Sunday, June 28, 2015

January Makamba adhaminiwa na wanaCCM 8,300 mkoani Singida.

Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba, akipokewa na baadhi ya wanaCCM na wananchi wa mkoa wa Singida jana (26/6/2015) akiwa kwenye harakati zake za kusaka wadhamini ili aweze kuteuliwa na CCM kupeperusha bendera ya CCM kwenye nafasi ya urais kwenye uchaguzi mkuu ujao.
Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba, akiwashukuru wanaCCM 8,300 wa mkoa wa Singida, waliomdhamini ili aweze kuteuliwa kupeperusha bendera ya CCM kwenye nafasi ya urais kwenye uchaguzi mkuu ujao.
Baadhi ya wana CCM na wananchi wa mkoa wa Singida,wakimsikiliza Naibu waziri wa mawasiliano,sayansi na teknolojia,Januari Makamba,wakati akiwashukru wana CCM 8,300 waliomdhamini ili CCM iweze kumteua kugombea nafasi ya urais kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka huu.

Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba, akionyesha karatasi yenye orodha ya wana CCM 8,300 waliomdhamini ili CCM iweze kumteua kugombea nafasi ya urais katika uchanguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika oktoba mwaka huu.Kushoto ni katibu CCM manispaa ya Singida, Magreth Ndwete.
Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba akiwa na mke wake, wakishiriki dua iliyotolewa na kiongozi wa dhehebu la dini ya kiislamu kwa ajili ya kumwombea Makamba kwenye safari ya kuusaka urais mwishoni mwa mwaka huu.

No comments:

Post a Comment