Friday, October 28, 2011

Mwenge Waanza Mbio Za Siku Mbili Tabora kutokea Singida

Mwalimu mkuu shule ya Msingi Uwanza, wilaya Iramba Maria Ntoga akisoma taarifa fupi ya msitu wa asili unaomilikiwa na vijiji viwili vya Gumanga na Msingi, kabla ya kuziduliwa rasmi na kiongozi wa mbio za Mwenge Fatuma Rashid Khalfan.

Wakimbiza mwenge wakiwa picha ya pamoja leo asubuhi katika kijiji cha Shelui,Iramba, kabla ya kuanza safari kuelekea mpakani mwa mikoa ya Singida na Tabora.

Mkuu wa wilaya Igunga hajati Fatuma Kimario akiwa na mkuu wa mkoa wa Tabora Fatuma Mwasa, wakisubiri mpakani kukabidhiwa Mwenge wa Uhuru kutoka kwa uongozi wa mkoa Singida

Mkuu wa mkoa Singida Dk.Parseko Kone(kushoto),akimkabidhi Mwenge wa Uhuru mkuu wa mkoa Tabora Fatuma Mwasa, leo asubuhi mpakani mwa mikoa hiyo.

Kiongozi wa mbio za Mwenge akiwa amewakabidhi chandarua, sare za shule na viatu watoto wanao ishi katika maingira hatarishi wanaosoma shule ya Uwanza, tarafa ya Kinampanda.vifaa hivyo vimegharamiwa na halmashauri ya wilaya ya Iramba

Jamii ya kabila la Kitaturu wanaoishi wilayani Igunga, wakiendelea na shamra shamra baada ya uongozi wa wilaya hiyo kukabidhiwa Mwenge wa uhuru kuendelea na mbio zake.

Mwenge wa uhuru umemaliza mbio zake za siku mbili mkoani Singida jana jioni, na leo jumatano asubuhi umekabidhiwa kwa uongozi wa mkoa wa Tabora, Ukiwa Singida umekimbizwa kilomita 348.7 na kuzindua,kufungua na kuweka mawe ya msingi katika miradi 18,ya thamani ya zaidi ya Sh.Milioni 448.7.

No comments:

Post a Comment