Friday, April 4, 2014

Queen Mlozi ashiriki operasheni ya kuondoa mawe makubwa yaliyokuwa yakitumiwa kuteka magari barabara kuu ya Singida-Dodoma.

Mkuu wa wilaya ya Singida,Queen Mlozi akipasua jiwe kubwa ili liweze kupandishwa kwenye lori kwa lengo kuondolewa kando kando ya barabara kuu ya Singida-Dodoma eneo la kijiji cha Kisaki manispaa ya Singida. Mawe hayo makubwa kwa kipindi kirefu yametumiwa na watu wanaodhaniwa ni majamabazi watekaji wa malori na kupora mali na fedha.
Mkazi wa kijiji cha Kisaki manispaa ya Singida, Juma akipasua jiwe kubwa lililokuwa likitumiwa na majambazi kwa ajili ya kuteka magari na kisha kupora abiria.
Askari Polisi, Jeshi na baadhi ya wakazi wa kijiji cha Kisaki manispaa ya Singida,wakipandisha jiwe kubwa kwenye lori. Zoezi hilo la kuondoa mawe makubwa kando kando ya barabara kuu ya Singida yaliyokuwa yakitumiwa na watu wanaodhaniwa ni majambazi katika kuteka magari na kupora abiria. Mawe hayo mwishoni mwa mwaka jana yalitumika kuteka gari la chuo cha SUA Morogoro na kisha maiti ndani ya sanduku. 

No comments:

Post a Comment