Monday, April 28, 2014

Watoto 4000 kupatiwa chanjo katika Wiki ya Chanjo – Parseko Kone, Singida.

Mkuu wa mkoa wa Singida, Dk.Parseko Kone, akizindua utoaji wa chanjo kimkoa katika hospitali ya St.Calorus iliyopo kijiji cha Mtinko. Jumla ya watoto 3,999 wanatarajiwa kupatiwa chanjo mbalimbali.

Mkuu wa mkoa wa Singida, Dk.Parseko Kone, akizungumza na wakazi wa tarafa ya Mtinko wilaya ya Singida, muda mfupi baada ya kuzindua zoezi la chanjo kimkoa lililoanza jana na linatarajiwa kumalizika Aprili 30 mwaka huu.

JUMLA ya watoto 3,999 mkoani Singida wanaositahili kupata chanjo mbalimbali,wanatarajiwa kupatiwa chanjo katika kipindi cha wiki ya chanjo iliyoanza aprili 24 hadi 30 mwaka huu.

Hayo yamesemwa na mkuu wa mkoa wa Singida,Dk.Parseko Kone, wakati akizungumza kwenye uzinduzi wa wiki ya chanjo kitaifa ngazi ya kimkoa uliofanyika katika hospitali ya St.Calorus kijiji cha Mtinko.

Mkuu huyo wa mkoa,amesisitiza kuwa ni muhimu sana kuhakikisha kila mtoto,anapata chanjo zote kwa wakati,ili kukidhibiti  milipuko ya magonjwa mbalimbali.

“Magonjwa yanayolengwa na mpango wa chanjo wa taifa,ni kifua kikuu,donda koo,kifaduro,polio,surua,pepo punda,homa ya ini,homa ya uti wa mgongo,kichomi na kuhara”,alifafanua.

Dk.Kone alisema ili lengo la utoaji chano hizo liweze kufikiwa, ni lazima wataalam,wasimamizi wa chanjo wabadilike kwa kubuni mbinu mpya za kuhamasisha wananchi kuwapeleka watoto wote wanaostahili kupatiwa chanjo mbalimbali kwenye vituo vya kutolea huduma.

“Kwa ujumla,kila mmoja wetu anawajibu wa kuhakikisha

Saturday, April 26, 2014

Halmashauri Mkoa na Manispaa Singida zadaiwa zaidi shilingi 6.3 bilioni na wakandarasi.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Mizengo Pinda.

SEKRETARIETI ya Mkoa na Halmashauri za wilaya na manispaa mkoani Singida zinadaiwa na wakandarasi,wazabuni na watumishi wa umma zaidi ya shilingi 6.3 bilioni hadi novemba mwaka jana.

Madeni hayo yameainishwa kwenye taarifa ya madeni ya mkoa wa Singida iliyotolewa mbele ya kikao cha kamati ya ushauri wa mkoa (RCC) kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa chuo cha VETA mjini Singida.

Taarifa hiyo imedai kwamba halmashauri za wilaya na manispaa,zinadaiwa zaidi ya shilingi 2.4 bilioni na wakandarasi,wakati wazabuni wanadai zaidi ya shilingi 314.9 milioni.

Kwa upande wa sekretariati ya mkoa,inadaiwa na wakandarasi zaidi ya shilingi milioni tisa na wazabuni shilingi 526.6 milioni.

Kwa upande wa madeni ya walimu na watumishi wasio walimu,halmashauri zinadaiwa zaidi ya shilingi 2.7 bilioni zikiwa ni madeni ya walimu na zaidi ya shilingi 1.3 bilioni na watumishi wasio walimu.

Sekretarieti ya mkoa inadaiwa na walimu zaidi ya shilingi 525.6 milioni na zaidi ya shilingi 120.7 milioni na watumishi wasio walimu.

Aidha, taarifa hiyo imetaja athari zinazosababishwa na madeni hayo makubwa,ni serikali kutoaminika na

Kanisa kutumia zaidi ya shilingi 214 milioni kujenga shule.

Waziri wa Mali asili na Utaliii na Mbunge wa jimbo la Singida kaskazini,Lazaro Nyalandu.

KANISA jipya la Miracle Assemblies of God Ministry (MAGM) mkoani Singida linatarajia kutumia zaidi ya shilingi 214.1 milioni kugharamia ujenzi wa shule ya awali ya bweni.

Hayo yalisemwa hivi karibuni na Magreth Ndwete wakati akisoma risala fupi ya kanisa hilo kwenye hafla ya kusimikwa kwa askofu wa kwanza wa kanisa hilo John Sanongo Tesha (58), Mgeni rasmi katika hafla hiyo,alikuwa Waziri wa Mali asili na Utaliii na Mbunge wa jimbo la Singida kaskazini,Lazaro Nyalandu.

Amesema shule hiyo ambayo tayari imeisha anza kwa kuwa na vyumba viwili vya madarasa itachukua wanafunzi wa madhehebu yote ya dini na wale ambao hawana dini kama watakuwepo.

Amesema kanisa hilo lililoanza rasmi juni 11 mwaka 2007 na kupata usajili novemba 21 mwaka jana,pamoja na kutoa huduma ya kiroho pia limeamua kutoa huduma ya kijamii kwa kuanzisha shule ya awali.

“Kwa kuanzia waumini wa kanisa hilo waliamua kuchangishana wao kwa wao na kufanikiwa kupata zaidi ya shilingi

Wajasirimali washauriwa kushiriki maonyesho yanayoandaliwa na SIDO.

Mkuu wa wilaya ya Singida, Queen Mlozi akizungumza wakati wa kufungua mafunzo ya usindikaji nyanya,biashara na masoko yaliyohudhuriwa na wajasiriamali 36 kutoka Manispaa na Wilaya ya Singida.Kulia ni meneja wa SIDO mkoa wa Singida, Shoma Kibende.

WAJASIRIAMALI Wilayani Singida wamehimizwa kujenga utamaduni wa kushiriki maonesho ya kanda ya kati yanayosimamiwa na SIDO ili pamoja na mambo mengine kutangaza bidhaa zao ziweze kupata soko la uhakika na linalolipa vizuri.

Wito huo umetolewa hivi karibuni na Mkuu wa Wilaya hiyo, Queen Mwashinga Mlozi wakati akifungua mafunzo ya usindikaji nyanya,biashara na masoko yaliyohudhuriwa na wajasiriamali 36 kutoka Manispaa na Wilaya ya Singida.

Amesema ili waweze kupata soko la uhakika na lenye manufaa wanapaswa kuhakikisha bidhaa zao zinakuwa na ubora unaokidhi mahitaji ya soko la ndani na nje ya nchi.

“Pia muelewe kuwa biashara yo yote inahitaji uelewa wa soko.Naamini mafunzo ya biashara na masoko mliyopata yatawawezesha kuwa na uelewa mzuri wa soko”amesema Mlozi na kuongeza;

“Nachukua nafasi hii kuwahimiza kuwa soko ni

Friday, April 18, 2014

Mwigulu awanunulia wananchi wake gari la kubebea wagonjwa.

Naibu Waziri wa Fedha na Mbunge wa jimbo la Iramba magharibi, Mh. Mwigulu Nchemba akihutubia wapiga kura wake na wananchi wa kata ya Mtoa tarafa ya Shelui ambapo pamoja na mambo mengine, alihimiza ujenzi wa zahanati kwa kila kijiji.
Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk.Kebwe Stephen Kebwe (MB) akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Mgongo tarafa ya Shelui jimbo la Iramba magharibi ambapo amewataka Wakurugenzi wa halmashauri za majiji, manispaa na wilaya kuhakikisha magari ya kubebea wagonjwa hayatumiki kusafirisha bidhaa yoyote ikiwemo mkaa.
Baadhi ya wakazi wa kata ya Kyengenge jimbo la Iramba magharibi, wakimsikiliza Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk.Kebwe Stephen Kebwe (hayupo kwenye picha) ambaye aliwataka waganga wakuu wa halmashauri za majiji, manispaa na wilaya, kusimamia kikamilifu matumizi ya dawa na vitendea kazi.
Ambulince T.821 CUV iliyotolewa msaada na mbunge wa jimbo la Iramba magharibi, Mh. Mwigullu Nchemba kwa wakazi wa tarafa ya Shelui.Ambulance hiyo imemgharimu Mwingullu zaidi ya shilingi 50 milioni.
Mbunge wa jimbo la Iramba magharibi, Mh. Mwigullu Nchemba akisalimiana na timu ya soka ya kijiji cha Kyengenge.

SERIKALI  imewaonya wakurugenzi wa halmashauri za majiji, manispaa na wilaya nchini, kuhakikisha wanasimamia kikamilifu matumizi sahihi ya magari ya kubebea wagonjwa (Ambulance), vinginevyo watachukuliwa hatua kali za kisheria.

Onyo hilo limetolewa na Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dk. Kebwe Stephen Kebwe (Mb), wakati akizungumza kwenye hafla iliyofana ya kukabidhi msaada wa gari la kubebea wagonjwa (Ambulance), lililotolewa na mbunge wa jimbo la Iramba magharibi, Mwigulu Nchemba kwa wakazi wa tarafa ya Shelui.

Alisema mfanyakazi/dereva akibainika amebadilisha matumizi ya magari hayo ya kubebea wagonjwa na kuanza  kubeba mikaa, abiria au nafaka, ahesabu moja kwa moja kwamba, amejifukuza kazi.

“Mkurugenzi wa halmashauri husika naye akibainika kutowajibika kikamilifu kuhusu kusimamia magari hayo yanatumika kwa lengo la kusafirisha wagonjwa tu, nao watachukuliwa hatu akali za kisheria”,alisisitiza Dk.Kebwe.

Aidha, Dk. Kebwe ambaye pia ni mbunge (CCM) wa jimbo la Sengerema, amewaasa waganga wakuu wa halmashauri za majiji, Manispaa na wilaya, kusimamia vizuri i matumizi ya madawa na vitendea kazi, ili huduma za afya ziweze kukidhi mahitaji ya wananchi.

“Mganga   mkuu ye yote katika halmashauri atakayebainika kuzembea au kuruhusu wizi wa dawa/vitendea kazi, atakuwa amepoteza sifa yake ya uganga mkuu na hivyo italazimika   kuchukuliwa hatua za ksiheria”,alisema.

Katika hatua nyingine,Dk. Kebwe amewataka wananchi

Waandishi wa habari Singida wapata mafunzo ya haki za binadamu.

Mwezeshaji wa mafunzo, Lilian Timbuka, akitoa mada yake kwenye mafunzo yanayohudhuriwa na waandishi wa habari mkoa wa Singida,yanayohusu maadili katika uandishi wa habari na kuripoti masuala yaliyo kwenye mazingira magumu.
Mwezeshaji Lilian Timbuka,akitoa mada yake wakati akifundisha waandishi wa habari mkoa wa Singida, juu ya maadili ya uandishi wa habari na kuripoti masuala yanayojitokeza kwenye mazingira magumu.Mafunzo hayo ya siku nne,yameandaliwa na kufadhiliwa na Baraza la habari Tanzania (MCT).
Mmoja wa waandishi wa habari katika mafunzo,Alice Achieng Obwanoa,akiwasilisha majumuisho ya kazi waliyopewa kuifanya katika kikundi chao ikiwa ni sehemu ya mafunzo ya maadili ya uandishi wa habari na masuala ya kuripoti habari za mazingira magumu.
Baadhi ya waandishi wa habari mkoa wa Singida, wanaohudhuria mafunzo ya siku nne yanayohusu maadili katika uandishi wa habari na kuripoti masuala yanayojitokeza kwenye mazingira magumu.

JUMLA ya waandishi wa habari 23 kutoka vyombo mbalimbali vya habari mkoani hapa wanahudhuria mafunzo yanayolenga kuwaongezea uwezo zaidi wa kuzingatia maadili ya uandishi wa habari na kuripoti kwa ufasaha masuala yaliyo kwenye mazingira magumu.

Mafunzo hayo ya siku nne,yameandaliwa na kufadhiliwa na Baraza la habari Tanzania (MCT) yanaendelea kwenye ukumbi wa mikutano wa Singida Press Club mjini hapa.

Baadhi ya mada zitakazotolewa au kufundishwa ni pamoja na haki za binadamu,haki za binadamu kimataifa,machafuko yanaanzaje,masuala ya usalama kwa mwandishi na wajibu wa wahariri wa habari.

Kwa upande wake Mwezeshaji wa Mafunzo hayo,Lilian Timbuka amewataka waandishi wa habari kufanya kazi kwa kujitambua na kwa weledi wa hali ya juu.

“Mwandishi wa habari kwa kutumia kalamu yako unaweza ukaijenga nchi yako kwa kipindi kirefu.Lakini pia kwa kutumia kalamu hiyo hiyo unaweza

Monday, April 14, 2014

Wananchi waomba serikali kurudisha oparesheni tokomeza ujangili.

Mkuu wa wilaya ya Manyoni, Fatuma Toufiq (wa kwanza kushoto) na anayefuata ni Dc wa wilaya ya Iramba,Yahaya Nawanda na mkuu wa wilaya mpya ya Ikungi, Manju Masambya (wa tatu kushoto).

SERIKALI wilaya ya Manyoni mkoani Singida imeiomba serikali kuu kuangalia uwezekano wa kurejesha mapema zoezi la oparesheni ‘tokomeza ujangili’, ili kudhibiti kasi kubwa iliyopo ya majangili kuua wanyama pori hasa tembo.

Ombi hilo limetolewa hivi karibuni na Mkuu wa Wilaya ya Manyoni,Fatuma Toufiq wakati akizungumza na waandishi wa habari juu ya wimbi kubwa la majangili kuua wanyama pori na zaidi tembo katika hifadhi za wilaya hiyo.

Amesema kuwa katika kipindi cha miezi miwili iliyopita,majangili katika hifadhi ya Rungwa,Kizigo na Kihesi wilayani humo yameuawa tembo 35.

Aidha,Mkuu huyo wa wilaya amesema kuwa kwa ushirikiano na Jeshi la Polisi wameweza kukamata meno ya tembo mara mbili kati ya Januari na sasa katika kizuizi cha kijiji cha Kayui kata ya Mgandu.

“Kama hiyo haitoshi, hivi karibuni tena tumemkamata Afisa Mtendaji wa kijiji cha Kayui Philemon Kanyonga na watu wengine wanne kwa tuhuma ya kumiliki meno ya tembo kilo160 na bunduki ya kivita SMG moja pamoja na risasi zake 195″, amesema.

Toufiq amesema kutokana na kasi hiyo ya uwindaji haramu unaotishia ustawi wa wanyamapori wakiwemo tembo,upo umuhimu mkubwa wa

Wanafunzi 2,006 hawajaripoti kidato cha kwanza mkoani Singida.

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dk. Shukuru Kawambwa.

JUMLA ya wanafunzi 2,006 waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka huu mkoani hapa bado hawajaripoti katika shule walizopangiwa.

Hayo yamesemwa hivi karibuni na Afisa Kazi Sekretariati mkoani Singida,Jacob Elias wakati akitoa taarifa ya usajili wa wanafunzi kidato cha kwanza mwaka huu mbele ya kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) kilichofanyika katika ukumbi wa mkutano wa Chuo cha Mafunzo na Ufundi Stadi (VETA) mjini Singida.

Amesema wanafunzi hao ambao bado hawajaripoti hadi sasa ni sawa na asilimia 19 ya wanafunzi wote 10,802 waliofaulu mtihani wa taifa wa kumaliza shule za msingi.

Akifafanua,Jacob amesema wilaya ya Manyoni inaongoza kwa wanafunzi 585 ambao hawajaripoti kuanza kidato cha kwanza hadi sasa.

“Manyoni inafuatiwa na Wilaya ya

Friday, April 11, 2014

TANROADS Singida yatumia zaidi ya sh 5.1 B kutengeneza barabara zake Julai mwaka jana na februari mwaka huu.

Mkuu wa mkoa wa Singida na mwenyekiti wa bodi ya barabara, Dk.Parseko Vicent Kone, akifungua kikao cha bodi ya barabara cha 36 kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa VETA mjini Singida. Kulia (aliyekaa) ni katibu tawala mkoa wa Singida,Liana Hassan.
Meneja wa wakala wa barabara mkoa wa Singida (TANROADS), Mhandisi Yustaki Kangole, akitoa ufafanuzi juu ya sheria zinazotawala akiba/hifadhi  ya barabara kwenye kikao cha 36 cha bodi ya barabara mkoa wa Singida.
Mbunge wa jimbo la Manyoni Magharibi, John Lwanji akichangia hoja kwenye kikao cha 36 cha bodi ya barabara mkoa wa Singida kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano cha VETA mjini Singida.
Mkuu wa wilaya ya Mkalama, Edward Ole Lenga, akichangia hoja kwenye kikao cha 36 cha bodi ya barabara mkoa wa Singida kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa VETA mjini Singida.

Baadhi ya wajumbe wa bodi ya barabara mkoa wa Singida, waliohudhuria kikao cha 36 cha  bodi ya barabara mkoani Singida kilichofanyika  kwenye ukumbi wa mikutano cha VETA mjini Singida.

WAKALA wa barabara (TANROADS) mkoa wa Singida, umetumia zaidi ya shilingi 5.1 bilioni kugharamia matengenezo mbalimbali ya barabara zake kwa kipindi cha kati ya Julai mwaka jana na Februari mwaka huu.

Hayo yamesemwa na meneja wa TANROADS mkoa wa Singida, Mhandisi Yustaki Kangole, wakati akitoa taarifa yake ya utekelezaji na makadirio ya mpango kwa mwaka 2014/2015 mbele ya kikoa cha 36 cha bodi ya barabara.

Amesema matengenezo ya kawaida kwa barabara za lami, yametumia zaidi ya shilingi 409.8 milioni,wakati matengenezo ya kawaida kwa barabara za changarawe, zimetumia zaidi ya shilingi bilioni moja.

“Kwa upande wa sehemu korofi (lami), tumemia zaidi ya shilingi 52.5 milioni, barabara za changarawe shilingi 536.5 milioni”, amefafanua mhandisi Kangole.

Aidha, amesema katika kipindi hicho matengenezo ya vipindi maalum (lami), wametumia zaidi ya shilingi
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dk. Shukuru Kawambwa.

JUMLA ya wanafunzi 2,006 waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka huu mkoani hapa bado hawajaripoti katika shule walizopangiwa.

Hayo yamesemwa hivi karibuni na Afisa Kazi Sekretariati mkoani Singida,Jacob Elias wakati akitoa taarifa ya usajili wa wanafunzi kidato cha kwanza mwaka huu mbele ya kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) kilichofanyika katika ukumbi wa mkutano wa Chuo cha Mafunzo na Ufundi Stadi (VETA) mjini Singida.

Amesema wanafunzi hao ambao bado hawajaripoti hadi sasa ni sawa na asilimia 19 ya wanafunzi wote 10,802 waliofaulu mtihani wa taifa wa kumaliza shule za msingi.

Akifafanua,Jacob amesema wilaya ya Manyoni inaongoza kwa wanafunzi 585 ambao hawajaripoti kuanza kidato cha kwanza hadi sasa.

“Manyoni inafuatiwa na Wilaya ya Ikungi ambayo wanafunzi 503 hawajaripoti kuanza kidato cha kwanza hadi sasa.Iramba 318, Manispaa ya Singida 270, Singida vijijini 238 na Mkalama 92″, amesema Jacob.

Amesema kila Halmashauri na Manispaa zinapaswa kuweka mikakati bora na sahihi ili kuhakikisha kila mwanafunzi aliyefaulu, ajulikane yupo wapi aweze kufuatiliwa na kuanza masomo.

Kuhusu ajira ya walimu wapya,Jacob amesema mkoa umepangiwa walimu wapya

Viongozi wanachangia kuporomoka kwa mchezo wa riadha nchini.

Mwanariadha mkongwe mkoani Singida, Pius Ikuu (68) akizungumza na mwakilishi wa mtandao wa Habari wa MOblog mkoa wa Singida, Nathaniel Limu. Mzee Ikuu katika enzi zake, amewahi kusinda medali mbili katika mchezo wa kukimbia mita 10,000 na tatu za mita 5,000.Pia maewahi kushiriki mashindano yaliyofanyika nchini Nageria (mwaka hakumbuki) na kushika nafasi ya saba.

KUPOROMOKA kwa mchezo wa riadha nchini kwa kiasi kikubwa imedaiwa kuwa kumechangiwa na viongozi walioko madarakani.

Akizungumza na MO blog hivi karibuni, mwanariadha aliyewahi kuwika kwenye mchezo huo katika miaka ya 60 mwishoni na mapema 1970,Pius Ikuu (78) amesema mchezo huo ambao una fursa kubwa kutoa nafasi kwa vijana wenye vipaji kujiajiri na kuajiriwa,kuachwa kutiliwa mkazo stahiki kuanzia ngazi ya shule za msingi na kusababisha upoteze mwelekeo.

Akifafanua zaidi,amesema uongozi hasa wa  ngazi ya taifa,umechangia kwa kiasi kikubwa kuuawa riadha  nchini,baada ya kuanza utamaduni wa kupendeleana katika maeneo ya mijini na kuyapa kisogo maeneo ya vijijini yaliyojaa vijana wenye vipaji vya riadha.

“Huyu Selemani Nyambui niliwahi kushiriki naye kwenye shindano la kukimbia mita 10,000 mwaka 1972 pale Dar-es-salaam.Katika uongozi wake kwa sasa hafanyi vizuri kwa sababu amesahau kuendeleza riadha kuanzia ngazi ya vijijini na shule za msingi,’ amesema.

Ikuu ambaye kwa sasa ni kiongozi wa kikundi cha uhamasishaji cha Chief Mpahi,amehimiza

Serikali, wananchi wahimizwa kuendeleza miradi iliyoanzishwa na wahisani.


Mratibu wa mradi wa ushiriki sawa wa wanaume katika masuala ya afya ya uzazi na ujinsia (TMEP) mkoa wa Singida, Mary Sirima, akitoa taarifa yake ya utekelezaji wa mradi huo kwa waandishi wa habari (hawapo kwenye picha)
Baadhi ya wataribu wa mradi wa ushiriki sawa wa wanaume katika masuala ya afya ya uzazi na ujinsia (TMEP) waliohudhuria semina ya siku moja ambayo ilihusu kuwajengea uwezo zaidi wa kutoa elimu kwa jamii.
SERIKALI na Asasi zake zimeshauriwa kujenga utamaduni wa kuendeleza miradi ya maendeleo inayoanzishwa na wahisani wa maendeleo ili pamoja na mambo mengine kuifanya miradi hiy ya wananchi kuwa endelevu.

Imedaiwa miradi mingi ya maendeleo ya wananchi inayoanzishwa na wahisani wa maendeleo kufa baada ya kukabidhiwa wananchi na serikali,

Wito huo umetolewa mwishoni mwa wiki na Mratibu wa Mradi wa ushiriki sawa wa wanaume katika masuala ya afya ya uzazi na jinsia (TMEP) Mkoa wa Singida,Mary Sirima wakati akitoa taarifa yake ya maendeleo ya mradi huo ulioanza mwaka 2010/2011 ambao umepangwa kukamilika desemba mwaka huu.

Amesema miradi karibu yote inayoanzishwa na wahisani wa maendeleo lengo kuu huwa ni kuisaidia serikali katika juhudi zake za kuwaondolea wananchi kero mbalimbali zinazowakabili.

Akifafanua zaidi, Sirima amesema pamoja na kuwaondolea kero wananchi ipo miradi mingi tu ambayo inakuwa chachu ya maendeleo katika sehemu husika.

“Kutokana na ukweli huo upo umuhimu mkubwa kwa serikali na taasisi mbalimbali na hata watu wenye uchumi mzuri kuchukua hatua ya kuendeleza miradi inayoanzishwa na wahisani ili iwe endelevu “,amesema Mratibu huyo.

Kuhusu TMEP, Sirima amesema kuanzishwa kwa mradi huo katika

Wakazi wa singida washauriwa kununua ving’amuzi kwa mawakala walioteuliwa.

Meneja Mawsiliano TRCA, Bw. Innocent Mungy.

WAKAZI wa Manispaa ya Singida wameshauriwa kununua ving’amuzi kwa wakala walioteuliwa na mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA), ili kuondoa uwezekano wa kupoteza fedha zao kwa kununua ving’amuzi ‘feki’.

Tahadhari hiyo imetolewa hivi karibuni na Meneja Mawsiliano TRCA, Innocent Mungy, wakati akizungumzia uzimaji wa mitambo ya kurusha matangazo ya televisheni ya mfumo wa utangazaji wa analojia utakaofanyika Singida Machi 31 mwaka huu saa sita usiku.

Amesema mawakala walioteuliwa na TRCA kuuza ving’amuzi Singida,kwa sasa wana ving’amuzi vya kutosha kukidhi mahitaji  yaliyopo.

Alitaja mawakala hao kuwa ni Mushi Original, Saimon Malya, Baltazar Mushi (ana maduka mawili), Kweka Elextronic na Msele.

“Kwa hiyo kila mwenye hitaji la king’amuzi,ahakikishe ananunua kwenye maduka ya mawakala wetu,watakaonunua nje ya maduka hayo kuna uwezekano mkubwa wakanunua  ving’amuzi vyenye

SACCOS Singida yatoa zaidi ya shilingi 329 milioni.

Mwenyekiti wa chama cha ushirika cha akiba na mikopo cha RS SACCOS Ltd, Mkoa wa Singida,Samson Ntuga akiwa ofisini kwake akitekeleza majukumu yake ya kila siku.Wanachama wa SACCOS hiyo ni watumishi wa katibu tawala mkoa wa Singida iliyochini ya ofisi ya mkuu wa mkoa.

CHAMA cha ushirika cha akiba na mikopo cha RS SACCOS ltd,mkoani Singida kimetoa mikopo mbali mbali yenye thamani ya zaidi ya shilingi 329 milioni kwa kipindi cha kati ya mwaka 2008 na mwaka huu.

Hayo yamesemwa hivi karibuni na mwenyekiti wa chama hicho, Samson Ntunga wakati akitoa taarifa yake ya mwaka mbele ya mkutano mkuu wa mwaka uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa ofisi ya mkuu wa mkoa mjini hapa.

Amesema mikopo hiyo midogo na mikubwa imeweza kuwasaidia wanachama ambao ni watumishi wa ofisi ya katibu tawala mkoa wa Singida kupunguza makali ya maisha.

Akifafanua zaidi, Ntunga amesema kuwa mikopo hiyo imewawezesha wanachama hao kugharamia masomo ya watoto wao,ujenzi wa nyumba na kuongeza mitaji kwa ajili ya miradi/biashara zao.

“Katika mafaniko mengine,chama kimebuni mradi wa viwanja kwa ajili ya wananchama vya gharama nafuu.Wakati wo wote kuanzia sasa tunatarajia wanachama wetu wapatao 222 kila mmoja atakabidhiwa

Friday, April 4, 2014

Wafanyabiashara watekwa na maafisa usalama feki.

Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Singida, SACP Geofrey Kamwela, akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) ofisini kwake.

WAFANYABIASHARA wa Manyoni mjini mume na mke,wametekwa na watu watatu waliojifanya kuwa ni maafisa usalama wa taifa makao makuu jijini Dar-es-salaam.

Waathirika wa utekaji huo ni Methew Dominik @ Cheupe (46) na mke wake Selina Methew (42).

Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Singida, SACP Geofrey Kamwela amesema tukio hilo limetokea juzi saa tisa alasiri Manyoni mjini.

Amesema Faraja George (35) mfanyabiashara wa Dodoma mjini,mganga wa tiba asilia na mkazi wa mkoa wa Tanga,Saidi Mgolola @Pesa mbili (49) Michael Peter  na Michael Peter (26) mkazi wa Moshi mjini na dereva wa gari lililotumika katika utekaji huo.

Amesema siku ya tukio watuhumiwa wakiwa na gari T.242 CBM aina ya toyota prado,walifika dukani kwa Methew baada ya kudai kuwa wao ni maafisa usalama taifa,walimwamuru mwenye duka kuwa wanamhitaji Singida mjini kwa ajili ya mahojiano.

“Methew aliwaomba maafisa hao bandia kuwa aambatane na mke wake huko kwenye mahojiano hayo.Baada ya waathirika hao kuingia ndani ya gari,gari hilo badala ya kuelekea Singida mjini,lilibadili na kuelekea Dodoma”,amesema.

Kamwela amesema bahati nzuri polisi Manyoni mjini walipata taarifa ya tukio hilo mapema na wakawasiliana na wenzao wa Bahi mkoani Dodoma ambao walifanikiwa kuwanasa watuhumiwa hapo kwenye kizuizi.

Amesema uchunguzi wa awali umebaini kuwa chanzo cha tukio hilo,ni watuhumiwa kutaka

Singpress yapata katibu mtendaji mpya.

Mwenyekiti wa klabu ya waandishi wa habari (Singpress) mkoa wa Singida, Seif Takaza akifungua mkutano mkuu wa kawaida wa klabu hiyo uliofanyika mjini Manyoni mwishoni mwa wiki.Kulia ni makamu mwenyekiti Damiano Mkumbo na kulia ni kaimu katibu mtendaji,Emmanuel Michael.
Baadhi ya wanachama wa klabu ya waandishi wa habari (Singpress) mkoa wa Singida,wakifuatilia mkutano mkuu wa kawaida wa (mwaka 2013) klabu hiyo uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa kanisa Katoliki mjini Manyoni.

KLABU ya waandishi wa habari (Singpress) mkoa wa Singida imemchagua kwa kishindo Pascal Tantau (32),kuwa katibu wake mtendaji kuziba nafasi iliyoachwa wazi na Abby Nkungu ambaye anadai kwa sasa afya yake ina mgogoro.

Pascal kijana aliyemaliza chuo kikuu cha Dodoma (UDOM) alipata kura 15 za ndio,mbili zilimkataa na moja iliharibika.

Pascal atakuwa madarakani hadi mwishoni mwakwani (2015) uchaguzi mkuu utakapofanyika kwa mujibu wa katiba ya klabu hiyo.

Pascal aliwashukuru wanachama wenzake kwa kumwamini na kumkabidhi nafasi hiyo nyeti. Ameahidi kwamba atawatumikia kwa nguvu zake zote na kwa maarifa lengo kuu ikiwa ni  klabu hiyo iweze kupaa kimaendeleo katika kipindi chake cha uongozi.

“Niwaahidi pia kwamba katika uongozi wangu nitatumia mbinu shirikishi ili kila mwananchama aweze kutoa mchango wake mbalimbali kuendeleza klabu na kuboresha ustawi wa wananchama.Nitajitahidipia kuhakikisha klabu inakuwa na mahusiano mazuri na wadau wake mbalimbali”, alisema kwa kujiamini.

Abby Nkungu amelazimika kujiuzulu nafasi ya ukatibu mtendaji wa Singpress,kwa madai kwamba ameagizwa na daktari wake aishiye nchini

Queen Mlozi ashiriki operasheni ya kuondoa mawe makubwa yaliyokuwa yakitumiwa kuteka magari barabara kuu ya Singida-Dodoma.

Mkuu wa wilaya ya Singida,Queen Mlozi akipasua jiwe kubwa ili liweze kupandishwa kwenye lori kwa lengo kuondolewa kando kando ya barabara kuu ya Singida-Dodoma eneo la kijiji cha Kisaki manispaa ya Singida. Mawe hayo makubwa kwa kipindi kirefu yametumiwa na watu wanaodhaniwa ni majamabazi watekaji wa malori na kupora mali na fedha.
Mkazi wa kijiji cha Kisaki manispaa ya Singida, Juma akipasua jiwe kubwa lililokuwa likitumiwa na majambazi kwa ajili ya kuteka magari na kisha kupora abiria.
Askari Polisi, Jeshi na baadhi ya wakazi wa kijiji cha Kisaki manispaa ya Singida,wakipandisha jiwe kubwa kwenye lori. Zoezi hilo la kuondoa mawe makubwa kando kando ya barabara kuu ya Singida yaliyokuwa yakitumiwa na watu wanaodhaniwa ni majambazi katika kuteka magari na kupora abiria. Mawe hayo mwishoni mwa mwaka jana yalitumika kuteka gari la chuo cha SUA Morogoro na kisha maiti ndani ya sanduku. 

China kuwekeza kwenye kilimo mkoani Singida.

Mkuu wa mkoa wa Singida, Dk.Parseko Kone (wa kwanza kulia) akimwonyesha Balozi wa Jamhuri ya watu wa China,Dk.Lu Youqing (katikati) eneo lililopo katika kijiji cha Kisasida manispaa ya Singida mahali umeme wa nishati ya upepo utazalishwa  na kampuni kutoka nchini China. Kushoto ni mwakilishi mkuu wa uwakilishi wa kiuchumi na kibiashara wa Jamhuri ya watu wa China nchini, Lin Zhiyong.
Mkuu wa mkoa wa Singida Dk.Parseko Kone (mwenye suti nyeusi) akibadilishana mawazo na Balozi wa Jamhuri ya watu wa China (katikati) wakati Balozi huyo alipotembelea eneo la kijiji cha Kisasida manispaa ya Singida mahali kampuni ya Kichina, inatarajiwa kuanza kuzalisha umeme wa nishati ya upepo.
Mkuu wa mkoa wa Singida,Dk.Parseko Kone (kulia) akizungumza ofisini kwake na baadhi ya viongozi waliokuwa wameambatana na Balozi wa Jamhuri ya watu wa China hapa nchini, Dk.Lu Youqing katika ziara ya balozi huyo mkoani Singida.

BALOZI wa Jamhuri ya watu wa China hapa nchini, Dk.Lu Youqing amesema nchi yake inatarajia kuwekeza kwenye sekta mbalimbali mkoani Singida ikiwemo sekta ya kilimo na ufugaji, ili kuharakisha kukuza uchumi wa mkoa huo.

Balozi Youqing aliyasema hayo wakati akizungumza ofisini kwa mkuu wa mkoa wa Singida,Dk.Parseko Kone alipofanya ziara ya kikazi ya siku moja mkoani humo.

Amesema uwekezaji huo utawanufaisha wakazi wengi wa mkoa wa Singida ambao ni wakulima na wafugaji.

Balozi Youqing alifafanua zaidi kwa kusema kuwa kwa kuanzia,China kupitia kampuni yake moja imeonyesha nia ya kuwekeza katika kufua umeme wa kutumia nishati ya upepo.


“Tanzania ina hitaji kubwa la umeme wa upepo ambao utakuwa wa gharama ndogo na hauchafui mazingira”,amesema.

Akisisitiza zaidi, amesema kuwa kutokana na historia ya ushirikiano mzuri uliopo kati ya Tanzania na China, sekretarieti za mikoa na serikali za mitaa, zina fursa ya kushirikiana na mamlaka za serikali za mikoa nchini China ili kujifunza teknolijia mbalimbali.

Akiijengea nguvu hoja yake hiyo, Balozi Youqing amesema

Mamlaka ya maji Singida yadai zaidi shilingi milioni 210.

Mkuu wa mkoa wa Singida,Dk.Parseko Kone, akizungumza kwenye uzinduzi wa wiki ya maji manispaa ya Singida.Wa kwanza kulia (walioketi) ni Kaimu Mkurugenzi wa SUWASA ,Eng.Kombe Mushi, anayefuatia ni Meya Mstahiki manispaa ya Singida na Sheikh mkoa wa Singida, Salum Mahami na Mkuu wa wilaya ya Singida,Queen Mlozi.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa mamlaka ya Masi safi na mazingira safi (SUWASA) Singida mjini, Eng.Kombe Mushi,akitoa taarifa yake ya utendaji wakati wa uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya maji.
Mkurugenzi wa manispaa ya Singida, Joseph Mchina, akitoa nasaha zake kwenye maadhimisho ya wiki ya maji katika manispaa hiyo yaliyofanyika Mandewa mjini Singida.
Mwenyekiti wa bodi ya SUWASA, Kisenge akitoa nasaha zake kwenye uzinduzi wa wiki ya maji manispaa ya Singida.
Tanki la maji la SUWASA lililopo Mandewa mjini Singida.

MAMLAKA ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira (SUWASA) Singida mjini, inadai wateja wake mbalimbali zaidi ya shilingi 210.9 milioni, kitendo kinachochangia kudhoofisha utendaji wa mamlaka hiyo.

Hayo yamesemwa hivi karibuni na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji SUWASA, Eng. Kombe Mushi wakati akizungumza kwenye uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya maji uliofanyika Mandewa nje kidogo ya mji wa Singida.

Amesema kati ya madeni hayo, wateja binafsi wanadaiwa zaidi ya shilingi 123.7 milioni, wakati wafanyabiashara mbali mbali, wanadaiwa zaidi ya shilingi 12.9 milioni.

“Taasisi mbali mbali za serikali, tunazidai shilingi 70,750,185 na madhehebu ya dini tunayadai zaidi ya shilingi 3.6 milioni.  Fedha hizi nyingi, endapo tutalipwa zote, zitatusaidia mno kuboresha utoaji wa huduma zetu”,amesema Kaimu Mkurugenzi huyo.

Aidha, Eng.Kombe amesema mbaya zaidi ni kwamba badhi ya wadaiwa hao, hushindwa kurejesha huduma ya maji na badala yake, kununua maji kutoka kwa majirani au kujiunganishia maji na kuchepusha dira za maji.

“Changamoto zingine tunayokabiliana nayo ni, upotevu wa maji kupitia mifimo chakavu ya maji.  Kwa wastani upotevu huo ni asilimia 43.  Hata hivyo tumejipanga vizuri kwa ajili ya kulimaliza tatizo hilo”,alifafanua.

Katika hatua nyingine, Eng. Mushi amewataka wananchi kuwafichua watu wanaojiunganishia maji kiholela na wanaochepusha dira ya maji.  Bingo ya shilingi

Soko la Nyuki ni mkombozi wa kiuchumi kwa Wafugaji – Dk. Kone.

Mkuu wa mkoa wa Singida, Dk.Parseko Kone, (wa nne kulia) akikata utepe kuashiria kuzinduliwa kwa utundikaji wa mizinga ya Nyuki mkoani Singida.Wa pili kushoto ni mkuu wa wilaya ya Mkalama Edward Ole Lenga.
Mkuu wa wilaya ya Mkalama mkoa wa Singida, Edward Ole Lenga, akizungumza kwenye hafla ya utundikaji mizinga ya nyuki kimkoa zilizofanyika katika kijiji cha Nkungi wilayani Mkalama.Wa pili kulia walioketi,ni mkuu wa mkoa wa Singida,Dk.Parseko Kone na (wa kwanza kulia) ni Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Mkalama,James.Kushoto (aliyekaa), ni Katibu tawala mkoa wa Singida Liana Hassan.
Mkuu wa mkoa wa Singida,Dk.Parseko Kone, akiweka nta kwenye mzinga wa Nyuki kama njia moja wapo ya kuwavutia Nyuki ili waweze kupanga kwenye mzinga huo.

MKUU wa Mkoa wa Singida,Dk.Parseko Kone ameziagiza Halmashauri na Manispaa ya Singida, kuanzisha au kuunda ushirika utakaosaidia wafugaji kupata soko zuri la mazao ya nyuki ili waweze kuharakisha kujikomboa kiuchumi.

 Dk.Kone ametoa agizo hilo hivi karibuni wakati akizungumza kwenye maadhimisho ya siku ya taifa ya utundukaji mizinga ngazi ya mkoa yaliyofanyika kimkoa wilayani Mkalama.

Amesema utundikaji huo wa ushirika wa wafuga nyuki ni agizo lililotolewa na Waziri Mkuu kuwa kila mkoa uwe na ushirika huo.

Akifafanua zaidi,Dk.Kone amesema ushirika wa wafugaji nyuki,una faida nyingi ikiwemo wafugaji kupata soko zuri na la uhakika.

Kuhusu siku ya utundikaji mizinga,amesema lengo lake ni kuhamasisha ufugaji nyuki ili kuongeza uzalishaji wa mazao ya nyuki kwa kuzingatia ubora na teknolojia sahihi.

 “Kwa kutumia teknolojia sahihi,wananchi watazalisha

Albino mbaroni kwa kumchuna Ngozi Mtoto sehemu yake ya siri.

Kamanda wa jeshi la polisi mkoani Singida SACP, Geofrey Kamwela.

MKULIMA mkazi wa kijiji cha Nkalankala kata ya Mwanga,tarafa ya Nduguti wilaya ya Mkalama mkoani Singida ambaye ni mlemavu wa ngozi (albino) ,Hidaya Omari (20),anashikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma ya kumnyonga hadi kufa, mtoto wake wa kiume mwenye umri wa mwaka moja na nusu,na kisha kumchuna ngozi katika sehemu yake ya siri.

Mtoto aliyenyongwa na kuchunwa ngozi ya sehemu yake  ya siri na kutupwa kwenye kisima cha maji chenye kina cha mita moja,ni Richard Paulo.

Imedaiwa pia mama yake mzazi na mtuhumiwa Hidaya,Neema Paulo (35), naye anashikiliwa na polisi kwa tuhuma ya kuhusika  kumnyonga Daudi Richard na kumsababishia kifo.

Kamanda wa jeshi la polisi mkoani Singida,SACP,Geofrey Kamwela,alisema tukio hilo la kusikitisha,limetokea machi 13 mwaka huu saa moja na nusu asubuhi huko katika kijiji cha Nkalankala wilayani Mkalama.

Alisema mtoto huyo Daudi,aliokotwa akiwa anaelea juu ya maji ya kisima chenye urefu wa mita moja.

Kamwela alisema uchunguzi wa awali wa jeshi la polisi,umebaini kuwa Daudi (marehemu) aliuawa na kuchunwa