Tuesday, February 11, 2014

Tanesco kutumia shilingi 48 bilioni kusambaza Umeme Vijijini Singida.

Meneja wa TANESCO mkoa wa Singida, Maclean Mbonile akiwa ofisini kwake kutekeleza majukumu yake ya kila siku.

SHIRIKA la umeme Tanzania (TANESCO) Mkoa wa singida linatarajia kutumia zaidi ya shs. 48.3 bilioni kugharamiwa awamu mbili za miradi ya usambazaji umeme vijijini chini ya mpango wa matokeo makubwa sasa (BRN).

Akizungumuza na waandishi wa habari ofisini kwake hivi karibun, Meneja wa TANESCO mkoa wa singida, Maclean Mbonile amesema miradi yote inafadhiliwa na wakala wa nishati vijijini (REA ).

Amesema awamu ya kwanza utekelezaji wake ilianza julai 2010 na kukamilika mwishoni mwa Septemba mwaka jana. Awamu hiyo imegharimu  dola za kimarekani 9.94 milioni.

Amesema awamu ya pili imeanza kutekeleza mapema oktomba jana (2013), na inatarajiwa kukamilika ndani ya miezi 24. Awamu hii ya pili, inakadiriwa kugharimu jumla ya dola za kimarekani 20 milioni.

Mbonile amesema utekelezaji wa miradi hiyo, unasimamiwa na TANESCO  pamoja na uongozi wa serikali ya mkoa wa Singida .Ujenzi wake unafanywa na mkadarasi  binafsi aliyeshinda zabuni  M/S Spencon Services Ltd.

“Awamu ya kwanza tumeweza kuwapatia huduma ya umeme wananchi /wateja

Wednesday, February 5, 2014

Matembezi ya mshikamano ya CCM manispaa ya Singida.

Baadhi ya wanachama wa CCM manispaa ya Singida,wakishiriki matembezi ya mshikamano ya kilomita kumi ikiwa ni sehemu ya sherehe ya maadhimisho ya CCM kutimiza miaka 37 toka kianzishwe.
Katibu wa CCM mkoa wa Singida,Naomi Kampambala ( mstari wa pili wa kwanza kulia mwenye kofia kapelo) akijumuika na wanaCCM wa manispaa ya Singida,kwenye matembezi ya mshikamano yaliyofanyika jana ya kilomita kumi.

Mstahiki meya wa halmashauri ya manispaa ya Singida na sheikh wa mkoa wa Singida,Sheikh Salum Mahami,(wa pili kushoto) akishiriki matembezi ya kilomita kumi ya mshikamano ya CCM .

Shirika lisilo la Kiserikali latumia zaidi ya shilingi 562 milioni kugharamia sekta ya maji na usafi wa mazingira

Mkurugenzi wa shirika lisilo la kiserikali la Health Actions Promotion Association (HAPA) la mjini Singida, David Mkanje, akiwa ofisini kwake akitekeleza majukumu yake.

SHIRIKA lisilo la kiserikali la Health Action Promotion Association (HAPA) la mkoani hapa limetumia zaidi ya shilingi 562 milioni kugharamia sekta ya maji na usafi wa mazingira katika mkoa wa Singida na Morogoro.

Hayo yamesemwa hivi karibuni na mkurugenzi wa HAPA,David Mnkaje wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi ofisini kwake juu ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ya wananchi katika kipindi cha kuanzia januari hadi desemba mwaka jana.

Amesema kati ya fedha hizo,zimetumika kwenye ujenzi wa vyoo bora na vya kisasa katika shule za msingi tano wilayani Iramba.Shule hizo zilizonufaika na mradi huo ni Dominiki,Midimbwi,Munguli,Nyahaa na Lugongo.

Aidha,Mnkeje amesema kupitia projecti ya WFP,wamejenga matenki 48 ya kuvunia maji ya mvua katika baadhi ya shule za msingi zilizopo wilaya ya Kishapu mkoa wa Shinyanga,Kondoa (Dodoma),Iramba,Singida vijijini na Ikungi zote za mkoa wa Singida.

“Pia katika mwaka uliopita,tumeweza kujenga zahanati na kusaidia baadhi ya vitendea kazi katika vijiji vya Kinampundu na Milade vya wilaya ya Mkalama.Kazi hii ya kujivunia,tumesaidina na vijana wa kujitolea (volunteers) kutoka nje ya nchi (ulaya) na wakazi wa vijiji husika”,amesema Mnkeje kwa kujiamini.

Katika hatua nyingine,Mkurugenzi huyo amesema kupitia project nyingine iliyofadhiliwa na Care,alisema kujenga vyoo bora kabisa katika shule za msingi za Mkundi,Chaumbele na Madege vya wilaya ya Mvomero katika mkoa wa Morogoro.Shule hizo pia zilijengewa matanki ya kuvunia maji ya mvua.

“Kwa mkoa wa Morogoro,kupitia mradi mwingine wa WADA,tumeweza kujenga

Shirika lisilo la kiserikali toka Uingereza lakabidhi vifaa vya thamani Tsh 20m kwa mafundi wadogo.

Katibu tawala mkoa wa Singida, Hassan Liana, akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi vifaa kwa mafundi wadogo wa useremala,ushonaji wa nguo,uhunzi na ujenzi.Vifaa hivyo vyenye thamani ya zaidi ya shilingi 20 milioni,vimetolewa na shirika la Tools for self reliance la nchini Wales Uingereza na zimepitia SIDO mkoa wa Singida.


Katibu tawala mkoa wa Singida, Hassan Liana (wa pili kulia) akikabidhi cherehani kwa mmoja wa kiongozi wa vikundi 17 vilivyonufaika na msaada wa vifaa vya ufundi vilivyotolewa na shirika la Tools for self reliance la nchini Wales Uingereza.Wa kwanza kulia ni meneja wa SIDO mkoa wa Singida, Shoma Kibende.
Katibu tawala mkoa wa Singida, Hassan Liana, akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wa vikundi 17 vya mafundi wa fani mbalimbali muda mfupi baada ya kuwakabidhi vifaa vya ufundi vilivyotolewa na shirika la Tools for self reliance la nchini Wales Uingereza.Wa kwanza kushoto ni mejena wa SIDO mkoa wa Singida, ndugu Shoma Kibende.

Wakazi wa kanda ya kati waomba kutoa taarifa sahihi ya nguvu kazi ya Taifa.

Mkuu wa wilaya ya Singida,Queen Mlozi, akizungumza kwenye ufunguzi wa mafunzo ya wiki mbili ya wadadisi na wahariri wa utafiti wa watu wenye uwezo wa kufanya kazi katika mikoa ya Singida ,Dodoma, Tabora na Kigoma.Mafunzo hayo yanafanyikia kwenye ukumbi wa mikutano wa VETA mjini Singida.
Baadhi ya wadadisi na wahariri wa utafiti wa watu wenye uwezo wa kufanya kazi katika mikoa ya Kigoma, Tabora, Singida na Dodoma wakiwa kwenye mafunzo ya wiki mbili yanayohusu utafiti huo unaotarajiwa kufanyika mapema mwezi ujao.
Mkuu wa wilaya ya Singida, Queen Mlozi (wa pili kulia) akiwa kwenye picha ya pamoja na wadadisi na wahariri wa utafiti wa watu wenye uwezo wa kufanya kazi katika mikoa ya Singida,Kigoma,Tabora na Dodoma na wakufunzi wao.

MKUU  wa Mkoa wa Singida, Dk. Parseko Kone amewataka wakazi wa kanda ya kati kutoa taarifa sahihi kwa wadadisi na wahariri wa utafiti wa watu wenye uwezo wa kufanya kazi ili serikali iweze kutambua hali halisi ya ajira nchini.

Dr. Kone ametoa wito huo hivi karibuni wakati akifungua mafunzo ya wadadisi na wahariri wa utafiti wa watu wenye uwezo wa kufanya kazi wa mwaka 2014.

Amesema utafiti huo ambao mahojiano yake yanatarajiwa kufanywa katika kaya 11,520 nchini, unatarajiwa kuanza mapema mwezi ujao wa februari.

Dk. Kone amesema utafiti huo wa nguvu kazi nchini, utatoa viashiria muhimu ikiwemo kujua hali ya ajira nchini katika sekta rasmi na isiyo rasmi.

“Pia utatusaidia kujua kiwango cha ukosefu wa ajira, kiwango cha ajira isiyo timilifu, ajira mbaya, ajira hatarishi kwa watoto, hali ya kipato kutokana na ajira, matumizi ya muda na ajira mpya zilizozalishwa katika kipindi cha kuanzia mwaka 2006/ hadi 2013”,amesema.

Aidha Mkuu huyo wa mkoa katika hotuba yake ilisomwa kwa niaba yake na DC wa Singida, Queen Mlozi, amewahakikishia wananchi kwamba taarifa watakazotoa zitakuwa ni za siri na zitatumika tu kwa matumizi ya kitakwimu pekee.

Kutokana na umuhimu wa utafiti huo, Dk. Kone amewahimiza wananchi wa mikoa ya Singida, Dodoma, Tabora na Kigoma kutoa

Shirika lisilo la kiserikali latumia shilingi 1.5 bilioni kwenye miradi

Mkurugenzi wa shirika lisilo la kiserikali la Health Actions Promotion Association (HAPA) la mjini Singida,David Mkanje akiwa ofisini kwake akitekeleza majukumu yake.

SHIRIKA lisilo la kiserikali la Health Actions Promotion Association (HAPA) limetumia zaidi ya shilingi 1.5 bilioni katika kutekeleza miradi miwili mkoani hapa katika kipindi cha kuanzia janauari hadi desemba mwaka jana.

Miradi hiyo ni wa ushiriki sawa wa wanaume katika afya ya uzazi na jinsia (TMEP), uliofadhiliwa na shirika la RFSU la nchini Sweden kwa zaidi ya shilingi bilioni moja.

Mradi mwingine ni ule wa Pamoja Tunaweza (UFBR) ambao umefadhiliwa na shirika la SIMAVI la nchini Uholanzi, kwa kiasi cha shilingi milioni mia tano.

Hayo yamesemwa hivi karibuni na Mkurugenzi wa HAPA,David Mkanje alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi ofisini kwake juu ya shughuli zilizofanywa na shirika hilo kongwe, kwa kipindi cha mwaka jana.

Kuhusu mradi wa ushiriki sawa wa wanaume katika afya ya uzani na jinsia,Mkanje amesema kuwa kata 21 za wilaya ya Manyoni,zimenufaika na maradi huo.

“Kwa upande wa manispaa ya Singida,jumla ya kata 13 ns Singida vijijini kata 28 nazo zimenufaika na mradi huo”,amesema na kuongeza kwa kusema;

“Mradi huu ni wa uhamasishaji kuhusu masuala ya afya ya uzazi na jinsia,ambapo wanaume wanalengwa kuwa chachu ya mabadiliko katika kuhakikisha matatizo yatokanayo na uzazu,yanakwisha”alifafanua Mkurugenzi huyo.

Katika hatua nyingine,Mkanje amesema kuwa mradi wa Pamoja Tunaweza (UFBR), umetekelezwa kwenye wilaya ya

Chadema kuendelea kuwavua uanachama viongozi mamluki.

Baadhi ya wakazi wa mji wa Singida,wakipokea helkopta iliyombeba mwanasheria wa CHADEMA, Tundu Lissu,ambaye alihutubia kwenye uwanja wa Ukombozi mjini Singida.
Mwanasheria wa CHADEMA Tundu Lissu,akihutubia mamia ya wakazi wa mji wa Singida katika operation ya kuimarisha chama hicho.Mkutano huo ulifanyika katika uwanja vya Ukombozi mjini Singida.

Baadhi wa wakazi wa Singida mjini,wakimsikiliza mwanasheria wa CHADEMA Tundu Lissu, wakati akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Ukombozi mjini Singida.

MWENYEKITI wa Baraza la Vijana Taifa (BAVITA), John Heche amesema Chadema kitaendelea kuwavua uanachama kiongozi au mwanachama  yeyote, pindi anapobainika kusaliti ustawi wa chama hicho.

Heche aliyasema hayo hivi karibuni wakati akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa ukombozi mjini hapa.

Amesema CHADEMA kamwe haitawalea wasaliti kama CCM ambayo inalea mafisadi na mawaziri mizigo,itaendelea kuwavua uanachama wasaliti bila kujali umaarufu wa mtu au kiongozi.

 “Kelele zimepingwa sana kwamba CHADEMA sasa kinakufa kisa eti Zitto Kabwe,amevuliwa nafasi zake zote za uongozi.Wanasingida,hivi kweli CHADEMA ife kwa sababu ya mtu mmoja tu.Haitatokea kabisa”,amesema na kuongeza;

 “Viongozi wote mashuhuri hivi sasa kwenye chama cha CHADEMA,hata wakiondoka,chama kitabaki pale pale na hakitaterereka.Hakuna kiongozi au mwanachama ambaye yupo juu ya CHADEMA,kwa hiyo sisi viongozi tutaondoka,lakini CHADEMA itabaki pale pale”,alisisitiza Mwenyekiti huyo.

Heche amesema CHADEMA ikichukua dola,haitawalinda mafisadi au viongozi mizigo kama inavyofanya CCM,CHADEMA itawafukizia mbali na endapo kutakuwa na adhabu ya kuwanyonga hadi wafe,adhabu hiyo itatekelezwa bila ubishi.

Kwa upande wake Mwanasheria wa CHADEMA,Tundu Lissu amewataka Watanzania mwakani (2015),kuchagua