Wednesday, October 8, 2014

Mwalimu achomwa kisu sehemu mbalimbali za mwili wake.

Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Singida, SACP, Geofrey Kamwela.

WATU wawili mkoani Singida wamefariki dunia katika matukio tofauti, likiwemo la Mwalimu wa shule ya msingi Kigogo jijini Dar-es-salaam, Hawa Idd  (34) baada ya kuchomwa kisu sehemu mbalimbali za mwili wake na mdogo wake Ramadhan Iddi (24) anayedaiwa kuwa na matatizo ya akili.

Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Singida, SACP, Geofrey Kamwela alisema tukio hilo limetokea Septemba 23 mwaka huu saa 9.30 alasiri huko katika hospitali ya mkoa mjini Singida.

Alisema Septemba 22 mwaka huu  saa 5.30 asubuhi  kijana Ramadhan ilidaiwa alitoka nyumbani kwao kwa mazingira ya kutatanisha na ndipo mwalimu Hawa ambaye alikuja kwa ajili ya kushughulikia matatizo ya mdogo wake huyo,walianza msako wa kumtafuta katika maeneo mbalimbali mjini Singida.

“Baada ya kumtafuta katika mitaa mbalimbali hapa mjini na kumkosa, Hawa alirejea nyumbani kwao Kibaoni na kumkuta mdogo wake Ramadhan,ameisha rejea nyumbani. Haikuchukua muda wanandugu hao walianza

Walipwa fidia ya mil 263/- kupisha ujenzi wa chuo.

Mkurugenzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania tawi la Singida, Hassanal Issaya akiwa ofisini kwake akitekeleza majukumu yake ya kila siku.
Baadhi ya wanafunzi wa chuo cha utumishi wa  umma Tanzania tawi la Singida wakiwa kwenye darasa wakati wa masomo.

Meya ataka wasio na shughuli mijini kurejea vijijini.

Mstahiki Meya wa Nanispaa ya Singida, Sheikh Salum Mohammed Mahami ,akizungumza kwenya hafla ya uzinduzi wa shirika la TUSIFO. Hafla hiyo imefanykia katika shule ya msingi Kibaoni na Sheikh Mahami, alitumia fursa hiyo kuwasihi wakazi ambao hawana shughuli za kufanya mjini,warejee/waende vijijini kwa madai kuwa kwa sasa mazingira ya mjini, sio rafiki kwao tena. Kushoto ni mkurugenzi wa shirika la TUSIFO, Costantino Charles.
Mkurugenzi wa shirika lisilola kiserikali la Tunawakaribisha Singida Foundation (TUSIFO) la mjini Singida, Costantino Charles akizungumza muda mfupi kabla hajamkaribisha mgeni rasmi Mstahiki Meya wa manispa ya Singida, Sheikh Salum Mohammed Mahami, kuzindua rasmi shirika lisilo la kiserikali la Tunawakaribisha Singida Foundation (TUSIFO).T USIFO linajishughulisha na kutoa misaada ya madaftari, kalamu, sabuni na sare kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari katika katika masniapaa ya Singida.Kulia ni mstahiki meya wa manispaa ya Singida, Sheikh Salum Mohammed Mahami.
Mstahiki meya wa manispaa ya Singida, Sheikh Salum Mohammed Mahami, akikabidhi msaada wa daftari na kalamu kwa baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi Kibaoni mjini Singida.

Tuesday, October 7, 2014

Subirini kupiga kura, sio kuandamana waambiwa Singida.

Baadhi ya magari ya jeshi la polisi mkoa wa Singida, yakiwa yamebeba askari kwa ajili ya kuzuia maandamano ya wanachama wa CHADEMA ya kupiga kuendelea kwa Bunge Maalum la Katiba. Hadi tunakwenda mtamboni,wanachama hao pamoja na mabango yao walishitukia nguvu ya polisi na kufuta maandamano hayo.
Baadhi ya wanachama wa Chama cha Maendeleo na Demokrasia (CHADEMA) manispaa ya Singida,wakiwa nje ya ofisi ya CHADEMA mkoa Singida mjini kwa kusudio la kufanya maandamo ya amani kwa ajili ya kutoa ujumbe kuwa Bunge Maalum la Katiba linaloendelea hivi sasa ni batili. Maandamano hayo hayakufanikiwa kwa kile kilichodaiwa kuwa yakuwa na kibali halali. Ilidaiwa zaidi ya wanachama 200 wangeshiriki maandamano hayo kuanzia ofisi ya CHADEMA mkoa hadi bomani kupitia viwanja vya Peoples.

Mchungaji Singida awataka walemavu wasijinyanyapae.

Mkufunzi kutoka kituo cha Breli kilichoko chini ya kanisa la Pentekoste (FPCT) Tanzania, Ibrahimu Ikomba, akitoa maelezo muda mfupi kabla ya mafunzo ya siku tatu yaliyohusu ujasiriamali yaliyohudhuriwa na walemavu wa macho 60 wa mkoa wa Singida.
Mmoja wa wanasemina ya mafunzo ya ujasiriamali kwa walemavu wasioona, Potifa Sungi akisoma risala yao muda mfupi kabla mafunzo yao ya ujasiriamali hayajafungwa rasmi na mchungaji wa kanisa na FPCT, Amosi Maghasi.
Mchungaji wa kanisa la Pentekoste (FPCT) Kibaoni mjini Singida, Amosi Maghasi akizungumza kwenye ufungaji wa mafunzo ya siku tatu yaliyohudhuriwa na walemavu wa macho 60 wa mkoa wa Singida.Mafunzo hayo yalifanyika kwenye kanisa la Pentekoste Kibaoni.

Mfuga nyuki wa tuzo ya ‘Rais’ akoromea wanavijiji.

Rais wa shirikisho la wafuga nyuki duniani Gilles Ratia (wa tatu kulia) akifafanua jambo kuhusu mizinga ya nyuki kwa Kaimu Mkurugenzi misitu Gladnees Mkamba.Wa kwanza kulia ni mtendaji mkuu misitu, Juma Mgoo na anayefuatia ni Meneja shirika la Future Development Initiatives Jonathan Njau.

MSHINDI wa tuzo ya Rais  juu ya ufugaji  bora wa nyuki  kwa mwaka jana  Jackson Sombi,  wa mkoani Singida, ameibua tuhuma nzito  dhidi ya wana-kijiji wenzake akidai kuwa  ndio wanaokwamisha juhudi zake za kutaka kujikomboa kiuchumi kupitia uzalishaji wa asali na nta.

Sombi ametoa tuhuma hizo mbele ya Rais wa Shirikisho la Kimataifa la wafugaji  wa nyuki (APIMONDIA), Gilles Ratia,  wakati alipotembelea eneo la  hifadhi ya mfugaji nyuki huyo iliyopo katika kijiji cha Msikii halmashauri ya Wilaya ya Singida.

Amedai kuwa hifadhi yake yenye ukubwa wa kilometa za mraba 1,364 ikiwa na jumla ya mizinga

SEMA yatumia shilingi milioni 380 kusambaza Maji Iramba.

Mtendaji mkuu wa shirika la MEDICOR la nchini Uingereza, Fortunat Walther (wa kwanza kushoto) akitoa maelezo juu ya ujenzi wa visima vya maji kwa meneja wa SEMA, Ivo Manyaku, wakati Walther alipotembelea miradi hiyo inayofadhiliwa na shirika lake.
Meneja wa shirika la SEMA, Ivo Manyaku (wa pili kulia mbele), akitoa maelezo juu ya ujenzi wa visima vya maji wilaya ya Iramba, kwa mtendaji mkuu wa shirika la MEDICOR la nchini Uingereza, Fortunat Walther (wa kwanza kushoto).Shirika la MEDICOR linafadhili miradi ya maji na usafi wa mazingira inayotekelezwa na SEMA.