Friday, November 25, 2011

Waandishi Wa Habari Singida Wapata Uongozi Mpya

Mwakilishi wa umuoja wa klabu za waandishi wa habari nchini(UTPC), Bw.Victor Maleko kutoka Mwanza akitoa nasaha kwa uongozi mpya.

Waandishi wa habari mkoa Singida wakiwa mkutanoni, tayari kushiriki uchaguzi kupata viongozi wapya.

Mwenyekiti mpya wa SINGPRESS(aliyesimama), Seif Takaza, akiwa na timu mpya iliyochaguliwa kuongoza klabu hiyo kwa miaka mitatu ijayo, mwenye kofia ni katibu wa chama hicho Bw. Abby Nkunu.

Aliyekuwa katibu wa SINGPRESS, Bi. Doris Meghji, akisoma risala kwa mgeni rasmi, mkuu wa mkoa Singida(mbele), Dk.Parseko Kone,kabla ya uchaguzi kuanza.

Viongozi wapya wa Chama Cha Wanahabari mkoa Singida(SINGPRESS), wakiwa katika picha ya pamoja baada ya uchaguzi jana, kutoka kulia mbele ni Nathaniel Limu, Joseph Lujuo, Awila Sila, Jumbe Ismailly na Elisante John; nyuma kutoka kushoto ni Emmanuel Michael, Abby Nkungu, Seif Takaza na Mchungaji Immanuel Barnaba.


MKUTANO mkuu wa Chama Cha Waandishi wa habari mkoa wa Singida(SINGPRESS), umepata viongozi wapya, watakaodumu madarakani kwa kipindi cha miaka mitatu, kulingana na katiba yao.
Waliochaguliwa na mkutano huo uliofanyika ukumbi wa kanisa katoliki mjini Singida na nyadhifa zao kwenye mabano ni Seif Takaza(mwenyekiti), Abby Nkungu(katibu) na Awila Sila(mhazini).
Wengine ni Jumbe Ismailly(mwenyekiti msaidizi), Emmanuel Michael(katibu msaidizi), Nathaniel Lim(mhazini msaidizi), na wajumbe watatu wa kamati ya utendaji ambao ni Elisante John,mchungaji Immanuel Barnaba na Joseph Lujuo.
Mapema akifungua mkutano huo, mkuu wa mkoa Singida Dk.Parseko Kone alipongeza hatua iliyochukuliwa na SINGPRESS, katika kuandaa uchaguzi huo, akidai kuwa waandishi wa Singida wameonyesha mfano halisi wa Demokrasia.
Hata hivyo aliwataka kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao kwa ukweli na ufanisi, pasipo kumuonea mtu au mdau yeyote katika utoaji wa taarifa.
Alikemea tabia ya waandishi wachache wanaochafua taaluma ya habari kwa kuandika habari zenye mlengo wa kukosanisha jamii na viongozi wanaowangoza.
Katika uchaguzi huo, ulisimamiwa na mwakilishi kutoka Muugano wa klabu za waandishi wa habari Tanzania(UTPC) Victor Maleko, na katibu tawala msaidizi mkoa Singida anayeshughulikia masuala ya maendeleo ya jamii, Zuhura Karya.

No comments:

Post a Comment