Saturday, December 31, 2011

Mkuu wa kanisa KKKT nchini Alex Malasusa(kulia), akiwa na Askofu wa kanisa hilo Dayosisi ya kati, Singida, akiwa amesimama mbele ya msalaba wa Yubile ya miaka 100 tangu kuanzishwa kwa kanisa hilo Mkoani Singida, mwaka 1911, mbele ya msalaba ni mti mkubwa uliotumika kama kanisa la kwanza,ambapo watu wanne mwaka huo walibatizwa hapo na wamisionari Leipzing kutoka nchini Ujerumani.

Mmoja wa Wachungaji wa kanisa hilo kutoka Ujerumani, akitumia sherehe hizo kubatiza mtoto katika eneo lililotumiwa kwa mara ya kwanza na Wamisionari mwaka 1911, kwa kutumia jiwe lililotunzia maji ya ubatizo,(kushoto) ni askofu mkuu wa KKKT nchini, Alex Malasusa.


Askofu mkuu wa KKKT Alex Malasusa (kulia),akiwa amesimama na Askofu wa Dayosisi ya kati, Eliufoo Sima, mbele ya msalaba uliojengwa mbele ya mti (nyuma) ambao ulitumiwa na wamisionari kutoka Ujerumani, kama kanisa mwaka 1911, ambapo watu wazima wanne walibatizwa

ASKOFU mstaafu wa Kanisa la KKKT, Dayosisi ya kaskazini, iliyopo Mkoa wa Kilimanjaro, Erasto Kweka, amewataka waumini wa dini na wananchi kwa ujumla kufanya kazi kwa bidii, ili kujiletea maendeleo.

Amesema hayo,kwenye sherehe za Jubile ya miaka mia moja ya KKKT, Dayosisi ya kati, ambazo kilele chake kitafikia leo(Jumapili),eneo la kitovu cha kanisa hilo, katika kijiji cha Ruruma, kilichopo Iramba,Mkoani Singida.

Wageni mbalimbali, wakiwemo wachungaji,maaskofu na wengine kutoka nje ya nchi,wamealikwa kwenye sherehe hizo,baadhi wakiwemo kutoka barani Ulaya na nchini Marekani, kutokana na umuhimu na mchango wao katika kueneza Injili, Dayosisi ya kati.

Askofu wa Dayosisi ya kati, Eliufoo Sima, amesema Wamisionari wa kwanza eneo hilo ni Leipzing Lutheran la Ujerumani 1911-1917,baadaye Augustina la Marekani mwaka 1926-1958, kisha kanisa likaendeshwa na wazalendo kuanzia mwaka 1958 hadi sasa.

No comments:

Post a Comment