Friday, September 27, 2013

Wanahabari wa Singida watahadharishwa kuhusu Ukimwi.


 Baadhi ya wananchama wa klabu ya waandishi wa habari (Singpress) mkoa wa Singida wakijifunza uandishi wa habari kupitia mtandao. Mafunzo hayo ya siku nne yamefanyikia katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya mkuu wa wilaya Iramba. Mwenye fulana ya misitari ni mkufunzi wa mafunzo hayo ya uandishi kupitia mtandao (on line journalism),John Mnubi akiwaelekeza wanachama wa Singpress namna ya kufungua blog.

Wanachama wa Klabu ya Waandishi wa Habari (Singpress) Mkoa wa Singida, wametahadharishwa na vitendo vya ngono zembe vinavyochochea maambukizi mapya ya virusi  Ukimwi kwa madai kwamba baadhi ya wanawake wa mjini Kiomboi Wilaya ya Iramba hawajui kusema ‘hapana’ pindi wanapoombwa kuwa na mahusiano ya kimapenzi.

Mwenyekiti wa Singpress,Seif Takaza ambaye ni mkazi wa mjini New Kiomboi,ametoa tahadhari hiyo wakati akiwakaribisha wanachama 15 wa Singpress wanaohudhuria mafunzo ya siku nne ya uandishi bora wa habari kupitia mtandao (on line Journalism).

Mafunzo hayo yanayosimamiwa na Mwezeshaji John Mnubi kutoka mkoa wa Iringa,yanaendelea kwenye ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Iramba mkoani  Singida.

Akifafanua,Takaza alisema baadhi ya wanawake na wasichana wa mjini hapa,wana tabia ya kuchangamkia wageni hususani wanaokuja kuhudhuria

Wednesday, September 25, 2013

Halmashauri za Wilaya na Manispaa waaswa kutotoza ushuru kwa ‘Lumbesa’

 Mkuu wa wilaya ya Singida, mwalimu Queen Mlozi akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi msaada  mizani za vipimoaina mbalimbali  iliyotolewa na wakala wa vipimo uliopo chini ya wiraza ya viwanda na biashara kwa lengo la kupiga vita magunia maarufu kwa jina la Lumbesa.Wa pili kulia ni kamishina msaidizi wa wakala wa vipimo,Peter Samwel Masinga na wa kwanza kulia ni makamu mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Singida, Elia Digha.
 Kamishina msaidizi wa wakala wa vipimo,Peter Samwel Masingida akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi msaada wa mizani ya aina mbalimbali iliyotolewa msaada na wakala wa vipimo kwa ajili ya kukabiliana na tatizo sugu la gunia maarufu kwa jina la Lumbesa.Wa kwanza kushoto ni mkuu wa wilaya ya Singida,mwalimu Queen Mlozi na kulia ni makamu mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Singida na diwani wa kata ya Msange, Elia Didha.
 Kamishina msaidizi wa wakala wa vipimo Peter Samwel  Masinga (kulia)akimkabidhi mkuu wa wilaya ya Singida,mwalimu Queen Mlozi moja ya mizani iliyotolewa na wakala wa vipimo kwa ajili ya kukabiliana na gunia aina ya lumbesa linalodaiwa kuwadhulumu wakulima jasho lao.
 Mkuu wa wilaya ya Singida,mwalimu Queen Mlozi (kushoto) akimkabidhi mstahiki meya wa manispaa ya Singida moja ya mzani uliotolewa na wakala wa vipimo kwa lengo la kutokomeza gunia maarufu kwa jina la lumbesa linalodaiwa kuwapunja mapato wakulima.
Mkuu wa wilaya ya Singida, mwalimu Queen Mlozi (kushoto) akimkabidhi makamu mwenyekiti wa halmashauri ya Singida na diwani wa kata ya Msange,Elia Digha moja ya mzani uliotolewa msaada na wakala wa vipimo kwa lengo la kutokomeza gunia aina ya Lumbesa.

Halmashauri za Wilaya na Manispaa Mkoa wa Singida, zimeaswa kutotoza ushuru kwa kutumia kipimo cha ‘gunia’ ambacho kimedaiwa kushawishi wafanyabiashara na wasafirishaji kutumia kitendo hicho cha kujaza gunia maarufu kama ‘Lumbesa’ kwa lengo la kulipa ushuru kidogo.

Hayo yamesemwa hivi karibuni na Kamishina Msaidizi wa Wakala wa Vipimo Ndugu Peter Samwel Masinga,wakati akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi mizani za viwango mbalimbali ambazo zimetolewa  kwa msaada na Wizara ya Viwanda na Biashara.

Msaada huo umetolewa kwa halmashauri ya wilaya na manispaa ya  Singida Ndugu Masinga  amesema matumizi ya kipimo cha kutumia gunia kutoza ushuru yalibainika juni mwaka huu wakati afisa mtendaji mkuu wa wakala wa vipimo, Magdalena Chuwa alipotembelea mkoa wa Singida.

Masinga alisema halmashauri kuendelea kutoza ushuru kwa kutumia kipimo cha

Friday, September 20, 2013

Serikali ya Mkoani Tabora imewaagiza madiwani kusimamia kikamilifu fedha za umma

 Katibu tawala mkoa wa Tabora, Kudra Mwinyijuma akizungumza kwenye hafla ya kumuaga aliyekuwa mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Igunga Protace Magayane Kwa sasa Magayane ni mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Ikungi mkoa wa Singida. Pia katika hafla hiyo iliyofanyika Igunga mjini,mkurugenzi mpya wa halmashauri ya Igunga, mwalimu Rustika Turuka alikaribishwa rasmi.Wa kwanza kulia (walioketi) ni mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Ikungi,Protace Mgayane na anayefuatia ni mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Igunga, Abubakari Shaban.
 Katibu tawala mkoa wa Tabora, Kudra Mwinyijuma (kulia) akimkabidhi mweka hazina wa halmashauri ya wilaya ya Igunga,Gordon Julius Dinga,cheti maalum baada kuiwezesha halmashauri hiyo kupata hati safa ya mahesabu kwa kipindi cha mwaka wa fedha wa 2010/2011 na 2011/2012.
 Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Igunga mkoani Tabora, Abubakari Shaban akitoa nasaha zake kwenye halfla iliyofana ya kumuaga aliyekuwa mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Igunga, Protace Magayane aliyehamia wilaya ya Ikungi mkoa wa Singida. Pia kumkaribisha mkurugenzi mpya wa halmashauri ya Igunga, mwalimu Rustika Taruka.Wa pili kushoto ni mkurugenzi Protace Magayane na wa kwanza kushoto ni mke wake mkurugenzi Magayane.
 Aliyekuwa mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Igunga,Protace Magayane akitoa nasaha zake wakati akizungumza kwenye hafla ya yeye kuagwa na viongozi na wananchi wa halmashauri ya wilaya ya Igunga.
 Mkurugenzi wa halmashauri mpya ya Ikungi mkoa wa Singida, Protace Magayane (kushoto) akijadiliana mambo ya Afisa wake wa Kilimo Ayubu Sengo wakati wa hafla ya kuagwa (Magayane) iliyofanyika Igunga mjini.
 Baadhi ya viongozi na wananchi wa halmashauri ya wilaya ya Igunga mkoa wa Tabora, wakipata msosi kwenye hafla ya kumuaga aliyekuwa mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Igunga, Protace Magayane na kumkaribisha mkurugenzi mpya wa halmashauri ya wilaya ya Igunga, mwalimu Rustika Turuka.Hafla hiyo ilifanyika  Igunga mjini.
Mtaalam wa kufungua champeni wa wilaya ya Igunga ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja akifungua Shampeni  kwenye hafla ya kumuaga aliyekuwa mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Igunga, Protace Magayane na kumkaribisha mkurugenzi mpya mwalimu Rustika Turuka.

SERIKALI mkoa wa Tabora,imewaagiza madiwani wa Halmashauri ya Wilaya na Manispaa,kusimamia kikamilifu matumizi ya mali za umma ikiwemo fedha, kwa kuzingatia kanuni,taratibu na sheria za nchi.

 Hatua hiyo itasaidia pamoja na mambo mengine,Halmashauri kupata hati safi za mahesabu ya fedha za umma.

 Changamoto hiyo imetolewa juzi na Katibu Tawala Mkoa wa Tabora,Kudra Mwinyimvua,wakati akizungumza kwenye sherehe ya kupongezana watumishi wa Halmashauri ya Igunga kwa kupata hati safi kwa miaka miwili mfululizo (2010/2011 na 2011/2012).

 Alisema dawa pekee ya kuwa na uhakika wa halmashauri kupata hati safi,ni kuimarisha usimamizi wa ndani wa matumizi ya mali za umma ikiwemo fedha za umma.

 Mwinyimvua alisema usimamizi huo pia utasaidia utoaji huduma bora zitakazokidhi matarajio ya wananchi na utekelezaji  wa miradi mbalimbali ya wananchi kuwa ubora unaofanana na fedha za umma zilizotumika.

 “Kwa halmashauri ya Igunga,nitumie jioni hii kuwapongeza kwa dhati kabisa madiwani na watendaji kwa juhudi zao zilizofanikisha halmashauri kupata

Tuesday, September 17, 2013

MEZA YA MAGAZETI LEO JUMANNE TAREHE 17 - 09 - 2013





Wafanyakazi wa Wakala Jiolojia wajeruhiwa wakidhaniwa ni Majambazi na wanyonyaji Damu

 Mfanyakazi wa muda wa wakala waJiolojia mkoani Dodoma na mwanafunzi wa mwaka wa pili katika chuo kikuu Dodoma anayesomea masomo ya Jiolojia, Edwin Rwekiza (25) akipatiwa matibabu katika hospitali ya mkoa baada ya kupigwa vibaya na baadhi ya wananchi wa kijiji cha Irisya wilaya ya Ikungi kwa kuhisiwa kuwa ni Jambazi na mnyonya damu za Binadamu. Edwin amesafirishwa kupelekwa hospitali ya KCMC Moshi mkoani Kilimanjaro kwa matibabu zaidi.
 Mfanyakazi wa wakala wa Jiolojia  Dodoma mjini,Peter Lucas akiwa katika hospitali ya mkoa mjini Singida kutibiwa majeraha yaliyotokana na kupigwa vibaya na wananchi wa kijiji cha Irisya. Wananchi hao pamoja na kuonyeshwa vitambulisho na wafanyakazi hao,hawakuwaamini na kuendelea na imani yao kuwa ni Majambazi na wanyonya Damu za Binadamu.
 Mganga wa zamu katika hospitali ya mkoa, Dk.Reginald Pweleza akizungumzia hali za majeruhi (wafanyakazi wa wakala wa Jiolojia kutoka Dodoma) waliopigwa na wananchi wa kijiji cha Irisya baada ya kuwahisi kuwa ni majambazi na wanyonya Damu za Binadamu.
 Kamishna msaidizi wa madini kanda ya kati Singida,Manase Mbasha,akitoa taarifa kwa waandishi wa habari (hawapo kwenye picha) juu ya wafanyakazi wa wakala wa Jiolojia  kutoka Dodoma,kupigwa na wananchi wa kijiji cha Irisya wilaya ya Ikungi.
    Jengo la ofisi ya madini mkoani Singida.
WAFANYAKAZI wawili wa Wakala wa Jiolojia kutoka Dodoma mjini,wamepigwa na kujeruhiwa vibaya wakiwa kazini na baadhi ya wananchi wa kijiji cha Irisya tarafa ya Sepuka wilaya ya Ikungi,kwa madai ya kuhisiwa kuwa ni majambazi na wanyonyaji damu.

Wananchi hao waliwavamia Peter Lucas (30) na Edwin Rwekiza (25), wakiwa kazini na kuwapiga kwa kutumia silaha za jadi ikiwemo marungu.

Wafanyakazi hao wameumizwa vibaya vichwani na Edwin ambaye ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu Dodoma mwaka wa pili akichukua masomo ya Jiolojia,amevunjika mifupa ya kichwani na hali yake ni mbaya.

Juzi jioni Edwin amesafirishwa kwa ndege kupelekwa hospitali ya KCMC Moshi mkoani Kilimanjaro,kwa matibabu zaidi.Kwa upande wake Peter,yeye anaendelea na matibabu katika hospitali ya mkoa mjini hapa.

Wakala huo ambao unafanya kazi chini ya Wizara ya Madini na Nishati,wafanyakazi wake hao wako mkoani Singida kwa kazi ya kuchora ramani za kijolojia.

Shughuli zingine ni uchunguzi kwa kutumia kemikali,ili kubaini madini na kwa ujumla walikuwa

Monday, September 16, 2013

MEZA YA MAGAZETI LEO JUMATATU TAREHE 16 - 09 - 2013





Watahiniwa wa darasa la saba wamebambwa wakiwa hawajui kusoma na kuandika

JUMLA ya wanafunzi 22 wa shule tatu za msingi wilaya ya Ikungi mkoani Singida,’wamebambwa’ wakiwa kwenye vyumba vya kufanyia mtihani wa taifa darasa la saba,huku wakiwa hawajui kusoma wala kuandika.

 Wanafunzi hao na idadi yao kwenye mabano walikuwa kwenye shule ya msingi Muhintiri (2),Iglansoni (16) na Kinyampee (4) tarafa ya Ihanja wilaya ya Ikungi.

 Wakati kwenye shule ya msingi Mnyange tarafa hiyo hiyo ya Ihanja mwanafunzi mmoja wa kike hakufika kufanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi hakuhudhuria kufanya mtihani huo kwa kile kilichodaiwa tayari ameishaozwa.

 Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Ikungi Protace Magayane,aliyekuwa akikagua maendeleo ya zoezi la kufanya mtihani huo katika siku yake ya mwisho juzi, aliagiza wazazi wa mwanafunzi huyo wa kike ambaye hakufanya mtihani,wachukuliwe hatua stahiki za kisheria haraka iwezekanavyo.

 Baadhi ya wasimamizi akiwemo Ernest Mahendeka wa shule ya Kinyampembee, Rebeca Julius wa Muhintiri na Salum Jafari wa Iglanson wamesema ilibidi wajaze fomu maalumu kulingana na maelekezo kabla ya kuwaacha waendelee na mtihani kulingana na jinsi wanavyoelewa.

 Kwa upande wao  wahitimu akiwemo Perpetua Msengi na John Martin, wamesema wana matumaini makubwa ya kufaulu mtihihani huo, ingawa somo la hisabati lilionekana kuwa gumu kwa upande wao.

 Katika hatua nyingine,Mkurugenzi Magayane amesema wamejipanga vizuri kuhakikisha mwakani