Friday, May 17, 2013

Mkuu wa Wilaya ya Singida aitisha mkutano wa hadhara kuzungumzia mradi wa umeme wa upepo.

Mwenyekiti wa kijiji cha Unyambwa manispaa ya Singida, Athumani Omari Njera akifungua mkutano wa hadhara ulioitishwa kwa ajili ya mkuu wa wilaya ya Singida (hayupo kwenye picha) kuzungumza na wananchi wa kijiji hicho kuhusu mradi wa kufua umeme wa upepo.
Mkuu wa wilaya ya Singida, mwalimu Queen Mlozi akizungumza na baadhi ya wananchi wa kijiji cha Unyambwa kuhusu mradi wa kufua umeme katika kata ya Unyambwa manispaa ya Singida.
Mkulima wa kijiji cha Unyambwa Juma Mwiru akichangia hoja ya mradi wa kufufua umeme wa upepo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika kitongoji cha Ijanuka manispaa ya Singida.
Baadhi ya wakazi wa kijiji cha Unyambwa waliohudhuria mkutano wa hadhara ulioitishwa na mkuu wa wilaya ya Singida, Mwalimu Queen Mlozi kuzungumza nao kuhusu mradi wa kufua umeme wa upepo.

No comments:

Post a Comment