Sunday, October 19, 2014

Taarifa fupi ya mafanikio ya utekelezaji wa shughuli za serikali mkoani Singida kipindi cha 2005 – 2014.

 Mkuu wa Mkoa wa Singida Dokta Parseko Vicent Kone.
 Katibu Tawala Mkoa wa Singida Bw. Liana Hassan.
 Jengo la OPD katika Hospitali Mpya ya rufaa ya Mkoa wa Singida.

Lissu akerwa na uongozi wa Chadema Singida kwa kumdodesha.

Mwenyekiti CHADEMA jimbo la kanda ya kati, Tundu Lissu, akihutubia wana CHADEMA na baadhi ya wakazi wa manispaa ya Singida kwenye viwanja vya Peoples mjini Singida.Tundu pamoja na mambo mengine, amewahimiza wananchi kuikataa rasimu ya katiba mpya kwa madai kwamba imechakachuliwa.

Baadhi ya wananchi wa manispaa ya Singida,wakimsikiliza mwenyekiti CHADEMA jimbo la kanda ya kati na mbunge wa jimbo la Singida mashariki, Tundu Lissu, wakati akiwahutubia.

IDADI  ndogo ya wanachama na wasio wanachama wa CHADEMA waliohudhuria mkutano wa hadhara ulioitishwa kwa ajili ya mwenyekiti wa jimbo la kanda ya kati, Tundu Lissu, kuzungumza nao, ilimuudhi mgeni huyo rasmi na kutangaza kwamba viongozi wa CHADEMA Manispaa ya Singida, hawana sifa ya uongozi.

Tundu akionyesha kukerwa mno na mahudhurio hayo, alisema wananchi wa mji wa Singida kwa kipindi cha miaka sita, hawajapata viongozi wanaowastahiki.

“Haya maneno yaliyosemwa na viongozi wa CHADEMA manispaa ya Singida, kwamba wananachi wa mji huu, ni waoga kuhudhuria mikutano ya CHADEMA, ni

Matere wabamiza timu inayokusanya michango ya maabara.

Kamanda wa polisi mkoa wa Singida, SACP,Geofrey Kamwela.

TIMU ya ukusanyaji michango kwa ajili ya ujenzi wa maabara kata ya Mwangeza wilaya ya Mkalama mkoa wa Singida,imeshambuliwa na kujeruhiwa vibaya na baadhi ya wananchi wa kitongoji cha Matere kijiji cha Dominiki.

Timu hiyo iliyokuwa inaongozwa na afisa mtendaji kata ya Mwangeza,Halfa Mrisho,imekubana na dhahama hiyo ikiwa kazini, oktoba mosi mwaka huu majira ya mchana huko katika kitongoji cha Matere kijiji cha Dominiki.

Akizungumza kwa njia ya simu na Mwandishi wa Singida Blog, Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Mkalama, James Mkwega, ametaja wengine waliojeruhiwa kuwa ni Mtendaji wa kijiji cha Dominiki, Juma Saidi, Afisa mifugo Joseph Doto, Mratibu elimu kata Saidi Nyika na Askari mgambo, Koyo Maduhu.

Alisema watendaji hao baada ya kujeruhiwa vibaya kwa silaha za jadi, walikimbizwa katika hospitali ya misheni ya Hydomu mkoa wa Manyara ambako wanaendelea na matibabu.

Akifafanua, alisema siku ya tukio watendaji hao wakiwa kazini kukusanya michango ya maabara, walivamiwa na watu ambao kuna kila dalili kwamba

Kisaki kupata maji salama.

Mhandishi wa maji manispaa ya Singida, Max Kaaya akitoa maelezo juu ya miradi ya maji kwa Naibu Waziri wa Maji Eng. Benelith Mahenge aliyekuwa ziarani mkoani Singida.

WANANCHI wa Kijiji cha Kisaki, katika Manispaa ya Singida wanatarajia kuanza kunufaika na huduma za maji safi na salama ifikapo mwishoni mwa mwezi ujao, baada ya mradi wa maji unaotarajiwa kutumia zaidi ya shilingi milioni 55.1 utakapokamilika.

Mhandisi wa maji wa Manispaa ya Singida,Injinia Max Kaaya alifafanua kwamba mradi huo ulioanza kutekelezwa kuanzia mwezi, julai mwaka jana unatarajiwa kukamilika kujengwa mwishoni mwa mwezi ujao.

Kwa mujibu wa Injinia huyo kati ya kiasi hicho cha fedha, nguvu kazi za wananchi zinatarajiwa kuokoa zaidi ya shilingi

Friday, October 10, 2014

Tamasha la Fiesta 2014 laiteka Singida.

Baadhi ya mwashabiki wa tamasha la Fiesta 2014 wakishangilia kwa hisia,wakati shoo ikiendelea jukwaani ndani uwanja wa Namfua mjini Singida.
Msanii wa muziki wa kizazi kipya kutoka kampuni ya No Fake Zone,Linah Sanga ambaye kwa sasa anatamba na wimbo wake wa Oletemba,akiimba jukwaani mbele ya umati wa watu wakati wa tamasha la Fiesta lililofanyika jana katika uwanja wa Namfua,kulia ni mmoja wa wacheza shoo wake akiwajibika jukwaani.
Kundi mahiri la muziki wa kizazi kipya litambulikalo kwa jina la Makomando wakilishambulia jukwaa la Fiesta hapo jana ndani ya uwanja wa Namfua mjini Singida.
Sehemu ya umati wa watu wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri kwenye jukwaa la Fiesta ndani ya Uwanja wa Namfua hapo jana mjini Singida.

Wednesday, October 8, 2014

Mwalimu achomwa kisu sehemu mbalimbali za mwili wake.

Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Singida, SACP, Geofrey Kamwela.

WATU wawili mkoani Singida wamefariki dunia katika matukio tofauti, likiwemo la Mwalimu wa shule ya msingi Kigogo jijini Dar-es-salaam, Hawa Idd  (34) baada ya kuchomwa kisu sehemu mbalimbali za mwili wake na mdogo wake Ramadhan Iddi (24) anayedaiwa kuwa na matatizo ya akili.

Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Singida, SACP, Geofrey Kamwela alisema tukio hilo limetokea Septemba 23 mwaka huu saa 9.30 alasiri huko katika hospitali ya mkoa mjini Singida.

Alisema Septemba 22 mwaka huu  saa 5.30 asubuhi  kijana Ramadhan ilidaiwa alitoka nyumbani kwao kwa mazingira ya kutatanisha na ndipo mwalimu Hawa ambaye alikuja kwa ajili ya kushughulikia matatizo ya mdogo wake huyo,walianza msako wa kumtafuta katika maeneo mbalimbali mjini Singida.

“Baada ya kumtafuta katika mitaa mbalimbali hapa mjini na kumkosa, Hawa alirejea nyumbani kwao Kibaoni na kumkuta mdogo wake Ramadhan,ameisha rejea nyumbani. Haikuchukua muda wanandugu hao walianza

Walipwa fidia ya mil 263/- kupisha ujenzi wa chuo.

Mkurugenzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania tawi la Singida, Hassanal Issaya akiwa ofisini kwake akitekeleza majukumu yake ya kila siku.
Baadhi ya wanafunzi wa chuo cha utumishi wa  umma Tanzania tawi la Singida wakiwa kwenye darasa wakati wa masomo.

Meya ataka wasio na shughuli mijini kurejea vijijini.

Mstahiki Meya wa Nanispaa ya Singida, Sheikh Salum Mohammed Mahami ,akizungumza kwenya hafla ya uzinduzi wa shirika la TUSIFO. Hafla hiyo imefanykia katika shule ya msingi Kibaoni na Sheikh Mahami, alitumia fursa hiyo kuwasihi wakazi ambao hawana shughuli za kufanya mjini,warejee/waende vijijini kwa madai kuwa kwa sasa mazingira ya mjini, sio rafiki kwao tena. Kushoto ni mkurugenzi wa shirika la TUSIFO, Costantino Charles.
Mkurugenzi wa shirika lisilola kiserikali la Tunawakaribisha Singida Foundation (TUSIFO) la mjini Singida, Costantino Charles akizungumza muda mfupi kabla hajamkaribisha mgeni rasmi Mstahiki Meya wa manispa ya Singida, Sheikh Salum Mohammed Mahami, kuzindua rasmi shirika lisilo la kiserikali la Tunawakaribisha Singida Foundation (TUSIFO).T USIFO linajishughulisha na kutoa misaada ya madaftari, kalamu, sabuni na sare kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari katika katika masniapaa ya Singida.Kulia ni mstahiki meya wa manispaa ya Singida, Sheikh Salum Mohammed Mahami.
Mstahiki meya wa manispaa ya Singida, Sheikh Salum Mohammed Mahami, akikabidhi msaada wa daftari na kalamu kwa baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi Kibaoni mjini Singida.

Tuesday, October 7, 2014

Subirini kupiga kura, sio kuandamana waambiwa Singida.

Baadhi ya magari ya jeshi la polisi mkoa wa Singida, yakiwa yamebeba askari kwa ajili ya kuzuia maandamano ya wanachama wa CHADEMA ya kupiga kuendelea kwa Bunge Maalum la Katiba. Hadi tunakwenda mtamboni,wanachama hao pamoja na mabango yao walishitukia nguvu ya polisi na kufuta maandamano hayo.
Baadhi ya wanachama wa Chama cha Maendeleo na Demokrasia (CHADEMA) manispaa ya Singida,wakiwa nje ya ofisi ya CHADEMA mkoa Singida mjini kwa kusudio la kufanya maandamo ya amani kwa ajili ya kutoa ujumbe kuwa Bunge Maalum la Katiba linaloendelea hivi sasa ni batili. Maandamano hayo hayakufanikiwa kwa kile kilichodaiwa kuwa yakuwa na kibali halali. Ilidaiwa zaidi ya wanachama 200 wangeshiriki maandamano hayo kuanzia ofisi ya CHADEMA mkoa hadi bomani kupitia viwanja vya Peoples.

Mchungaji Singida awataka walemavu wasijinyanyapae.

Mkufunzi kutoka kituo cha Breli kilichoko chini ya kanisa la Pentekoste (FPCT) Tanzania, Ibrahimu Ikomba, akitoa maelezo muda mfupi kabla ya mafunzo ya siku tatu yaliyohusu ujasiriamali yaliyohudhuriwa na walemavu wa macho 60 wa mkoa wa Singida.
Mmoja wa wanasemina ya mafunzo ya ujasiriamali kwa walemavu wasioona, Potifa Sungi akisoma risala yao muda mfupi kabla mafunzo yao ya ujasiriamali hayajafungwa rasmi na mchungaji wa kanisa na FPCT, Amosi Maghasi.
Mchungaji wa kanisa la Pentekoste (FPCT) Kibaoni mjini Singida, Amosi Maghasi akizungumza kwenye ufungaji wa mafunzo ya siku tatu yaliyohudhuriwa na walemavu wa macho 60 wa mkoa wa Singida.Mafunzo hayo yalifanyika kwenye kanisa la Pentekoste Kibaoni.

Mfuga nyuki wa tuzo ya ‘Rais’ akoromea wanavijiji.

Rais wa shirikisho la wafuga nyuki duniani Gilles Ratia (wa tatu kulia) akifafanua jambo kuhusu mizinga ya nyuki kwa Kaimu Mkurugenzi misitu Gladnees Mkamba.Wa kwanza kulia ni mtendaji mkuu misitu, Juma Mgoo na anayefuatia ni Meneja shirika la Future Development Initiatives Jonathan Njau.

MSHINDI wa tuzo ya Rais  juu ya ufugaji  bora wa nyuki  kwa mwaka jana  Jackson Sombi,  wa mkoani Singida, ameibua tuhuma nzito  dhidi ya wana-kijiji wenzake akidai kuwa  ndio wanaokwamisha juhudi zake za kutaka kujikomboa kiuchumi kupitia uzalishaji wa asali na nta.

Sombi ametoa tuhuma hizo mbele ya Rais wa Shirikisho la Kimataifa la wafugaji  wa nyuki (APIMONDIA), Gilles Ratia,  wakati alipotembelea eneo la  hifadhi ya mfugaji nyuki huyo iliyopo katika kijiji cha Msikii halmashauri ya Wilaya ya Singida.

Amedai kuwa hifadhi yake yenye ukubwa wa kilometa za mraba 1,364 ikiwa na jumla ya mizinga

SEMA yatumia shilingi milioni 380 kusambaza Maji Iramba.

Mtendaji mkuu wa shirika la MEDICOR la nchini Uingereza, Fortunat Walther (wa kwanza kushoto) akitoa maelezo juu ya ujenzi wa visima vya maji kwa meneja wa SEMA, Ivo Manyaku, wakati Walther alipotembelea miradi hiyo inayofadhiliwa na shirika lake.
Meneja wa shirika la SEMA, Ivo Manyaku (wa pili kulia mbele), akitoa maelezo juu ya ujenzi wa visima vya maji wilaya ya Iramba, kwa mtendaji mkuu wa shirika la MEDICOR la nchini Uingereza, Fortunat Walther (wa kwanza kushoto).Shirika la MEDICOR linafadhili miradi ya maji na usafi wa mazingira inayotekelezwa na SEMA.

Shirika la FU-DI kutumia zaidi ya Mil 90 kwa miradi ya nyuki.

Meneja wa shirika lisilo la kiserikali la Future Development Initiatives (FU-DI) lenye makazi yake Ikungi mkoa wa Singida, Jonathan Njau akimkaribisha ofisini kwake rais wa shirikisho la wafuga nyuki duniani, Gilles Ratia.
Rais wa shirikisho la wafuga nyuki duniani Gilles Ratia (wa tatu kulia) akifafanua jambo kuhusu mizinga ya nyuki kwa Kaimu Mkurugenzi misitu Gladnees Mkamba.Wa kwanza kulia ni mtendaji mkuu misitu, Juma Mgoo na anayefuatia ni Meneja shirika la Future Development Initiatives Jonathan Njau.
Mizinga ya kienyeji iliopo kwenye shamba darasa la ufugaji nyuki kisasa katika kijiji cha Mahambe tarafa ya Ikungi mkoa wa Singida.

Mampando wakabidhiwa kituo na vyoo vya kisasa.

Meneja wa shirika la HAPA la mkoa wa Singida, David Mkanje, akiwa katika kutekeleza majukumu yake mbalimbali.

SHIRIKA lisilo la kiserikali linalojishughulisha na masuala ya afya, maji na usafi wa mazingira (HAPA) la mkoa wa Singida, limetumia zaidi ya shilingi 15 milioni kujenga kituo cha ushauri na ujenzi wa vyoo bora katika kijiji cha Mampando kata ya Ntutu wilaya ya Ikungi.

Ujenzi wa kituo hicho cha aina yake katika wilaya ya Ikungi, umefadhiliwa na shirika la Health, Australian Tanzania (HAT) na kusimamiwa na shirika la HAPA.

Akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi kituo hicho, Mkurugenzi wa HAPA, David Mkanje, ametoa wito kwa wakazi wa wilaya ya Ikungi, kujitokeza kwa wingi kufika katika kituo cha ushauri na ujenzi wa vyoo bora,ili kujifunza ujenzi huo ambao una faida nyingi.

Alisema kuwa  ujenzi wa vyoo bora una faida nyingi ambazo unaimarisha mazingira bora na pia

Watatu wafariki dunia katika matukio tofauti mkoani Singida.

Kamanda wa jeshi la polisi mkoani Singida, SACP  Geofrey Kamwela.

WATU watatu mkoani Singida, wamefariki dunia katika matukio tofauti likiwemo la mkulima moja  kupigwa vibaya na askari mgambo akituhumiwa kuvunja mlango wa ofisi ya afisa mtendaji wa kijiji.

Kamanda wa jeshi la polisi mkoani Singida, SACP  Geofrey Kamwela alisema katika tukio la kwanza,mkulima mkazi wa kijiji cha Milade tarafa ya Kinyangiri wilaya ya Mkalama,Salum Abrahamani (42) amefariki dunia Septemba mbili mwaka huu saa 6.10 usiku.

Alisema siku ya tukio. Abrahaman alivunja mlango wa ofisi ya mtendaji wa kijiji hicho alikokuwa amefungiwa kwa kosa la kumjeruhi Saidi Nyuha (25).

“Baada ya kuvunja mlango huo, marehemu alienda nyumbani kwake kulala. Baada ya kubaini kuvunjwa kwa mlango huo,askari mgambo Shaban Idd (28),Aman Ramadhan na Shaban Adamu,walimfuata marehemu nyumbani kwake na