Baadhi ya wananchama wa klabu ya waandishi wa habari (Singpress) mkoa wa Singida wakijifunza uandishi wa habari kupitia mtandao. Mafunzo hayo ya siku nne yamefanyikia katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya mkuu wa wilaya Iramba. Mwenye fulana ya misitari ni mkufunzi wa mafunzo hayo ya uandishi kupitia mtandao (on line journalism),John Mnubi akiwaelekeza wanachama wa Singpress namna ya kufungua blog.
Wanachama wa Klabu ya Waandishi wa Habari (Singpress) Mkoa wa Singida, wametahadharishwa na vitendo vya ngono zembe vinavyochochea maambukizi mapya ya virusi Ukimwi kwa madai kwamba baadhi ya wanawake wa mjini Kiomboi Wilaya ya Iramba hawajui kusema ‘hapana’ pindi wanapoombwa kuwa na mahusiano ya kimapenzi.
Mwenyekiti wa Singpress,Seif Takaza ambaye ni mkazi wa mjini New Kiomboi,ametoa tahadhari hiyo wakati akiwakaribisha wanachama 15 wa Singpress wanaohudhuria mafunzo ya siku nne ya uandishi bora wa habari kupitia mtandao (on line Journalism).
Mafunzo hayo yanayosimamiwa na Mwezeshaji John Mnubi kutoka mkoa wa Iringa,yanaendelea kwenye ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Iramba mkoani Singida.
Akifafanua,Takaza alisema baadhi ya wanawake na wasichana wa mjini hapa,wana tabia ya kuchangamkia wageni hususani wanaokuja kuhudhuria























