Monday, July 21, 2014

Manyoni yalipa fidia zaidi ya shilingi 158 milioni kupisha zoezi la huduma ya umeme vijijini.

Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya Manyoni Mseya, akitoa taafira yake ya ulipaji fidia kwa baadhi ya wakazi wa kijiji cha Maweni, Mwanzi na Lusillile ili wapishe mradi wa njia ya umeme 400 KV.

HALMASHAURI ya wilaya ya Manyoni mkoani Singida, imetumia zaidi ya shilingi 158 milioni kulipa fidia kwa baadhi ya wakazi wa vijiji vitatu,ili kupisha zoezi la utoaji wa huduma ya umeme vijijini.

Fidia hiyo imetolewa mapema mwaka huu kwa wakazi wa vijiji vya Maweni,Mwanzi na Lusilile.

Hayo yamesemwa hivi karibuni na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo,Supeet Roine Mseya wakati akitoa taarifa yake kwa naibu wa nishati na madini Charles Kitwanga (Mb),aliyekuwa kwenye ziara ya kikazi ya siku moja wilayani humo.

Amesema fidia hiyo imelipwa kwa
wakazi waliokuwa eneo ambalo mradi wa njia ya umeme ya 400KV unapita.

Akifafanua,Mseya amesema fidia hiyo imefanyika katika vijiji hivyo ambavyo havikuwemo kwenye fidia ya kwanza iliyotolewa mwaka 2012.

“Shule ya msingi Lusilile ambayo katika fidia ya kwanza ililipwa fidia ya zaidi ya shilingi 3.6 milioni,uongozi wa shule hiyo ulilalamikia fidia hiyo kuwa ni ndogo.Baada ya malalamiko hayo kufanyiwa uchunguzi,ilibainika malalamiko hayo yana ukweli ndani yake”,amesema Mkurugenzi huyo.

Mseya amesema shirika la TANESCO,liliweza kuagiza shule hiyo iongezewe fidia ya shilingi 7,442,728,lakini ilibadilisha uamuzi huona kuagiza malipo hayo yasitishwe.


“Ofisi yangu iliishandaa tayari hundi ya malipo hayo ya fidia ya pili kwa uongozi wa shule ya msingi Lusilile.Sisi ni wakala tu wa TANESCO,leo hii wakituagiza tuukabidhi uongozi wa shule ya Lusilile hundi hiyo,tutaikabidhi haraka”,amesema Mseya.

No comments:

Post a Comment