Wednesday, December 18, 2013

Wilaya ya Ikungi kuvuna tani 144,826 ya mazao ya chakula.

Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Ikungi, Bw.Protace Magayaye, akitoa taarifa yake kwa waandishi wa habari (hawapo kwenye picha)  ya utekelezaji wa shughuli za kilimo msimu wa 2013/2014 ambapo wanatarajia kuvuna tani 144,826 mazao ya chakula na hivyo kuwa na ziada tani 83,090.Mahitaji ya wakazi wa wilaya hiyo 225,521,ni tani 61,736 kwa mwaka.
Afisa kilimo halmashauri ya wilaya ya Ikungi mkoa wa Singida, Ayubu Sengo.

HALMASHAURI ya Wilaya ya Ikungi mkoani Singida inatarajia kulima hekta 84,014 za mazao ya chakula msimu huu wa 2013/2014 na wanatarajia kuvuna tani 144,826.

Halmashauri hiyo ya Ikungi yenye jumla ya wakazi 225,521 ambao mahitaji yao ya chakula kwa mwaka ni tani 61,736, kwa matarajio ya mavuno ya msimu huu ya tani 144,826, halmashauri hiyo mpya itakuwa na ziada ya tani 83,090 ya mazao ya chakula.

Hayo yamesemwa hivi karibuni na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Protace Magayane wakati akitoa taarifa yake ya utekelezaji wa shughuli za kilimo msimu wa 2013/2014.

Alitaja mazao hayo na hekta zake kwenye mabano kuwa ni mtama (34,498), uwele (35,629), mounga (3,012), mhogo (1,500) na viazi vitamu (4,500).

Magayane alitaja mazao mengine ya chakula kuwa ni maharage (2,875), kunde (1,500) na njugumawe (500).

Mkurugenzi huyo amesema mafaniko hayo yatatokana na upatikanaji wa mvua yenye mtawanyiko mzuri kanuni bora za kilimo ikiwemo matumizi ya mbolea na mbegu bora.

Kwa upande wa mazao ya biashara, Magayane amesema wamejiwekea lengo la kulima hekta 22,097 na matarajio ni kuvuna tani 45,431.3.


Wakati huo huo, Mkurugenzi huyo, amesema wamesambaza

MAJAMBAZI MAWILI YAUWAWA (Samahani Kwa Picha Hizi)


WATU wawili wakazi wa manispaa ya Singida ambao majina yao bado hayajajulikana,wakiwa kwenye Jokofu la kuhifadhia maiti baada ya kuuawa wakati wa majibishano ya risasi na polisi.
Kamanda wa polisi mkoa wa Singida,SACP Geofrey Kamwela,akionyesha bunduki ya kijeshi aina ya SMG no.34555  iliyokuwa ikitumiwa na watu wawili wanaodhaniwa kuwa majamabazi katika kijiji cha Manga manispaa ya Singida.

JESHI  la Polisi mkoani Singida limewauwa watu wawili wanaodhaniwa kuwa ni majambazi wakati wa kurushiana rasasi.
Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Singida, SACP, Geofrey Kamwela amesema tukio hilo limetokea desemba tisa mwaka huu saa 12:00 jioni, huko katika kijiji cha Manga nje kidogo ya mji wa Singida.
Amesema watu watatu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi wakiwa na bunduki moja ya kijeshi aina ya SMG, walifika kijijini hapo kwa lengo la kufanya uhalifu.
Kamanda Kamwela, amesema watu hao ambao miili yao imehifadhi kwenye chumba cha mochwari katika hospitali ya mkoa, majina na makazi yao bado hayajajulikana.
Akifafanua, amesema taarifa za siri kutoka kwa raia wema zilifikia jeshi la polisi na ndipo askari polisi walipofika kwenye eneo la tukio.
“Baada ya polisi kufika kijijini hapo watu hao walistuka kuwa wanafuatilwa na askari polisi na hivyo kuanza kukimbia kuelekea kijiji cha Uhamaka kwa kutumia pikipiki yenye namba za usajili T. 634 BTW aina ya Sanlag yenye rangi nyeusi”,amesema Kamwela.
Amesema walipoona Polisi wanawakaribia waliamua kutelekeza pikipiki yao hiyo na kuanza kukimbilia porini kwa miguu.
“Hali ilipokuwa ngumu zaidi, walianza kuwarushia polisi risasi, hivyo polisi nao ikwabidi kujibu mapigo.  Katika majibizao hayo ya risasi, majambazi mawili yaliweza kujeruhiwa huku mmoja akifanikiwa kutoroka”
Amesema majambazi hayo yaliyojeruhiwa yalifariki dunia wakati yanakimbizwa katika hospitali ya mkoa kwa matibabu,lakini yakafia njiani.
Amesema katika eneo la tukio, ilipatikana

Wednesday, December 11, 2013

Unyanyapaa bado ni tatizo mkoani Singida.

Meneja mradi wa Global Fund uliopo chini ya AMREF Tanzania, Andulile Kanza, akitoa maelezo juu ya mradi wao wa uhamasiahaji wa upimaji wa afya wenye lengo la ifikapo mwaka 2015 maambukizi mpya ya Virusi vinavyosababisha UKIMWI,kiwango kifikie 0, vifo vitokanavyo na UKIMWI, 0 na unyanyampaa ufikie kiwango cha 0. Andulile alikuwa akitoa maelezo hayo  kwenye kituo kikuu cha mabasi mjini Singida.
Mkazi wa Singida mjini, akishikiriki kupima Afya yake kwenye zoezi lililokuwa likiendeshwa na shirika la AMREF lililofanyika katika kituo kikuu cha mabasi mjini Singida.
Mwanakikundi maarufu cha ‘Mtaa wa saba’ cha Majengo mjini Singida, akitoa burudani katika hafla ya zoezi la upimaji wa afya lililoendeshwa na AMREF kwenye kituo cha mabasi cha mjini Singida.
Kikundi cha sarakasi kutoka jijini Dar-es-salaam, kikitoa burudani wakati wa kampeni ya uhamasishaji upimaji wa afya iliyokuwa ikiendeshwa na shirika la AMREF katika kituo cha mabasi mjini Singida.

UNYANYAPAA na woga wa baadhi ya watu unachangia watu wengi zaidi kupima afya zao nyakati za usiku wakati wa kampeni za upimaji afya zinazofanyika nyakati hizo, imeelezwa.

 Hayo yamesemwa na Meneja Mradi wa Global Fund uliopo chini ya AMREF Tanzania, Andulile Kanza, wakati akizungumza na waandishi wa habari juu ya kauli mbiu ya ‘Getting zero’ katika masuala ya UKIMWI.

 Amesema kuwa watu wengi wamekuwa wakiogopa kupima afya zao asubuhi au mchana kwa hofu kwamba watu watawaona na hivyo wataanza kuwanyanyapaa na kuwatenga.

 “Ndio maana sisi AMREF kwenye kampeni hii ya kuhakikisha Tanzania ifikapo 2015, kiwango cha maambukizi mapya ya Ukimwi kitakuwa sifuri vifo vitokanavyo na ukimwi vitafikia sifuri  tunapima afya hadi saa tatu usiku na malengo yetu yanaenda vizuri”,alifafanua Andulile.

 Katika hatua nyingine, Maria Edward aliyepima afya yake baada ya kuhamasishwa na AMREF, ametoa wito kwamba  watu na hasa wanawake wajitokeze kwa wingi kupima afya zao ili waweze kujitambua endapo wameambukizwa au laa virusi vinavyosababisha ugonjwa wa UKIMWI.

“Natoa wito kwa wanawake wenzangu kwanza waelewe kwamba baadhi ya wanaume wetu wana mitandao ya ngono tofauti na wanawake Hivyo tunalazimika kupima afya zetu mara kwa mara ili kujua kama tumeathirika au la”,amesema.

 Amesema faida ya kutambua afya yako zipo nyingi ikiwemo endapo utagundulika una maambukizi uweze kupata ushauri nasaha utakaokuwezesha kuishi maisha marefu.


 Kwa upande wake Bakari Ramadhani, amesema kazi yake ya kusafiri sehemu nyingi hapa Tanzania , imechangia awe na  mtandao mingi ya hatari ya ngono lakini baada ya kupima na kugundulika

Tuesday, December 3, 2013

BREAKING NEWS....! MWENYEKITI WA CHADEMA MKOA WA SINGIDA KAJIUZULU.

                                                                                                                 
                                                                                                                    WILFRED NOEL KITUNDU
MWENYEKITI CHADEMA MKOA SINGIDA
S.L.P 260
3.12.2013
KATIBU WA CHADEMA MKOA
S.L.P 260
SINGIDA
YAH: - KUJIUZURU UENYEKITI MKOA SINGIDA
Somo hapo lahusika,
Ninapenda kukuarifu kuwa nimeamua kujiuuzuru nafasi yangu ya uenyekiti wa mkoa ambayo nimekuwa nikiitumikia kwa kipindi kirefu sasa kama kielelezo cha kuamini na kudai demokrasia ya kweli ndani ya chama.

Ikumbukwe kwamba mimi ndio mwanachama wa kwanza kujiunga na CHADEMA mkoa wa SINGIDA na ni mwanachama wa 300 kitaifa, hiyo ni heshima kubwa sana kwangu na sipo tayari kuipoteza kwa kukubali kuwa sehemu ya udharirishaji huu wa demokrasia uliopitiliza

Maamuzi na vitendo vinavyoendelea ndani ya chama chetu kwa sasa ni ubakaji na udharirishaji wa demokrasia ya kweli tunayoihubiri mbele ya umma.

Kwa barua hii basi, nimeonelea bora upate ufahamu huo kuwa si vema mimi kuendelea kupingana na dhamira yangu inayonituma kuwa mwanademokrasia wa kweli.

Kwa kipindi hiki kifupi mnaweza mkaendelea kuitumia anuani yangu ya posta mpaka hapo mtakapopata anuani yenu tayari.

Ninatanguliza shukrani zangu za dhati kwa wanachadema wote wanaopinga upuuzi huu uliofanywa na kamati kuu ya chama.

Kusimamia haki, katiba na misingi ya chama ni wajibu wangu, hivyo kwa namna yoyote ile sitaweza kuwa tayari kufumba macho pindi ujinga wa namna hii unapoendelea kutekelezwa kwa uwoga wa uchaguzi.


Nakutakia kila la heri kwenye majukumu yako.

………………………………………………….
Wilfred N. Kitundu
0764619335/0786215181

MSIMAMO WA MWENYEKITI CHADEMA MKOA WA SINGIDA DHIDI YA UAMUZI WA KAMATI KUU YA CHAMA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


 UTANGULIZI
Ikumbukwe kwamba mimi ndio mwanachama wa kwanza kujiunga na CHADEMA mkoa wa SINGIDA na ni mtu wa  300 kitaifa kujiunga na Chama hiki. Nimejiunga mwaka 1992 siku ya mkutano mkuu kwanza wa uzinduzi chama uliofanyika mnazi mmoja.

Nimekuwa nikijitolea vya kutosha nguvu, muda na akili zangu nyingi kukijenga na kukilinda chama hiki mpaka sasa mkoa wetu wa singida umepata wabunge watatu mmoja wa kuchaguliwa na wawili wa viti maalum.

Tangu mwaka 1992 mpaka 2011, chadema imekuwa ikitumia nyumba yangu kama

Klabu ya Waandishi wa Habari waaswa kuacha makundi.

Katibu mtendaji  wa klabu ya waandishi wa habari (Singpress) mkoa wa Singida, Abby Nkungu akitoa taarifa yake juu ya baadhi ya wanachama na viongozi wa klabu hiyo waliosimamishwa Uanachama kutokana na tuhuma mbalimbali.
Mkurugenzi mtendaji wa Umoja wa vilabu vya waandishi wa habari (UTPC) Tanzania, Abubakari Karsan akitoa nasaha zake mbele ya mkutano mkuu maalum wa klabu ya waandishi wa habari (Singpress) mkoa wa Singida.Mkutano huo uliitishwa kwa ajili ya kuwajadili baadhi ya wananchama ambao hawajishughulishi kikamilifu na kazi ya uandishi wa habari.
Baadhi ya wananchama wa klabu ya waandishi wa habari (Singpress) mkoa wa Singida, wakifuatilia kwa makini taarifa zilizokuwa zikitolewa kwenye mkutano mkuu maalum wa klabu hiyo.
WANACHAMA wa Klabu ya Waandishi wa Habari (Singpress) Mkoa wa Singida wameaswa kuacha kuendeleza makundi kwa madai kwamba yatadumaza ustawi wa klabu hiyo.

Wito huo umetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Umoja wa Vilabu vya Waandishi wa Habari (UTPC) Tanzania, Abubakar Karsan wakati akizungumza kwenye Mkutano Mkuu maalum wa klabu hiyo ya Singpress.

Amesema makundi kwenye chama au kikundi chochote cha watu ni sumu ya maendeleo kwa umoja wa wahusika.

Karsan amesema kuwa maendeleo endelevu ya kikundi au chama cho chote yataletwa na ushirikiano wa dhati baina ya wahusika wa chama au kikundi.

“Mimi niwaombe tu muepuke kuwa na makundi imarisheni ushirikiano upendo na kuvumiliana kwa lengo la kuendeleza klabu yenu Pia viongozi watumikieni kikamilifu wanachama wenu kwa kuwapa fursa kwanza”,amesema.

Katika hatua nyingine, Karsan amesema UTPC imesikitishwa sana na kitendo cha baadhi askari polisi wa Mkoa wa Singida kuwanyanyasa na kuwazuia waandishi wa habari kutekeleza majukumu yao.

“Hata hivyo niwaombeni mfahamu kwamba kitendo hicho hakijafanywa na Jeshi la Polisi isipokuwa kimefanywa na wahuni wachache walioko katika Jeshi la Polisi, Polisi kwa ushirikiano na UTPC itawachukulia hatu stahiki wahuni hao”,alifafanua Karsan.

Mkutano huo maalum, umemchagua Jenifrida Hongoa kuwa Mweka Hazina wa klabu hiyo baada ya kuzoa kura 11 za ndio kati za 15 zilizopigwa.

Hongoa ameziba nafasi hiyo baada ya aliyekuwa Mweka Hazina Awila Silla, kuvuliwa wadhifa huo kwa madai kuwa sio mwanachama halali na pia hana uwezo wa  kumudu nafasi hiyo.

Aidha, Mkutano huo umemchagua Damiano Mkumbo kuwa Makamu Mwenyekiti na Hudson Kazonta kuwa mjumbe wa Kamati ya Utendaji.

Wakati huo huo, Mkutano huo umewaagiza Doris Meghji na Daudi Nkuki kuwasilisha kwa kamati ya utendaji vielelezo vya

Monday, December 2, 2013

Dk. Kone afunga semina ya siku mbili ya soko la kukuza Ujasiriamali (EGM).

Mkuu wa mkoa wa Singida,Dk.Parseko Vicent Kone, akifungua semina ya siku mbili iliyohusu soko la kukuza ujasiriamali (EGM) iliyoandaliwa na soko la hisa la Dar-es-salaam (DSE) na kufadhiliwa na Financial Sector Deepening trust (FSDT).Semina hiyo imefanyika kwenye ukumbi wa Aque Vitae hotel mjini Singida. Kushoto ni Afisa Mahusiano na mshauri wa masula ya Kisheria wa soko la Hisa  Dar-es-salaam, Bi.Mary Mniwasa na kulia ni mwenyekiti  wa TCCIA mkoa wa Singida,Francis Mashuda.
Baadhi ya wajasiriamali na wafanyabiashara mjini Singida,waliohudhuria semina ya siku mbili iliyohusu soko la kukuza Ujasiriamali (EGM) iliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Aqua Vitae hoteli mjini Singida.
Mkuu wa mkoa wa Singida,Dk.Parseko Vicent Kone (wa pili kushoto) akijadiliana jambo na Afisa Mahusiano na mshauri wa masuala ya Kisheria wa soko la Hisa la Dar-es-salaam,Bi. Mary Mniwasa,(wa pili kulia) muda mfupi baada ya kufungua semina ya siku mbili iliyohusu soko la kukuza Ujasiriamali (EGM).
Mkuu wa mkoa wa Singida,Dk.Parseko Vicent Kone,(wa pili kulia walioketi) akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wajasiriamali na wafanyabiashara wa mjini Singida waliohudhuria semina ya siku mbili ya soko la kukuza Ujasiriamali (EGM).Wa kwanza kulia (walioketi) ni afisa mahusiano na mshauri wa masuala la kisheria wa soko la hisa la Dar-es-salaam (DSE) Mary Mniwasa na kushoto ni mwenyekiti wa TCCIA mkoa wa Singida,Francis Mashuda.

WAJASIRIAMALI na wafanyabiashara mkoani Singida wametakiwa kuchangamkia fursa zilizopo Soko la Hisa la Dar es Salaam ili kuboresha na kuendeleza biashara zao.
Mwito huo umetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk Parseko Kone wakati akifungua semina ya siku mbili juu ya Soko la kukuza ujasiriamali iliyofanyika ukumbi wa Aqua Vitae mjini hapa.

Dk Kone alisema kuwa Soko la Hisa la Dar es Salaam kupitia kitengo chake kipya kijulikanacho kama “Soko la Kukuza Ujasiriamali”, ni suluhisho la upatikanaji wa mitaji kwa wajasiriamali kote nchini.
Alisema kuwa soko hilo litatoa suluhisho kwa changamoto zinazowakabili wajasiriamali katika upatikanaji wa uhakika wa mitaji ya muda mrefu kwa ajili ya kuendeleza biashara zao, jambo ambalo limekuwa likiwasumbua wajasiriamali na wafanyabiashara.

“Kwa hiyo basi, soko la kukuza ujasiriamali litasaidia kuleta msukumo wa utekelezaji sera mbalimbali za serikali zinazolenga kuondoa changamoto hizo na kuleta urahisi wa upatikanaji wa mitaji kwa ajili ya kukuza biashara zao,” Dk Kone alisema.
Aidha, alieleza kuwa soko hilo linatarajiwa kulichangamsha soko kwa ujumla kupitia ongezeko la utoaji na uorodheshaji wa hisa, kupanua wigo na fursa za kuwekeza mitaji na kuongeza

Enock Rajabu kutoka Singida aibuka mshindi kwenye droo ya “Chomoka na Mwananchi"


Mwalimu wa shule ya msingi Mwanzi ya Manyoni mjini, mkoani Singida, Enock Rajabu (kulia) akikabidhiwa hundi yenye thamani ya shilingi milioni moja baada ya kushinda droo ya  ’Chomoka na Mwananchi’ na meneja mauzo wa kampuni ya Mwananchi mikoa ya Singida na Tabora, Bw. Aretas Mroso. Shindano hilo la kuwania shilingi milioni moja,bado linaendelea katika droo ya kila siku na inamwezesha mhusika kuingia kwenye droo kubwa ya kujishindia gari kubwa jipya kabisa aina ya TATA safari.

Sunday, December 1, 2013

AMPIGA FIMBO YA KICHWA MAMA MKWE NA KUMSABABISHIA MAUTI, KISA KACHOKA KUMLEA.

Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Singida, ACP. Geofrey Kamwela akitoa taarifa kwa waandishi wa habari (hawapo kwenye picha) juu ya matukio ya kuuawa watu wawili mkoani Singida, likiwemo la Egila Petro kumpiga kwa fimbo mama mkwe wake mwenye umri wa miaka 80 na kusababisha kifo chake.

WATU wawili mkoani Singida wamefariki dunia kwenye matukio tofauti likiwemo la kikongwe mmoja mwenye umri wa miaka 80, kupigwa fimbo kichwani na mkwewe kwa kile kilichodaiwa kuwa mkwewe huyo, amechoka kumlea.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida SACP,Geofrey Kamwela, amesema Egila Petro (42) mkazi wa kijiji cha Mpora kata ya Iseke tarafa ya Nkoko wilayani Manyoni amempiga fimbo kichwani mama mkwe wake Doris Chiwiche na kumsababishia kifo chake siku tisa baadaye.

Amesema kikongwe huyo Doris alipigwa fimbo kichwani na Egila Novemba 18 mwaka huu saa nane mchana na alifariki Novemba 27 mwaka huu saa 12 asubuhi.

Kamwela amesema chanzo cha mauaji hayo ni mgogoro wa chini kwa chini kati ya Egila na mama mkwe wake Doris huku ikidaiwa kuwa Egila amekuwa akimshinikiza mumewe Benard Mdemu amwondoe mama yake huyo na kumpeleka kwa ndugu zake wengine kwa vile yeye amechoka kumlea.

Katika tukio jingine Kamanda Kamwela amesema John Liongo (37) mkazi wa Misuna Singida mjini amefariki dunia baada ya kupigwa risasi kichwani na tumboni na watu wasiojulikana.

Amesema tukio hilo limetokea Novemba 27 mwaka huu saa 6.10 mchana huko katika kijiji cha Mnang’ana kata na tarafa ya Sepuka wilayani Ikungi.

“Uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa marehemu akiwa na watu wasiojulikana siku ya tukio aliondoka Singida mjini kwa gari ambalo bado halijajulikana namba zake za usajili Walipofika katika kijiji cha Mnang’ana waliingia porini na huko ndiko walipomuulia John”,alifafanua Kamwela.

Kamanda huyo amesema katika eneo hilo la mauaji waliokota

Wakulima Singida wahimizwa kulima Mihogo.

Diwani wa kata ya Ikungi wilaya ya Ikungi, Haji Mukhandi akitoa nasaha zake kwenye mkutano wa uchaguzi wa kamati ya shule ya msingi Ikungi mchanganyiko uliofanyika kwenye viwanja wa shule hiyo kongwe iliyojengwa mwaka 1944.Wa kwanza kulia waliokaa,ni mwalimu mkuu wa shule hiyo,Olivary Kamilly na anayefuata ni mwenyekiti wa kamati ya shule inayomaliza muda wake, Naftali Gukwi.
Mwenyekiti wa kamati ya shule ya msingi Ikungi mchanganyiko anayemaliza muda wake, Naftali Gukwi (ata tetea nafasi yake hiyo), akifungua mkutano wa uchaguzi wa kamati ya shule hiyo uliyofanyika shuleni hapo.Wa kwanza kulia ni mwalimu mkuu Olivarry Kamilly na kushoto ni diwani wa kata ya Ikungi, Haji Mukhandi.
Baadhi ya wazazi/walezi wakipiga kura kuchangua kamati ya shule ya msingi Ikungi mchanganyiko wilaya ya Ikungi katika uchaguzi uliofanyika shuleni hapo.
Baadhi ya wazazi/walezi wakifutatlia kwa makini mkutano wa uchaguzi wa kamati ya shule ya msingi Ikungi mchanganyiko.

DIWANI (CCM) Kata ya Ikungi wilayani Ikungi Haji Mukhandi amewaagiza wakulima kulima mashamba ya kutosha ya muhogo, ili pamoja na mambo mengine, kupunguza makali ya uhaba wa chakula.

 Haji ametoa agizo hilo wakati akizungumza kwenye mkutano wa uchaguzi wa kamati ya shule ya msingi Ikungi mchanganyiko, uliofanyika kwenye viwanja vya shule hiyo iliyojengwa mwaka 1944.

Amesema zao la muhogo ni zao ambalo limepewa kipaumbele na mkoa kwa vile linastahimili ukame na ni kwa ajili ya kinga ya njaa.

 Aidha, amesema zao la muhogo lina soko kubwa kutokana na matumizi yake ambayo ni pamoja na kuliwa kama ugali, vitafunwa mbalimbali na majani yake hutengenezwa mboga (Kisamvu).

 “Matumizi mengine ni kutengeneza vinywaji vya aina ya togwa na pombe. Viwandani muhogo hutumika kutengeneza biskuti, wanga na huchanganywa na mazo mengine kupata chakula cha mifugo”,alifafanua zaidi diwani huyo.

 Amesema kutokana na matumizi hayo, muhogo una soko kubwa ambalo lina mkubwa wa kumwezesha mkulima kuinua kipato chake.

 Mkutano huo wa uchaguzi uliosimamiwa na Mwenyekiti wa Kamati inayemaliza muda wake,Naftal Gukwi, ulimchagua mwalimu mstaafu Rashidi Msaru kutoka kijiji cha Ikungi kuwa mjumbe wa kamati ya shule hiyo kwa kipindi cha miaka mitatu ijayo kuanzia januari mwakani.

 Kwa mujibu wa mwalimu mkuu wa shule hiyo Olivary Kamilly, Msaru anaugana na wajumbe wengine  waliochaguliwa kutoka vijiji vya Muungano na Mbwajiki, ambao ni Selemani Ng’amo na Yoel Isingo.

 Wajumbe wengine wa kamati hiyo ni Hamisi Mdachi, Mwajuma Sambe na Deodatus Mtaturu ambao wamechaguliwa na serikali ya kijiji cha Ikungi.

 “Pia kwenye kamati hiyo watakuwepo