Friday, October 28, 2011

Miradi 10 Yazinduliwa Na Mwenge Wa Uhuru Singida

Mkuu wa mkoa Dodoma Rehema Nchimbi akimkabidhi Mwenge wa Uhuru mwenzake wa mkoa Singida Dk.Parseko Kone, katika kijiji cha Lusilile,wilayani Manyoni

Katibu tawala wa mkoa wa Singida Liana Hassan(Kulia), akiteta jambo na wasaidizi wake, kabla ya kuupokea Mwenge wa Uhuru ulioanza mbio zake mkoani Singida leo jumatatu.

Kiongozi wa mbio za Mwenge mwaka huu Mtumwa Rashid Khalfani,kutoka mkoa wa Kaskazini Unguja, akiweka jiwe la msingi, jengo la utawala shule ya sekondari Ikungi, wilayani Singida jana lililojengwa kwa gharama ya zaidi ya Sh.Milioni 38.

Mkuu wa mkoa wa Dodoma akiauaga Mwenge kwa kuselelebuka, katika kijiji cha Lusilile kilichopo mpakani mwa Singida na Dodoma

Oktoba 24,2011:JUMLA ya miradi kumi yenye thamani ya zaidi ya Shilingi Bilioni 129.2, imezinduliwa, kufunguliwa na kuwekewa mawe ya msingi, na Mwenge wa Uhuru mwaka huu, mkoani Dodoma.
Hayo yamebainishwa jana na Mkuu wa mkoa huo, Rehema Nchimbi, kwenye makabidhiano ya Mwenge wa Uhuru, kwa uongozi wa mkoa wa Singida,yaliyofanyika katika kijiji cha Lusilile,wilayani Manyoni

No comments:

Post a Comment