Saturday, October 22, 2011

Mkuu Wa Mkoa Wa Singida Akagua Ujenzi Wa Barabara Manyoni-Ch​aya(Tabora​)

Barabara hii ya Manyoni-Chaya(Tabora), ikijengwa kwa kasi,moja ya lori likionekana likimwaga mchanga kwenye barabara hiyo inayoigharimu serikali zaidi ya Sh.Bilioni 109.6, mradi huu unajengwa na kampuni ya Sinohydro,kutoka nchini China, wakati mkuu wa mkoa wa Singida Dk.Parseko Kone alipotembelea kujionea maendeleo yake

:Mkuu wa mkoa Singida Dk.Parseko Kone mwenye kofia ya bluu, akitaka ufafanuzi kwa mhandisi mshauri wa mradi wa barabara hiyo, kampuni ya Nicolous Odoya ya nchini Island,Bw. Patrick Gayer.

Mkuu wa mkoa wa Singida Dk.Parseko Kone akionyeshwa moja ya karo yanayotumika kuhifadhia maji kabla ya kutumiwa kwenye shughuli za ujenzi wa barabara hiyo yenye umbali wa kilomita 89.3, kutoka Manyoni(Singida) hadi Chaya(Tabora)

MKUU wa mkoa wa Singida Dk.Parseko Kone ameyataka makampuni yanayojishughulisha na kandarasi za ujenzi wa barabara, kukamilisha mapema miradi yao, ili kuendana sawa na mikataba wanayoingia na serikali.Dk.Kone ameyasema hayo leo, wakati akikagua mradi mkubwa wa ujenzi wa barabara ya Manyoni(Singida) hadi Chaya mkoani Tabora, kilomita 89.3, unaotekelezwa na kampuni ya SINOHYDRO,kutoka nchini China, kwa gharama ya zaidi ya Sh.Bilioni 109.6.
Hata hivyo aliipongeza kampuni hiyo kwa msingi wa barabara ambao mradi huo upo mbele kwa siku 53, lakini ameitaka kuchukua tahadhari wakati wa masika ambapo mvua huadhiri maendeleo ya ujenzi

No comments:

Post a Comment