Wednesday, April 8, 2015

Sherehe za maadhimisho ya siku ya utundikaji mizinga kimkoa yafana.

Mkuu wa mkoa wa Singida Dk.Parseko Kone, akishiriki kutundika mizinga ya nyuki katika siku ya maadhimisho ya utundikaji mizinga kitaifa ambapo kimkoa yamefanyika katika kijiji cha Pohama jimbo la Singida kaskazini.

Vijana wawili wakazi wa kijiji cha Pohama jimbo la Singida kaskazini, wakiteremka baada ya kumaliza kutundika mizinga ya nyuki katika siku ya maadhimisho ya utundukaji wa mizinga kitaifa ambapo kimkoa yalifanyika katika kijiji cha Pohama.

Mkuu wa mkoa wa Singida, Dk.Parseko Vicent Kone, akihutubia wananchi wa tarafa ya Mgori jimbo la Singida kaskazini waliohudhuria kilele cha maadhimisho ya siku ya utundikaji mizinga ya nyuki kitaifa yaliyofanyika kimkoa katika kijiji cha Pohama.Pamoja na mambo mengine, Dk.Kone ameagiza wakazi wa mkoa huo,kuanzisha vikundi vya wafugaji ili wapate huduma ya pamoja kwa kufikiwa kwa urahisi na kutengewa maeneo ya kufugia nyuki kisheria.
Baadhi ya wajasiriamali kutoka mkoa wa Dodoma wakisubiri wateja kuuza mazao ya nyuki ambayo ni asali na nta kwa wateja wa tarafa ya Mgori kijiji cha Pohama.

No comments:

Post a Comment