Saturday, August 31, 2013

Makundi ya watu tofauti mkoani Singida wapendekeza Tanzania kuwa na muundo wa serikali tatu.

 Mjumbe wa baraza la Katiba kwa watu wa makundi mbalimbali mkoani Singida Mussa Sima akitoa maoni ya kikundi chao juu ya uboreshaji wa rasimu ya Katiba katika kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa chuo cha wananchi mjini Singida.
 Baadhi ya viongozi wa mashirika yasiyo ya kiserikali ya mkoa wa Singida wakishiriki kikao cha rasimu ya katiba katika kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano cha chuo cha maendeleo ya wananchi mjini Singida.
Baadhi ya wajumbe wa baraza la rasimu ya Katiba kutoka kwenye makundi mbalimbali, wakiwa kwenye kikundi kujadili uboreshaji wa rasimu ya katiba.

Baadhi ya wajumbe wa baraza la rasimu ya katiba kwa watu kutoka makundi mbalimbali katika manispaa ya Singida, wamependekeza kuundwa kwa muungano wa serikali tatu na kudai kila serikali inufaike na raslimali zake.

Wakifafanua, wamependekeza muungano huo uwe na serikali ya muungano wa Tanzania, serikali ya Tanzania bara na serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Wamesema kila serikali inufaike peke yake na

Wednesday, August 28, 2013

HISTORIA MPYA YAANDIKWA, CHIDY BENZ NA NEY WA MITEGO WAPATANISHWA MKOANI SINGIDA.

Yeyote ambae damu yake ipo sana kwenye muziki wa bongofleva ni lazima atakua anafahamu kuhusu ugomvi wa muda mrefu, kutoelewana kwa Chidi Benz na Ney wa Mitego, ishu ambayo ilihusishwa hata kwenye nyimbo zao.
Shuhuda mkuu wa tukio lenyewe ni msanii Madee ambae naanza kwa kumkariri anasema ‘hizi ndio faida za Serengeti Fiesta, kujuana na kukutana na watu wengi, hiki ni kitu ambacho nilikipanga mimi… watu wanafikiria tu sisi tunakwenda kule kufanya muziki, mbali na pesa tunazolipwa vizuri sasa hivi kwenye Fiesta, kuna faida nyingine pia, niliposikia Chidi Benz yupo kwenye Fiesta nilijipanga lazima nifanye hivi manake Chidi na Ney wote nawajua, nimekaa nao’
Kwenye sentensi ya pili, Madee anasema ‘niligundua Chidi ni mwepesi kukasirika, kuna wakati kwenye basi la Wasanii kulitokea kama purukushani kuhusu hawa wawili so nikasubiri tu time nzuri ifike nifanye yangu’
‘Tulikua Club, nilipoona Chidi katulia nikamfata, nikamchukua alafu bila kumwambia kitu nikampeleka alipokuwepo Ney wa Mitego, nikamwambia haya…. simama pale nikupige picha, wakati huo sijasema chochote kuhusu ugomvi na Shilole alikua ndio kasimama na Ney, nikawapiga wakiwa watatu alafu badae nikamwambia Shilole aondoke wakabaki wawili, yani Ney na Chidi’ – Madee
Madee anakwambia baada ya kupiga picha hazikuongelewa stori zozote za ugomvi wa Chidi na Ney, kwanza zilipigwa stori za mtaani tu… za ujana alafu kitu kikaitika manake Ney wa Mitego na Chidi Benz wote walikua na furaha na walikua wanachangia mada kwa pamoja, yani kama washkaji….
Hii ishu ilitokea wakati wa show ya Serengeti Fiesta 2013 Singida ambapo kikubwa alichokua anaongea Chidi ni kuhusu

MATUKIO MBALIMBALI YA SERENGETI FIESTA 2013 MKOANI SINGIDA.MAHUDHURIO YAVUNJA REKODI.















                                                                      Peter Msechu






Sunday, August 25, 2013

LIVERPOOL YAIBUKA WASHINDI KATIKA TAMASHA LA SERENGETI FIESTA SOKA BONANZA MKOANI SINGIDA.

 Meneja wa kampuni ya bia serengenti kanda ya ziwa (kulia) akimkabidhi Kapteni wa timu ya soka ya Liverpool ya Utemini mjini Singida Mohammed Saidi feza taslimu shilingi Laki Tatu baada ya kuibuka washindi katika fainali ya Bonanza liliyofanyika kwenye uwanja wa michezo wa Peoples Club Utemini.
 Meneja wa kampuni ya bia Serengeti kanda ya ziwa (kulia) akimkabidhi kapteni Mohammed Saidi kombe baada ya kuibuka washindi katika fainali ya Soka ya Bonanza lililoandaliwa na kampuni ya Serengeti. Bonanza hilo lilitumika kuitangza bia ya Serengeti mkoani Singida.
 Timu ya Bayern Munich ya Majengo Singida mjini iliyocheza fainali ya Bonanza la Serengeti Bia kati yake na Liverpool.F.C.ya Utemini.
 Athumani Ntandu wa Chelsea F.C. ya Kibaoni mjini Singida akipiga mpira wa penalti dhidi ya Liverpool.Mpira huo ulipanguliwa na kipa Sudi wa Liverpool.
Baadhi ya wakazi wa Singida mjini,wakiburudika na Bia aina ya Serengeti kwenye viwanja vya Peoples Club wakati wa Bonaza lililoandaliwa na kampuni ya kutengeneza Bia ya Serengeti.

CHEKI YALIOJIRI KATIKA TAMASHA LA SERENGETI FIESTA SOKA BONANZA MKOANI SINGIDA

 Timu ya Liverpool moani Singida imefanikiwa kunyakua kikombe na zawadi nono ya fedha baada ya kuwafunga Beryen Munich magoli 2-0 katika mchezo wa fainali wa Serengeti Fiesta Soka Bonanza uliofanyika kwenye viwanja vya Peoples Club mjini Singida.

Kabla ya mchezo huo wa fainali, mapema Liverpol iliwaondosha Bacelona na Chelse, wakati nayo Beryen Munich iliwafunga AC Milan 1-0 na Arsenal