Friday, June 19, 2015

Waziri Nyalandu atangaza nia na kuchukua fomu, asema uwekezaji kwenye rasilimali umma ni muhimu.

Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Lazaro Nyalandu na mkewe Bi.Faraja Nyalandu wakiingia uwanja wa Namfua Mjini Singida kabla ya kuhutubia wananchi kwa kutangaza nia ya kugombea Urais.

Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Lazaro Nyalandu akiteta jambo na Mwenyekiti wa CCM Wilaya wa Singida, Barnabas Hanje kabla kutangaza nia ya kugombea urais wa Tanzania kwenye mkutano uliofanyika uwanja wa Namfua Mjini Singida.
Bi. Faraja Nyalandu akiongea na wananchi kabla ya hotuba ya mumewe Mhe. Lazaro Nyalandu ya kutangaza nia ya kugombea  urais wa Tanzania.

Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Lazaro Nyalandu akiwahutubia wananchi  waliojitoeza kwa wingi uwanja wa Namfua Mjini Singida, wakati wa kutangaza nia ya kugombea Urais wa Tanzania kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi.
 Wasanii wa kundi la Yamoto Bendi wakitumbuiza kabla ya hotuba ya Mhe. Nyalandu.
 Sehemu ya umati mkubwa uliojitokeza uwanja wa Namfua Mjini Singida.
Mhe Nyalandu na Mkewe wakisakata rumba mara baada ya utoba yake ya kutangaza nia.

Mhe. Lazaro Nyalandu na Mkewe Bi.Faraja Nyalandu wakinyanyua mkoba juu mara baada ya kuchuka fomu ya kugombea urais kwa tiketi ya CCM kwenye ofisi za chama cha mapinduzi mjini Dodoma.
Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Lazaro Nyalandu akiongea na waandishi wa habari mara baada ya kuchukua fomu za kugombea urais.

No comments:

Post a Comment