Tuesday, September 16, 2014

Hospitali ya vitanda 1000 kunufaisha kanda ya ziwa.

Moja kati ya nyumba 10 zilizojengwa na Shirika la Nyumba la Taifa Tanzania { NHC } zilizopoa katika eneo la Madewa Veta Mkoani Singida.
Kaimu  Mkurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa Tanzania Nd. Peter Buheja akimkaguza Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alipotembelea mradi wa  nyumba zinazojengwa na shirika la Nyumba Tanzania  Mjini Singida.
Kaimu  Mkurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa Tanzania Nd. Peter Buheja akimpatia maelezo Balozi  Seif juu ya mashine 24 za Kufyatulia Matofali zilizotolewa na shirika hilo kwa ajili ya kupewa Vijana waliounda vikundi vya ushirika katika wilaya zote za Mkoa wa Singida kabla ya kukabidhi mashine hizo kwa Mkuu wa Mkoa huo Dr. Parseko Visent Koni.

Mil 500 kutumika zoezi la Chanjo ya Surua na Rubella Mkoa wa Singida.7

Mkuu wa mkoa wa Singida, Dk.Parseko Kone.

MKOA wa Singida, unatarajia kutumia zaidi ya shilingi 500 milioni kwa ajili ya kugharamia zoezi la kampenin ya taifa ya chanjo mpya ya surua na rubella, kwa watoto wenye umri wa chini ya miaka 15.

Zoezi hilo la nchi nzima,linatarajiwa kuanza mwezi huu wa septemba kuanzia tarehe

Serikali ijenge mazingira rafiki kwa majengo yote ya kusomea ili kuwasaidia walemavu – TASI.

Katibu wa chama cha watu wenye ulemavu wa ngozi (albino) nchini, TASI, Ziada Msembo (kulia) akimkabidhi mwalimu wa wanafunzi walemavu wakiwakiwemo Albino shule ya msingi Ikungi mchanganyiko, Donard Bilali  vitabu vya sheria zinazowahusu walemavu.
Katibu wa chama cha watu wenye ulemavu wa ngozi (Albino) nchini, Ziada Msembo akimkabidhi losheni ya kujikinga na miale ya jua mwanafunzi mwenye ulemavu wa ngozi (Albino) wa shule ya msingi Ikungi mchanganyiko.
Katibu wa chama cha watu wenye ulemavu wa ngozi (Albino) nchini, Ziada Msembo (wa kwanza kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya walimu wa shule ya msingi Ikungi mchanganyiko.

MO apata wapinzani Chadema.

WANACHAMA watatu wa Chama Cha Demokrasi na Maendeleo (CHADEMA) mkoa wa Singida, inadaiwa wameonyesha nia ya dhati kumng’oa Mbunge wa jimbo la Singida Mohammed Gullam Dewji, katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwakani.

Wanachama hao ambao inadaiwa wana uwezo mkubwa wa kulipaisha kimaendeleo jimbo hilo ni aliyewahi kuthubutu kumwangusha Dewji kwenye uchaguzi mkuu uliopita na kuangukia pua, Josephat Isango (kwa sasa ni mwandishi wa habari wa gazeti la Tanzania daima).

Katika uchaguzi mkuu wa chama hicho uliofanyika juzi, Josephat Isango ambaye alikuwa akiomba nafasi ya uenyekiti wa mkoa, aliambulia kura mbili, wakati mshindi Shaban Limu akizoa kura 74.

Wengine ni Vicent Mughwai (mdogo wake na mbunge Tundu Lissu) na Selemani Majindu.

Wanachama hao walitangaza nia zao hizo kwenye mkutano mkuu wa uchaguzi wa chama hicho uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Cheyo Clief,mjini Singida.

Kwa upande wa jimbo la Singida kaskazini linaloshikiliwa na Waziri wa Maliasili ya Utalii, Lazaro Nyalandu,wanachama wa

Kampuni ya Shanta ya uchimbaji wa dhahabu yakabidhi hundi ya milioni 41.5 kwa kikundi cha Aminika Gold Mine cha Sambaru,

Meneja mkuu wa shanta akizungumza kwenye mkutano wa makabidhiano ya hundi hiyo jana.
Kaimu Katibu Mkuu wa kikundi cha Aminika Antony Muhenyi akisoma agenda ya mkutano huo maalumu kwa wanachama wa Aminika.

Meneja Mkuu wa Kampuni ya Shanta, Gold Mining  Limited, Zone Swanepoel (kulia) akimkabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi milioni 41.5 Mwenyekiti wa kikundi cha Aminika Gold Mining Cooperative Society Limited, Francis Mbassa kwenye hafla fupi ya makabidhiano ya hundi hiyo iliyofanyika katika kijiji cha Sambaru.

Wawili wapoteza maisha na 52 wajeruhiwa ajali ya basi Singida.

Askari wa usalama barabarani wilaya ya Ikungi, akikagua basi la kampuni ya KISBO, T.534 CHX baada ya kupinduka katika eneo la kijiji cha Kambi ya mkaa kata ya Issuna wilaya ya Ikungi na kusababisha vifo vya watu wawili na kujeruhi wengine 52.
Basi la kampuni ya KISBO T.534 CHX linavyoonekana baada ya kupasuka tairi la mbele kulia na kuacha barabara na kisha kupinduka katika kijiji cha Kambi ya mkaa kata ya Issuna wilaya ya Ikungi.
Mwili wa abiria wa kike anayedaiwa kuwa na umri katika ya miaka 20-23 aliyefariki dunia kwenye ajali ya basi la KISBO iliyotokea katika kijiji cha Kambi ya mkaa kata ya Issuna wilaya ya Ikungi.

Dereva Gabreil Joseph wa basi la ABC apongezwa na abiria.

Basi la ABC T.433 CVL linaloendeshwa na dereva mbunifu,Gabriel Joseph.
Dereva wa basi la kampuni ya ABC,Gabriel Joseph ifanyayo safari zake kati ya Singida-Dar-es-salaam apongezwa kwa nidhamu yake ya kuwajali wateja wake kwa kuwaita ni sehemu ya familia ya kampuni ya ABC. Pichani ni Dereva Gabriel,a kitoa matangazo mbalimbali wakati wa safari ikiwemo kuwahimza wanafamilia kuhakikisha wamefunga mikanda ya usalama.

DEREVA wa kampuni ya mabasi ya ABC yafanyayo safari zake kati ya Singida na Dar-es-salaam, Gabriel Joseph, amepongezwa kwa hatua yake ya kupandisha hadhi ya wateja wake kwa kuwabatiza jina la wanafamilia wa ABC, badala ya jina la abiria lililozoeleka kwenye vyombo mbalimbali vya usafiri.

Gabriel pamoja na kupandisha hadhi ya abiria wake na kuwaita wanafamilia ya ABC, pia amebuni mbinu mpya ya kuwavutia wanafamilia wa ABC,kwa kuwapa taarifa za mara kwa mara pindi wanapomaliza wilaya na mkoa husika na kuwaarifu wanaingia wilaya nyingine na kutaja mkoa na kilometa za kutembea katika wilaya hiyo.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wanafamilia hao waliokuwa wakisafiri na basi T.433 CVL lililokuwa likiendeshwa na Gabriel,wamedai kwamba kuitwa

Tuesday, September 2, 2014

Mfanyabiashara wa madini apata ajali mbaya ya gari lake iliyopelekea kupasuka kichwa na kufariki papo hapo.

Gari lililokuwa limebeba mwili wa mfanyabiashara wa madini ya Coper Henrico Kairuki likiwa katika hospitali ya mkoa wa Singida.
Hii ni sehemu ya kichwa cha marehemu Kairuki kilichopasuka hadi Ubongo kutoka nje.
 Ndugu jamaa wakishusha mwili wa mpiganaji Kairuki kwenye gari katika chumba cha maiti.

Afariki baada ya kutibiwa na daktari feki Singida.

Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Singida, SACP Geofrey Kamwela.

MKULIMA na mkazi wa kijiji cha Iyumbu tarafa ya Sepuka wilaya ya Ikungi mkoa wa Singida,Jubulu Mahende,amefariki dunia muda mfupi baada ya kupewa matibabu na mtu anayedaiwa kuwa ni daktari feki.

Imedaiwa kuwa Jubulu aliyekuwa akisumbuliwa na kifua, kiuno na mgongo alizidishiwa dawa kitendo kilichopelekea hali yake kuwa mbaya zaidi.

Daktari huyo ambaye amekiri hana cheti cha aina yo yote kutoka vyuo vya afya,Prospa Simson,baada ya kubaini hali ya mteja wake inakuwa mbaya,alimpa

Waandishi waaswa kuhimiza Afya ya Uzazi na Jinsia.

Mratibu wa TACAIDS mkoa wa Singida, Fedes  Mdala, akizindua uhamasishaji wa masula ya ushiriki sawa wa masuala ya Afya ya Uzazi na Ujinsia kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata ya Mandewa mjini Singida.
Mratibu wa shirika lisilo la kiserikali la YMC la mjini Singida, Fidelius Yunde, akihamasisha wananchi wakiwemo vijana na wanaume wa Mandewa mjini Singida, umuhimu wa ushiriki sawa wa wanaume katika masuala ya afya ya uzazi na ujinsia.
Kikundi cha uhamasishaji cha YMC cha mjini Singida, kikitoa burudani ya sarakasi kwenye mkutano wa hadhara  uliofanyika katika viwanja vya  Mandewa mjini Singida kwa ajili ya kuhamasisha na kuelimisha wanaume kushiriki masuala ya afya ya uzazi na ujinsia.

Binti wa kazi ajeruhiwa vibaya kwa kumwagiwa uji wa moto na mke wa bosi wake, kisa wivu wa kimapenzi.

Msichana Jackline Lasway akiwa amelazwa katika wodi ya kina mama namba mbili katika hospitali ya Mkoa wa Singida baada ya kujeruhiwa kwa kumwagiwa uji wa moto wakati akiwa dukani kwa bosi wake eneo la soko kuu Manispaa ya Singida.
 Waandishi wa habari wakimchukua maelezo msichana huyo.
 Msichana Jackline akilia wakati akiwaonesha waandishi wa habari jeraha alilomwagiwa uji na mke wa bosi wake.