Thursday, November 17, 2011

Ziara Ya Mo Dewji Kwenye Mradi Wa BADEA


Mkurugenzi wa Mamlaka ya maji safi na taka Singida,SUWASA, Marin Churi akifafanua jambo kwa ugeni ulioambatana na Mbunge wa Singida Mjini ,Mohammed Dewj (kuhoto) pamoja na wengine walioambatana kwenye msafara huo wakiwemo viongozi wa siasa.

Mbunge wa Singida Mjini,Mohammed Dewji akisalimiana na watendaji wakuu wanaosimamia mradi huo wa BADEA, Mr. Ragpathy (Contracts Manager) pembeni yake,Ashork Patel (Site Incharge) wa kampuni ya SPENCON SERVICE LTD.

Tanki la maji likiwa kwenye hatua ya ujenzi likionekana kwa sasa ambapo ujenzi wake unatarajia kumalizika mwakani, ambapo mradi huo utakuwa na matumaini makubwa kwa wananchi wa Singida ukikamilika.

Mo Dewji akipata maelezo ya sehemu mbalimbali ndani ya eneo la Ujenzi la mradi wa Tanki kubwa na lala kisasa kutoka kwa mmoja wa wataalum wa kampuni ya Spencon Service Ltd alipotembelea huko eneo la Mandewa.

Mkurugenzi wa SUWASA,Injinia Isaack Nyalonji Akitoa maelezo ya kisima kikubwa cha mradi wa BADEA katika eneo la Mwankoko, kushoto kwake Mbunge Mo Dewji alipotembelea kukagua mradi huo ambao unatarajia kumalizika mpaka Julai 12, mwakani. Wa pili kushoto, Mstahiki Meya, Shehe Salum Mahami, eneo la chanzo cha mradi huo wa maji.

Mo Dewji akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi mbalimbali mara baada ya kumaliza kukagua ujenzi wa mradi huo wa BADEA ambao unatarajia kumalizika Julai mwakani.

No comments:

Post a Comment