Wednesday, November 2, 2011

Madiwani Wa CCM Wamlalamik​ia Meya Wao

Diwani wa kata Mungumaji Hassan Mkata akiongea kwenye baraza la madiwani, Manispaa ya Singida, kuhusiana na maamuzi mbalimbali yanayoafikiwa na baraza hilo, lakini hayatekelezwi

Diwani wa kata ya Utemini Bartazar Kimario akiongea kwa hisia kali katika baraza hilo, kulalamikia maamuzi mbalimbali yanayotolewa na baraza hilo, lakini hayatekelewi hali aliyotishia kutoka kwenye kikao hicho.hata hivyo alibaki baada ya mawazo yake kukubaika

Madiwani wakifuatilia hoja kupitia katika makablasha yao

.:Meya wa manispaa Singida Shekhe Salum Mahami akifungua baraza hilo, kulia ni mkurugenzi wa mniapsaa Yona Maki

MADIWANI wa manispaa ya Singida wamemlalamikia Meya shekhe Salumu Mahami, wakidai hayatendea haki maamuzi ya baraza hilo na hiyo inaweza klutoa nafasi kwa wapinzani, siku za usoni.

Baadhi ya madiwani waliotoa shutuma hizo ni Hassan Mkata (Mungumaji), Shaaban Sattu(Unyambwa), Baltazar Kimario(Utemini) na Moses Ikaku(Unyamikumbi).
“Meya lazima sasa tusome nyakati, umekuwa kama kinyonga, unabadilika badilika rangi kutokana na eneo unalokuwa….mnaifichaficha nini, mkurugenzi naye tunaweza kumtoa nje ili tumjadili, tukiona amekosea tutaamua hapa hapa,”alisisitiza Mkata.
Baraza la madiwani, manispaa ya Singida lina jumla wajumbe 21, wote kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM) pekee, wakiwemo wawakilishi kata 14, viti maalumu watano na wabunge wawili.

No comments:

Post a Comment