Thursday, October 8, 2015

Magufuli amshawishi MO kujenga kiwanda Singida ili kutoa fursa ya ajira.

Mgombea urais kupitia tiketi ya CCM, Dkt. John Pombe Magufuli akimwaga sifa kwa aliyekuwa Mbunge wa jimbo la Singida Mjini (Mbunge Mstaafu), Mohamed Dewji baada ya kutumikia vyema na kwa uadilifu kiti chake cha Ubunge jimboni humo wakati wa mkutano wa kampeni za mgombea urais huyo kwa tiketi ya CCM uliofanyika katika viwanja wa Peoples mjini humo.









MGOMBEA urais kupitia CCM Dk.John Pombe Magufuli,amemshawishi aliyekuwa mbunge wa jimbo la Singida mjini Mohammed Dewji,kujenga kiwanda mkoani humo, ili pamoja na mambo mengine,kupunguza uhaba wa ajira.

Amedai Dewji maarufu kwa jina la MO katika kipindi chake cha ubunge miaka 10 iliyopita, ameonyesha mapenzi makubwa na ya aina yake kwa wakazi wa jimbo la Singida na mkoa kwa ujumla.

Dk.Magufuli alisema kutokana na ukweli huo,sasa anapaswa kuhamishia mapenzi hayo kwa kujenga kiwanda mkoani Singida kitakachoajiri vijana, na pia kuinua pato la mkoa na taifa kwa ujumla.

Mgombea urais huyo aliyasema hayo kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika katika viwanja vya Peoples mjini Singida na kuhudhuriwa na mamia ya wakazi wa jimbo la Singida na maeneo ya jirani.

“Katika kipindi chako cha ubunge umeonyesha uzalendo wa hali ya juu,umewatumikia vema wananchi wa jimbo la Singida mjini. Ndio maana hadi sasa bado wana mapenzi makubwa sana kwako,naomba uwajengee kiwanda. Nakuhakikishia mimi binafsi napenda wawekezaji wazalendo wanaoipenda nchi yao na wewe ni mmoja wao”,alisema Dk.Magufuli.

Aidha, Dk.Magufuli amemuahidi kumpa ushirikiano pindi atakapohitaji kuwekeza katika viwanda mkoani Singida.

Akisisitiza,alisema “Dewji nakuomba sasa sana ikiwezekana jenga hata viwanda vitatu ili wananchi wa mkoa wa Singida wapate ajira. Nitakuunga mkono kwa asilimia 100.Kama ni kibali unataka,nitakupa leo hii kwa kuwa mmenihakikishia nitakuwa rais wa tano”.

Awali akizungumza kwenye mkutano huo wa kampeni, Dewji aliwaahidi wakazi wa jimbo la Singida mjini kwamba ataendelea kushirikiana nao katika kulipaisha jimbo hilo kimaendeleo.

MGOMBEA urais kupitia CCM Dk.John Pombe Magufuli,amemshawishi aliyekuwa mbunge wa jimbo la Singida mjini Mohammed Dewji,kujenga kiwanda mkoani humo, ili pamoja na mambo mengine,kupunguza uhaba wa ajira.

Amedai Dewji maarufu kwa jina la MO katika kipindi chake cha ubunge miaka 10 iliyopita, ameonyesha mapenzi makubwa na ya aina yake kwa wakazi wa jimbo la Singida na mkoa kwa ujumla.

Dk.Magufuli alisema kutokana na ukweli huo,sasa anapaswa kuhamishia mapenzi hayo kwa kujenga kiwanda mkoani Singida kitakachoajiri vijana, na pia kuinua pato la mkoa na taifa kwa ujumla.

Mgombea urais huyo aliyasema hayo kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika katika viwanja vya Peoples mjini Singida na kuhudhuriwa na mamia ya wakazi wa jimbo la Singida na maeneo ya jirani.

“Katika kipindi chako cha ubunge umeonyesha uzalendo wa hali ya juu,umewatumikia vema wananchi wa jimbo la Singida mjini. Ndio maana hadi sasa bado wana mapenzi makubwa sana kwako,naomba uwajengee kiwanda. Nakuhakikishia mimi binafsi napenda wawekezaji wazalendo wanaoipenda nchi yao na wewe ni mmoja wao”,alisema Dk.Magufuli.

Aidha, Dk.Magufuli amemuahidi kumpa ushirikiano pindi atakapohitaji kuwekeza katika viwanda mkoani Singida.

Akisisitiza,alisema “Dewji nakuomba sasa sana ikiwezekana jenga hata viwanda vitatu ili wananchi wa mkoa wa Singida wapate ajira. Nitakuunga mkono kwa asilimia 100.Kama ni kibali unataka,nitakupa leo hii kwa kuwa mmenihakikishia nitakuwa rais wa tano”.


Awali akizungumza kwenye mkutano huo wa kampeni, Dewji aliwaahidi wakazi wa jimbo la Singida mjini kwamba ataendelea kushirikiana nao katika kulipaisha jimbo hilo kimaendeleo.

No comments:

Post a Comment