Thursday, October 8, 2015

Magufuli amshawishi MO kujenga kiwanda Singida ili kutoa fursa ya ajira.

Mgombea urais kupitia tiketi ya CCM, Dkt. John Pombe Magufuli akimwaga sifa kwa aliyekuwa Mbunge wa jimbo la Singida Mjini (Mbunge Mstaafu), Mohamed Dewji baada ya kutumikia vyema na kwa uadilifu kiti chake cha Ubunge jimboni humo wakati wa mkutano wa kampeni za mgombea urais huyo kwa tiketi ya CCM uliofanyika katika viwanja wa Peoples mjini humo.


PICHA 15 ZA MAGUFULI NDANI YA SINGIDA




MO atua Singida kushiriki mkutano wa kampeni za Urais.

Aliyekuwa Mbunge wa jimbo la Singida mjini, Mohammed Dewji akisalimiana na mmoja wa madiwani waliofika kumpokea mara tu baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Singida mjini pamoja na wasaidizi wake.
Aliyekuwa Mbunge wa jimbo la Singida mjini, Mohammed Dewji akiwa ameambatana na Mgombea Ubunge wa jimbo la Bumbuli, January Makamba ambaye pia ni mmoja wa wanakamati wa timu ya ushindi ya kampeni za Mgombea urais kupitia tiketi ya CCM, Dk.John Pombe Magufuli, wakielekea sehemu ya mapokezi mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege Singida mjini.
Aliyekuwa Mbunge wa jimbo la Singida mjini, Mohammed Dewji akilakiwa kwa furaha na watoto wanaoishi kwenye eneo la uwanja wa ndege Singida mjini.

Wednesday, October 7, 2015

Ajali ya basi la City Boys yaua 3, Singida, mwingine agongwa na Noah.1

Kamanda wa polisI Mkoani Singida (ACP) Thobias Sedoyeka (pichani)akizungumza na waandishi wa habari  juu ya kutokea kwa ajali ya basi la City Boys na kusababisha vifo vya watu watatu Wilayani Iramba  na mwingine kugongwa na Noah Singida vijijini.

WATU wanne wamefariki dunia Mkoani Singida baada ya kupata ajali ya kugongwa na basi la City Boys na mwingine Noah wakati wakivuka barabara eneo la Ulemo barabara kuu ya Singida- Nzega.

Kamanda wa polisi Mkoani Singida (ACP), Thobias Sedoyeka alisema ajaili hiyo imetokea jana majira ya 1:00 usiku katika kijiji cha Kitukutu Kata ya Ulemo, Tarafa ya Kinampanda ,Wilayani Iramba.

Alisema siku ya tukio, basi lenye namba za usajili T 846 CDU aina ya Scania  mali ya kampuni ya City Boys likitokea Jijini Dar es Salaam kwenda Kahama lilikuwa likiendeshwa na dereva Adam George (33) mkazi wa Dar es Salaam.

 Aidha alisema dereva huyo alipofika eneo na Kitukutu kutokana na kile kinachosadikiwa kuwa ni

DORIS MOLLEL FOUNDATION: Yakabidhi vitabu 200 kwa Shule ya Msingi Midamigha Ilongero SINGIDA.

Mwalimu wa taaluma wa shule Msingi Midamigha Ilongero, Singida akipokea vitabu hivyo kutoka taasisi ya Dmf wakati wa kukabidhi vitabu hivyo.
[SINGIDA] Taasisi inayoshughulikia na utetezi wa watoto njiti ya Doris Mollel ‘DORIS MOLLEL FOUNDATION’(Dmf)  mwishoni mwa wiki imekabidhi vitabu 200 kwa ajili ya kujifunzia  katika shule ya msingi Midamigha ilongero, singida.

Vitabu hivyo vitakuwa chachu na changamoto kwa wanafunzi wa shule hiyo ambapo watapata furasa za kujifunza mambo mbalimbali katika elimu yao.

Dmf imetoa vitabu hivyo ni kutokana na ufadhili wa taasisi ya Kituruki iitwayo Rhema Trust.

Taasisi ya Dmf  imekuwa mstari wa mbele katika harakati za kutetea watoto hasa watoto njiti wasipoteze maisha kutokana na kukosa vifaa vya kufanya watoto hao waweze kuishi na kufikia malengo kama watoto wengine ambao hawakuzaliwa na wakiwa njiti.

Msindai awatangazia neema mama ntilie, machinga, waendesha boda boda.

Mgombe Ubunge wa Jimbo la Singida Mjini (CHADEMA) Mgana Msindai, akizungumza na wafanyabiashara wa soko kuu mjini Singida wakati wa Mkutano wa kampeni kuomba ridhaa ya wananchi kumchagua kuwa Mbunge ili kuondoa kero ndogo ndogo za kutozwa ushuru kwa wamachinga na mama ntilie.

MGOMBEA Ubunge wa Jimbo la Singida Mjini (CHADEMA ) Mgana Msindai ameahidi kuondoa kero na kodi ndogondogo wanazotozwa wafanyabiashara wadogo wakiwemo mama ntilie.

Akizungumza jana kwenye  Mkutano wa Kampeni wa chama chake eneo la soko kuu, Msindai alisema mojawapo ya kero hizo ni pamoja na kusumbuliwa kwa kina mama lishe bila kujali ugumu wa maisha unaowakabili hivyo akichaguliwa ataziondoa kodi hizo mara moja.

“Hizi kero za mama ntilie kutozwa shilingi 20,000 kwa mwezi na meza ndogo ndogo za matunda na mboga mboga nitazifuta kwa kushirikiana na madiwani wenzangu wa Ukawa, kwani hii sio sheria kuu, ni sheria ndogo ndogo zinazotungwa na madiwani, sisi tutazifuta mara moja  ili watu hawa waweze kubadilika.”Alisema Msindai maarufu kwa jina la CRDB.

Hata hivyo ili kuendena na hadhi ya Manispaa, Msindai ameahidi kushirikiana na madiwani wenzake kujenga soko jipya la kisasa kwa kuvunja

Nitaondoa njaa, wakulima watatumia helkopta kumwagilia mashamba, nitajenga vituo maalumu vya Albino na wazee – Rungwe

Mgombea Urais wa CHAUMA,Hashim Rungwe katika pozi tofauti akihutubia wananchi wa Singida mjini jana.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha ukombozi wa Umma (CHAUMA) Hashim Rungwe akizungumza kwenye Mkutano wa Kampeni Mkoani  Singida, ambapo aliahidi kuwaondolea wananchi njaa.
Mgombea mwenza wa CHAUMA Issa Abas Husein nae akihutubia wananchi wa Singida mjini.
WANANCHI wakimsikiliza Mgombea Urais wa CHAUMA kwenye kituo cha stendi ya zamani Mjini Singida jana.