Friday, January 4, 2013

Mvua zaleta maafa Singida, Mchina afa maji magari 300 yakwama.

 Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Singida (wa kwanza kushoto mwenye fimbo) akiangalia daraja lililobomoka la Munung’una lililopo barabara kuu ya Singida – Mwanza eneo la  kijiji cha Msisi wilaya ya Singida.
 Mhandisi wa TANROADS mkoa wa Singida,Yustaki Kangole akiwaelekeza jambo wahandisi wa kampuni ya CHICO iliyojenga daraja lililobomokajuzi la kijiji cha Msisi wilaya ya Singida.Daraja hilo lililopo kwenye barabara kuu ya Singida – Mwanza,limebomoka baada ya kuzidiwa na maji ya mvua kubwa iliyonyesha siku moja kabla ya mwaka mpya.
Baadhi wa wasafiri waliokwama baada ya daraja la Munung’una lililopo katika barabara kuu ya Singida – Mwanza eneo la kijiji cha Msisi wilayani Singida, kubomoka juzi kufuatia mvua kubwa zilizonyesha mkoani Singida.

Mvua kubwa zinazoendelea kunyesha mkoani Singida,zimeendelea kuleta maadhara makubwa ikiwemo kuvunja daraja na barabara kuu ya Singida – Mwanza na kuua raia moja  wa nchini China.
Juzi mvua hizo zilisababisha familia ya watu wanne

Thursday, January 3, 2013

Wanne wa Familia moja wateketea kwa Moto kuelekea mkesha wa Mwaka Mpya mkoani Singida.

Kamanda wa polisi mkoa wa Singida Linus Sinzumwa akitoa taarifa kwa waandishi wa habari (hawapo kwenye picha) ya wanafamilia wanne kufariki dunia baada ya kuangukiwa na nyumba ya Tembe.

 Watu wanne wa familia moja wakazi wa kijiji cha Kilunda tarafa ya Nduguti wilaya ya Mkalama mkoani Singida wamefariki dunia papo hapo baada ya

Viongozi ngazi mbalimbali Singida watakiwa kuhakikisha wananchi hasa wa vijijini wanakuwa na uelewa wa haki zao za msingi.

 Mkuu wa wilaya ya Singida Mwalimu Queen Mlozi akizungumza kwenye ufunguzi wa mdahalo uliohusu uimarishaji wa mahusiano kati ya wananchi, wabunge, madiwani na watendaji wa serikali.Mdahalo huo uliandaliwa na shirika lisilo la kisereikali la SINGONET.
 Mratibu wa SINGONET Maendeleo Makoye,akitoa taarifa yake mbele ya mdahalo uliohusu uimarishaji wa mahusiano kati ya wananchi,wabunge na watendaji wa serikali uliofanyika mjini Singida.
Baadhi ya wadau wa maendeleo wa mkoa wa Singida waliohudhuria mdahalo maalum uliohusu uimarishwaji wa mawasiliano kati ya wananchi,wabunge, madiwani na watendaji wa serikali.Mdahalo huo uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa kanisa katoliki mjini Singida, uliandaliwa na shirika la SINGONET.

 Mkuu wa Wilaya ya Singida  Mwalimu Queen Mlozi amewaagiza viongozi wa ngazi mbalimbali wakiwemo wa mashirika yasiyo ya kiserikali ( NGos), kuongeza kasi ya kuhakikisha kila mwananchi na hasa wa

Tuesday, December 18, 2012

SAJUKI AANGUKA JUKWAANI ARUSHA

 Sajuki akitafakari kwa kina mara baada ya kuanguka chini ya jukwaa huku wenzake wakimpa pole
 msanii wa filamu nchini,Sajuki akiwa ameshikwa na wasanii wenzake mara baada ya kuanguka jukwaani juzi ndani ya uwanja wa Sheikh Amri katika tamasha la wasanii wa muziki wa kizazi kipya na wale wa filamu.
msanii wa filamu nchini,Sajuki akiwa ameshikiliwa na wenzake wakimshusha chini ya jukwaa mara baada ya kuanguka alipopewa nafasi ya kuwasalimia mashabiki wake


HALI ya msanii  wa filamu nchini,Juma Said Kilowoko maarufu kama Sajuki imeelezwa si ya kuridhisha  mara baada ya msanii huyo juzi kuanguka jukwaani mara baada ya kuishiwa nguvu wakati alipopewa

Kesi ya Vigogo wa CHADEMA wanaodaiwa kumtukana Mbunge wa Iramba yaendelea kupigwa danadana yaahirishwa hadi leo.

 Vigogo wa CHADEMA Dkt. Kitila Mkumbo mshauri wa CHADEMA na mhadhiri wa chuo kikuu cha Dar-es-salaam (kulia) katibu wa sera na utafiti wa CHADEMA makao makuu Mwita Waitara (katikati) na Pela Ngunangwa aliyejitambulisha kuwa ni dereva kiongozi ofisi za CHADEMA makao makuu, wakiwa wanaelekea kuingia kwenye mahakama ya hakimu mkazi mjini Singida.
Wakili wa vigogo wa CHADEMA Raymond Kimu (wa kwanza kushoto aliyenyoosha kidole) akiteta na wateja wake Mwita Waitara (katikati) na wa pili kulia mwenye miwani Dk.Kitila Mkumbo.

 Kesi inayowakabili vigogo wa CHADEMA ya kumtolea lugha ya matusi mbunge wa jimbo la Iramba Magharibi  (CCM) Mwigulu Lameck Nchemba, iliyoanza kusikilizwa jana kwenye mahakama ya hakimu mkazi mjini Singida imeahirishwa hadi leo.  
Kesi hiyo imeahirishwa baada ya kukosekana kwa hati za

Waandishi 17 mkoani Singida wapatiwa mafunzo ya biashara na uchumi na kutakiwa kujiendeleza kielimu.

 Mkufunzi Mnaku Ambani akitoa mafunzo ya biashara na uchumi yaliyohudhuriwa na waandishi wa habari 17 wa mkoa wa Singida. Mafunzo hayo ya siku nne yalifanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa kanisa katoliki mjini Singida.
Baadhi ya waandishi wa habari mkoa wa Singida wakimsikiliza kwa makini mkufunzi Mnaku Ambani (hayupo kwenye picha) akitoa mada zake za biashara na uchumi.

 Wanachama wa klabu ya waandishi wa habari mkoani Singida(Singpress), wamehimizwa kufanya juhudi za makusudi kumiliki ardhi ili pamoja na mambo mengine, kujijengea mazingira mazuri ya

Monday, December 17, 2012

Serikali Wilayani Singida yazindua awamu ya pili ya kampeni ya Vita dhidi ya Jangwa.

 Mkuu wa wilaya ya Singida Mwalimu Queen Mlozi akizindua upandaji miti katika kijiji cha Kitope manispaa ya Singida.

 Mkuu wa wilaya ya Singida mwalimu Queen Mlozi akishiriki kampeni ya kupanda miti ili kuokoa wilaya hiyo isikumbwe na balaa la Jangwa.


 Mtoto Juma Sungi wa darasa la tatu katika shule ya msingi ya Mwankoko manispaa ya Singida akishiriki kampeni ya kupanda miti kwa lengo la kunusuru manispaa hiyo isigeuke jangwa.
Mkuu wa wilaya ya Singida mwalimu Queen Mlozi akionyesha miche ya miti maji ambayo amedai kuwa inatumika kuvuna mbao na pia kutengenezea sabuni.

 Serikali wilayani Singida imepiga marufuku mara moja uvunaji ovyo wa misitu, kwa madai kwamba uvunaji wa aina hiyo, unatishia