Thursday, May 22, 2014

Shanta yatoa leseni, Mtaji, huku Tan Discovery yakabidhi vifaa kwa kikundi cha uchimbaji wa Dhahabu cha Aminika Singida.

Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida Manju Msambya akizungumza na wananchi wa kijiji cha Sambaru kwenye hafla hiyo ya makabidhiano ya leseni tatu.
Naibu Waziri wa Nishati na madini Steven Maselle akizungumza na wananchi wa kijiji cha Samabru Wilaya ya Ikungi Mkoa wa Singida wakati wa makabidhiano ya leseni tatu kwa wanakikundi cha Aminika Ltd.
Katibu wa kikundi cha Aminika Ltd akimkabidhi zawadi ya Mbuzi jike Naibu Waziri wa Nishati na madini Steven Maselle.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Steven Maselle akimkabidhi Mmoja ya wanakikundi Aminika Ltd cha kijiji cha Mang’onyi Wilayani Ikungi Sprian Danford ,moja ya leseni tatu za uchimbaji wa madini ya dhahabu zilizotolewa na Kampuni ya Shanta Mining Ltd, katika hafla fupi za makabidhiano iliyofanyika Kijiji cha Sambaru.

Kamanda wa UVCCM kata ya Kindai akabidhi vifaa vya michezo kwa vijana.

Kamanda wa (UVCCM) Kata ya Kindai, Omary Kinyeto (kushoto) akimkabidhi vifaa kwa Manahodha wa timu za soka ya Mperani Fc, Mahembe Fc, Munangi Boys na Kindai Boys  wakati wa hafla fupi ya kukabidhi vifaa kwa timu nne kwenye ofisi ya CCM ya Kata ya Kindai Manispaa Singida .
Kamanda wa (UVCCM) Kata ya Kindai, Omary Kinyeto akizungumza na vijana ofisi ya CCM Kata ya kindai Manispaa ya Singida.


VIJANA nchini wametakiwa kutambua kuwa hakuna biashara yenye kuingiza fedha nyingi popote duniani na kwa muda mfupi wa dakika tisini kama biashara ya kucheza mpira.

Changamoto hiyo imetolewa juzi mjini hapa na Kamanda wa Umoja wa Vijana (UVCCM)wa Kata ya Kindai Omary Salum ( Kinyeto) wakati akizungmza kwenye hafla fupi ya kukabishi vifaa vya michezo kwa timu nne za kata hiyo zitakazoshiriki ligi ya Kamanda Cup.

Kinyeto alisema kwa kutambua hivyo, vijana wamehimizwa kuzingatia michezo na kuithamini ili kupata ajira yenye kuingiza kipato kikubwa duniani kwa haraka zaidi.

“Ndugu zangu mimi haya mafanikio niliyonayo sasa ni kutokana na kucheza mpira, mimi nilikuwa mlinda mlango mahiri , kwa hiyo msinione nafanya haya mkadhani nafanya ilimradi tu, hii kitu mpira iko ndani ya damu yangu.” Alisema Kinyeto.

Aidha alisema anajitoa kwa hali na mali katika kuisaidia timu ya soka ya Singida United ambayo iko kwenye mashindano kituo cha Shinyanga, na kuwaomba wadau wengine kuisaidia timu hiyo.

Kinyeto alisema vifaa hivyo ambavyo ni

Waandishi wa habari wapewa changamoto ya ubunifu na kujituma.

Baadhi ya waandishi wa habari mkoa wa Singida,wakifuatilia mada   zilizokuwa zinatolewa na maafisa kutoka Mfuko wa Habari Tanzania (TMF) juu ya kuchangamkia ruzuku zinazotolewa na mfuko huo.
Afisa kutoka Mfuko wa Waandishi wa Habari Tanzania (TMF) Alex Kanyambo akitoa mada yake juu ya umuhimu wa vilabu vya waandishi wa habari kuchangamkia ruzuku zinazotolewa na TMF.Wa kwanza kushoto ni Afisa Habari wa TMF,Japhet Sanga na katikati ni Mwenyekiti wa klabu ya waandishi wa habari (Singpress) mkoa wa Singida,Seif Takaza.
Afisa kutoka Mfuko wa Waandishi wa Habari Tanzania (TMF) Alex Kanyambo akitoa mada yake juu ya umuhimu wa vilabu vya waandishi wa habari kuchangamkia ruzuku zinazotolewa na TMF.Wa kwanza kushoto ni Afisa Habari wa TMF,Japhet Sanga na katikati ni Mwenyekiti wa klabu ya waandishi wa habari (Singpress) mkoa wa Singida,Seif Takaza.

WAANDISHI wa Habari mkoani Singida, wamehimizwa kuondokana na uandishi habari wa mazoea na badala yake wabadilike na kuwa wabunifu ili kazi yao iweze kukidhi viwango vya wakati uliopo.

Changamoto hiyo imetolewa hivi karibuni na mwandishi wa habari mkongwe, Eda Sanga wakati akizungmza kwenye semina ya Uhabarisho wa Mfuko wa Habari Tanzania (Tanzania Media Fund TMF) kwa waandishi wa habari mkoa wa Singida.

Amesema waandishi wa habari ule wa business as usual, haufai umepitwa na wakati unadumaza maendeleo ya mhusika.

amesema uandishi wa habari kwa sasa umetakiwa mwandishi wa habari ujitume, uwe mbunifu, ufanye uchunguzi wa kina ili ukiandika habari watu wakupongeze au wakusifu.

“Ninyi mnapaswa katika kutekeleza majukumu yenu muiangalie Singida kwa upana wake. Ni kero gani zinawasibu wananchi. Nini kifanyike ii kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu kero hizo”

Awali Afisa Habari wa TMF makao makuu,Japhet Sanga amewahimiza waandishi wa habari nchini kujenga utamaduni wa kuomba

Monday, May 19, 2014

SSRA wahimizwa kujituma ili mifuko ya hifadhi ya jamii itoe taarifa sahihi kwa wanachama.

Mkuu wa Wilaya ya Singida, Queen Mlozi.

MKUU wa Wilaya ya Singida,Queen Mlozi ameihimiza Mamlaka ya Usimamizi wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) kujituma zaidi katika kuhakikisha mifuko mbalimbali ya hifadhi ya jamii inatoa taarifa sahihi kwa wananchi na wanachama watarajiwa juu ya haki zao kabla hawajajiunga.

Amedai kwamba wananchi na wanachama watarajiwa wakizitambua vema haki zao hizo watakuwa wamejengewa uwezo wa kufikia maamuzi sahihi katika kujiunga na mifuko hiyo ambayo Tanzania,ipo sita.

Mlozi ametoa rai hiyo hivi karibuni wakati akifungua semina ya siku moja iliyohusu uhabarisho wa shughuli za Mamlaka ya Usimamizi wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) kwa wadau mbalimbali wa mkoa wa Singida.

Amesema kwa vile SSRA inasimamia mifuko yote hiyo sita ya hifadhi ya jamii ambayo ina mifuko tofauti tofauti ina jukumu kubwa la kusimamia mifuko hiyo inatoa taarifa za haki wanazopaswa kupewa wananchi na wanachama watarajiwa kabla ya kujiunga.

“Tumeshuhudia baadhi ya mifuko ikipewa fursa ya kuwaeleza wananchama watarajiwa shughuli zao na mafao wanayoyatoa,pindi watumishi hao wapya wakijiunga nayo”,amesema Mlozi na kuongeza;

“Hiyo ni hatua nzuri lakini usimamizi na ufuatiliaji zaidi unahitajika kutoka mamlaka ya usimamizi kwani mifuko hii ya hifadhi ya jamii inatofautiana kwa maana ya uzoefu,mtandao wa ofisi za matawi na watumishi na hata kwenye suala la uwekezaji”.

Akiijengea nguvu hoja yake hiyo, amesema suala la kutoa taarifa juu ya haki ya mwanachama mtarajiwa ni kwa mujibu wa sheria na 8 (nane) ya mwaka 2008 na kama ilivyorekebishwa mwaka 2012.

Amesema lengo kuu la sheria hiyo ni

Elekezeni nguvu zenu kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa – Tindu Lissu.

Mbunge Tundu Lissu, Singida Mashariki

MBUNGE wa Jimbo la Singida mashariki kupitia tiketi ya CHADEMA, Tundu Lissu amewataka wananchama wa chama hicho kata ya Iseke tarafa ya Ihanja wasibweteke na ushindi wa udiwani walioupata katikati ya mwaka jana, na badala yake waelekeze nguvu zao zote kwenye uchanguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika oktoba mwaka huu.

Amesema ushindi huo utakuwa na maana zaidi endapo CHADEMA itazoa nafasi zote za uenyeviti wa vitongoji na vijiji katika wilaya yote ya Ikungi, mkoa wa Singida.

Tundu alitoa wito huo hivi karibuni wakati akizungumza kwenye hafla ya kupongezana kwa ushindi wa nafasi ya udiwani wa kata ya Iseke, uliopatikana Juni mwaka jana kwenye uchaguzi mdogo.Hafla hiyo iliyofana ilifanyika kwenye bwalo la shule ya sekondari Iseke.

Amesema Halmashauri ya wilaya ya Ikungi,ina madiwani 35 kati yao wa CHADEMA ni watatu tu idadi ambayo inachangia kutokuwepo na uwiano mzuri katika kutoa mchango kwenye vikao vya maamuzi.

“Kwa hali hii ukiangalia idadi hiyo utabaini kwamba bado kazi kubwa ipo mbele ya CHADEMA ya kuhakikisha inakuwa na idadi inayoshabiriana na ya CCM au kuwa na idadi kubwa zaidi ya CCM lengo hasa iwe ni kuwa na idadi kubwa zaidi ya CCM”,alifafanua Mbunge huyo.

Aidha,Tundu amesema ushindi walioupata wana CHADEMA Iseke ni ukombozi mkubwa kwao kwa sababu
Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Dkt, Charles Kimei.

BENKI ya CRDB   imetenga kiasi cha zaidi ya shilingi  bilioni  moja katika bajeti  yake mwaka huu kwa ajili ya kuchangia katika  shughuli  mbalimbali za uboreshaji wa  huduma za kijamii  nchini.

Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Dkt, Charles Kimei amesema hayo kwenye hafla ya kukabidhi visima kwa shule tatu za msingi na sekondari mkoani Singida vilivyofadhiliwa na benki hiyo.

Dkt. Kimei amesema fedha zilizotumika kwa shughuli hiyo ni sehemu ya  zaidi ya shilingi bilioni moja  ikiwa  ni asilimia  moja ya faida  inayotengwa  na benki hiyo kila mwaka kusaidia huduma za jamii.

Amesema mwaka  jana, benki ya  CRDB ilipata faida ya zaidi ya shilingi bilioni 100 hivyo kulazimika kutenga kiasi hicho cha fedha  kama ilivyo sera yake ya kurejesha sehemu ya faida kwa wateja.

Kutokana na hali hiyo, Dkt.  Kimei ametoa wito kwa wadau wengine kuendelea kuunga mkono juhudi za serikali katika kuboresha huduma za kijamii hususa ni maji safi na salama ambayo bado ni changamoto kubwa Vijijini.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Yahaya Nawanda, ameishukuru benki hiyo kwa

Dereva wa Halmashauri Iramba afia gesti akifanya mapenzi.

DEREVA wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba mkoani Singida Juma Juma (52) amefariki dunia wakati akifanya mapenzi na mwanamke mhudumu wa baa kwenye nyumba ya kulala wageni.
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Singida,SACP Geofrey Kamwela amesema tukio hilo limetokea mei tatu mwaka huu saa nane za usiku chumba no.S.2 nyumba ya kulala wageni ijulikanayo kwa jina la Top Life New Kiomboi mjini.
Amesema siku ya tukio,dereva Juma saa sita za usiku alimwaga mpangaji wake kuwa anatoka mara moja na hatachelewa kurudi nyumba kwa kwa hiyo alifunga mlango wa mbele ya nyumba.
Amesema kuwa saa mbili baadaye Juma alionekana akiwa baa iliyoko kwenye nyumba hiyo la kulala wageni iliyoko umbali wa mita 50 kutoka nyumbani kwake.
“Muda huo Juma alionekana akiwa na mmoja wa wahudumu wa baa hiyo alitwaye Agness Mayo (32) anayesadikika kuwa na uhusinao wa kimapenzi na Juma.”,amesema.
Kamwela amesema mhudumu huyo wa baa, mpenzi wa Juma,

Sunday, May 11, 2014

Mzee aishi wodini kwa miaka 45 tangu Januari mosi mwaka 1971.


Mzee Abdi Nkhambi Lanjui (75) akiwa wodi namba nne katika hospitali ya mkoa mjini Singida. Mzee Lanjui mzaliwa wa kijiji cha Mhintiri tarafa ya Ihanja, aliyekuwa dereva wa kampuni ya mamlaka ya Pamba Mwanza, alipata ajali katikati ya mwaka 1968 na kulazwa katika hospitali ya Sekoture Mwanza na baadaye mwishoni mwa mwaka 1970,alihamishiwa hospitali ya mkoa wa Singida, ambako anaishi hadi sasa. Ajali hiyo ilisababisha kukatika mawasiliano kati ya kuanzia kiunoni na kushuka chini ambako kumepooza na sasa kuna vidonda na sehemu ya mwili juu ya kiuno, bado inafanya kazi.

MZEE Abdi Nkhambi Lanjui (75) ambaye ameishi wodini kwa miaka 45 sasa ameiomba serikali,Asasi na jamii kwa ujumla kumsaidia huduma ya chakula kwa madai kwamba hana ndugu wa kumsaidia huduma hiyo.

Akizungumza na SINGIDA YETU BLOG hivi karibuni, Mzee Abdi ambaye kwa sasa hawezi kabisa kunyanyuka kitandani amesema kuwa kwa miaka mingi uongozi wa hospitali ya mkoa umemhudumia vizuri chakula cha kutosha.

 Akifafanua amesema baada ya hospitali hiyo kusitisha huduma ya chakula kwa wagonjwa amekuwa omba omba na maisha yake yamebaki ya mlo moja kwa siku.


 “Kwa vile siwezi kunyanyuka kitandani na sina ndugu ye yote nimekuwa nikiwaomba msaada manesi na watumishi wengine wa hospitani hapa na nashukuru sana hawaniangushi wamekuwa wakinisaidia bila kuchoka na wananiwezesha kupata angalau mlo wa siku moja”,amesema.

Mzee Abdi pia ametumia fursa hiyo kuomba msaada wa fedha na msindikizaji kwa ajili ya kwenda hospitali ya KCMC Moshi mkoa wa Kilimanjaro ili akapatiwe huduma ya matibabu.

 “Sababu ya mimi kugeuza wodi kuwa makazi yangu ya kudumu ni kutokana na ajali iliyosababisha

Waliopoteza maisha katika ajali Ikungi waombewa.

Diwani wa kata ya Mungaa Matheo Alex akizungumza kwenye hafla ya sala kuwaombea watu waliopoteza maisha baada ya kugongwa na basi la kampuni ya summary aprili 28 mwaka huu.Sala hiyo maalum,imefanyika jana eneo ilikotokea ajali hiyo.
Mke wa marehemu mwenyekiti wa kijiji cha Utaho Paulo Hamisi (41) aliyefariki dunia kwa kugongwa na basi la Summry Aprili 28 mwaka huu.
Baadhi ya wananchi wa kijiji cha Utaho tarafa ya Ihanja wilaya ya Ikungi,waliohudhuria sala maalum ya kuwaombea ndugu zao 15 waliopoteza maisha baada ya kugongwa na basi la kamuni ya summry Aprili 28 mwaka huu.

WAUMINI wa madhehebu mbalimbali ya dini wakazi wa kata ya Utaho tarafa ya Ihanja wilaya ya Ikungi mkoa wa Singid hivi karibuni wameungana na kufanya sala maalum katika kuwaombea ndugu zao 15 waliofariki dunia baada ya kugongwa na basi la kampuni ya summary.

Sala hiyo maalum imefanyikia kando kando ya barabara kuu itokayo Singida – Dodoma eneo la kambi la kampuni ya SIETCO kijiji cha Utaho  ajali hiyo mbaya ilitokea Aprili 28 mwaka huu saa 2.45 usiku.

Akihubiri kwenye hafla hiyo ya sala,Mchungaji wa kanisa la Free Pentekoste kijiji cha Utaho,Francis Pius amewataka waumini wa dini mbalimbali na wananchi kwa ujumla wazingatie sheria za usalama barabarani kama njia mojawapo ya kupunguza ajali zinazochangia watu kupoteza maisha pamoja na mali zao.

Amesema baada ya kujengwa barabara kwa kiwango cha lami ajali zimeongezeka mara dufu kutokana na baadhi ya watu kutokuwa waangalifu na kwa kiasi kikubwa kutokutii sheria za usalama barabara.

“Tabia ya watu kutokuzingatia sheria za usalama babarani inachangia mwenye baiskeli kumdharau mwenye pikipiki na mwenye pikipiki kumdharau mwenye gari kinachotokea ni kwamba wananyang’anyana barabara na kusababisha ajali zinazopoteza maisha ya watu na mali zao”alifafanua zaidi Mchungaji

Mchungaji huyo amesema makosa ya aina hiyo,hayapaswi kufanywa na binadamu mwenye akili tofauti na mnyama kwa hiyo tunapaswa kuzingatia matumizi sahihi ya barabara ili kupunguza ajali.

 “Tuwe makini wakati wa kuvuka barabara na pia wakati tukivusha mifugo yetu tukifanya dharau barabarani kuwa dereva wa gari,pikipiki na hata baiskeli eti atakuona ili asikugonge tutakosea sana kwa sababu tutakuwa tunasababisha ajali kila kukicha”,amesema Mchungaji Francis.

Akifafanua zaidi,amesema

Singpress yatoa msaada wa zaidi ya laki nane kwa Walemavu Siku ya Uhuru wa Habari.

Mwalimu mkuu shule ya msingi mchanganyiko Ikungi waliya ya Ikungi, Olivary Kamilly, akizungumza ofisini kwake na wanachama wa klabu ya waandishi mkoa wa Singida, ambapo kwa kuadhimisha Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani, walitoa msaada wenye thamani ya zaidi ya shilingi laki nane kwa wanafunzi walemavu wakiwemo Albino katika shule hiyo.
Mwalimu mkuu wa shule ya msingi mchanganyiko Ikungi wilaya ya Ikungi, Olivary Kamilly (wa pili kulia) akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wananchama wa Singida Press Club (Singpress).Wa tatu kulia ni mwenyekiti wa Singpress, Seif Takaza na wa kwanza kushoto ni mweka hazina wa Singpress na anayefuatia ni makamu mwenyekiti Damiano Mkumbo.
Mwanafunzi wa darasa la sita katika shule ya msingi mchanganyiko Ikungi wilaya ya Ikungi, Julius Charles, akionyesha umahiri wake katika kutumia vidole vya mguu wa kulia kuandika viruzi herufi kubwa na ndogo.Mwanafunzi huyo ambaye hana mikono, anafanya vizuri katika masomo yake.
Makamu mwalimu mkuu wa pili kitengo cha walemavu katika shule ya msingi mchanganyiko Ikungi,Donard Adamu Bilali, akizungumza na wanachama wa Singida Press Club, waliotembelea shule hiyo na kutoa msaada wa zaidi ya shilingi laki nane, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari.

WANACHAMA wa klabu ya waandishi wa habari (Singpress) mkoa wa Singida wameadhimisha siku ya uhuru wa vyombo vya habari duniani kwa kutoa msaada wenye thamani ya zaidi ya shilingi laki nane kwa wanafunzi wenye ulemavu mbalimbali wakiwemo wenye ulemavu wa ngozi (albino).

Wanafunzi walionufaika na msaada huo ambao ni pamoja na sembe kilo 100,sukari kilo 50 na mchele kilo 150 ni wa shule ya msingi mchanganyiko Ikungi wilaya ya Ikungi mkoani Singida.

Akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi msaada huo,Mwenyekiti wa Singpress,Seif Takaza amesema katika kuadhimisho ya siku ya uhuru wa vyombo vya habari duniani mwaka huu,klabu ya Singpress kwa dhati kabisa imeamua kushirikiana na wanafunzi walemavu wa shule ya msingi mchanganyiko Ikungi.


Akifafanua,Takaza amesema lengo na madhumuni ni kuwapatia wanafunzi walemavu zawadi na msaada mbalimbali ya kibinadamu ili waendelee kuamini kuwa na wao ni sehemu ya Watanzania.Vile vile kuwapunguzia makali ya maisha.

“Pia tunatarajia wanafunzi na walimu wa shule hii ya Ikungi,leo wanaweza kutumia fursa ya uwepo wetu kupaza sauti zao kwa kutoa chanagamoto na kero zinazowakabili,ili sisi tuweze kutekeleza jukumu letu la kuyaanika hadharani na jamii na serikali kwa ujumla iweze kuyatafutia ufumbuzi wa kudumu”amesema Takaza ambaye ni mwandishi wa habari wa gazeti la Mtanzania kwa mkoa wa Singida.

Akiongezea nguvu hoja yake hiyo,amesema waandishi wa habari wakiwemo wa Singpress jukumu lao ni

Sunday, May 4, 2014

Dkt. Kone awahimiza Wanafunzi kusoma masomo ya Sayansi.

Mkuu wa mkoa wa Singida,Dk.Parseko Vicent Kone, akizungumza kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani (mei mosi),yaliyofanyika kimkoa katika uwanja wa namfua mjini Singida (01/5/2014).Maadhimisho ya mwaka huu kwa mkoa wa Singida yalihudhuriwa na watumishi wa umma na wananchi wachache ukilinganisha na miaka iliyopita.Kushoto ni mratibu wa RAAWU mkoa wa Singida na mwenyekiti wa kilele cha maadhimisho ya  sherehe ya siku kuu ya wafanyakazi duniani (Mei mosi mwaka huu).
Mkuu wa mkoa wa Singida Dk.Parseko Vicent Kone.(wa tatu kulia) akishiriki kuimba wito wa mshikamano wa wafanyakazi.Wa kwanza kulia ni Misholi (wa pili kulia) ni Blandina Marwa wenyekiti wa sherehe za mei mosi mkoa wa Singida na mratibu wa RAAWU mkoani Singida.
Mkuu wa mkoa wa Singida,Dk.Parseko Kone, akimkabidhi cheti mfanyakazi bora wa mwaka huu wa TANESCO mkoani Singida ikiwa ni sehemu ya kilele cha maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani – Mei Mosi.Pamoja na cheti, mfanyakazi huyo Ps wa menejaTANESCO makao makuu mkoani Singida, pia alizawadiwa Tv screen yenye thamani ya shilingi laki nane.
Baadhi ya viongozi na watendaji wa serikali waliohudhuria kilele cha maadhimisho ya wafanyakazi duniani yaliyofanyika kimkoa kwenye uwanja wa Namfua mjini Singida.Mwenye miwani ni hakimu mfawidhi mkoa wa Singida,Minde.
Baadhi ya wafanyakazi wa TANROADS mkoa wa Singida,waliohudhuria kilele cha maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani (mei mosi) yaliyofanyika kwenye uwanja wa Namfua mjini Singida.

MKUU wa Mkoa wa Singida,Dk.Vicent Kone amewahimiza walimu,wazazi na walezi kuongeza juhudi katika kuwashawishi wanafunzi wengi zaidi kusomea masomo ya sayansi ili kama si kupunguza basi kulimaliza kabisa tatizo la uhaba wa walimu wa sayansi.

Dk.Kone ametoa wito huo hivi karibuni wakati akizungumza kwenye kilele cha sherehe za siku kuu ya wafanyakazi (Mei Mosi) duniani zilizofanyika kimkoa katika manispaa ya Singida.

Amesema kumekuwepo na kilio cha muda mrefu cha uhaba wa walimu wa masomo ya sanyansi katika shule karibu zote za sekondari mkoani na Tanzania kwa ujumla.


Amesema mwarubaini wa kulimaliza tatizo hilo ni kushawishi wanafunzi wengi kusoma masomo ya sayansi ili watakapohitimu warudi kuja kufundisha katika shule za hapa mkoani.

Aidha,Dk.Kone amewasisitiza wananchi waendelee  kuiunga mkono serikali katika kuimarisha na kuboresha sekta ya elimu nchini hususani katika kukamilisha ujenzi wa vyumba vitatu vya maabara ya masomo ya kemia,fizikia na baolojia.

Katika hatua nyingine,Mkuu huyo wa mkoa amesema kuwa madeni ya wafanyakazi wakiwemo walimu ya zaidi ya shilingi 2.2 bilioni,yanaendelea kuhakikiwa ili yaweze kulipwa.

Kwa upande wa wafanyakazi katika risala yao wamewaomba

Mkapa awataka watanzania kuandika katiba itakayodumisha amani.

Rais mstaafu wa awamu ya tatu,Benjamen Williamu Mkapa (mwenye fimbo), akipokewa na mkuu wa mkoa wa Singida,Dk.Parseko Kone (wa pili kulia) kwenye viwanja vya zahanati ya kijiji cha Senenemfuru tarafa ya Mtinko wilaya ya Singida.Wa kwanza kushoto ni mwenyekiti CCM wilaya ya Singida, Narumba Hanje na anayefuatia ni mkuu wa wilaya ya Singida, Queen Mlozi.

Rais mstaafu Mkapa ambaye pia ni msarifu wa taasisi ya Benjamin William Mkapa HIV/AIDS foundation (BMAF),jana amekabidhi nyumba 30 za watumishi wa afya mkoani Singida zilizogharimu zaidi ya shilingi 1.9 bilioni.
Rais mstaafu Benjamin William Mkapa, akivishwa mgorole na wazee wa kata ya Ughandi wilaya ya Singida, muda mfupi kabla ya kuzungumza na wananchi waliohudhuria hafla ya kukabidhi nyumba 30 za watumishi wa zahanati mkoa wa Singida.
Rais mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin William Mkapa, akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi nyumba 30 za watumishi wa zahanati,zilizojengwa na taasisi yake.Hafla hiyo imefanyika kwenye viwanja vya zahanati ya kijiji cha Senenemfuru wilaya ya Singida.
Afisa mtendaji mkuu wa taasisi ya Benjamin William Mkapa HIV/AIDS foundation (BMAF), Dk.Ellen Mkondya Senkoro,akitoa taarifa yake kwenye hafla ya kukabidhi nyumba 30 za watumishi wa zahanati zilizojengwa na taasisi hiyo ya Mkapa.
Mkuu wa mkoa wa Singida, Dk.Parseko Kone, akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi nyumba 30 za watumishi wa zahanati zilizojengwa na taasisi ya Benjamin Mkapa.Hafla hiyo imefanyika kwenye viwanja vya zahanati ya Senenemfuru wilaya ya Singida.
Rais mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin William Mkapa, akipeana mkono na mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya ujenzi ya C.F.Bulilders LTD ya jijini Mwanza, Ferdnard Chacha, muda mfupi baada ya kukagua nyumba ya kuishi mtumishi wa zahanati ya kijiji cha Senenemfuru, iliyojengwa na taasisi ya Benjamin William Mkapa.

RAIS Mstaafu wa awamu ya tatu,Benjamin William Mkapa amewaasa Watanzania kuwa makini na waagalifu wakati huu wa mchakato wa upatikanaji wa katiba mpya ili lengo la kupata katiba itakayoendelea kudumisha amani,upendo,utulivu na ushirikiano liweze kufikiwa.

Mkapa ametoa wito huo hivi karibuni wakati akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi nyumba bora 30 za watumishi wa vituo vya huduma ya afya mkoani hapa, nyumba hizo zimejengwa kwa zaidi ya shilingi 1.9 bilioni na taasisi ya Benjamin William Mkapa HIV/AIDS foundation (BMAF).

Amesema kuwa kunaweza kuwepo kwa kuhitalifiana lakini kamwe kusiwepo na kupigana au kufarakana kwa namna yoyote ile.


“Vyovyote mchakato wa katiba utakavyoishia tuhakikishe tunabaki na amani na utulivu wetu kwa ajili ya ustawi wa nchi yetu tuhitalifiane bila kupigana”,alisisitiza.

Alisisitizia zaidi hoja yake hiyo,Mkapa amesema Watanzania wanapaswa kwa pamoja kuhakikisha hawajiharibii nchi yao na zaidi wahakikishe kizazi cha sasa na kile kijacho kinaendelea kuwaenzi waasisi wetu kwa uadilifu mkubwa.

Kuhusu kukabidhi nyumba hizo 30 bora za watumishi wa afya,amesema anafarijika kufahamu kwamba wananchi wanaohudumiwa na zahanati 15 ambapo

Thursday, May 1, 2014

Wakulima wapongezwa kwa kupanua kilimo cha mazao ya chakula.

MKUU wa Mkoa wa Singida,Dk.Parseko Vicent Kone amewapongeza wakulima kwa kuongeza juhudi ya kupanua kilimo cha mazao ya chakula na biashara msimu huu ikilinganishwa na misimu iliyopita.

Dk.Kone ametoa pongezi hizo wakati akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi wa chanjo kimkoa,iliyofanyika katika kijiji cha Mtinko jimbo la Singida kaskazini.

Amesema juhudi hizo za wakulima pamoja na kiwango cha mvua iliyonyesha cha mm 562 msimu huu kunaashiria kutakuwa na mavuno mengi mwaka huu.

Akiijengea nguvu hoja yake hiyo,Dk.Kone amesema hadi machi mwaka huu,jumla ya hekta 457,468 za mazao ya chakula na hekta 263,709 za mazao ya biashara zimelimwa.

“Mtarajio ni kuvuna tani

Viazi vitamu ni mkombozi wa kiuchumi kwa wakulima.

VIJANA wa wilaya ya Ikungi mkoani Singida wamehimzwa kuondokana na uvivu na badala yake waelekeze nguvu zao katika kilimo cha kibiashara cha viazi vitamu ili waweze kujikomboa kiuchumi.

Changamoto hiyo imetolewa na mkulima na mfanyabiashara wa zao la viazi vitamu na mkazi wa kijiji cha Nkuninkana,Ibrahimu Kilu (34) wakati akizungumza na MOblog juu ya kilimo hicho cha viazi vitamu ambacho pia ni  zao la chakula.

Amesema kuwa zao la viazi vitamu ambalo miaka ya nyuma lilikuwa ni zao la ziada (halikupewa umuhimu unaostahili) hivi sasa zao hilo lina soko zuri ndani na nje ya nchi.

“Viazi vitamu kutoka wilaya yetu ya Ikungi vinakimbiliwa sana na wafanyabiashara kutoka mkoa wa Dodoma,Morogoro,Dar-es-salaam,Tanga na mikoa mingine nchini, pia kuna wafanyabiashara wanatoka Zambia na Comoro Kwa hali hiyo soko la zao hilo ni kubwa na linalipa vizuri”,alifafanua Ibrahimu.

Ibrahimu amesema toka aanze kulima zao hilo kibishara miaka mitano iliyopita limemwezesha kujenga nyumba bora na ya kisasa yenye choo ndani,amenunua pikipiki,anao mtaji wa kutosha na anasomesha watoto wake bila shida.

“Kilimo cha kibiashara cha viazi vitamu kina faida nyingi kinainua mhusika kiuchumi na pia uhakika wa kukabiliana na makali ya njaa unakuwepo.Mfano mzuri ni kwamba mimi msimu uliopita nililima uwele katika mashamba yangu yote na nilipata chakula cha kutosha kwa miaka miwili mfululizo”,amesema na kuongeza;

“Msimu huu,kwa sababu nina chakula cha kutosha mashamba yote nimelima viazi vitamu kwa lengo la kuboresha uchumi wa familia yangu matarajio ni kwamba natarajia kuingiza mapato ya zaidi ya shilingi milioni tatu”.

Akifafanua zaidi, Ibrahimu amesema faida ya kilimo cha viazi vitamu ni kwamba msimu huu