Tuesday, November 8, 2011

Kituo Cha Mafuta Chauza Maji Badala Ya Petrol Singida

Mhusika wa gari hilo akihangaikia, baada ya kuwa limejazwa maji badala ya petrol, kwenye kituo cha Gapco mjini Singida, ambacho ni mali ya M/S Joel Traders wa Dar es Salaam

Rav 4 ikisaidiwa kupelekwa gereji

Magari mawili yakiwa katika eneo la kituo cha Gapco mjini Singida,baada ya kushindwa kufanya kazi kufuatia kujazwa maji,badala ya mafuta ya Petrol.

Fundi magari, akionekana kulifanyia matengenezo gari ilililojazwa maji badala ya petrol, matengenezo hayo yalihusu kubadilisha pampu na tenki la mafuta.

Meneja akinyanyua pampu, kwa madai kuwa iligongwa na gari, hivyo kusababisha maji kuingia, wakati huohuo akidai hitilafu ya umeme imesababisha maji kuingia,ajabu!.

KITUO cha mafuta cha GAPCO, mjini Singida kimewajazia maji wateja wake kwenye magari,badala ya petrol.
Tukio hilo limetokea jana jumatatu,ikiwa ni siku moja tabngu Mamlaka ya udhibiti wa Nishati na Maji(Ewura) kutangaza kupanda bei ya mafuta aina zote.
Hali hiyo imesababisha injini za magari hayo kuzima, kila mojawapo lilipojazwa maji badala ya mafuta, majira ya saa tatu asubuhi,kwenye kituo hicho, kilichopo eneo la Boma, jirani na ofisi za TRA,Singida.
Baadhi ya wateja walioathirika,Thomas Petro na Elisante Mkumbo, walishangazwa na kituo hicho,baada ya kubaini kiwango cha mafuta kwenye magari yao ni kidogo,kuliko mafuta.
Walidai, magari yao mawili, ni kati ya manne yaliyojazwa mafuta, kabla ya zoezi hilo kusitishwa na uongozi wa kituo hicho cha GAPCO, baada ya magari hayo kuzima,kila yalipokuwa yamejazwa mafuta.
Magari mengine, yaliyojazwa petrol kwenye kituo hicho yalibainika kuwa na maji hadi lita 20.
Hata hivyo wakati jeshi la polisi, kupitia kamanda wa mkoa,Celina Kaluba, likisema halifahamu chochote juu ya tukio hilo,meneja wa kituo cha Gapco, Kiwelu Amos, alisema maji hayo yametokana na mvua iliyonyesha.
Maelezo ya meneja huyo yalionekana kutofautiana kila alipoeleza, awali alidai athari hiyo ilitokana na maji ya mvua, na baadaye akasema imesababishwa na tatizo la umeme,lakini bila ya kufafanua zaidi.
Kituo hicho kinamilikiwa na M/S Joel Traders Ltd-Singida, anayeishi Dar es Salaam, na hii ni mara ya pili kufungiwa, awali kiliwahi kufungiwa baada ya kukiuka utaratibu wa kuweka rangi, kwenye mafuta yake.

No comments:

Post a Comment