Wednesday, November 18, 2015

Wanawake wajawazito Manyoni wanapoteza maisha kwa kufuata Huduma za Afya umbali wa zaidi ya KM 30 hadi 40.

Mmoja wa watoto waliofika katika ofisi za Kijiji cha Maweni kwa ajili ya kuhudhuria Kliniki tembezi kutoka katika Hospitali ya misheni ya Kilimatinde,wilayani Manyoni akipimwa uzito na wahudumu wa afya wa Hospitali hiyo.
Watoto wakisalimiana wakati wakisubiri kupatiwa huduma za chanjo kutoka kwa wataalamu wa afya kutoka katika Hospitali ya misheni ya Kilimatinde,wilayani Manyoni.

Mkoa wa Singida mwenyeji maadhimisho ya siku ya Ukimwi duniani, Desemba Mosi mwaka huu.

Mkuu wa mkoa wa Singida,Dk.Parseko Vicent Kone,jana akitoa taarifa kwa waandishi wa habari (hawapo kwenye picha) juu ya kufanyika kwa maadhimisho ya siku ya UKIMWI duniani kitaifa mkoani Singida.
Baadhi ya waandishi wa habari mkoani Singida,wakiwa kwenye harakati za kupata picha bora ya mkuu wa mkoa wa Singida,Dk.Parseko Vicent Kone (hayupo kwenye picha) jana.Mkuu huyo wa mkoa,alikuwa akitoa taarifa ya kufanyika kwa maadhimisho ya siku ya UKIMWI duniani itakayofanyika kitaifa mkoani Singida.

Rais mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye maadhimisho ya siku ya UKIMWI duniani, ambayo kitaifa inatarajiwa kufanyika mkoani hapa  Desemba mosi mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisni kwake jana,mkuu wa mkoa wa Singida,Dk.Parseko Kone,alisema maadhimisho hayo yanatarajiwa kuanza novemba 24 mwaka huu kwenye viwanja vya peoples mjini hapa, na yatazinduliwa rasmi  novemba 25.

Alisema katika wiki ya maadhimisho hayo,wadau mbalimbali watapata fursa ya

Watu sita wapoteza maisha mkoani Singida.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, ACP. Thobias Sedoyeka akiongea na waandishi wa habari  Mkoani Singida alipokuwa akitoa taarifa za matukio ya mauaji ya watu sita Mkoani hapa.
Baadhi ya wananchi wa Kijiji cha Mukhola, kata ya Mgori wakiwa katika safari ya kumtafuta mtu aliyewauwa wanawake wawili akiwemo mtalaka wake kwa kugombea mashamba.

WATU sita wamefariki dunia na mtu mmoja kujeruhiwa katika matukio manne tofauti yaliyotokea Mkoani Singida kati ya Okt,31 na Nov,01,mwaka huu.

Kamanda wa polisi Mkoa wa Singida, ACP.Thobias Sedoyeka alifafanua kwamba matukio hayo yalitokea katika Vijiji vya Kintanula, wilayani Manyoni, kata ya Kindai, katika Manispaa ya Singida, Kijiji cha Kinyamwambo, kata ya Merya Singida vijijini na Kijiji cha Kamenyanga, wilayani Manyoni.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na ACP. Sedoyeka zimesema kuwa katika tukio la kwanza lililotokea okt,31,mwaka huu saa 2:30 usiku watu watano wasiofahamika wakiwa na mapanga walivamia

YMC yaendesha mafunzo ya siku mbili ya utafiti wa taaluma shule za msingi Manispaa ya Singida.

Mratbu wa shirika la Uwezo mkoa wa Singida, Nason W.Nason, akitoa nasaha zake kwenye mafunzo yaliyohusu kufanywa kwa utafiti juu ya taaluma shule za msingi manispaa ya Singida.Wa pili kulia ni Kaimu Afisa Elimu shule za msingi manispaa ya Singida, Samwel Mwaikenda na (wa pili kushoto) ni Mkurugenzi wa YMC mkoa wa Singida, Fidelis Yunde.
Kaimu Afisa Elimu manispaa ya Singida, Samwel Mwaikenda, akizungumza kwenye ufungaji wa mafunzo ya namna bora ya kufanya utafiti wa taaluma katika shule za msingi manispaa ya Singida.Wa pili kushoto ni Mkurugenzi wa shirika la YMC mkoa wa Singida, Fidelis Yunde.
Kaimu Afisa Elimu shule za msingi manispaa ya Singida, Samwel Mwaikenda, akimkabidhi kijana Juma cheti kwa kuhitimu mafunzo juu ya utafiti wa taaluma katika shule za msingi manispaa ya Singida. Mkurugenzi wa shirika la YMC mkoani Singida, Fidelis Yunde (suti nyeusi) na wa kwanza kulia, ni Mratibu wa shirika la Uwezo Nason W.Nason.

Thursday, October 8, 2015

Magufuli amshawishi MO kujenga kiwanda Singida ili kutoa fursa ya ajira.

Mgombea urais kupitia tiketi ya CCM, Dkt. John Pombe Magufuli akimwaga sifa kwa aliyekuwa Mbunge wa jimbo la Singida Mjini (Mbunge Mstaafu), Mohamed Dewji baada ya kutumikia vyema na kwa uadilifu kiti chake cha Ubunge jimboni humo wakati wa mkutano wa kampeni za mgombea urais huyo kwa tiketi ya CCM uliofanyika katika viwanja wa Peoples mjini humo.


PICHA 15 ZA MAGUFULI NDANI YA SINGIDA




MO atua Singida kushiriki mkutano wa kampeni za Urais.

Aliyekuwa Mbunge wa jimbo la Singida mjini, Mohammed Dewji akisalimiana na mmoja wa madiwani waliofika kumpokea mara tu baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Singida mjini pamoja na wasaidizi wake.
Aliyekuwa Mbunge wa jimbo la Singida mjini, Mohammed Dewji akiwa ameambatana na Mgombea Ubunge wa jimbo la Bumbuli, January Makamba ambaye pia ni mmoja wa wanakamati wa timu ya ushindi ya kampeni za Mgombea urais kupitia tiketi ya CCM, Dk.John Pombe Magufuli, wakielekea sehemu ya mapokezi mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege Singida mjini.
Aliyekuwa Mbunge wa jimbo la Singida mjini, Mohammed Dewji akilakiwa kwa furaha na watoto wanaoishi kwenye eneo la uwanja wa ndege Singida mjini.

Wednesday, October 7, 2015

Ajali ya basi la City Boys yaua 3, Singida, mwingine agongwa na Noah.1

Kamanda wa polisI Mkoani Singida (ACP) Thobias Sedoyeka (pichani)akizungumza na waandishi wa habari  juu ya kutokea kwa ajali ya basi la City Boys na kusababisha vifo vya watu watatu Wilayani Iramba  na mwingine kugongwa na Noah Singida vijijini.

WATU wanne wamefariki dunia Mkoani Singida baada ya kupata ajali ya kugongwa na basi la City Boys na mwingine Noah wakati wakivuka barabara eneo la Ulemo barabara kuu ya Singida- Nzega.

Kamanda wa polisi Mkoani Singida (ACP), Thobias Sedoyeka alisema ajaili hiyo imetokea jana majira ya 1:00 usiku katika kijiji cha Kitukutu Kata ya Ulemo, Tarafa ya Kinampanda ,Wilayani Iramba.

Alisema siku ya tukio, basi lenye namba za usajili T 846 CDU aina ya Scania  mali ya kampuni ya City Boys likitokea Jijini Dar es Salaam kwenda Kahama lilikuwa likiendeshwa na dereva Adam George (33) mkazi wa Dar es Salaam.

 Aidha alisema dereva huyo alipofika eneo na Kitukutu kutokana na kile kinachosadikiwa kuwa ni

DORIS MOLLEL FOUNDATION: Yakabidhi vitabu 200 kwa Shule ya Msingi Midamigha Ilongero SINGIDA.

Mwalimu wa taaluma wa shule Msingi Midamigha Ilongero, Singida akipokea vitabu hivyo kutoka taasisi ya Dmf wakati wa kukabidhi vitabu hivyo.
[SINGIDA] Taasisi inayoshughulikia na utetezi wa watoto njiti ya Doris Mollel ‘DORIS MOLLEL FOUNDATION’(Dmf)  mwishoni mwa wiki imekabidhi vitabu 200 kwa ajili ya kujifunzia  katika shule ya msingi Midamigha ilongero, singida.

Vitabu hivyo vitakuwa chachu na changamoto kwa wanafunzi wa shule hiyo ambapo watapata furasa za kujifunza mambo mbalimbali katika elimu yao.

Dmf imetoa vitabu hivyo ni kutokana na ufadhili wa taasisi ya Kituruki iitwayo Rhema Trust.

Taasisi ya Dmf  imekuwa mstari wa mbele katika harakati za kutetea watoto hasa watoto njiti wasipoteze maisha kutokana na kukosa vifaa vya kufanya watoto hao waweze kuishi na kufikia malengo kama watoto wengine ambao hawakuzaliwa na wakiwa njiti.

Msindai awatangazia neema mama ntilie, machinga, waendesha boda boda.

Mgombe Ubunge wa Jimbo la Singida Mjini (CHADEMA) Mgana Msindai, akizungumza na wafanyabiashara wa soko kuu mjini Singida wakati wa Mkutano wa kampeni kuomba ridhaa ya wananchi kumchagua kuwa Mbunge ili kuondoa kero ndogo ndogo za kutozwa ushuru kwa wamachinga na mama ntilie.

MGOMBEA Ubunge wa Jimbo la Singida Mjini (CHADEMA ) Mgana Msindai ameahidi kuondoa kero na kodi ndogondogo wanazotozwa wafanyabiashara wadogo wakiwemo mama ntilie.

Akizungumza jana kwenye  Mkutano wa Kampeni wa chama chake eneo la soko kuu, Msindai alisema mojawapo ya kero hizo ni pamoja na kusumbuliwa kwa kina mama lishe bila kujali ugumu wa maisha unaowakabili hivyo akichaguliwa ataziondoa kodi hizo mara moja.

“Hizi kero za mama ntilie kutozwa shilingi 20,000 kwa mwezi na meza ndogo ndogo za matunda na mboga mboga nitazifuta kwa kushirikiana na madiwani wenzangu wa Ukawa, kwani hii sio sheria kuu, ni sheria ndogo ndogo zinazotungwa na madiwani, sisi tutazifuta mara moja  ili watu hawa waweze kubadilika.”Alisema Msindai maarufu kwa jina la CRDB.

Hata hivyo ili kuendena na hadhi ya Manispaa, Msindai ameahidi kushirikiana na madiwani wenzake kujenga soko jipya la kisasa kwa kuvunja

Nitaondoa njaa, wakulima watatumia helkopta kumwagilia mashamba, nitajenga vituo maalumu vya Albino na wazee – Rungwe

Mgombea Urais wa CHAUMA,Hashim Rungwe katika pozi tofauti akihutubia wananchi wa Singida mjini jana.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha ukombozi wa Umma (CHAUMA) Hashim Rungwe akizungumza kwenye Mkutano wa Kampeni Mkoani  Singida, ambapo aliahidi kuwaondolea wananchi njaa.
Mgombea mwenza wa CHAUMA Issa Abas Husein nae akihutubia wananchi wa Singida mjini.
WANANCHI wakimsikiliza Mgombea Urais wa CHAUMA kwenye kituo cha stendi ya zamani Mjini Singida jana.

Friday, September 18, 2015

Zaidi ya wakazi 5,000 hatarini kukumbwa na magonjwa ya mlipuko.

Kaimu Katibu Tawala wa mkoa wa Singida, Aziza Mumba akikata utepe kuzindua nyota mpya ya kijani.
Baadhi ya wananchi wa kata ya Mang’onyi wakiwa kwenye mkutano wa uzinduzi wa kampeni za uchaguzi mkuu kumnadi mgombea wa ubunge wa jimbo hilo.

ZAIDI ya wakazi 5,000 wa Kijiji cha Sambaru,kata ya Mang’onyi,wilaya ya Ikungi,Mkoani Singida wamo hatarini kupatwa na magonjwa ya mlipuko kutokana na kujisaidia vichakani kwa kutokuwa na vyoo vya kudumu kutokana na idadi kubwa ya wahamiaji wanaoishi kwenye vitongoji saba vilivyopo katika Kijiji hicho.

Ofisa mtendaji wa Kijiji cha Sambaru,Bwana Baraka Njiku amesema wakazi hao wapo kwenye hatari ya kukumbwa na magonjwa ya kuharisha,kuhara damu pamoja na kipindupindu kutokana na kula uchafu wa kinyesi wanachojisaidia kwenye vichaka vilivyopo karibu na nyumba zao za makazi.

Aidha ofisa mtendaji huyo amefafanua kwamba  wakazi hao wapatao 5,870 wanaoishi katika kaya 899 wanahitaji matundu 899,lakini matundu ya vyoo vya muda yaliyopo ni 320 kati ya mahitaji wa wakazi wote wa Kijiji hicho.

Kwa mujibu wa Bwana Njiku katika Kitongoji cha Taru namba saba chenye kaya 99 kinahitaji jumla ya matundu ya vyoo 498 yaliyopo kwa sasa ni matundu ya muda

Uzazi wa mpango utekelezwe na familia kwa vitendo, ili kustawi vyema na kuimarika kiuchumi

Kaimu Katibu Tawala wa mkoa wa Singida, Aziza Mumba akikata utepe kuzindua nyota mpya ya kijani.
Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida Aziza Mumba akizungumza na wananchi wa Mkoa wa Singida wakati wa uzinduzi wa kampeni mpya ya nyota ya kijani kwenye viwanja vya peoples Mjini Singida.
 Kaimu Mganga mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk. Mussa Kimala akizungumza kwenye sherehe hizo.

Thursday, September 17, 2015

Tundu Lissu amshukia Dk.Slaa kwa madai ya kuponzwa na mkewe.

Mwanasheria wa CHADEMA na mgombea ubunge jimbo la Singida mashariki, Tundu Lissu,akizungumza kwenye mkutano wa kampeni ya Ukawa mkoa wa Singida uliofanyika kwenye uwanja wa Peoples mjini hapa.Pamoja na mambo mengine,Tundu amewaomba wakazi wa Singida, kumpa kura ya ndiyo mgombea urais kwa tiketi ya Ukawa, Edward Ngoyai Lowassa, wabunge na madiwani wa Ukawa,ili kuigaragaza CCM kwa madai imechoka na umechuja mbele ya macho ya Watanzania.

Mgombea ubunge jimbo la Singida mjini kupitia ukawa, Mgana Izumbe Msindai, akiomba kura kwenye mkutano wa kampeni wa Ukawa uliofanyika kwenye uwanja wa Peoples mjini hapa. Msindai ambaye amewahi kuwa mbunge wa jimbo la Iramba mashariki kwa vipindi vitatu mfululizo na mwenyekiti wa wenyeviti wa CCM wa mikoa nchini,amewata wakazi wa jimbo la Singida mjini kujitokeza kwa wingi oktoba 25 mwaka huu kuichana chana CCM kwa kadi zao za kupigia kura.

Hospitali ya Mkoa Singida yapigwa tafu ya mashuka na benki ya Posta nchini.

Meneja wa benki ya Posta tawi la Singida, Redenoter Rweyemamu, akizungumza kwenye hafla ya benki hiyo kutoa msaada wa shuka 104 yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni mbili, kwa hospitali ya mkoa mjini hapa, inayokabiliwa na uhaba wa shuka na kusababisha wagonjwa kutumia mashuka yao binafsi kitendo ambacho ni kinyume na taratibu.
Mganga mfawidhi wa hospitali ya mkoa mjini hapa, Dk. Daniel Tarimo, akitoa shukrani zake kwa benki ya posta tawi la Singida mjini kwa msaada wake wa mashuka kwa hospitali hiyo.Dk.Tarimo amedai kuwa bado hospitali hiyo inaupungufu wa shuka 2,000 na magodoro 236.
Meneja wa benki ya Posta tawi la Singida mjini (katikati),akimkabidhi Mganga mfawidhi wa hospitali ya mkoa mjini hapa, Dk.Daniel Tarimo mashuka 104. Mashuka hayo yamepunguza makali ya uhaba mkubwa wa shuka na sasa, kuna upungufu wa shuka 2,000 na magodoro 236.

BENKI  ya Posta Tawi la Singida Mjni, imetoa msaada wa shuka 104 yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni mbili kwa hospitali ya mkoa ya mjini hapa, ili kupunguza uhaba mkubwa unaoikabili hospitali hiyo.

Akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi msaada huo, Redempter Rywemamu, alisema hatua hiyo imechukuliwa  na benki ya posta,ikiwa ni  ni kuitikia  wito uliotolewa na

Taasisi za fedha ziwezeshe wajasiriamali wadogo.

Mkuu wa mkoa wa Singida, Dk.Parseko Kone, akikagua vyungu vilivyotengenezwa na wajasiriamali wa wilaya ya Iramba ambao wanashiriki maonesho ya 12 ya SIDO kanda ya kati yanayoendelea mjini Singida.
Afisa Mwanadaamizi wa Masoko wa Shirika la viwango (TBS), Gladness Kaseka (kushoto) akimpa maelezo Mkuu wa mkoa wa Singida, Dk.Parseko Kone, juu ya shughuli zinazofanywa na shirika hilo. Dk.Kone alikuwa akikagua mabanda ya wajasiriamali na taasisi mbalimbali wanaoshiriki maonesho ya bidhaa mbalimbali yaliyoandaliwa na SIDO kanda ya kati yanayoendelea mjini Singida.
Mkuu wa mkoa wa Singida, Dk.Parseko Kone, akionyesha kupendezwa na mkuki uliotengenezwa na wahunzi wa kijiji cha Kisonga wilaya ya Iramba wanaoshiriki maonesho ya SIDO kanda ya kati yanayoendelea mjini Singida.

Kaimu Msimamizi wa uchaguzi Singida mjini atupilia mbali pingamizi la CHADEMA dhidi ya mgombea wa CCM

Kaimu msimamizi wa uchaguzi jimbo la Singida mjini, Gerald Muhabuki Zephyrin,akizungumza na SingidaYetu Blog juu ya uchaguzi ubunge jimbo la 
Singida mjini.

PINGAMIZI lililowekwa na Chama Cha Maendeleo na Demokrasia (CHADEMA),jimbo la Singida mjini, dhidi ya mgombea wa CCM Mussa Ramadhan Sima kuwa

Maonyesho ya SIDO kwa wajasiriamali kwa kanda ya kati kufanyika Agosti 26 hadi Septemba Mosi mwaka huu Mkoani Singida.

Mkuu wa mkoa wa Singida, Dk.Parseko Vicent Kone, akitoa taarifa kwa waandishi wa habari  juu  ya kufanyika kwa maonesho ya SIDO kanda ya kati kuanzia Agosti 26 hadi septemba mosi mwaka huu mjini Singida. SIDO kanda ya kati inajumuisha mikoa ya Singida, Tabora na Kigoma.Katika maonesho hayo, bidhaa mbalimbali zinazozalishwa na wajasiriamali na wafanyabiashara ndogo.

Waandishi wa habari watakiwa kutumia kalamu zao kudhibiti madereva waenda kasi na mabasi nchini.

Mkuu wa Kitengo cha usalama barabarani Wilaya ya Singida (DTO), Antony Sempanga akimwonesha Mwenyekiti wa kamati ya usalama barabarani Mkoa wa Singida Akhlan Ghalib,kifaa cha kisasa cha kupima mwendo kasi (speed radar) wakati wa akitoa taarifa juu ya wiki ya nenda kwa usalama barabarani Mkoa wa Singida kwa waandishi wa habari (hawapo pichani).
Mkuu wa Kitengo cha usalama barabarani Wilaya ya Singida (DTO), Antony Sempanga akiwaonesha waandishi wa habari jinsi speed radar ya kisasa inavyofanya kazi.
 Antony akiwa na kifaa cha kupima mwendo kasi.
Antony akionesha waandishi wa habari nama ya kupokea sms kwa njia ya mtandao kutoka kwenye speed radar kwenda kwenye simu ya mkononi.

Hillary Shoo wa Jambo Leo Singida, anyakua cheti maalumu kwa uandishi bora wa habari za Usalama Barabarani mkoa wa Singida.

Mwandishi wa habari wa Gazeti la Jamboleo Mkoa wa Singida, Hillary Shoo,akipokea cheti maalumu kutoka kwa Katibu Tawala Msaidizi wa Mkoa wa Singida, Aziza Mumba ikiwa ni mchango wake mkubwa katika kuandika habari za kuelimisha jamii juu ya wiki ya nenda kwa usalama barabara Mkoa wa Singida, halfa hiyo ilifanyika jana kwenye viwanja vya kituo cha mabasi yaendeyo mikoani, kulia ni Kamanda wa polisi Mkoani humo Thobias Sedoyeka.

Serikali kuboresha zaidi mazingira ya kufanyia shughuli za wajasiriamali mkoani Singida.

Meneja mradi wa kuwajengea uwezo wafanyabiashara wadogo,Florentina Sallah, akitoa nasaha zake kwenye ufunguzi wa mafunzo ya siku tano yanayohudhuriwa na wafanyabiashara wadogo 150 wa mkoa wa Singida.Wa kwanza kulia ni Mkuu wa mkoa wa Singida,D k.Parseko Kone na anayefuatia ni,Dk.Willhelm Ngasamiaku,mhadhiri wa uchumi idara ya uchumi chuo kikuu cha Dar-es-salaam.
Mkuu wa mkoa wa Singida, Dk.Parseko Kone,akizungumza kwenye uzinduzi wa mafunzo ya siku tano yanayohudhuiwa na wafanyabiashara wadogo 150 yanayoendelea kwenye ukumbi wa mikutano wa chuo cha maendeleo ya wananchi mjini hapa. Dk.Kone ameahidi kuwa serikali mkoani hapa itaendelea kuwajengea mazingira mazuri wafanyabiashara hao, ili shughuli zao ziwe za tija zaidi.
Mhadhiri wa uchumi idara ya uchumi chuo kikuu cha Dar-es-salaam, Dk.Wilhelm Ngasamiaku,akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi wa mafunzo ya wafanyabiashara wadogo 150 wa mkoa wa Singida yanayoendelea kwenye chuo cha maendeleo ya wananchi mjini hapa.Wa pili kulia ni mkuu wa mkoa wa Singida,Dk.Parseko Kone na wa kwanza kulia ni mkuu wa wilaya ya Singida,Iddi Amanzi. Kushoto ni Meneja mradi wa kuwajengea uwezo wafanyabiashara wadogo,Florentina Sallah.