Thursday, January 9, 2014

Wakala wa M-pesa ajipiga risasi kichwani na kufa papo hapo.

Baadhi ya wakazi wa mjini Singida, wakiwa wamekusanyika katika duka la wakala wa M-pesa lililopo kwenye taasisi ya elimu ya watu wazima, muda mfupi baada ya mmiliki wa duka hilo Mashaka Omari Makiya,kujipiga risasi kwa kutumia Bastola yake na kusababisha kifo chake.
Mwandishi wa habari wa radio na TV Clouds mkoani Singida, John,akisoma wosia (haupo kwenye picha)  ulioachwa na mfanyabiashara Mashaka Omari Makiya,aliyejiua kwa kujipiga risasi kwa bastola yake.Wosia huo umedai kuwa wadogo wa marehemu wakabidhiwe nyumba na fedha alizoziacha.

WAKALA Maarufa wa M-pesa Vodacom na Mkazi wa Kibaoni mjini Singida Mashaka Omari Makiya (30) amejipiga risasi kichwani na kusababisha kifo chake papo hapo.

Mashaka maarufu kwa jina la Mashakom, amejipiga risasi kwa kutumia bastola yake aina ya ‘silencer’ usiku wa Desemba 27 mwaka huu, nyumbani kwake Ipembe mjini hapa.

Shuhuda wa tukio hilo,Shija John amesema Desemba 28 mwaka huu saa saba mchana askari polisi walifika nyumbani kwa marehemu iliyopo mkabala na nyumba ya kulala wageni ya Meatu eneo la Ipembe.

Amesema askari polisi hao waliingia chumbani kwa Mashaka ambapo walikuta mwili wa mfanyabiashara huyo ukiwa sakafuni.Pia walikuta bastola yake ikiwa pembeni mwa mwili huo pamoja na simu zake tatu.

“Taarifa nilizonazo ni kwamba mfanyakazi wa Mashaka aligundua tukio hilo na kisha alitoa taarifa kituo kikuu cha kati cha polisi na askari walifika mara moja”,amesema.

Katika hatua nyingine, mwandishi wa habari hizi aliweza kufika kwenye moja ya maduka yake matatu ya M-pesa na kushuhudia ujumbe wa maandishi ulioachwa na Mashaka ndani ya gari lake jeusi.

Pamoja na askari polisi kukataa kutoa kibali kwa waandishi habari  kusoma ujumbe huo au kuupiga picha,watu waliobahatika kuusoma ukiwa ndani ya gari wamedai kuwa marehemu amemhusisha na kifo chake mfanyabiashara mmoja (jina tunalo) aliyekuwa na mahusiano ya karibu ya kibiashara pia marehemu Mashaka ameagiza kuwa nyumba na fedha zake wapewe wadogo zake.

Kifo cha Mashaka kimezua hofu kubwa na kazi ya uwakala wa M-pesa kwa madai kwamba katika miaka michache waliokuwa wafanyabiasha wa uwakala huo,Tembs na Rweyemamu wote wamepoteza maisha kwa kupigwa risasi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, SACP Geofrey Kamwela amesema

bado hajapata taarifa hizo na ameahidi kulifuatilia na kutoa habari ili jamii iweze kujua kilichojiri.

No comments:

Post a Comment