Wednesday, January 8, 2014

Halmashauri ya Ikungi kutumia shilling 512.3milioni kwenye miradi ya maendeleo.

Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Ikungi, Protace Magayaye, akitoa taarifa yake kwa waandishi wa habari (hawapo kwenye picha)  ya utekelezaji wa shughuli za kilimo msimu wa 2013/2014 ambapo wanatarajia kuvuna tani 144,826 mazao ya chakula na hivyo kuwa na ziada tani 83,090.Mahitaji ya wakazi wa wilaya hiyo 225,521,ni tani 61,736 kwa mwaka.

HALMASHAURI ya Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida inatarajia kutumia zaidi ya shilingi 512.3 milioni kugharamia miradi mbalimbali ya maendeleo ya wananchi katika kipindi cha mwaka wa fedha wa 2013/2014.
Fedha hizo zimepokelewa na Halmashauri hiyo hadi kufikia mwezi huu wa Desemba mwaka huu.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Protace Magayane wakati akizungumza na moja ya magazeti ya kila siku ofisini kwake juu ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya wananchi.
Alitaja baadhi ya miradi ya maendeleo wanayoitekeleza kuwa ni ujenzi wa hostel katika shule ya sekondari Ikungi ujenzi wa nyumba ya watumishi ya kijiji cha Kimbwi na kuboresha mazingira ya kujifunzia kwa watoto wenye mahitaji maalum wa shule ya msingi Ikungi.

Magayane alitaja miradi mingine kuwa ni kuendesha mafunzo ya mashamba darasani kwa wakulima 10 na ununuzi wa mbegu bora, ukarabati wa tanki la maji Iyumbu na matengenezo ya barabara za vijiji vya Mungaa-Ntuntu,Utaho-Makiungu na Ikungi- Ndung’unyi.
Katika hatua nyingine, Mkurugenzi huyo alitaja baadhi ya mikakati ya kuboresha utekelezaji miradi kuwa ni uongozi wa Halmashauri kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo kuendelea kuzihamasisha jamii kushiriki kuchangia, kutunza na kumiliki miradi yao.

“Kuhakikisha vijiji na kata zinatoa taarifa za

Waandishi wa Habari wa Singida wahimizwa kujitathimini kwenye utendaji wao wa kazi.

Mkuu wa wilaya ya Iramba mkoa wa Singida,Yahaya Nawanda, akifungua mkutano wa wadau wa habari na wanachama wa klabu ya waandishi wa habari (Singpress) mkoa wa Singida  uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri ya wilaya ya Iramba.
Baadhi ya wanachama wa klabu ya waandishi wa habari (Singpress) mkoa wa Singida,wakifuatilia kwa makini mada zilizokuwa zinatolewa kwenye mkutano wa wadau wa habari uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri ya wilaya ya Iramba.

WAANDISHI wa Habari mkoani Singida wamehimizwa kufanya tathimini ya kina juu ya utendaji wao wote wa mwaka huu ili kujijengea mazingira mazuri zaidi ya utendaji wao katika kipindi cha mwaka ujao.

 Changamoto hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Iramba Mkoa wa Singida,Yahaya Nawanda wakati akifungua mkutano wa pamoja kati ya wadau wa habari na wanachama wa klabu ya Waandishi wa Habari (Singpress) Mkoa wa Singida.

Amesema utamaduni wa mtu kujikagua na kujitathimini mara kwa mara,kunachochea mhusika kuboresha utendaji wake na hivyo kwa kiasi kikubwa kujiletea maendeleo endelevu.

 “Usipojitathimini,utadumaza utendaji wako au utashindwa kuboresha maisha/maendeleo na kwa kiasi kikubwa maendeleo yako yataporomoka kwa kasim kubwa”,alifafanua Nawanda.

 Akifafanua zaidi,mkuu huyo wa wilaya,alisema mwandishi wa habari anapaswa kujiuliza mwaka huu,ameandika habari zipi na ipi imemletea mafanikio zaidi,ili mwakani aweze kuja na mbinu mpya zaidi na mikakati itakayomsaidia kupiga hatua zaidi.

 Aidha,Nawanda aliwataka wawe wabunifu na wajenge utamaduni wa kufanya tafiti za kina zitakazowasaidia kuibuka na stori zenye ubora wa hali ya juu.

 “Mwandishi wa habari acheni tabia ya kusubiri kuletewa habari,fanyeni tafiti za kina katika masuala ya kijamii utamaduni na kiuchumi Kwa njia hiyo mtakuwa waandishi wa habari wa viwango vya juu”,amesema.

 Katika hatua nyingine,Nawanda aliwaasa

Majambazi yalioua askari yajulikana.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Singida, SACP Geofrey Kamwela, akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusiana na tukio la kujulikana kwa Majambazi yaliyoua askari mkoani Singida.

WATU Wanne wanaodhaniwa kuwa ni majambazi wakazi wa Majengo Itigi tarafa ya Itigi wilaya ya Manyoni Mkoa wa Singida waliouwa askari wakati wa kurushiana risasi majina yao yamekwisha fahamika.

 Majambazi hayo yanadaiwa Desemba 21 mwaka huu saa 4.30 usiku huko katika kijiji cha Tambuka reli kata ya Majengo tarafa ya Itigi wilayani Manyoni yalimuuawa askari polisi D.6466 D/SGT Zakaria Williamu (43),baada ya kumpiga risasi shingoni.

Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Singida, SACP Geofrey Kamwela alitaja majina ya majambazi hayo kuwa ni Joseph Hamed (21) mkulima na mkazi wa kijiji cha Siuyu wilaya ya Ikungi.

 “Wengine ni Juma Ramadhani (20) mkulima na mkazi wa Kizota Dodoma,Abdallah Hamisi (21) mkulima na mkazi wa kitongoji cha Milera wilaya ya Ikungi na Stanley Mpaki @ Babu Mpaki (28)”amesema.

Kamwela amesema watu hao walikamatwa nyumbani kwa mtuhumiwa Stanley Mpaki ambaye ni mfanyabiashara.

 “Askari polisi waliokuwa kwenye doria siku ya tukio,walipata taarifa kutoka kwa raia wema kuwa ndani ya nyumba ya mfanyabiashara Stanley,kuna majambazi yamejificha humo,haraka walifika kwenye nyumba hiyo na baadhi waliingia ndani na kumwacha D/SGT Zakaria akiwa nje na alipigwa risasi ya shingoni na kufariki papo hapo”,amesema Kamwela kwa masikitiko.

Amesema katika eneo hilo la tukio,bunduki aina ya

Halmashauri ya Ikungi kukusanya Tsh 25.6 bilioni 2014/2015.

 Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Ikungi mkoa wa Singida, Bw. Protace Magayane,akitoa ufafanuzi wa jambo katika kikao maalum cha Madiwani kwa ajili ya kupitisha bajeti ya halmashauri hiyo ya mwaka wa fedha wa 2013/2014 jana.Wa pili kushoto walioketi ni mkuu wa wilaya ya Ikungi, Manju Msambya na anayefuata ni mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Bw. Selestin Yunde.’
 Mbunge wa viti maalum (CHADEMA) mkoa wa Singida, Bw. Christo Waja akichangia hoja kwenye kikao maalum cha Madiwani kilichokuwa kikipitisha bajeti ya mwaka ujao wa halmashauri hiyo.Kikoa hicho kilipitisha mapendekezo ya bajeti ya zaidi ya bilioni 25.
Diwani wa kata ya Ikungi (CCM) wilaya ya Ikungi mkoa wa Singida, Bw. Haji Mukhandi akichangia hoja katika kikao maalum cha bajeti ya halmashauri ya wilaya ya Ikungi kwa mwaka wa fedha ujao.
Diwani wa viti maalum (CCM) kata ya Ikungi, Bi. Asha Munjori, akitoa uchangia mapendekezo ya bajeti ya halmashauri ya Ikungi ya mwaka wa fedha wa 2013/2014 kwenye kikao maalum cha Madiwani.

HALMASHAURI ya wilaya ya Ikungi mkoani Singida inatarajia kukusanya zaidi ya shilingi bilioni 25.6 kutoka kwenye vyanzo vyake mbalimbali vya mapato  katika mwaka wa fedha wa 2014/2015.

Hayo yamesemwa hivi karibuni na Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo,Ally Nkhangaa wakati akiwasilisha mapendekezo ya bajeti kwa mwaka ujao wa fedha.

Amesema zaidi ya shilingi 723 milioni zitatoka kwenye vyanzo vya mapato vya halmashauri yenyewe na zaidi ya shilingi 336 milioni ni ruzuku kutoka serikali kuu ikiwa ni fidia ya kodi na ushuru uliofutwa.

Nkhangaa amesema wanatarajia kupatiwa ruzuku na serikali kuu zaidi ya shilingi 15.4 bilioni kwa ajili ya kulipia mishahara ya watumishi wa umma.

“Serikali kuu pia itatupatia ruzuku ya zaidi ya shilingi 1.9 bilioni kwa ajili ya kugharamia matumizi yasiyo ya mishahara na ruzuku nyingine ya zaidi ya shilingi 7.5 bilioni kwa matumizi ya kugharamia miradi ya maendeleo ya wananchi”,amesema.

Nkhangaa ambaye ni Diwani wa kata ya Ntunduu (CCM), alitaja baadhi ya mambo yaliyozingatiwa katika bajeti ni kuandaa mpango mkakati wa halmashauri wa miaka mitano kwa kuzingatia dira ya maendeleo ya kitaifa ya 2025 na ilani ya uchaguzi ya chama tawala.

Alitaja mambo mengine yaliyozingatiwa kuwa ni upimaji wa viwanja makao makuu ya wilaya Ikungi na mpango wa matumizi bora ya ardhi katika vijiji na kujenga ofisi ya halmashauri, nyumba ya Mkurugenzi Mtendaji, nyumba za watumishi na ununuzi wa samani za ofisi.

“Pia bajeti hii imezingatia kuongeza

Mvua kubwa zaleta madhara Singida, watu watano wahofiwa kufa maji.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Singida, SACP Geofrey Kamwela, akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusiana na tukio la maafa ya mvua kubwa iliyosababisha vifo.

MVUA kubwa zilizoanza kunyesha mkoani Singida zimeanza kuleta maafa baada ya watu watano kuhofiwa kufa maji kutokana na gari waliolokuwa wakisafiria kusombwa na maji ya mto.

 Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Singida, SACP Geofrey Kamwela amesema tukio hilo limetokea Desemba saba mwaka huu saa 3:30 asubuhi huko katika mto wa Nzalala kijiji cha Kisimba tarafa ya Kisiriri wilayani Iramba.

Amesema siku ya tukio, abiria 16 waliokuwa wakitoka kijiji cha Doromoni kwa kutumia Landrover 110 TDI lenye namba za usajili T.499 ATR, lilisombwa na maji ya mto wakati dereva wake akijaribu kuvuka mto Nzalala.

 Akifafanua, amesema walimpofika kwenye mto huo abiria hao walimwomba dereva huyo asubiri maji ya mto yapungue ili waweze kuvuka lakini dereva huyo alikataa kwa madai maji ni machache.

 “Wakati gari hilo lilipofika katikati ya mto, lilizimika ghafla na wakati huo huo maji ya mto yaliongezeka na kulifunika gari.  Dereva na kondakta waliweza kufanikiwa kutoka na kukimbilia kusikojulikana”

 Aidha, amesema abiria 11 waliweza kuokolewa na wamelazwa katika hospitali ya wilaya ya Iramba na watano hadi sasa haijulikani iwapo wamekufa ndani ya landrover au wamesomba na maji na kupelekwa kusikojulikana.

 Katika hatua nyingine, Kamanda Kamwela, ametoa wito kwa madereva wa vyomba vya moto, baiskeli na watembea kwa miguu kuchukua tahadhari wakati wa kuvuka mito au mabonde kipindi hiki cha mvua kubwa zinazoendelea kunyesha.

 Alitumia fursa hiyo kushauri mamlaka zinazohusika kutengeneza madaraja kwenye mito au mabonde badala ya kuweka zege ambalo husaidia tu katika kipindi cha kiangazi.

 “Aidha nashauri abiria nao wasikubali

Wednesday, December 18, 2013

Wilaya ya Ikungi kuvuna tani 144,826 ya mazao ya chakula.

Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Ikungi, Bw.Protace Magayaye, akitoa taarifa yake kwa waandishi wa habari (hawapo kwenye picha)  ya utekelezaji wa shughuli za kilimo msimu wa 2013/2014 ambapo wanatarajia kuvuna tani 144,826 mazao ya chakula na hivyo kuwa na ziada tani 83,090.Mahitaji ya wakazi wa wilaya hiyo 225,521,ni tani 61,736 kwa mwaka.
Afisa kilimo halmashauri ya wilaya ya Ikungi mkoa wa Singida, Ayubu Sengo.

HALMASHAURI ya Wilaya ya Ikungi mkoani Singida inatarajia kulima hekta 84,014 za mazao ya chakula msimu huu wa 2013/2014 na wanatarajia kuvuna tani 144,826.

Halmashauri hiyo ya Ikungi yenye jumla ya wakazi 225,521 ambao mahitaji yao ya chakula kwa mwaka ni tani 61,736, kwa matarajio ya mavuno ya msimu huu ya tani 144,826, halmashauri hiyo mpya itakuwa na ziada ya tani 83,090 ya mazao ya chakula.

Hayo yamesemwa hivi karibuni na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Protace Magayane wakati akitoa taarifa yake ya utekelezaji wa shughuli za kilimo msimu wa 2013/2014.

Alitaja mazao hayo na hekta zake kwenye mabano kuwa ni mtama (34,498), uwele (35,629), mounga (3,012), mhogo (1,500) na viazi vitamu (4,500).

Magayane alitaja mazao mengine ya chakula kuwa ni maharage (2,875), kunde (1,500) na njugumawe (500).

Mkurugenzi huyo amesema mafaniko hayo yatatokana na upatikanaji wa mvua yenye mtawanyiko mzuri kanuni bora za kilimo ikiwemo matumizi ya mbolea na mbegu bora.

Kwa upande wa mazao ya biashara, Magayane amesema wamejiwekea lengo la kulima hekta 22,097 na matarajio ni kuvuna tani 45,431.3.


Wakati huo huo, Mkurugenzi huyo, amesema wamesambaza

MAJAMBAZI MAWILI YAUWAWA (Samahani Kwa Picha Hizi)


WATU wawili wakazi wa manispaa ya Singida ambao majina yao bado hayajajulikana,wakiwa kwenye Jokofu la kuhifadhia maiti baada ya kuuawa wakati wa majibishano ya risasi na polisi.
Kamanda wa polisi mkoa wa Singida,SACP Geofrey Kamwela,akionyesha bunduki ya kijeshi aina ya SMG no.34555  iliyokuwa ikitumiwa na watu wawili wanaodhaniwa kuwa majamabazi katika kijiji cha Manga manispaa ya Singida.

JESHI  la Polisi mkoani Singida limewauwa watu wawili wanaodhaniwa kuwa ni majambazi wakati wa kurushiana rasasi.
Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Singida, SACP, Geofrey Kamwela amesema tukio hilo limetokea desemba tisa mwaka huu saa 12:00 jioni, huko katika kijiji cha Manga nje kidogo ya mji wa Singida.
Amesema watu watatu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi wakiwa na bunduki moja ya kijeshi aina ya SMG, walifika kijijini hapo kwa lengo la kufanya uhalifu.
Kamanda Kamwela, amesema watu hao ambao miili yao imehifadhi kwenye chumba cha mochwari katika hospitali ya mkoa, majina na makazi yao bado hayajajulikana.
Akifafanua, amesema taarifa za siri kutoka kwa raia wema zilifikia jeshi la polisi na ndipo askari polisi walipofika kwenye eneo la tukio.
“Baada ya polisi kufika kijijini hapo watu hao walistuka kuwa wanafuatilwa na askari polisi na hivyo kuanza kukimbia kuelekea kijiji cha Uhamaka kwa kutumia pikipiki yenye namba za usajili T. 634 BTW aina ya Sanlag yenye rangi nyeusi”,amesema Kamwela.
Amesema walipoona Polisi wanawakaribia waliamua kutelekeza pikipiki yao hiyo na kuanza kukimbilia porini kwa miguu.
“Hali ilipokuwa ngumu zaidi, walianza kuwarushia polisi risasi, hivyo polisi nao ikwabidi kujibu mapigo.  Katika majibizao hayo ya risasi, majambazi mawili yaliweza kujeruhiwa huku mmoja akifanikiwa kutoroka”
Amesema majambazi hayo yaliyojeruhiwa yalifariki dunia wakati yanakimbizwa katika hospitali ya mkoa kwa matibabu,lakini yakafia njiani.
Amesema katika eneo la tukio, ilipatikana