Tuesday, October 7, 2014

Shirika la FU-DI kutumia zaidi ya Mil 90 kwa miradi ya nyuki.

Meneja wa shirika lisilo la kiserikali la Future Development Initiatives (FU-DI) lenye makazi yake Ikungi mkoa wa Singida, Jonathan Njau akimkaribisha ofisini kwake rais wa shirikisho la wafuga nyuki duniani, Gilles Ratia.
Rais wa shirikisho la wafuga nyuki duniani Gilles Ratia (wa tatu kulia) akifafanua jambo kuhusu mizinga ya nyuki kwa Kaimu Mkurugenzi misitu Gladnees Mkamba.Wa kwanza kulia ni mtendaji mkuu misitu, Juma Mgoo na anayefuatia ni Meneja shirika la Future Development Initiatives Jonathan Njau.
Mizinga ya kienyeji iliopo kwenye shamba darasa la ufugaji nyuki kisasa katika kijiji cha Mahambe tarafa ya Ikungi mkoa wa Singida.

Mampando wakabidhiwa kituo na vyoo vya kisasa.

Meneja wa shirika la HAPA la mkoa wa Singida, David Mkanje, akiwa katika kutekeleza majukumu yake mbalimbali.

SHIRIKA lisilo la kiserikali linalojishughulisha na masuala ya afya, maji na usafi wa mazingira (HAPA) la mkoa wa Singida, limetumia zaidi ya shilingi 15 milioni kujenga kituo cha ushauri na ujenzi wa vyoo bora katika kijiji cha Mampando kata ya Ntutu wilaya ya Ikungi.

Ujenzi wa kituo hicho cha aina yake katika wilaya ya Ikungi, umefadhiliwa na shirika la Health, Australian Tanzania (HAT) na kusimamiwa na shirika la HAPA.

Akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi kituo hicho, Mkurugenzi wa HAPA, David Mkanje, ametoa wito kwa wakazi wa wilaya ya Ikungi, kujitokeza kwa wingi kufika katika kituo cha ushauri na ujenzi wa vyoo bora,ili kujifunza ujenzi huo ambao una faida nyingi.

Alisema kuwa  ujenzi wa vyoo bora una faida nyingi ambazo unaimarisha mazingira bora na pia

Watatu wafariki dunia katika matukio tofauti mkoani Singida.

Kamanda wa jeshi la polisi mkoani Singida, SACP  Geofrey Kamwela.

WATU watatu mkoani Singida, wamefariki dunia katika matukio tofauti likiwemo la mkulima moja  kupigwa vibaya na askari mgambo akituhumiwa kuvunja mlango wa ofisi ya afisa mtendaji wa kijiji.

Kamanda wa jeshi la polisi mkoani Singida, SACP  Geofrey Kamwela alisema katika tukio la kwanza,mkulima mkazi wa kijiji cha Milade tarafa ya Kinyangiri wilaya ya Mkalama,Salum Abrahamani (42) amefariki dunia Septemba mbili mwaka huu saa 6.10 usiku.

Alisema siku ya tukio. Abrahaman alivunja mlango wa ofisi ya mtendaji wa kijiji hicho alikokuwa amefungiwa kwa kosa la kumjeruhi Saidi Nyuha (25).

“Baada ya kuvunja mlango huo, marehemu alienda nyumbani kwake kulala. Baada ya kubaini kuvunjwa kwa mlango huo,askari mgambo Shaban Idd (28),Aman Ramadhan na Shaban Adamu,walimfuata marehemu nyumbani kwake na

Tuesday, September 16, 2014

Hospitali ya vitanda 1000 kunufaisha kanda ya ziwa.

Moja kati ya nyumba 10 zilizojengwa na Shirika la Nyumba la Taifa Tanzania { NHC } zilizopoa katika eneo la Madewa Veta Mkoani Singida.
Kaimu  Mkurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa Tanzania Nd. Peter Buheja akimkaguza Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alipotembelea mradi wa  nyumba zinazojengwa na shirika la Nyumba Tanzania  Mjini Singida.
Kaimu  Mkurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa Tanzania Nd. Peter Buheja akimpatia maelezo Balozi  Seif juu ya mashine 24 za Kufyatulia Matofali zilizotolewa na shirika hilo kwa ajili ya kupewa Vijana waliounda vikundi vya ushirika katika wilaya zote za Mkoa wa Singida kabla ya kukabidhi mashine hizo kwa Mkuu wa Mkoa huo Dr. Parseko Visent Koni.

Mil 500 kutumika zoezi la Chanjo ya Surua na Rubella Mkoa wa Singida.7

Mkuu wa mkoa wa Singida, Dk.Parseko Kone.

MKOA wa Singida, unatarajia kutumia zaidi ya shilingi 500 milioni kwa ajili ya kugharamia zoezi la kampenin ya taifa ya chanjo mpya ya surua na rubella, kwa watoto wenye umri wa chini ya miaka 15.

Zoezi hilo la nchi nzima,linatarajiwa kuanza mwezi huu wa septemba kuanzia tarehe

Serikali ijenge mazingira rafiki kwa majengo yote ya kusomea ili kuwasaidia walemavu – TASI.

Katibu wa chama cha watu wenye ulemavu wa ngozi (albino) nchini, TASI, Ziada Msembo (kulia) akimkabidhi mwalimu wa wanafunzi walemavu wakiwakiwemo Albino shule ya msingi Ikungi mchanganyiko, Donard Bilali  vitabu vya sheria zinazowahusu walemavu.
Katibu wa chama cha watu wenye ulemavu wa ngozi (Albino) nchini, Ziada Msembo akimkabidhi losheni ya kujikinga na miale ya jua mwanafunzi mwenye ulemavu wa ngozi (Albino) wa shule ya msingi Ikungi mchanganyiko.
Katibu wa chama cha watu wenye ulemavu wa ngozi (Albino) nchini, Ziada Msembo (wa kwanza kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya walimu wa shule ya msingi Ikungi mchanganyiko.

MO apata wapinzani Chadema.

WANACHAMA watatu wa Chama Cha Demokrasi na Maendeleo (CHADEMA) mkoa wa Singida, inadaiwa wameonyesha nia ya dhati kumng’oa Mbunge wa jimbo la Singida Mohammed Gullam Dewji, katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwakani.

Wanachama hao ambao inadaiwa wana uwezo mkubwa wa kulipaisha kimaendeleo jimbo hilo ni aliyewahi kuthubutu kumwangusha Dewji kwenye uchaguzi mkuu uliopita na kuangukia pua, Josephat Isango (kwa sasa ni mwandishi wa habari wa gazeti la Tanzania daima).

Katika uchaguzi mkuu wa chama hicho uliofanyika juzi, Josephat Isango ambaye alikuwa akiomba nafasi ya uenyekiti wa mkoa, aliambulia kura mbili, wakati mshindi Shaban Limu akizoa kura 74.

Wengine ni Vicent Mughwai (mdogo wake na mbunge Tundu Lissu) na Selemani Majindu.

Wanachama hao walitangaza nia zao hizo kwenye mkutano mkuu wa uchaguzi wa chama hicho uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Cheyo Clief,mjini Singida.

Kwa upande wa jimbo la Singida kaskazini linaloshikiliwa na Waziri wa Maliasili ya Utalii, Lazaro Nyalandu,wanachama wa