Mwalimu mkuu shule ya Msingi Uwanza, wilaya Iramba Maria Ntoga akisoma taarifa fupi ya msitu wa asili unaomilikiwa na vijiji viwili vya Gumanga na Msingi, kabla ya kuziduliwa rasmi na kiongozi wa mbio za Mwenge Fatuma Rashid Khalfan.
Wakimbiza mwenge wakiwa picha ya pamoja leo asubuhi katika kijiji cha Shelui,Iramba, kabla ya kuanza safari kuelekea mpakani mwa mikoa ya Singida na Tabora.
Mkuu wa wilaya Igunga hajati Fatuma Kimario akiwa na mkuu wa mkoa wa Tabora Fatuma Mwasa, wakisubiri mpakani kukabidhiwa Mwenge wa Uhuru kutoka kwa uongozi wa mkoa Singida
Mkuu wa mkoa Singida Dk.Parseko Kone(kushoto),akimkabidhi Mwenge wa Uhuru mkuu wa mkoa Tabora Fatuma Mwasa, leo asubuhi mpakani mwa mikoa hiyo.
Kiongozi wa mbio za Mwenge akiwa amewakabidhi chandarua, sare za shule na viatu watoto wanao ishi katika maingira hatarishi wanaosoma shule ya Uwanza, tarafa ya Kinampanda.vifaa hivyo vimegharamiwa na halmashauri ya wilaya ya Iramba
Jamii ya kabila la Kitaturu wanaoishi wilayani Igunga, wakiendelea na shamra shamra baada ya uongozi wa wilaya hiyo kukabidhiwa Mwenge wa uhuru kuendelea na mbio zake.
Mwenge wa uhuru umemaliza mbio zake za siku mbili mkoani Singida jana jioni, na leo jumatano asubuhi umekabidhiwa kwa uongozi wa mkoa wa Tabora, Ukiwa Singida umekimbizwa kilomita 348.7 na kuzindua,kufungua na kuweka mawe ya msingi katika miradi 18,ya thamani ya zaidi ya Sh.Milioni 448.7.
Friday, October 28, 2011
Miradi 10 Yazinduliwa Na Mwenge Wa Uhuru Singida
Mkuu wa mkoa Dodoma Rehema Nchimbi akimkabidhi Mwenge wa Uhuru mwenzake wa mkoa Singida Dk.Parseko Kone, katika kijiji cha Lusilile,wilayani Manyoni
Katibu tawala wa mkoa wa Singida Liana Hassan(Kulia), akiteta jambo na wasaidizi wake, kabla ya kuupokea Mwenge wa Uhuru ulioanza mbio zake mkoani Singida leo jumatatu.
Kiongozi wa mbio za Mwenge mwaka huu Mtumwa Rashid Khalfani,kutoka mkoa wa Kaskazini Unguja, akiweka jiwe la msingi, jengo la utawala shule ya sekondari Ikungi, wilayani Singida jana lililojengwa kwa gharama ya zaidi ya Sh.Milioni 38.
Mkuu wa mkoa wa Dodoma akiauaga Mwenge kwa kuselelebuka, katika kijiji cha Lusilile kilichopo mpakani mwa Singida na Dodoma
Oktoba 24,2011:JUMLA ya miradi kumi yenye thamani ya zaidi ya Shilingi Bilioni 129.2, imezinduliwa, kufunguliwa na kuwekewa mawe ya msingi, na Mwenge wa Uhuru mwaka huu, mkoani Dodoma.
Hayo yamebainishwa jana na Mkuu wa mkoa huo, Rehema Nchimbi, kwenye makabidhiano ya Mwenge wa Uhuru, kwa uongozi wa mkoa wa Singida,yaliyofanyika katika kijiji cha Lusilile,wilayani Manyoni
Katibu tawala wa mkoa wa Singida Liana Hassan(Kulia), akiteta jambo na wasaidizi wake, kabla ya kuupokea Mwenge wa Uhuru ulioanza mbio zake mkoani Singida leo jumatatu.
Kiongozi wa mbio za Mwenge mwaka huu Mtumwa Rashid Khalfani,kutoka mkoa wa Kaskazini Unguja, akiweka jiwe la msingi, jengo la utawala shule ya sekondari Ikungi, wilayani Singida jana lililojengwa kwa gharama ya zaidi ya Sh.Milioni 38.
Mkuu wa mkoa wa Dodoma akiauaga Mwenge kwa kuselelebuka, katika kijiji cha Lusilile kilichopo mpakani mwa Singida na Dodoma
Oktoba 24,2011:JUMLA ya miradi kumi yenye thamani ya zaidi ya Shilingi Bilioni 129.2, imezinduliwa, kufunguliwa na kuwekewa mawe ya msingi, na Mwenge wa Uhuru mwaka huu, mkoani Dodoma.
Hayo yamebainishwa jana na Mkuu wa mkoa huo, Rehema Nchimbi, kwenye makabidhiano ya Mwenge wa Uhuru, kwa uongozi wa mkoa wa Singida,yaliyofanyika katika kijiji cha Lusilile,wilayani Manyoni
Msafara Wa Punda!
Na mbwa wamo ingawa hawaonekani. Pichani msafara wa punda waliobeba magunia ya mkawa ukielekea Singida Mjini kutoka vijiji vya kando ya mji. Picha hii nimeipiga leo alfajiri kabla ya kupambazuka
Sunday, October 23, 2011
Vita CCM yamgusa mtoto wa JK, Ikulu;MAKUNDI MAWILI YATUNISHIANA MISULI URAIS 2015
MINYUKANO inayohusisha makundi mawili ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), sasa imeanza kugusa taasisi ya Urais baada ya jina la Rais Jakaya Kikwete, mwanawe, Ridhwan na Ikulu kuanza kuhusishwa katika malumbano yanayoendelea.Jina la Rais na Ikulu limeanza kutajwa hivi karibuni katika mgogoro ulioanza baada ya moja ya kundi la Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa chama hicho, (UVCCM), likiongozwa na Kaimu Mwenyekiti wake wa taifa, Benno
Malisa na baadhi ya wenyeviti wa mikoa wa umoja huo, kuzuiwa na Jeshi la Polisi kufugua matawi mkoani Arusha, kwa kile kilichodaiwa maelekezo ya mtoto wa kigogo.
Ingawa Malisa na wenzake hawakutaja jina la mtoto huyo wa kigogo
walipohutubia mkutano wa hadhara uliofanyika eneo la Hospitali ya St. Thomas mjini Arusha, Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Arusha, James Ole Millya alimtaja,Ridhwani Kikwete kuhusika na njama za kuzuia shughuli hiyo alipozungumza na waandishi wa habari katika Hoteli ya Lash Garden, walikofikia viongozi hao.
“Ingawa polisi wanadai kutunyima kibali cha maandamano ya kufungua mashina ya Umoja wa Vijana na mkutano wa hadhara kwa kile wanachodai taarifa za kiintelijensia kugundua kutatokea uvunjifu wa amani, tumepata habari kuwa Ridhwan ndiye kapiga simu kuelekeza tunyimwe.Sisi tutaendelea na shughuli yetu liwalo na liwe, wacha watupige mabomu kama Chadema,” alisema Millya.
Millya pia alimshambulia Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Halmashauri Kuu ya CCM, Nape Nnauye na kumtaja kama ugonjwa wa saratani kwa chama hicho na kuonya kwamba kama hatadhibitiwa, atasababisha anguko la chama.
Millya alizungumzia pia tamko la Baraza la UVCCM Mkoa wa Pwani lilotolewa mapema mwaka huu na kuzua mtafaruku miongoni mwa wanaCCM kuwa rais ajaye hawezi kutoka Kanda ya Kaskazini na kwamba ni Rais Kikwete pekee ndiye anayemjua mrithi wake.
Mwenyekiti huyo alisema kauli hiyo ni tata, kandamizi na yenye kuonyesha dharau kwa watu wa Kanda ya Kaskazini na demokrasia nchini na kuongeza kuwa Ikulu na Rais Kikwete, ilipaswa kutolea kauli ya kuthibitisha au kukanusha maneno hayo ya vijana wa Mkoa wa Pwani yaliyotamkwa mbele ya Ridhwan lakini hadi sasa hakuna ufafanuzi uliotolewa, hivyo kuzua hofu kuwa pengine vijana hao walielekezwa kutoa ujumbe huo na mamlaka za juu za nchi (Rais na Ikulu).
Kiongozi mwingine wa CCM ambaye wiki hii alimrushia kombora Nape, ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Arusha, Onesmo Ole Nangole aliyedai kuwa Katibu huyo kwa sasa hafanyi kazi ya kueneza na kujenga chama badala yake anakibomoa kwa kung’ang’ania hoja ya kujivua gamba, akilenga watu binafsi hivyo kupotosha nia njema ya Rais Kikwete iliyeanisha falsafa hiyo, akilenga marekebisho ya mfumo mzima wa uongozi, uanachama na chaguzi ndani ya chama.
Ole Nangole ambaye pia alizungumza na waandishi mjini Arusha, alienda mbali zaidi kwa kumuita Nape kuwa ‘muasi namba moja’ ndani ya CCM baada ya kutajwa kuwa miongoni mwa waasisi wa Chama Cha Jamii (CCJ), kilichokwama kupata usajili baada ya kushindwa kutimiza masharti.
Mtu mwingine aliyemshambulia hadharani Nape ni Kaimu Mwenyekiti wa UVCCM taifa, Malisa aliyedai Katibu huyo wa Itikadi na Uenezi, anapotosha nia na kauli ya Rais Kikwete kuhusu dhana ya kujivua gamba kwa kung’ang’ania kutaja majina ya viongozi wachache ndani ya chama kuwa ndio walengwa wa falsafa hiyo.
Akijibu tuhuma hizo Nape, alisema kuna kundi dogo la watu ndani ya chama hicho wenye nguvu ya pesa, wanaotaka kufanya njama za kumng'oa mwenyekiti wa CCM Rais Kikwete, kwa kigezo cha kutenganisha kofia mbili, urais na uenyekiti.
Matukio makubwa yaliyotokea wiki hii ya Makamu Mwenyekiti wa UVCCM taifa, Malisa kutoa matamshi mazito ya kumshutumu Mwenyekiti wa Kamati ya Miradi na Uchumi ya Umoja huo Ridhwan hadharani, yameibua sura mpya ya mvutano huo.
Malisa ambaye awali alikuwa swahiba mkubwa wa Ridhiwan ambaye ni mtoto wa Mwenyekiti wa taifa wa CCM Rais Kikwete, wakati wa kampeni za kuwania Uenyekiti wa Umoja huo mjini Dodoma, walikuwa kambi moja wakipigana kushawishi wajumbe, sasa hawako pamoja tena.
Nguvu za makundi ikoje?
Kundi la watuhumiwa wa ufisadi
Nguvu kubwa ya kundi hili linalodaiwa kuongozwa na makada wanaohumiwa kwa ufisadi ndani ya chama hicho ni;
1. Kuwa na mtandao mkubwa ndani ya chama ambao ulitumika kumwingiza Rais Jakaya Kikwete madarakani katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005.
2. Jumuia zote za chama ukiwemo Umoja wa Vijana (UVCCM), Umoja wa Wanawake (UWT) na Jumuiya ya Wazazi ambazo zina wanachama hadi ngazi ya shina.
3. Kundi hili linaungwa mkono pia na wenyeviti wa mikoa
19 wa CCM kutoka bara na visiwani
4. Lina nusu ya wajumbe wa Halmashuari Kuu ya Taifa
(NEC) wanaoweza kushinikiza maamuzi magumu
yakapitishwa na chama.
5. Kundi hili pia lina nguvu kubwa ndani ya bunge likiwa
na wabunge wengi wa CCM wanaoliunga mkono.
6. Lina nguvu kubwa ya fedha inayolifanya kutumia
kuwashawishi wana CCM wengi kuliunga mkono.
Nguvu ya kundi la Mwenyekiti Kikwete
Kundi hili ni lile la wana CCM wanaounga mkono maamuzi ya Mwenyekiti wa chama hicho, Rais Kikwete ya chama kujivua gamba.
1. Kundi hili linaungwa mkono na viongozi ndani ya CCM ambao wanapambana na ufisadi wakiwamo baadhi ya wabunge, mawaziri, makada na wanachama wa kawaida wa chama hicho.
2. Nguvu nyingine ya kundi hili, ni kwamba linaongozwa na Mwenyekiti ambaye ana dola, ana uwezo wa kuteua viongozi mbalimbali hususan makatibu wa CCM wa mikoa na wilaya.
3. Mwenyekiti ana nguvu kwenye vikao, anaweza kunishikiza jambo ambalo analitaka na likafanyika kama anataka.
4. Mwenyekiti anaungwa mkono na wanachama wa kawaida wa CCM ambao wengi wao wapo katika ngazi ya matawi.
5. Raslimali zote za chama zipo chini ya Mwenyekiti.
6. Nguvu ya kundi hili pia inatokana na kuungwa mkono na kundi la viongozi wastaafu wa chama wakiwamo baadhi ya mawaziri wakuu.
Kauli za makada wa CCM
Kada wa CCM Mwanza
KADA wa CCM na Diwani wa Kata ya Lugata Kome wilayani Sengerema, Adrian Tizeba amesema falsafa ya chama chake ya kujivua gamba haina lolote kwani haina nia ya kukinusuru bali kuongeza minyukano ya makundi ambayo alisema yatasababisha kifo cha chama hicho.
Aliiambia Mwananchi Jumapili kuwa kutokana na hali ilivyo na jinsi anavyoona mambo ndani ya CCM, chama hicho hivi sasa kimegawanyika katika sura mbili kwa wakati mmoja, hivyo kinaweza kufa.
“Ninachoweza kutabiri juu ya chama changu ni jambo ambalo liko wazi, kutokana na kuwa na makundi mawili moja linalomtii na kuamini misingi ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere, na lingine linaloamini katika kujilimbikizia mali basi, kutaibua fujo kubwa ndani ya chama na kitavunjika,” alieleza.
Alisema kwa upande mwingine wananchi wameanza kuonekana kukichoka kutokana na kutupa misingi ya Baba wa Taifa, hatua ambayo imesababisha chama kutekwa na kundi la wafanyabiashara wanaotaka kujinufaisha.
Mwenyekiti CCM Shinyanga
Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Hamis Mgeja, alisema wana CCM wanapaswa kurudi kwenye kanuni na kutoa matatizo yao kwa njia za vikao na kubainisha kuwa kuyasema majukwaani ama hadharani kunakifanya chama kuonekana kama kina matatizo makubwa.
Mgeja alisema hali inavyoonekana sasa siyo nzuri, hii inatokana na baadhi ya wanachama kukiuka utaratibu wa vikao na kuwa wazungumzaji nje ya vikao.Alionya kwamba iwapo jambo hilo litaendelea basi upo uwezekano wa CCM kupoteza mwelekeo.
“Ninavyoona mwelekeo wa sasa siyo mzuri, chama kinaoutaratibu wa kutumia vikao, lakini kama watu wanazungumza nje ya vikao ni tatizo, cha muhimu ni kuwaomba wanaCCM kurejea kwenye utaribu wa vikao. Tukiendelea kuzungumza nje ya vikao, chama kitaonekana kina matatizo makubwa sana,” alieleza Mgeja.
Ole Millya
Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Arusha, Millya anasema kimsingi mgongano wa kimawazo unaoibuka sasa haulengi kukidhoofisha chama hicho bali ni kuboresha.
"Hiki ni kipindi cha mpito isionekane watu kutoa mawazo kuwa, wanatumiwa au wana njaa, hali kama hii iliwahi kuvikuta vyama vya Labour nchini Uingereza na Democrat nchini Marekani na walikaa na kufikia maamuzi ambayo yamewafanya kuendelea kushika dola,"alisema Millya.
Alisema suala la kusikilizwa maoni ya vijana linapaswa kupewa uzito kwani wao ndio wapigakura wengi kwa sasa na wanaweza kuwa na mawazo chanya ya kukiboresha chama kuelekea uchaguzi mkuu.
"Haya ambayo yanatokea isionekane kuna mpasuko, hapana sote tunataka kujenga chama chetu hivyo maoni na ushauri ufanyiwe kazi na sio kundi moja kudharau lingine,"alisema Millya.
Akizungumzia kauli yake ya mtoto mmoja wa kigogo kuyumbisha chama hicho mkoani Arusha, alisisitiza ni jambo lililowazi na ana ushahidi nalo kama atahitajika kusema.
"Sisi sio vichaa kuibuka majukwaani na kulalamikia hili, tuna ushahidi na nia yetu sio kulumbana ni kutaka mambo yaende vizuri na CCM iendelee kushika dola,"alisema Millya.
Kanda mwingine wa CCM, Julius Mollel alisema katika kila chama ni busara kuzingatia maoni ya pande zote na kufikia maamuzi sahihi badala ya kudharauliana.
"Mimi ninachoona hali ndani ya CCM ni nzuri tu kwani watu wanasema na kuna marekebisho yanafanyika,"alisema Mollel.
Hata hivyo, wanaCCM wengine, Jeremiah Nkya na Solomon Singu, kwa nyakati tofauti walisema kuumbuana hadharani kwa vigogo wa CCM ni mwelekeo wa chama hicho kopoteza heshima na nguvu ya kushika dola.
Nkya alisema ni aibu chama chenye dola, viongozi wake waanze kulaumiana hadharani na kushutumiana kuwa wanataka kuuana halafu waseme ni uhuru wa mawazo.
"Kuna matatizo ndani ya CCM, la muhimu ni kumaliza malalamiko kupitia vikao sahihi," alisema Nkya.
Kwa upande wake, Singu alifafanua zaidi na kusema makundi ndani ya chama hicho, yamekifikisha pabaya na sasa viongozi wake wameshindwa kuheshimiana.
"Leo Nape (Katibu wa Itikadi na Uenezi) anasema hivi, kesho anaibuka Mwenyekiti wa UVCCM anasema vile, hivyo hivyo hata kwa mawaziri hapa hakuna chama tena kila mtu anafanyakazi kivyake"alisema Singu.
Kauli ya Nape
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape alipotafutwa na Mwananchi Jumapili kwa njia ya simu jana, alijibu kwa kifupi kuwa masuala yote hayo yatazungumzwa kwenye vikao vya chama.
“Masuala yote haya yatajadiliwa kwenye vikao vya chama vitakavyokuja,” alisema Nape bila kutaja ni kikao gani ambacho kitajadili mvutano huo.
“Uamuzi wa kikao gani tutazungumza ni wetu sio wenu, kikao kitakachokuwa na hadhi ya kujadili jambo hili basi litajadiliwa,” aliongeza Nape.
Ridhiwan Kikwete
Ridhwan alipotafutwa kwa njia ya simu kuzungumzia hali hiyo hakupatikana na hata alipoandikiwa ujumbe mfupi wa simu, hakujibu.
Katika kuonyesha kuongezeka kwa fukuto la kisiasa ndani ya chama hicho, kada wa maarufu wa chama hicho, aliyekuwa pia Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz, Juni mwaka huu alitangaza kujivua nyadhifa zote ndani ya chama, huku akiweka wazi kwamba amechoshwa na siasa uchwara zinazoendeshwa na baadhi ya wanasiasa ndani ya chama hicho.
Edward Lowassa
Wiki hii Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa naye alivunja ukimya kwa kuzungumzia tuhuma mbalimbali zinazoelekezwa kwake, huku akisisitiza kuwa amechoka kukashifiwa na sasa kamwe hatawavumilia wanaomzulia mambo.
Alisema kuanzia sasa hatakubali kuchafuliwa jina na mtu yeyote au chombo chochote cha habari na atakayefanya hivyo, ajiandae kukabiliana na mkono wa sheria.
Alisisitiza kuwa ni jambo lisiloingia akilini kumhusisha yeye na kile kinachodaiwa mkakati wa kumhujumu Rais Kikwete au CCM, wakati yeye ni mbunge anayetokana na chama hicho na kiongozi wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya nje, Ulinzi na Usalama .
Gaddafi ana utajiri wa Sh 140 trilioni:NI SAWA NA BAJETI YA TANZANIA KWA MIAKA 12
KIONGOZI wa Libya aliyeuawa juzi na wapiganaji wa Serikali ya Mpito (NTC), anadaiwa kuacha utajiri wa Sh 139 trioni kiasi ambacho ni sawa na bajeti ya Tanzania kwa miaka 12. Habari zilizopatikana jana zimeeleza kuwa fedha hizo ni zile zinazofahamika, alizoweka kwenye benki za nchi kadhaa duniani, huenda alikuwa na hazina zaidi mbali na hiyo.
Kwa mujibu wa habari hizo, Gaddafi alikuwa anamiliki Pauni 29 bilioni nchini Uingereza (Sh78 trilioni), Dola 32 bilioni nchini Marekani (Sh54 trilioni) , Dola 2.4 bilioni nchini Canada( Sh4 trilioni) na Dola 1.7 bilioni nchini Australia (Sh3 trilioni). Kwa fedha ya Tanzania. Pauni moja ya Uingereza ni sawa na Sh 2,720, Dola moja ya Marekani Sh 1,704, Dola moja ya Canada, Sh 1,692 na Dola ya Australia ni Sh 1,769.
Fedha hiyo kwa ujumla wake ni sawa na bajeti ya Tanzania kwa miaka 12. Juni mwaka huu, Bunge lilipitisha jumla ya Sh11 trilioni kwa matumizi ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2011/2012 .Kiasi hicho kikizidishwa mara miaka 12 zitakuwa Sh132 trilioni, hivyo ukichukulia kiwango hicho, inamaana kuwa fedha za Gaddafi zinatosha kuendesha Tanzania kwa miaka 12 na bado zitabaki Sh trilioni saba.
Alikuwa na nywele, sura bandia
Vipimo vya DNA vilivyofanywa kwenye mwili wa Gaddafi, vimebaini kuwa kiongozi huyo wa zamani wa Libya, alikuwa na nywele bandia, Jarida la Washington Post limeripoti.Waziri Mkuu wa muda wa Libya, Mahmoud Jibril aliliambia jarida hilo kuwa wachunguzi walifanya vipimo vya damu, mate na nywele na kugundua kuwa nywele hizo si halisi.
Mwili wa kiongozi huyo kwa sasa umehifadhiwa ndani ya msikiti mmoja nje ya mji wa Sirte alikokamatwa na kuuawa ukisubiri kuzikwa baada ya uchunguzi unaotarajiwa kufanywa na Umoja wa Mataifa.
Mwaka 1995, Gaddafi aliwahi kufanyiwa upasuaji wa uso kwa kile alichodai kuwa hataki kuonekana mzee.
“Aliniambia kuwa amekaa madarakani kwa miaka 25 wakati huo na kwamba hataki vijana wa taifa lake wamwone mzee,” alisema Dk Liacyr Ribeiro kutoka Brazil aliyemfanyia upasuaji huo.
Kwa mujibu wa Washington Post, Gaddafi aliwekewa nywele bandia pia aliwekewa mafuta kwenye uso wake yaliyotolewa tumboni, ili kupunguza uwezekano wa uso wake kuonekana wa kizee.
Familia yaomba mwili wa Gaddafi
Mke wa Kanali Gaddafi, Safia, ameibuka na kutaka apewe mwili wa mumewe ili ukazikwe na familia kisha Umoja wa Mataifa ufanye uchunguzi wa kina juu ya kifo chake.Akizungumza kupitia Televisheni ya Rai Tre ya Italia, akiwa uhamishoni nchini Algeria, Safia alisema ni muhimu uchunguzi wa kifo hicho ufanyike ili kujua kama haki ilitendeka ama la.
"Hayo ni makubaliano na familia yangu kwamba tunaomba ufanyike uchunguzi wa kina na baada ya kumalizika kwa uchunguzi tuletewe mwili wake, tutazika wenyewe,"alisema Safia.
Mazishi ya Gaddafi yanayoelezwa kutaka kufanywa kwa siri, yamesitishwa kutokana na tofauti zilizoibuka miongoni mwa maofisa wa Libya baada ya baadhi kutaka ahifadhiwe na wengine atupwe baharini.
Safia alisema; "Kwa utamaduni wa Kiislamu, maziko ya Gaddafi yanapaswa kufanyika haraka iwezekanavyo na sio kuhifadhiwa kwa siku kadhaa. Naomba uchunguzi ufanyike tena wa kimataifa ili ibainike chanzo cha kifo cha Gaddafi," alisema Safia ambaye alieleza kuwa wanawe, walipiga simu ya baba yao mara baada ya kusikia amefariki dunia, lakini mara zote simu hiyo ilipokelewa na waasi.
Kwa mujibu wa vituo vya televisheni vya Dubai na Jordan juzi, mtoto wa kike wa Gaddafi Ayesha, akizungumza kutoka Algeria, alilalamika kwamba waasi wamemuua baba yake na kumfanyia ukatili mkubwa.
"Niliposikia baba yangu ameuawa sikuamini nikampigia simu lakini, ikapokelewa na mapanya hao (waasi) wa Mediteranian," alisema. Ayesha aliungana na mama yake Safia kutaka wapewe mwili wa baba yao ili wakamzike wenyewe, badala ya kuzikwa na waasi hao alioeleza kuwa hawana haki tena dhidi yake, baada ya kumwua.
Ameutaka Umoja wa Mataifa (UN) usaidie urejeshwaji wa mwili wa Gaddafi kwa familia yake ili ndugu na jamaa wamwage na kumzika kwa heshima zote.Hata hivyo, Kamishna wa Kutetea Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, Navi Pillay, alisema ni lazima uchunguzi wa kina ufanyike dhidi ya kifo hicho.
Kaimu Waziri Mkuu wa Libya, Jibril alisema kwamba Kanali Gaddafi alipigwa risasi kichwani wakati alipojaribu kurushiana risasi na waasi.
Serikali mpya kutangazwa leo
Baada ya kifo cha Gaddafi, Serikali mpya ya nchi hiyo inatarajiwa kutangazwa leo. Msemaji wa Jeshi la Libya Abdel-Rahman Busin, alisema kwamba watatangaza kuzaliwa upya kwa Serikali yao katika mji wa Benghazi.
Alisema Serikali hiyo mpya inaiomba familia ya Gaddafi kuhudhuria sherehe hizo za utambulisho Serikali mpya bila wasiwasi wowote kwani baada ya mapinduzi hayo, Libya sasa ni nchi ya kidemokrasia.
“Leo (jana) watu wana furaha na furaha hiyo itaongezeka zaidi kesho (leo) baada ya kutangazwa kwa Serikali yetu mpya ambayo itakuwa ya wananchi wote bila ya ubaguzi,”alisema. Msemaji huyo wa jeshi alieleza kuwa mazishi ya Gaddafi bado hayajajulikana yatafanyika lini lakini kwa vyovyote vile yatasubiri uchunguzi unaotarajiwa kufanywa na Umoja wa Mataifa (UN) wakati wowote kuanzia sasa.
Mabomu, risasi yarindima
VURUGU, milio ya risasi za moto na mabomu ya machozi jana ziligubika mji wa Dodoma kufuatia wakazi wa Mtaa wa Njedengwa, Kata ya Dodoma Makulu kupambana na polisi kupinga hatua ya Manispaa ya Dodoma kuvunja nyumba zao.
Vurugu hizo zilizoanza saa 11.30 alfajiri zilisababisha watu 12 kujeruhiwa vibaya baada ya polisi kutumia mabomu ya machozi na risasi za moto kukabiliana na wakazi wa mtaa huo maarufu mjini Dodoma, wanaodaiwa kuvamia na kujenga katika eneo la mwekezaji.
Risasi za moto zilianza kusikika eneo la tukio huku kundi la polisi pamoja na vijana wenye nguvu (mabaunsa) wakiwa wametanda eneo hilo na kufanya ligeuke uwanja wa mapambano.Mabaunsa hao ambao walikuwa wamefunika nyuso na kuacha sehemu ya macho, waliingia kila nyumba na kuwashambulia waliokuwa ndani huku huku wakiwalazimisha kutoka nje.
Hata hivyo, licha ya polisi kuwa na silaha za moto, wenyeji hao hawakukubali kutii amri, walitoka na silaha za jadi mishale, mapanga na mawe ili kupambana kuzuia bomoa bomoa hiyo.
Baadhi yao walirusha mishale na wengine kutumia mapanga kujihami kila walipovamiwa na vijana hao wenye miraba minne . Hata hivyo wenyeji hao kutokana na silaha dhaifu, walizidiwa nguvu na kujikuta wengi wao wakiwekwa chini ya ulinzi.
Wakati wanaume wakipambana na askari hao, vilio vya akina mama na watoto vilisikika kutoka kila upande huku mabomu ya machozi yaliyokuwa yakipigwa mfululizo yakizidi kuwachaganya.
Hatua ya kubomoa nyumba hizo ilitokana na hukumu ya Mahakama iliyompa haki mtu anayefahamika kwa jina la Maimu (Sinana Enterprises ) kuwa ni mmiliki halali wa eneo hilo ambalo amepewa na Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA) kwa ajili ya kujenga shule.
Kwa mujibu wa maelezo kutoka kwa wenyeji wa eneo hilo, mwekezaji huyo wakati anapewa sehemu hiyo, tayari kulikuwa na nyumba za watu waliokuwa wakiishi hapo kwa muda mrefu.
“Kwa mfano mimi hapa, nilikuta kuna msitu mwaka 1987 nikaanza kulima na mwaka uliofuata nilijenga hii nyumba yangu, lakini huyo mwekezaji yeye alikuja mwaka 2004 sasa jamani kuna haki hapo?’’Alisema mama mmoja ambaye jina lake halikupatikana baada ya kutishiwa kukamatwa na askari aliyekuwa jirani na kumtaka aondoke ili tingatinga libomoe nyumba yake.
Eneo la tukio
Kwa kiasi kikubwa mabaunsa hao wa kampuni iliyopewa kazi na mwekezaji kusimamia ubomoaji huo, ndio walioonekana kuchochea moto huo zaidi, kwani kila wakati walisikika wakitoa lugha za vitisho kwa wenyeji huku wakiwa wamevalia kofia za kufunika uso.“Habaki bweha hapa, lazima mfundishwe adabu zenu maana sisi tumekuja kikazi zaidi na hamtatusahau kabisa maishani mwenu,’’ alisika mmoja wao akisema.
Mali zaharibiwa
Nyumba nyingi zilizobomolewa zilikuwa na vitu mbalimbali vya thamani, isipokuwa wale waliowahi kutoa vyombo vyao nje ambapo tingatinga hilo la CDA halikuweza kuvigusa.
Baadhi ya maduka yalivunjwa na bidhaa zikiwa ndani huku vijana waliokuwepo aneo hilo, wakisomba bia na kugawana baadhi ya vitu hali iliyolazimisha polisi kuanza kuwazuia.
CDA wakataa kubebeshwa lawama
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA), Martin Kitila alikanusha vikali kuhusika kwa mamlaka yake kwenye bomoa bomoa hiyo kwa maelezo kwamba anayevunja, ni mwenye eneo hilo.
“Sisi hatuhusiki kabisa katika uvunjaji huo maana tulishamlikisha mhusika, yeye ndiye mwenye mamlaka ya kufanya atakavyo,’’ alisema Kitila.
Alipotakiwa kueleza ni kwa nini vyombo vyake vimehusika Mkurugenzi huyo alisema, “Hilo sio tatizo kwani mtu yeyote anaweza kuja kuazima vifaa kwetu na tukifikia makubaliano, sisi tunampa’’.
Hata hivyo, Mkurugenzi huyo alipinga suala na wananchi kupewa namba na CDA kuwa ni kigezo cha kuhalalishwa na badala yake alisema namba zinazobandikwa huwa ni kwa ajili ya kuwatambua tu wakazi hao, lakini si uhalali wa kuishi au kupimiwa viwanja.
Vyombo vya habari
Vurugu hizo pia zilizua balaa kwa waandishi wa habari waliokuwa kazini eneo ambao walijikuta wakishambuliwa na polisi waliokuwa wakiwakataza kufanya kazi.
Waandishi wa Mwananchi, walijikuta pikipiki yao ikivunjwa kioo na polisi aliyewalalamikia kuwa gazeti lao ni wambeya huku akiwataka wakaandike chochote watakacho. Polisi pia walikuwa wakizuia waandishi kupiga picha.
Licha ya kuonyesha vitambulisho vyao, mwandishi Masoud Masasi na mfanyakazi mwenzake wa Kampuni ya Mwananchi Communications Ltd, Ali Jumanne waliofika eneo la tukio kwa pikipiki, walipigwa na kuzuiliwa kwa muda hadi mmoja wa waandishi alipofika na kuwasaidia ingawa baadaye askari hao waliomba radhi.
Katika vurugu hizo Jumanne alijeruhiwa mguu wa kushoto.
Kwa upande wao Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC), gari yao ilivunjwa vioo na wananchi kwa madai kuwa hawataki kuwaona kwani ni watu wa Serikali, kabla ya mtangazaji wa Radio Mwangaza, Jane Charles kushambuliwa kwa mawe na wananchi hao na kujeruhiwa.
Kamanda wa Polisi
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Zelothe Stephen hakuweza kuzungumzia tukio hilo kwani muda wote simu yake ilikuwa ikipokelewa na mtu aliyejitaja kwa jina la Yohana na kujitambulisha kuwa ni msaidizi wake.“Mimi ni msaidizi wa Kamanda naitwa Yohana, muda huu Kamanda hawezi kuzungumza na ninyi, yuko kwenye mapokezi ya Mwenge mtafute baadaye,’’alisema mtu huyo na kukata simu.
Mwenye Kampuni
Msemaji wa Kampuni la Sinana ambaye alijitambulisha kwa jina la Mujibu Ali, alisema kuwa kampuni hiyo ilipewa hati ya kumiliki eneo hilo tangu mwaka 2004 na kwamba hapakuwa na nyumba katika eneo lote.
“Hapa tunamiliki ekari 21 ambazo tunataka kujenga shule na tulianza kumiliki tangu mwaka 2004, lakini hawa jamaa walikataa kuondoka na kesi tulishinda mahakamani tangu Julai 25 mwaka huu na kuwapa notisi, lakini bado hawakuondoka,’’alisisitiza Ali.Majeruhi.Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa wa Dodoma, Dk Nassoro Mzee alisema walipokea majeruhi 12 na kukanusha kutokea kwa kifo kwenye tukio hilo.
“Ni kweli tumepokea majeruhi 12 hapa, lakini waliolazwa hadi sasa ni tisa, kati yao wanawake wawili na wanaume ni saba." Wagonjwa hao wanaonekana wamejeruhiwa katika maeneo mbalimbali ya miili yao hata hivyo siwezi kuthibitisha kama ni risasi maana hadi tuzitoe mwilini,’’alisema Mzee.
Akizungumza kwa tabu katika wodi namba moja mmoja wa majeruhi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mukoro Maro, alisema alikatwa mapanga na mabaunsa wakati akijaribu kukoa familia yake.
“Polisi walinikamata na kunipeleka kwa vijana waliovaa kofia za kuficha nyuso ambao walinishambulia kwa mapanga na kunipora simu yangu, alisema Maro huku akiwa amelowa damu kutokana na majeraha makubwa kichwani.
Kwa upande wake Yohana Charles, alisema kuwa yeye alistukia kitu cha moto katika paja la mguu wake wa kushoto wakati akienda kumsaidia mzee aliyekuwa anapigwa na polisi ghafla alianguka chini na kupoteza fahamu baadaye alijikuta hospitalini na kugundua kuwa amepigwa risasi.
Ulinzi hospitalini
Eneo la Hospitali ya Mkoa wa Dodoma lilikuwa na ulinzi mkali, polisi wakiwa wametanda kila kona na silaha za moto hali iliyowatisha watu wengi waliokuwa wakienda hapo kusalimia wagonjwa wao.
Vurugu hizo zilizoanza saa 11.30 alfajiri zilisababisha watu 12 kujeruhiwa vibaya baada ya polisi kutumia mabomu ya machozi na risasi za moto kukabiliana na wakazi wa mtaa huo maarufu mjini Dodoma, wanaodaiwa kuvamia na kujenga katika eneo la mwekezaji.
Risasi za moto zilianza kusikika eneo la tukio huku kundi la polisi pamoja na vijana wenye nguvu (mabaunsa) wakiwa wametanda eneo hilo na kufanya ligeuke uwanja wa mapambano.Mabaunsa hao ambao walikuwa wamefunika nyuso na kuacha sehemu ya macho, waliingia kila nyumba na kuwashambulia waliokuwa ndani huku huku wakiwalazimisha kutoka nje.
Hata hivyo, licha ya polisi kuwa na silaha za moto, wenyeji hao hawakukubali kutii amri, walitoka na silaha za jadi mishale, mapanga na mawe ili kupambana kuzuia bomoa bomoa hiyo.
Baadhi yao walirusha mishale na wengine kutumia mapanga kujihami kila walipovamiwa na vijana hao wenye miraba minne . Hata hivyo wenyeji hao kutokana na silaha dhaifu, walizidiwa nguvu na kujikuta wengi wao wakiwekwa chini ya ulinzi.
Wakati wanaume wakipambana na askari hao, vilio vya akina mama na watoto vilisikika kutoka kila upande huku mabomu ya machozi yaliyokuwa yakipigwa mfululizo yakizidi kuwachaganya.
Hatua ya kubomoa nyumba hizo ilitokana na hukumu ya Mahakama iliyompa haki mtu anayefahamika kwa jina la Maimu (Sinana Enterprises ) kuwa ni mmiliki halali wa eneo hilo ambalo amepewa na Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA) kwa ajili ya kujenga shule.
Kwa mujibu wa maelezo kutoka kwa wenyeji wa eneo hilo, mwekezaji huyo wakati anapewa sehemu hiyo, tayari kulikuwa na nyumba za watu waliokuwa wakiishi hapo kwa muda mrefu.
“Kwa mfano mimi hapa, nilikuta kuna msitu mwaka 1987 nikaanza kulima na mwaka uliofuata nilijenga hii nyumba yangu, lakini huyo mwekezaji yeye alikuja mwaka 2004 sasa jamani kuna haki hapo?’’Alisema mama mmoja ambaye jina lake halikupatikana baada ya kutishiwa kukamatwa na askari aliyekuwa jirani na kumtaka aondoke ili tingatinga libomoe nyumba yake.
Eneo la tukio
Kwa kiasi kikubwa mabaunsa hao wa kampuni iliyopewa kazi na mwekezaji kusimamia ubomoaji huo, ndio walioonekana kuchochea moto huo zaidi, kwani kila wakati walisikika wakitoa lugha za vitisho kwa wenyeji huku wakiwa wamevalia kofia za kufunika uso.“Habaki bweha hapa, lazima mfundishwe adabu zenu maana sisi tumekuja kikazi zaidi na hamtatusahau kabisa maishani mwenu,’’ alisika mmoja wao akisema.
Mali zaharibiwa
Nyumba nyingi zilizobomolewa zilikuwa na vitu mbalimbali vya thamani, isipokuwa wale waliowahi kutoa vyombo vyao nje ambapo tingatinga hilo la CDA halikuweza kuvigusa.
Baadhi ya maduka yalivunjwa na bidhaa zikiwa ndani huku vijana waliokuwepo aneo hilo, wakisomba bia na kugawana baadhi ya vitu hali iliyolazimisha polisi kuanza kuwazuia.
CDA wakataa kubebeshwa lawama
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA), Martin Kitila alikanusha vikali kuhusika kwa mamlaka yake kwenye bomoa bomoa hiyo kwa maelezo kwamba anayevunja, ni mwenye eneo hilo.
“Sisi hatuhusiki kabisa katika uvunjaji huo maana tulishamlikisha mhusika, yeye ndiye mwenye mamlaka ya kufanya atakavyo,’’ alisema Kitila.
Alipotakiwa kueleza ni kwa nini vyombo vyake vimehusika Mkurugenzi huyo alisema, “Hilo sio tatizo kwani mtu yeyote anaweza kuja kuazima vifaa kwetu na tukifikia makubaliano, sisi tunampa’’.
Hata hivyo, Mkurugenzi huyo alipinga suala na wananchi kupewa namba na CDA kuwa ni kigezo cha kuhalalishwa na badala yake alisema namba zinazobandikwa huwa ni kwa ajili ya kuwatambua tu wakazi hao, lakini si uhalali wa kuishi au kupimiwa viwanja.
Vyombo vya habari
Vurugu hizo pia zilizua balaa kwa waandishi wa habari waliokuwa kazini eneo ambao walijikuta wakishambuliwa na polisi waliokuwa wakiwakataza kufanya kazi.
Waandishi wa Mwananchi, walijikuta pikipiki yao ikivunjwa kioo na polisi aliyewalalamikia kuwa gazeti lao ni wambeya huku akiwataka wakaandike chochote watakacho. Polisi pia walikuwa wakizuia waandishi kupiga picha.
Licha ya kuonyesha vitambulisho vyao, mwandishi Masoud Masasi na mfanyakazi mwenzake wa Kampuni ya Mwananchi Communications Ltd, Ali Jumanne waliofika eneo la tukio kwa pikipiki, walipigwa na kuzuiliwa kwa muda hadi mmoja wa waandishi alipofika na kuwasaidia ingawa baadaye askari hao waliomba radhi.
Katika vurugu hizo Jumanne alijeruhiwa mguu wa kushoto.
Kwa upande wao Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC), gari yao ilivunjwa vioo na wananchi kwa madai kuwa hawataki kuwaona kwani ni watu wa Serikali, kabla ya mtangazaji wa Radio Mwangaza, Jane Charles kushambuliwa kwa mawe na wananchi hao na kujeruhiwa.
Kamanda wa Polisi
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Zelothe Stephen hakuweza kuzungumzia tukio hilo kwani muda wote simu yake ilikuwa ikipokelewa na mtu aliyejitaja kwa jina la Yohana na kujitambulisha kuwa ni msaidizi wake.“Mimi ni msaidizi wa Kamanda naitwa Yohana, muda huu Kamanda hawezi kuzungumza na ninyi, yuko kwenye mapokezi ya Mwenge mtafute baadaye,’’alisema mtu huyo na kukata simu.
Mwenye Kampuni
Msemaji wa Kampuni la Sinana ambaye alijitambulisha kwa jina la Mujibu Ali, alisema kuwa kampuni hiyo ilipewa hati ya kumiliki eneo hilo tangu mwaka 2004 na kwamba hapakuwa na nyumba katika eneo lote.
“Hapa tunamiliki ekari 21 ambazo tunataka kujenga shule na tulianza kumiliki tangu mwaka 2004, lakini hawa jamaa walikataa kuondoka na kesi tulishinda mahakamani tangu Julai 25 mwaka huu na kuwapa notisi, lakini bado hawakuondoka,’’alisisitiza Ali.Majeruhi.Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa wa Dodoma, Dk Nassoro Mzee alisema walipokea majeruhi 12 na kukanusha kutokea kwa kifo kwenye tukio hilo.
“Ni kweli tumepokea majeruhi 12 hapa, lakini waliolazwa hadi sasa ni tisa, kati yao wanawake wawili na wanaume ni saba." Wagonjwa hao wanaonekana wamejeruhiwa katika maeneo mbalimbali ya miili yao hata hivyo siwezi kuthibitisha kama ni risasi maana hadi tuzitoe mwilini,’’alisema Mzee.
Akizungumza kwa tabu katika wodi namba moja mmoja wa majeruhi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mukoro Maro, alisema alikatwa mapanga na mabaunsa wakati akijaribu kukoa familia yake.
“Polisi walinikamata na kunipeleka kwa vijana waliovaa kofia za kuficha nyuso ambao walinishambulia kwa mapanga na kunipora simu yangu, alisema Maro huku akiwa amelowa damu kutokana na majeraha makubwa kichwani.
Kwa upande wake Yohana Charles, alisema kuwa yeye alistukia kitu cha moto katika paja la mguu wake wa kushoto wakati akienda kumsaidia mzee aliyekuwa anapigwa na polisi ghafla alianguka chini na kupoteza fahamu baadaye alijikuta hospitalini na kugundua kuwa amepigwa risasi.
Ulinzi hospitalini
Eneo la Hospitali ya Mkoa wa Dodoma lilikuwa na ulinzi mkali, polisi wakiwa wametanda kila kona na silaha za moto hali iliyowatisha watu wengi waliokuwa wakienda hapo kusalimia wagonjwa wao.
Subscribe to:
Posts (Atom)







