Friday, November 22, 2013

KATA YA MTAMAA MANISPAA YA SINGIDA YAPATA NEEMA YA UMEME.


Mjumbe wa halmashauri kuu ya taifa CCM Bw. Hassan Mazala (Picha Kutoka Maktaba Yetu)

Kata ya mtamaa manispaa ya Singida inatarajiwa kuunganishiwa nishati ya umeme wa grid wa taifa kupitia mradi wa umeme vijijini REA ili kukabiliana na umasikini wa kipato kwa wananchi wa kata hiyo.

Mjumbe wa halmashauri kuu ya taifa CCM Bw. Hassan Mazala wakati akizungumza na wananchama wa CCM katika kata hiyo ambapo amesema upembuzi yakinifu juu ya mradi huo unatarajiwa kuanza mwezi huu.


Amesema kuwa endapo umeme ukiunganishwa katika kata hiyo kutasaidia wananchi kujishughulisha na shughuli za kiuchumi ambazo zinategemea nishati hiyo na hatimaye kuondokana na umasikini wa kipato unaowakabili wakazi wa kata hiyo


Aidha Bw Mazala ametoa wito kwa wananchi wa kata hiyo kuwa tayari kuonyesha nia ya kuhitaji huduma hiyo kwa kujiandikisha hali ambayo itaongeza juhudi za mradi huo wa REA kwenda kasi kutokana na mahitaji ya

Wednesday, November 20, 2013

Chuo Cha Utumishi wa Umma kuongeza matawi zaidi.

Mtendaji mkuu wa chuo cha utumishi wa umma Tanzania, Said Nassor kitoa taarifa yake kwenye mahafali ya 16 ya chuo hicho yaliyofanyika mjini Singida. Jumla ya wahitimu 1,909 kutoka chuo cha Tabora na Singida walihitimu katika ngazi mbalimbali.
Mkuu wa mkoa wa Singida,Dk.Parseko Kone akitoa nasaha zake kwenye mahafali ya 16 ya chuo cha utumishi wa umma Tanzania yaliyofanyika mjini Singida.Kulia aliyekaa,ni Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais Menenjimenti ya Utumishi wa Umma Tanzania, Mh.Celina Kombani ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mahafali hayo.
Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma Tanzania,Celina Kombani akizungumza kwenye mahafali ya 16 ya chuo cha Utumishi wa Umma Tannzania mjini Singida.
Baadhi ya wahitimu wa chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania,waliohitimu mafunzo yao.

WAHITIMU wa Chuo Cha Utumishi wa Umma Tanzania wameagizwa kutumia elimu walioipata kufanya kazi kwa ufanisi ili kuleta tija kwa lengo la kukuza na kuendeleza uchumi wa nchi.

 Agizo hilo limetolewa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Tanzania, Celina Kombani, wakati akizungumza kwenye sherehe ya mahafali ya 16 ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, mjini hapa.

 Aliwaasa kuwa wawe watendaji wazuri mara watakapoanza kazi,na hiyo iende sambamba na kuzingatia kanuni , sheria na taratibu za utumishi wa umma.

 “Tekelezeni majukumu yenu kwa ufanisi kwa kuonyesha uwezo wa kumudu majukumu,uadilifu  na kutoa huduma bora kwa wananchi na sio kufanya kazi kwa mazoea, ili kukamilisha lengo la serikali la kupata matokeo makubwa sasa” amesema Kombani

 Awali Mtendaji Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania Said Nassor, amesema wana mkakati wa kupanua vyuo vyake ambapo mwakani wanaanzisha tawi jipya mkoani mbeya.

 Aidha, amesema pia mwakani wanatarajia kuongeza madasa katika tawi la tabora na wataanza ujenzi wa Tawi la chuo cha mkoa wa singida.

 “kwa ujenzi wa tawi la mkoa wa singida, tayari tumekamilisha zoezi la la kulipa fidia kiasi cha shilingi

SEMA yagharamia ujenzi wa Vyoo kwa Tsh 155m shule tano za Manispaa ya Singida.

Meneja wa shrika la SEMA, Ivo Manyanku,(wa kwanza kulia) akitoa taarifa yake ya ujenzi wa vyoo bora katika shule tano za msingi manispaa ya Singida kwa Naibu Waziri TAMISEMI (Elimu), Mh. Kassim Majaliwa (mwenye miwani).Vyoo hivyo vimegharimu zaidi ya shilingi 155 milioni.
Naibu Waziri TAMISEMI (Elimu) Mh. Kassim Majaliwa (aliyeipa kisongo kamera) akizindua rasmi ujenzi wa vyoo bora katika shule ya msingi Unyankindi.Vyoo hivyo bora vimejengwa kwa gharama ya shilingi 155 milioni na shirika la SEMA.Kushoto ni meneja wa SEMA. Ivo Manyanku.
Naibu Waziri wa TAMISEMI (Elimu),Kassim Majaliwa akikata utepe kuashiria ufunguzi wa matumizi ya vyoo bora vya shule ya msingi Unyankindi mjini Singida.Vyoo hivyo vimejengwa na shirika la SEMA kwa gharama ya shilingi 155 milioni.
Moja ya vyoo bora vya shule ya msingi Unyankindi manispaa ya Singida vilivyojengwa na shirika la SEMA la mkoa wa Singida.

Shirika lisilo la kiserikali la Sustainable Environment Management Action (SEMA) la mkoani Singida limetumia zaidi ya shilingi 155 milioni kugharamia ujenzi wa vyoo bora katika shule tano za manispaa ya Singida.

 Shule zilizonufaika na mradi huo ni,Unyankindi,Singidani,Manguamitogho,Mtamaa na Mtisi.

 Hayo yamesemwa juzi na Meneja wa SEMA, Ivo Manyanku wakati akizungumza kwenye hafla iliyofana ya uzinduzi wa vyoo hivyo uliofanyika katika shule ya msingi Unyankindi Singida mjini.

 Amesema fedha hizo zilizotumika katika ujenzi huo zimetolewa ufadhili na shirika la WaterAid Tanzania kwa ajili ya kutekeleza mradi wa maji na usafi shuleni katika halmashauri ya manispaa ya Singida.

 “Vyoo hivi vina matundu 48 ambayo yana uwezo wa kuhudumia wanafunzi 2,903 kati yao wavulana ni 1,446 na wasichana ni 1,457.Idadi hiyo inajumuisha na walemavu 38 ambao 25 ni wavulana na 13 ni wasichana”,amesema Meneja huyo.

 Kwa upande wake mgeni rasmi katika uzinduzi huo,naibu waziri TAMISEMI (elimu),Kassimu Majaliwa,alitumia fursa hiyo kulipongeza shirika la SEMA kwa ujezi bora wa vyoo hivyo ambavyo vimekidhi vigezo vyote vinavyohitajika.

 Amesema serikali na wadau wengine wa maendeleo hawana budi kuliunga mkono shirika la SEMA kwa madai linatelekeza miradi yake kulingana na thamani ya fedha zilizotumika.

 “SEMA binafsi nawapongezeni sana ujenzi huu mtakuwa mmeisaidia serikali katika kupunguza

Tuesday, November 19, 2013

Waislamu Singia wamuenzi mjukuu wa Mtume Al – Imamul – Hussein (A.S)




Baadhi ya waumini wa Dhehebu la Shia mkoani Singida wakiwa kwenye matembezi ya kuadhimisha kumbukumbu za kifo cha mjukuu wa Mtume Al-Imamul Hussein (AS).

Mbaroni kwa kuvujisha mtihani wa kidato cha nne.

           Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Singida, ACP Geofrey Kamwela.

JESHI la polisi mkoa wa Singida, linawashikilia walimu wawili kwa tuhuma ya kuvunjisha matihani wa kidato cha nne unaoendelea kufanyika hivi sasa nchini kote.

Walimu hao ni walimu wa shule ya sekondari kata ya Nkinto wilaya ya Mkalama mkoani Singida, ambao ni mwalimu mkuu wa shule hiyo Monica Sebastian (30) na mwalimu Agaloslo Otieno (32).

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Singida, ACP Geofrey Kamwela, amesema kuwa tukio hilo limetokea novemba 13 mwaka huu kati ya saa tatu na tatu usiku katika shule ya sekondari ya Nkinto kata ya Mwangeza tarafa ya Kirumi wilaya ya Mkalama.

Amesema kuwa mwalimu Agaloslo akiwa anasimamia mtihani katika shule ya sekondari ya Mwangeza, alikuwa anaandika baadhi ya maswali ya masomo ya Kiswahili na Civics  kwenye simu yake ya kingajani na kumtumia mwalimu wake mkuu Monica akiwa shuleni kwake Nkinto.

Kamwela alisema baada ya Monica kupata maswali hayo,alikuwa anayatafutia majibu akiwa chooni na wanafunzi walikuwa wanamfuata huko huko chooni kupewa majibu hayo.

“Lengo lao ilikuwa ni kuwasaidia wanafunzi ili waweze kufanya vizuri katika mtihani wao wa kidato cha nne mwaka huu.Wanafunzi wenywe waliisha ambiwa kuwa wawe wanadanganya kwamba wanaenda kujisadia chooni,ili wakapatiwe majibu na mwalimu mkuu”,alifafanua kamanda na kuongeza;

“Uchunguzi wa awali wa polisi unaonyesha kuwa uvunjishaji huo ulifanyika kwa nyakati tofauti kati ya mwalimu mkuu Monica na mwalimu wake Agaloslo akiwa ana simamia mtihani huo katika shule nyingi.Baada ya mwali mkuu kutumiwa maswali alikuwa anajificha ndani ya choo cha shule yake na watahiniwa kwa nyakati tofauti huomba ruhusa kwa wasimamizi kwenda chooni kwa nia ya kujisaidia na hapo humkuta mwalimu mkuu huyo na kuwapa maelekezo ya namna ya kujibu maswali hayo”.

Amesema baada ya Polisi kupata taarifa ya siri kutoka kwa wasamaria wema, waliweka mtego katika shule ya sekondari ya Nkinto na kufanikiwa kumkamata mwalimu

Monday, November 18, 2013

Wachimbaji wadogo wa madini watakiwa kulipa kodi bila shuruti.

Kamishina msaidizi Madini kanda ya Kati, Manase Mbasha akizungumza kwenye ufunguzi wa mafunzo ya siku tano ya uchimbaji bora wa Madini yanayohudhuriwa na wachimbaji wadogo 35 kutoka mikoa 15 nchini.Mafunzo hayo yanafanyikia kwenye ukumbi wa mikutano wa kanisa katoliki mjini Singida. Kulia ni afisa mwandamizi wa ofisi ya madini mkoa wa Singida, Gabriely Senge na kushoto ni mkufunzi wa mafiunzo hayo,Dk.Eng.Crispin Kinabo kutoka chuo kikuu cha Dar-es-salaam.

Baadhi ya wachimbaji wadogo wakifuatilia kwa makini mada zilizokuwa zikitolewa za mafunzo ya uchimbaji bora wa Dhahabu.

Wachimbaji wadogo wa madini nchini,wametakiwa kujenga utamaduni wa kulipa kodi bila kushurutishwa,ili kuisaidia serikali kuwa na uwezo wa kutoa huduma bora zinazokidhi mahitaji ya wananchi.

 Wito huo umetolewa na Kamishina Msaidizi Madini Kanda ya Kati,Manase Mbasha,wakati akizungumza kwenye hafla ya ufunguzi wa mafunzo ya siku tano ya uchimbaji bora wa dhahabu yanatoendelea kwenye ukumbi wa mikutano wa kanisa katoliki mjini hapa.

 Amesema lengo la serikali ni kuhakikisha wachimbaji wadogo wa madini,wanakuwa walipaji wazuri wa kodi kwa mujibu wa sheria zilizowekwa za sekta ya madini.

 “Mchimbaji mdogo ukiwa mlipa kodi mzuri,kwanza utajijengea heshima mbele ya macho ya jamii,na kikubwa zaidi ni kwamba utakuwa umeisaidia serikali kuwa na uwezo mzuri wa kuhudumia wananchi wake”alifafanua Mbasha.

 Aidha,kamishina huyo msaidizi,ametumia fursa hiyo kuwahimiza wachimbaji wadogo kushiriki kikamilifu shindano la tuzo ya rais ya mazingira.

 Mbasha amesema endapo wachimbaji wadogo na wale wa ngazi mbalimbali watashiriki kikamilifu katika shindano la tuzo ya rais ya mazingira, kitendo hicho kitasaidia mno kuboresha mazingira.

 Kwa mujibu wa Mkufunzi wa Mafunzo hayo,Dk.Eng.Crispin Kinabo kutoka chuo kikuu cha Dar-es-salaam kitengo cha Jiolojia,baadhi ya mada za mafunzo hayo,ni

Bima ya Afya yaanda kongamano kwa wadau wake Singida.

Meneja mfuko wa Taifa Bima ya Afya (NHIF) mkoa wa Singida, Agnes Chaki (wa kwanza kushoto) akitoa taarifa kwa mwandishi wa habari wa MOblog (hayupo kwenye picha) juu ya kufanyika kwa kongamano la wadau 250 wa Mfuko wa Taifa Bima ya afya (NHIF) Mfuko wa Afya ya jamii (CHF)linalotarajiwa kufanyika kesho (13/11/2013) kwenye ukumbi wa mikutano wa hotel ya Katala Beach mjini Singida.Wa kwanza kulia ni mhasibu wa NHIF,Godlessen Bellium (mhasibu) na katikati ni Isaya Shekifu (Afisa matekelezo na uratibu NHIF mkoa wa Singida.
Jengo la ofisi ya Mfuko wa Taifa Bima ya Afya (NHIF) mkoani Singida.

MFUKO wa Taifa Bima ya Afya (NHIF) kwa ushirikiano na mfuko wa afya ya jamii (CHF) mkoani Singida,unatarajia kufanya kongamano kubwa la wadau wake kesho (leo 13/11/2013) asubuhi kwenye ukumbi wa mikutano wa hotel ya kitalii ya Katala Beach (KBH) iliyopo mjini hapa.

Akizungumza na MO blog ofisini kwake leo,meneja wa NHIF mkoa wa Singida,Agnes Chaki,alisema kongamano hilo litakalofunguliwa na mkuu wa mkoa wa Singida, Dk.Parseko Vicent Kone, litaanza mapema saa mbili asubuhi.

Alisema kuwa kongamano hilo la aina yake la kwanza kufanyika mkoani hapa, linatarajiwa kuhudhuriwa na wadau 250.

Chaki alitaja baadhi ya wadau hao kuwa ni pamoja na katibu tawala mkoa,wakuu wa wilaya,wakurugenzi wa halmashauri na manispaa,wabunge wote,waheshimiwa madiwani na waganga wakuu wa wilaya.

“Wengine ni wakuu wa vyombo vya usalama,viongozi wa dini,waratibu wa bima za afya wa halmashauri (NHIF na CHF,wawakilishi wa  wanachama wa mfuko,waajiri walioandikishwa na mfuko,watoa huduma na waandishi wa habari”,alisema meneja Chaki.

Alisema kuwa dhumuni la kongamano hilo,ni kutoa fursa kwa wadau wa