Tuesday, May 19, 2015

Wanawake wahimizwa kusaidia makundi yenye mahitaji maalumu.

Mwanyekiti wa Umoja wa Wanawake watumishi kanisa la Pentekoste (UWW) mjini Singida, Lessi Jared (kushoto) akimkabidhi vifaa tiba Kaimu mganga mfawidhi hospital ya mkoa ya mjini Singida, Dk.Daniel Tarimo.Vifaa tiba  hivyo vingi vikiwa kwa matumizi ya chumba cha upasuaji imedaiwa kuwa gharama yake ni mamilioni ya shilingi, vimetolewa na shirika lisilo la kiserikali la waumini wanawake kanisa Pentekoste nchini Denmark-Heart to Heart.
Mganga Kaimu mganga mfawidhi hospitali ya mkoa mjini Singida, Dk.Daniel Tarimo (wa tano kulia) akiwa kwenye picha ya pamoja na wanachama wa Umoja wa Wanawake watumishi FPCT Singida mjini na baadhi wa viongozi wa kanisa hilo, muda mfupi baada ya kukabidhi vifaa tiba.

Wagombea wa nafasi za uongozi Mkalama waonywa kutochafuana katika kipindi hiki.

Mbunge wa viti maalumu (CCM) Mkoa wa Singida, Bi Martha Mlata (wa pili kutoka kulia) akimkabidhi pikipiki Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Mkalama, Bi Elipendo Machafuko (aliyepanda pikipiki) atakayotumia kuwatembelea wanachama wa jumuiya hiyo. Wengine walioshuhudiwa hafla ya makabidhiano hayo ni pamoja na Katibu wa CCM wilaya ya Mkalama,Bw.Amosi Shimba(wa kwanza kulia),Bi Hadija Kisuda-mwenyekiti wa UWT wilaya ya Singida vijijini(wa tatu kutoka kulia) na katibu wa UWT Mkoa wa Singida,Bi Anjela Robert(wa kwanza kutoka kushoto).
Mbunge wa viti maalumu (CCM) Mkoa wa Singida, Bi Martha Mlata (wa kwanza kulia) akiwakabidhi makatibu wa matawi ya jumuiya ya UWT baiskeli moja kwa kila kata.

Thursday, May 14, 2015

Wananchi wenye sifa ya kupiga kura Mkalama washauriwa kujiandikisha

Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Mkalama mkoa wa Singida,James John Mkwenga,akizungumza kwenye ufunguzi wa kikao cha baraza la madiwani  kilichofanyika katika kijiji cha Nduguti.Kushoto ni Makamu Mwenyekiti Asma Seif na kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa halmashauri ya Mkalama,Cusbert Mwinuka.
Mkuu wa wilaya ya Mkalama mkoani Singida, Edward Ole Lenga, akizungumza mbele ya kikao cha kawaida cha baraza la madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Mkalama. Ele Lenga alitumia nafasi hiyo kuagiza madiwani na viongozi kuongeza juhudi kuhamasisha wananchi kuisoma na kuielewa vizuri Katiba iliyopendekezwa.

Singida wasogezewa karibu huduma ya Benki ya Posta Tanzania.

Mwenyekiti wa Benki ya Posta nchini, Lettice Rutashobya (kulia) akimkabuidhi kadi ya benki Mwenyekiti wa mtaa wa Majengo mjini Singida, Stamili Shomari baada ya kupewa offer na benki hiyo kufungua akaunti.
Afisa  Mtendaji Mkuu wa benki ya Posta nchini, Sabasaba Moshingi,akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi wa tawi la benki ya Posta mjini Singida.

Tuesday, May 12, 2015

TASAF yashindwa kukamilisha ujenzi wa meza za soko la kijiji cha Ndago, wilayani Iramba.

Soko la Kijiji cha Ndago,wilayani Iramba lililoshindikana kukamilishwa kwa meza za kufanyia biashara kwa wananchi wa Kijiji hicho kutokana na TASAF awamu ya pili kujitoa kukamilisha ujenzi wa meza hizo kwa kukosa fedha za kufanyikazi hiyo,baada ya kutotengwa kwa fedha za kazi hiyo.

Klabu ya waandishi wa habari mkoani Singida yatakiwa kuzingatia weledi katika taaluma yao.

Kaimu mkurugenzi mtendaji halmashauri ya wilaya ya Mkalama mkoa wa Singida, Cosbert Mwinuka, akizungumza kwenye ufunguzi wa mkutano mkuu wa Singida Press Club (Singpress) uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa hotel ya Muhai iliyopo kijiji cha Nduguti.Wa pili kulia (walioketi) ni mwenyekiti wa Singpress, Seif Takaza na wa kwanza kulia ni makamu mwenyekiti wa Singpress,Damiano Mkumbo.
Baadhi ya wanachama wa Singpress,waliohudhuria mkutano mkutano mkuu wa klabu hiyo uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Muhai iliyopo katika kijiji cha Nduguti wilaya ya Mkalama

Wanafunzi 365 na walimu wanane wachangia choo kimoja chenye matundu manane.

Baadhi ya wazazi wa shule ya msingi Kilimani waliohudhuria kwenye mkutano wa wazazi wa shule hiyo uliofanyika kwenye viwanja vilivyotengwa kwa ajili ya mikutano shuleni hapo.

Thursday, May 7, 2015

Fedha za TASAF Mkalama Singida wanaume wazipora na kunywea pombe.

Mwenyekiti wa kijiji cha Mwanga tarafa ya Nduguti wilaya ya Mkalama mkoa wa Singida, Jackson Mkoma, akifungua mkutano wa tathmini ya matumizi ya fedha za TASAF awamu ya nne uliofanyika kwenye viwanja vya ofisi ya kituo cha kilimo cha kijiji hicho.
Mratibu wa TASAF wilaya ya Mkalama, Athumani Jumanne Dulle, akizungumza kwenye  mkutano wa tathimini ya matumizi ya fedha za TASAF awamu ya nne uliofanyika kwenye viwanja vya ofisi ya kituo cha kilimo cha kijiji hicho.

Halmashauri ya Singida yakusanya mapato ya sh bil 11/-

Makamu mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Singida vijijini, Elia Digha, akitoa taarifa ya mapato na matumizi kwa kipindi cha kuanzia Julai mwaka jana hadi Machi 30 mwaka huu mbele ya kikao cha kawaiada cha madiwani. Digha alisema kuwa halmashauri hiyo ilikusanya zaidi yashilingi bilioni 11.4 ikiwa ni sawa na asilimia 49 ya  lengo la kukusanya zaidi ya shilingi bilioni 22.1.
Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Singida vijijini, Iddi Mnyampanda, akizungumza kwenye ufunguzi wa kikao cha kawaida cha madiwani kilichofanyika mjini Singida. Kulia ni mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya Singida vijijini Hajjat Farida Mwasumilwe na kushoto ni makamu mwenyekiti Elia Digha.

RC Singida awataka wafanyakazi kutekeleza majukumu yao katika kuzingatia mikataba.

Kaimu mkuu wa mkoa wa Singida na DC wilaya ya Singida, Saidi Alli Amanzi, akimkabidhi cheti cha mfanyakazi bora Nyalandu, ambaye ni Katibu tarafa wa tarafa ya Nduguti wilaya ya Mkalama, jana kwenye kilele cha sherehe za wafanyakazi duniani (mei mosi) zilizofanyika kwenye uwanja wa Namfua mjini hapa.

MKUU wa mkoa wa Singida, Dk.Parseko Vicent Kone, amewaasa watumishi wa umma kuwa wasiwe wepesi wa kudai haki zao, bali kwanza watimize wajibu wao kikamilifu kwa madai kwamba haki na wajibu huambatana pamoja.

Dk.Kone ametoa usia huo wakati akizungumza kwenye kilele cha sherehe za sikukuu ya wafanyakazi (Mei Mosi) mwaka huu, zilizofanyika kimkoa katika uwanja wa Namfua mjini hapa.

Alisema wafanyakazi wahakikishe wanatekeleza majukumu yao kwa mujibu wa mikataba yao ya kazi na kwa njia hiyo, watakuwa wamejijengea mazingira mazuri ya kudai haki zao kwa mwajiri.

Aidha,katika hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Mkuu wa wilaya ya Singida, Saidi Alli Amanzi, Dk.Kone alisema

Sherehe za sikukuu ya wafanyakazi duniani (Mei Mosi) mkoa wa Singida zafana.

Mkurugenzi mtendaji wa halmshauri ya wilaya ya Iramba mkoa wa Singida, Halima Mpita (wa kwanza kushoto akishirikiana na viongozi wa ngazi mbali mbali mkaoni Singida, kuimba wimbo wa mshikamano kwenye kilele cha sherehe za wafanyakazi duniani (mei mosi) zilizofanyika jana kwenye uwanja wa Namfua mjini hapa.
Kaimu mkuu wa mkoa wa Singida, Saidi Alli Amanzi (wa pili kushoto) akishiriki kuimba wimbo wa mshikamano kwenye kilele cha sherehe za wafanyakazi duniani (mei mosi) zilizofanyika jana kwenye uwanja wa Namfua mjini Singida.
Baadhi ya wafanyakazi wa TANROADS mkoa wa Singida wakiongozwa na meneja wao mhandisi Leonard Kapongo (katikati mbele anayepiga makofi) wakishiriki maandamano ikiwa ni sehemu ya sherehe ya sikukuu za wafanyakazi duniani zilizofanyika kwenye uwanja wa Namfua mjini hapa.