Meneja wa SEMA, Ivo Manyanku wakati akizungumza kwenye hafla iliyofana ya uzinduzi wa vyoo hivyo uliofanyika katika shule ya msingi Unyankindi Singida mjini.

 Amesema fedha hizo zilizotumika katika ujenzi huo zimetolewa ufadhili na shirika la WaterAid Tanzania kwa ajili ya kutekeleza mradi wa maji na usafi shuleni katika halmashauri ya manispaa ya Singida.

 “Vyoo hivi vina matundu 48 ambayo yana uwezo wa kuhudumia wanafunzi 2,903 kati yao wavulana ni 1,446 na wasichana ni 1,457.Idadi hiyo inajumuisha na walemavu 38 ambao 25 ni wavulana na 13 ni wasichana”,amesema Meneja huyo.

 Kwa upande wake mgeni rasmi katika uzinduzi huo,naibu waziri TAMISEMI (elimu),Kassimu Majaliwa,alitumia fursa hiyo kulipongeza shirika la SEMA kwa ujezi bora wa vyoo hivyo ambavyo vimekidhi vigezo vyote vinavyohitajika.

 Amesema serikali na wadau wengine wa maendeleo hawana budi kuliunga mkono shirika la SEMA kwa madai linatelekeza miradi yake kulingana na thamani ya fedha zilizotumika.

 “SEMA binafsi nawapongezeni sana ujenzi huu mtakuwa mmeisaidia serikali katika kupunguza

Tuesday, November 19, 2013

Waislamu Singia wamuenzi mjukuu wa Mtume Al – Imamul – Hussein (A.S)




Baadhi ya waumini wa Dhehebu la Shia mkoani Singida wakiwa kwenye matembezi ya kuadhimisha kumbukumbu za kifo cha mjukuu wa Mtume Al-Imamul Hussein (AS).

Mbaroni kwa kuvujisha mtihani wa kidato cha nne.

           Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Singida, ACP Geofrey Kamwela.

JESHI la polisi mkoa wa Singida, linawashikilia walimu wawili kwa tuhuma ya kuvunjisha matihani wa kidato cha nne unaoendelea kufanyika hivi sasa nchini kote.

Walimu hao ni walimu wa shule ya sekondari kata ya Nkinto wilaya ya Mkalama mkoani Singida, ambao ni mwalimu mkuu wa shule hiyo Monica Sebastian (30) na mwalimu Agaloslo Otieno (32).

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Singida, ACP Geofrey Kamwela, amesema kuwa tukio hilo limetokea novemba 13 mwaka huu kati ya saa tatu na tatu usiku katika shule ya sekondari ya Nkinto kata ya Mwangeza tarafa ya Kirumi wilaya ya Mkalama.

Amesema kuwa mwalimu Agaloslo akiwa anasimamia mtihani katika shule ya sekondari ya Mwangeza, alikuwa anaandika baadhi ya maswali ya masomo ya Kiswahili na Civics  kwenye simu yake ya kingajani na kumtumia mwalimu wake mkuu Monica akiwa shuleni kwake Nkinto.

Kamwela alisema baada ya Monica kupata maswali hayo,alikuwa anayatafutia majibu akiwa chooni na wanafunzi walikuwa wanamfuata huko huko chooni kupewa majibu hayo.

“Lengo lao ilikuwa ni kuwasaidia wanafunzi ili waweze kufanya vizuri katika mtihani wao wa kidato cha nne mwaka huu.Wanafunzi wenywe waliisha ambiwa kuwa wawe wanadanganya kwamba wanaenda kujisadia chooni,ili wakapatiwe majibu na mwalimu mkuu”,alifafanua kamanda na kuongeza;

“Uchunguzi wa awali wa polisi unaonyesha kuwa uvunjishaji huo ulifanyika kwa nyakati tofauti kati ya mwalimu mkuu Monica na mwalimu wake Agaloslo akiwa ana simamia mtihani huo katika shule nyingi.Baada ya mwali mkuu kutumiwa maswali alikuwa anajificha ndani ya choo cha shule yake na watahiniwa kwa nyakati tofauti huomba ruhusa kwa wasimamizi kwenda chooni kwa nia ya kujisaidia na hapo humkuta mwalimu mkuu huyo na kuwapa maelekezo ya namna ya kujibu maswali hayo”.

Amesema baada ya Polisi kupata taarifa ya siri kutoka kwa wasamaria wema, waliweka mtego katika shule ya sekondari ya Nkinto na kufanikiwa kumkamata mwalimu

Monday, November 18, 2013

Wachimbaji wadogo wa madini watakiwa kulipa kodi bila shuruti.

Kamishina msaidizi Madini kanda ya Kati, Manase Mbasha akizungumza kwenye ufunguzi wa mafunzo ya siku tano ya uchimbaji bora wa Madini yanayohudhuriwa na wachimbaji wadogo 35 kutoka mikoa 15 nchini.Mafunzo hayo yanafanyikia kwenye ukumbi wa mikutano wa kanisa katoliki mjini Singida. Kulia ni afisa mwandamizi wa ofisi ya madini mkoa wa Singida, Gabriely Senge na kushoto ni mkufunzi wa mafiunzo hayo,Dk.Eng.Crispin Kinabo kutoka chuo kikuu cha Dar-es-salaam.

Baadhi ya wachimbaji wadogo wakifuatilia kwa makini mada zilizokuwa zikitolewa za mafunzo ya uchimbaji bora wa Dhahabu.

Wachimbaji wadogo wa madini nchini,wametakiwa kujenga utamaduni wa kulipa kodi bila kushurutishwa,ili kuisaidia serikali kuwa na uwezo wa kutoa huduma bora zinazokidhi mahitaji ya wananchi.

 Wito huo umetolewa na Kamishina Msaidizi Madini Kanda ya Kati,Manase Mbasha,wakati akizungumza kwenye hafla ya ufunguzi wa mafunzo ya siku tano ya uchimbaji bora wa dhahabu yanatoendelea kwenye ukumbi wa mikutano wa kanisa katoliki mjini hapa.

 Amesema lengo la serikali ni kuhakikisha wachimbaji wadogo wa madini,wanakuwa walipaji wazuri wa kodi kwa mujibu wa sheria zilizowekwa za sekta ya madini.

 “Mchimbaji mdogo ukiwa mlipa kodi mzuri,kwanza utajijengea heshima mbele ya macho ya jamii,na kikubwa zaidi ni kwamba utakuwa umeisaidia serikali kuwa na uwezo mzuri wa kuhudumia wananchi wake”alifafanua Mbasha.

 Aidha,kamishina huyo msaidizi,ametumia fursa hiyo kuwahimiza wachimbaji wadogo kushiriki kikamilifu shindano la tuzo ya rais ya mazingira.

 Mbasha amesema endapo wachimbaji wadogo na wale wa ngazi mbalimbali watashiriki kikamilifu katika shindano la tuzo ya rais ya mazingira, kitendo hicho kitasaidia mno kuboresha mazingira.

 Kwa mujibu wa Mkufunzi wa Mafunzo hayo,Dk.Eng.Crispin Kinabo kutoka chuo kikuu cha Dar-es-salaam kitengo cha Jiolojia,baadhi ya mada za mafunzo hayo,ni

Bima ya Afya yaanda kongamano kwa wadau wake Singida.

Meneja mfuko wa Taifa Bima ya Afya (NHIF) mkoa wa Singida, Agnes Chaki (wa kwanza kushoto) akitoa taarifa kwa mwandishi wa habari wa MOblog (hayupo kwenye picha) juu ya kufanyika kwa kongamano la wadau 250 wa Mfuko wa Taifa Bima ya afya (NHIF) Mfuko wa Afya ya jamii (CHF)linalotarajiwa kufanyika kesho (13/11/2013) kwenye ukumbi wa mikutano wa hotel ya Katala Beach mjini Singida.Wa kwanza kulia ni mhasibu wa NHIF,Godlessen Bellium (mhasibu) na katikati ni Isaya Shekifu (Afisa matekelezo na uratibu NHIF mkoa wa Singida.
Jengo la ofisi ya Mfuko wa Taifa Bima ya Afya (NHIF) mkoani Singida.

MFUKO wa Taifa Bima ya Afya (NHIF) kwa ushirikiano na mfuko wa afya ya jamii (CHF) mkoani Singida,unatarajia kufanya kongamano kubwa la wadau wake kesho (leo 13/11/2013) asubuhi kwenye ukumbi wa mikutano wa hotel ya kitalii ya Katala Beach (KBH) iliyopo mjini hapa.

Akizungumza na MO blog ofisini kwake leo,meneja wa NHIF mkoa wa Singida,Agnes Chaki,alisema kongamano hilo litakalofunguliwa na mkuu wa mkoa wa Singida, Dk.Parseko Vicent Kone, litaanza mapema saa mbili asubuhi.

Alisema kuwa kongamano hilo la aina yake la kwanza kufanyika mkoani hapa, linatarajiwa kuhudhuriwa na wadau 250.

Chaki alitaja baadhi ya wadau hao kuwa ni pamoja na katibu tawala mkoa,wakuu wa wilaya,wakurugenzi wa halmashauri na manispaa,wabunge wote,waheshimiwa madiwani na waganga wakuu wa wilaya.

“Wengine ni wakuu wa vyombo vya usalama,viongozi wa dini,waratibu wa bima za afya wa halmashauri (NHIF na CHF,wawakilishi wa  wanachama wa mfuko,waajiri walioandikishwa na mfuko,watoa huduma na waandishi wa habari”,alisema meneja Chaki.

Alisema kuwa dhumuni la kongamano hilo,ni kutoa fursa kwa wadau wa

Thursday, November 14, 2013

Wanachama 51 wa Chadema wahamia CCM kata ya Mungaa, Singida.

Wanakikundi cha uhamasishaji cha kata ya Mungaa jimbo la Singida mashariki, wakitoa burudani kwenye hafla ya uzinduzi wa shina la wakereketwa wa CCM la Mzambarauni katika kijiji cha Makiungu.

Mjumbe wa Mkutano Mkuu  CCM (NEC) taifa wilaya ya Ikungi mkoani Singida, Jonathani Njau ameivunja ngome ya CHADEMA kata ya Mungaa, baada ya wanachama wake 51 kukihama na kurejea CCM.

 Wanachama hao ambao karibu wote ni vijana, katika risala yao wamedai wamehama CHADEMA, baada ya kubaini kuwa wanatumiwa vibaya na wanasiasa wa chama hicho.

 Wamedai kwamba wanasiasa wa CHADEMA wamejaa uchu wa madaraka, wanatumia uongo mkubwa, hila, kupandikiza chuki na wanatoa ahadi  za uongo katika kupata uongozi.

 “Kabla na baada ya uchaguzi, tuliahidiwa ahadi nyingi na viongozi wa CHADEMA kumbe ahadi zote hizo ni ahadi hewa.Vijana tumekwisha kuwagundua na hatudanganyiki tena.Kwa sababu sisi ni nguvu kazi ya taifa,tunatakiwa kutumika kwa maslahi ya taifa na si kwa maslahi ya mtu binafsi”,inasema sehemu ya risala yao.

 Katika hatua nyingine,vijana hao walishangiliwa kwa nguvu na umati uliohudhuria mkutano huo wa hadahara,wakati wakiimba wimbo maalum ambao ulidai kwamba CHADEMA ni sawa na kitanda cha kamba kilichojaa kunguni na hivyo,hakilaliki.

 Akizungumza muda mfupi baada ya kuzindua shina la wakereketwa  la Mzambarauni  waliorejea CCM, Mnec  Njau amesema mlango wa CCM upo

Wajasiriamali wahimizwa kujitangaza kupitia vyombo vya habari.

Mkuu wa wilaya ya Singida,Queen Mlozi akizungumza kwenye hafla ya ufungaji wa mafunzo ya ufugaji bora nyuki iliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa SIDO mjini Singida.Kulia ni meneja wa SIDO mkoa wa Singida, Shoma Kibende.
Meneja wa SIDO mkoa wa Singida,Shoma Kibende akitoa taarifa yake kwenye hafla ya ufungaji mafunzo ya ufugaji nyuki iliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa SIDO mjini Singida.Wa pili kulia (aliyeketi) ni mkuu wa wilaya ya Singida,Queen Mlozi.
Mkuu wa wilaya ya Singida,Queen Mlozi akimkabidhi mfugaji wa nyuki cheti cha kumaliza mafunzo ya ufugaji bora nyuki yaliyomalizika mwishoni mwa wiki mjini Singida.
Mkuu wa wilaya ya Singida,Queen Mlozi,(aliyeketi katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na wafugaji Nyuki waliohitimu mafunzo ya ufugaji bora wa Nyuki.Wa kwanza kushoto (walioketi) ni meneja wa SIDO mkoa wa Singida,Shoma Kibende na kulia ni mwenyekiti wa wafugaji Nyuki.

Serikali wilayani Singida, imewahimiza wajasiriamali na wafanyabiashara kujenga utamaduni wa kutangaza bidhaa zao kwenye vyombo vya habari ili pamoja na mambo mengine, waweze kujipatia soko la uhakika.

Wito huo umetolewa mwishoni mwa wiki na Mkuu wa Wilaya hiyo Queen Mlozi,wakati akizungumza kwenye hafla ya ufungaji mafunzo ya ufugaji bora wa nyuki na uchakataji wa asali.

Akifafanua amesema ushindani mkubwa wa biashara uliopo hivi sasa,mfanyabiashara atakayefanikiwa ni yule tu ambaye atatangaza biashara yake kikamilifu.

Mlozi amesema biashara bila matangazo,ni sawa na mtu asiye na biashara kwa sababu bidhaa zake,hazitajulikana.

Amesema pamoja na kujitangaza huko,kwanza wahakikishe bidhaa zao zina kuwa na ubora unaohitajika na pia wahakikishe wanashiriki maonyesho yanayoandaliwa na SIDO kanda ya kati.

Awali meneja wa SIDO mkoa wa Singida,Shoma Kibende, amesema kuwa SIDO inao mpango wa

Wednesday, November 13, 2013

Jeshi la Polisi lamshikilia mtuhumiwa kwa kosa la kubaka Kikongwe.

Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Singida, ACP. Geofrey Kamwela akitoa taarifa kwa waandishi wa habari (hawapo kwenye picha) juu ya kijana mmoja Saidi Hamisi (34) kumbaka Kikongwe mwenye umri wa miaka 80 (jina tunalo).Inadaiwa baada ya mtuhumiwa kumaliza kumbaka kikongwe huyo, alilala fo fofo kutokana na kulewa kupindukia hadi alipokuja kukamatwa akiwa amelala kwenye kitanda cha Kikongwe akiwa hajitambui.

JESHI la Polisi Mkoa wa Singida linamshikilia mkulima mkazi wa kijiji cha Wibia tarafa ya Mungaa wilaya ya Ikungi Saidi Hamisi (34) kwa tuhuma ya kumbaka bibi kizee mwenye umri wa miaka 80 na kumsababishia maumivu makali katika sehemu zake za siri.

Akizungumza na waandishi wa habari jana ofisini kwake, kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Singida, ACP Geofrey Kamwela, alisema tukio hilo la aibu na kusikitisha limetokea Novemba Sita mwaka huu huko katika kijiji cha Matongo kata na wilaya ya Ikungi.

Akifafanua, alisema siku ya tukio mtuhumiwa ambaye alikuwa katika kijiji cha Matongo kuwajulia ndugu zake hali, alikunywa kiwango kikubwa cha Pombe ya kienyeji na kupelekea amfanyie kitendo hicho cha kinyama Kikongwe huyo.

“Mtuhumiwa alitumia mwanya wa nyumba za Tembe kutokuwa na mlango imara na hivyo alivuta taratibu mlango uliotengenezwa kwa fito na

Thursday, November 7, 2013

TRA Singida yazindua rasmi siku ya mlipa kodi.

Afisa elimu na huduma kwa mlipa kodi TRA mkoa wa Singida, Zakaria Gwagilo akitoa taarifa kwa waandishi wa habari (hawapo kwenye picha) juu ya maadhimisho ya saba ya siku ya mlipa kodi ambayo yamezinduliwa rasmi juzi. Zakaria alitoa taarifa hiyo kwa niaba ya kaimu meneja TRA mkoa wa Singida Alistides Paulo.

MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Singida imezindua rasmi maadhimisho ya saba ya siku ya mlipa kodi Tanzania kwa kufanya shughuli mbalimbali ikiwemo ya kutoa misaada kwa makundi yenye mahitaji maalumu.

Hayo yamesemwa na Kaimu Meneja wa TRA Mkoa wa Singida, Alistides Paulo wakati akitoa taarifa yake kwa waandishi wa habari kuhusu maadhimisho ya saba ya siku ya mlipa kodi Tanzania kwa Mkoa wa Singida.

Katika taarifa yake hiyo iliyosomwa kwa niaba yake na Afisa Elimu na huduma kwa mlipa kodi Zakaria Gwagilo alitaja baadhi ya shughuli zitakazofanyika katika maadhimisho hayo kuwa ni pamoja na kutoa misaada kwenye wodi ya wazazi katika hospitali ya wilaya ya Manyoni.

Paulo alitaja shughuli zingine kuwa watafanya semina kwa makundi mbalimbali ya walipa kodi na pia kuwatembelea walipa kodi kwenye vituo vya biashara na kuzungumza nao kuweza kufahamu matatizo yao.

“Katika kilele cha siku ya mlipa kodi Novemba nane mwaka huu baadhi ya walipa kodi watazawadiwa vyeti kutokana na

Tuesday, November 5, 2013

Halmashauri ya Ikungi Singida yakusanya Tsh 154.9m ndani ya miezi mitatu.

Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Ikungi,Protace Magayane akifafanua jambo mbele ya kikao cha kawaida cha madiwani.Katikati ni mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Seelestin Yunde na wa kwanza kulia ni mwenyekiti CCM wilaya ya Ikungi, Hassan Tati.
Baadhi ya watendaji wa halmashauri ya wilaya ya Ikungi,wakifuatilia kwa makini ajenga zilizokuwa zikizungumzwa kwenye kikao cha kawaida cha baraza la Madini.
Diwani wa viti maalum Perpetua Nkuwi,akichangia ajenda iliyowasilishwa kwenye kikao cha kawaida cha baraza la madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Ikungi.
Mbunge (CHADEMA) wa jimbo la Singida mashariki,Tundu Lissu akichangia ajenda zilizokuwa zikiwasilishwa kwenye kikao cha kawaida cha baraza la madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Ikungi.
Mbunge (CCM) wa jimbo la Singida magharibi, Mohammed Missanga akizungumza kwenye kikao cha kawaida cha baraza la madiwani wa halmashauri ya wilaya Ikungi.

Halmashauri  ya Wilaya ya Ikungi Mkoa wa Singida imekusanya mapato ya zaidi ya shilingi 154.9m kutoka vyanzo vyake mbalimbali vya mapato kwa kipindi cha miezi mitatu ya Julai hadi Septemba mwaka huu.

Hayo yamesemwa na Mweka Hazina wa Halmashauri hiyo Celestine Muttashobya wakati akitoa taarifa yake mbele ya kikao cha madiwani wa halmashauri hiyo kilichofanyika mjini Singida.

Amesema makusanyo hayo ni sawa na asilimia moja ya lengo la kukusanya mapato ya zaidi ya shilingi 16.9 bilioni kwa kipindi cha mwaka wa fedha wa 2013/2014.

Akifafanua, Muttashobya amesema kati ya fedha hizo mapato ya ndani ya halmashauri yenyewe wamekusanya shilingi 57,757,484/m

“Serikali kuu imetupa ruzuku ya shilingi 30 milioni kufidia kodi na ushuru uliofutwa Pia serikali kuu imetupatia ruzuku ya zaidi ya shilingi 53 milioni kwa ajili ya matumizi yasiyo ya mishahara na zingine zaidi ya shilingi 14.1m  kwa ajili ya kugharamia miradi mbalimbali ya maendeleo ya wananchi”,amesema.

Mweka Hazina huyo amesema katika kipindi hicho cha miezi mitatu wametumia shilingi 59,853,962.26m sawa na asilimia tatu ya lengo la kutumia shilingi 16,106,933,419/m.

Katika hatua nyingine Muttashobya alitaja kata tatu za jimbo la Singida mashariki zilizofanya vizuri katika ukusanyaji wa mapato na asilimia iliyokusanywa kwenye mabano kuwa ni

Monday, November 4, 2013

Vifaa vya kufundishia wanafunzi wenye Ulemavu ni changamoto shule ya msingi Ikungi.


Wanafunzi wenye Ulemavu wa shule ya msingi Ikungi mchanganyiko wilaya ya Ikungi mkoa wa Singida, wakiwajibika darasani.

Shule ya Msingi Ikungi Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ya upungufu wa vifaa vya kufundishia na kujifunzia kwa wanafunzi wenye ulemavu wa kuona (upofu).

Hayo yamesemwa na Mwalimu Mkuu wa shule hiyo,Olivary Kamilly wakati akitoa taarifa yake kwenye mahafali ya 62 ya wahitimu 176 wa darasa la saba mwaka huu.

Amesema upungufu huo unaweza kuchangia wanafunzi hao wenye ulemavu wa kuona,wasifanye vizuri katika mitihani yao ukiwemo wa kumaliza elimu ya msingi.

Aidha, Kamilly alitaja baadhi ya changamoto zingine kuwa ni pamoja na ushirikiano mdogo wa wazazi wa watoto wenye ulemavu kwa kuwaficha watoto wao wenye ulemavu,ili wasipate fursa ya kupata elimu.

“Pia kuna baadhi ya wazazi wachache ambao huzua mambo ambayo huleta hali ya kutokuwa na maelewano mazuri kiasi kwamba hutumia muda mrefu kutatua mtafaruku huo,badala ya kusimamia utoaji wa taaluma”,alifafanua mwalimu mkuu huyo.

Pamoja na changamoto hizo,mwalimu Kamilly amesema wamejipanga vizuri kukabiliana na changamoto mbalimbali za kielimu na matarajio ni kushika nafasi ya kwanza kimkoa na kitaifa kwa ujumla.

“Mheshimiwa mkuu wa wilaya,tunatambua kipaumbele chako cha kutaka kuona elimu katika wilaya yako inapanda na inakuwa bora zaidi.Tunakuahidi

Sunday, November 3, 2013

Maelfu wamzika Mzee Gallawa.

Makamu mwenyekiti CCM taifa Tanzania bara, Phillipo Mangula (wa kwanza kulia) anayefuata ni waziri mkuu mstaafu Edward Lowassa,Mkuu wa mkoa wa Singida, Dk.Parseko Vicent Kone na pili kushoto ni Waziri wa Afya Dk.Hussein Mwinyi,wakiwa kwenye msiba wa mwenyekiti mstaafu CCM mkoa wa Singida, Abdallah Sumbu Gallawa.
Baadhi ya waombolezaji waliohudhuria mazishi ya mwenyekiti mstaafu CCM mkoa wa Singida, Mzee Abdallah Sumbu Gallawa katika kijiji cha Samumba kata ya Ikungi.
Makamu mwenyekiti wa CCM taifa Tanzania bara, Phillipo Mangula akizungumza kwenye mazishi ya mwenyekiti mstaafu CCM mkoa wa Singida, Mzee Abdallah Sumbu Gallawa.
Waziri wa Afya, Dk.Hussein Mwinyi akizungumza kwenye mazishi ya mwenyekiti mstaafu CCM mkoa wa Singida,Abdallah Sumbu Gallawa.Dk.Mwinyi alileta ubaini wa Rais Jakaya Mrisho Kikwete.
Mwili wa mwenyekiti mstaafu wa CCM mkoa wa Singida, Abdallah Sumbu Gallawa ukiingizwa kaburini.
Waziri wa Afya, Dk.Hussein Mwinyi akiweka mchanga ndani ya kaburi la mwenyekiti mstaafu wa CCM mkoa wa Singida,Abdallah Sumbu Gallawa aliyefariki dunia Oktoba 29 mwaka huu akipatiwa matibabu katika hospitali ya misheni ya kijiji cha Puma wilaya ya Ikungi.

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Philip Mangula amewaongoza maelfu ya wakazi wa Mkoa wa Singida na baadhi ya viongozi wa ngazi mbalimbali wakiwemo wa ngazi ya kitaifa kwenye mazishi ya Mwenyekiti Mstaafu wa CCM Mkoa wa Singida Mzee Abdallah Sumbu Gallawa (79).

Mazishi hayo yanayodaiwa kuvunja rekodi ya kuhudhuriwa na  maelfu  ya waombolezaji yalifanyika nyumbani kwa marehemu katika kijiji cha Sambaru kata ya Ikungi wilaya ya Mkoa wa Singida.

Akizungumza muda mfupi kabla ya mazishi,Mangula alitoa salamu za rambi rambi kutoka kutoka kwa mwenyekiti CCM taifa na Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania,Dk.Jakaya Mrisho Kikwete ambazo aliwatakia kila la kheri familia ya marehemu mzee Sumbu katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo.

Amesema Mwenyekiti huyo wa CCM taifa,alitamani angekuwepo kwenye mazishi hayo lakini ameshindwa kutokana na majukumu ya kikazi nje ya nchi.

Akizungumzia juu yamzee Gallawa,Mangula amesema alikuwa kiongozi bora na aliyekuwa karibu zaidi na watu na ndio maana mazishi yake yamehudhuriwa na maelfu ya wananchi.

Awali akisoma wasifu wa marehemu Gallawa,mbunge wa jimbo la Singida mashariki,Tundu Lissu amesema mzee Gallawa ni mzawa wa kwanza wa mkoa wa Singida kuchaguliwa kuwa mkuu wa wilaya na alianzia kazi hiyo wilaya ya Mbulu mkoa wa Manyara kuanzia mwaka 1962-1965.

Mwaka 1965 aligombea ubunge wa wilaya ya Singida na