Thursday, February 20, 2014

Mbaroni kwa kukutwa na meno ya Tembo.

                    Kamanda wa Polisi mkoa wa Singida, SACP Geofrey Kamwela.

JESHI la Polisi Mkoa wa Singida limefanikiwa kumkamata George James (30) mkazi wa kijiji cha Mwamagembe tarafa ya Itigi wilaya ya Manyoni mkoa wa Singida kwa tuhuma ya kumiliki kinyume cha sheria nyara za serikali vipande 21 vya meno ya tembo.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Singida,SACP Geofrey Kamwela amesema wamefanikiwa kumkamata George februari 13 mwaka huu saa 2.30 asubuhi huko katika kizuizi cha mazaoa ya misitu na chakula kilichopo katika kijiji cha Ukimbu kata ya Mgandu,tarafa ya Itigi,wilaya ya Manyoni.

Amesema mtuhumiwa huyo alikuwa akitumia gari aina ya toyota hieze T.797 CQL kusafirisha nyara hizo kutoka kijiji cha Mwamangembe kwenda Itigi mjini.

“Baada ya kufanya upekuzi makini,vijana wangu waliweza kuzikuta nyara hizo zikiwa kwenye

Sunday, February 16, 2014

Viongozi wa umma wahimizwa kushirikiana na wasimamizi wa utafiti.

Baadhi ya wadadisi na wasimamizi wa utafiti wa watu wenye uwezo wa kufanya kazi 2014 wakisikiliza mada zilizokuwa zikitolewa kwenye mafunzo yao yaliyomalizika mjini Singida.Wadadisi na wasimamizi hao wametoka mkoa wa Kigoma,Tabora,Singida na Dodoma.
Katibu tawala mkoa wa Singida,Lina Hassan (wa pili kulia walioketi) akiwa kwenye picha ya pamoja na wadadisi na wasimamizi wa utafiti wa watu wenye uwezo wa kufanya kazi mwaka 2014.Kushoto ni Afisa takwimu mkoa wa Singida Mazinza na anayefuata ni mwakilishi wa mkurugenzi mkuu,ofisi ya taifa ya takwimu Bakilla Bakilla na kulia ni mwakilishi wizara ya kazi na ajira,Thomas Saguda.

VIONGOZI wote wa serikali na wa ngazi zote katika mikoa ya Kigoma,Singida,Tabora na Dodoma,wamehimizwa kutoa ushirikiano,kuhamasisha na kuelimisha umma, umuhimu wa kushirikiana na wadadisi na wasimamizi wa utafiti wa watu wenye uwezo wa kufanya kazi wa mwaka 2014.

Imedaiwa kuwa hatua hiyo itasaidia kufikiwa kwa urahisi kwa lengo la serikali ambalo ni kujua soko la ajira nchini lilivyo hivi sasa.

Wito huo umetolewa juzi na Katibu Tawala mkoa wa Singida,Liana Hassan wakati akizungumza kwenye ufungaji wa mafunzo ya siku 14 ya wadadisi na wasimamizi wa utafiti wa watu wenye uwezo wa kufanya kazi mwaka 2014.Wadadisi na wasimamizi hao,wametoka mikoa ya Kigoma,Tabora,Singida na Dodoma.

Amesema umma wakijua umuhimu wa utafiti huo,watakuwa tayari kutoa

Jeshi la Polisi lahimizwa kuendesha kwa ufanisi madawati ya jinsia ili haki itendeke.

Mkuu wa wilaya ya Singida, Queen Mlozi akisoma hotuba ya Naibu Waziri wa Sheria na Katiba, Angellah Jasmine Kairuki kwenye kilele cha maadhimisho ya kupinga ukeketaji duniani yaliyofanyika kitaifa ijiji cha Ngimu wilaya ya Singida.Wa kwanza kushoto,ni mwakilishi wa jumuiya ya kikiristo Tanzania (CCT),Mary Shuma.
Mwakilishii wa jumuiya ya kikiristo Tanzania (CCT), Mary Shuma, akitoa taarifa yake kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya kimataifa ya kupinga ukeketaji duniani yaliyofanyika kitaifa katika kijiji cha Ngimu wilaya ya Singida.
Baadhi ya wakazi wa kijiji cha Ngimu wilaya ya Singida,wakifuatailia matukio yaliyokuwa yakijiri kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya kupinga ukeketaji duniani yaliyofanyika kitaifa katika kijiji cha Ngimu.

NAIBU Waziri wa Sheria na Katiba Angellah Jasmine Kairuki amelihimiza Jeshi la Polisi  nchini kuharakisha zoezi la  kuanzisha na kuendesha Madawati ya Jinsia Katika Wilaya zote ili haki iweze kutendeka kwa wahanga wa ukatili wa jinsia wakiwemo watoto wa kike wanaokeketwa wangali wachanga.

Naibu Waziri huyo ametoa changamoto hiyo hivi karibuni wakati akizungumza kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya Kimataifa ya kupinga ukeketaji duniani, iliyofanyika Kitaifa katika  kijiji cha Ngimu Wilayani Singida.

Katika hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na mkuu wa wilaya ya Singida,Queen Mlozi amesema

Friday, February 14, 2014

Washtakiwa wanne huru kwenye tuhuma za kumuua Mwenyekiti wa UVCCM.

Washitakiwa watano wanaokabiliwa na shitaka la mauaji ya mwenyekiti wa umoja wa vijana CCM kata ya Ndago jimbo la Iramba magharibi Yohana Mpinga,wakisindikizwa na polisi kurejea mahabusu baada ya kesi yao kuahirishwa hadi vikao vingine vijavyo.Mahakama kuu iliwaachia washitakiwa huru wanne waliokuwa wanakabiliwa na kesi ya mauaji hayo ya Mpinga baada mwendesha mashitakiwa kuwafutia mashitaka.

MAHAKAMA kuu kanda ya kati iliyoanza vikao vyake leo mjini Singida imewaachia huru washitakiwa wanne kati ya tisa waliokuwa wakikabiliwa na tuhuma ya kuuawa Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana CCM (UVCCM) kata ya Ndago jimbo la Iramba magharibi,Yohana Mpinga.

 Washitakiwa hao waliachiwa huru baada ya Mwendesha Mashitaka Mwanasheria wa serikali Caren Mrango,kudai mbele ya Jaji wa Mahakama kuu kanda ya kati,Cresentia Makuru kuwa Mwendesha Mashitaka mkuu hana nia ya kuendelea kuwashitaki washitakiwa hao.

Aliwataja washitakiwa hao wanaotakiwa kuondolewa kwenye kesi hiyo kuwa ni Frank Stanley,Francis Edward,Tito Nintwa Kishogere na Paulo Nashokingwa.

Baada ya ombi hilo,jaji aliridhia ombi hilo na kuwaeleza washitakiwa kwamba pamoja na kuachiwa huru,wanaweza tena kushitakiwa au kuunganishwa na kesi hiyo,endapo kutakuwa na umuhimu wa kufanya hivyo.

Washitakiwa waliobakia kuendelea na kesi hiyo,ni Manase Daud,William Elia,Charles Leonard,Emmanuel Shila na Josia Israel.

Mwendesha Mashitaka, Mrango alidai mbele ya jaji Makuru kuwa mnamo julai 14 mwaka 2012 saa tisa alasiri huko katika kijiji cha Nguvumali kata ya Ndago jimbo la Iramba magharibi mkoa wa Singida,washitakiwa kwa pamoja walimuuawa Yohana Mpinga baada ya kumpiga na kumsababishia kifo.

Amesema siku ya tukio CHADEMA walikuwa wameandaa mkutano wa hadhara ambao kiongozi wa chama hicho Mwita Waitara na Dk.Kitila Mkumbo walikuwa wautumie katika kueneza sera za chama hicho.

Amesema viongozi hao walitumia fursa hiyo kutoa

Wajasirimali 40 wapata mafunzo ya usimamizi na uthibiti wa fedha.

Mratibu wa shirika lisilo la kiserikali la Mother and Children of Central Tanzania (MCCT), Everline Lyimo akitoa nasaha zake kwenye mafunzo ya kuwajengea uwezo wanachama wa shiriki hilo ikiwemo usimamizi na uthibiti wa fedha.
Mwezeshaji Elihuruma Hema,akitoa mafunzo ya usimamizi na uthibiti wa fedha kwa wanachama 40 wa shirika lisilo la kiserikali la Mother and children of central Tanzania (MCCT).Mafunzo hayo yalifanyikia kwenye ukumbi wa mikutano wa hotel ya Stanley mjini.
Baadhi ya wanachama wa shirika lisilo la kiserikali la Mother and Children of Central Tanzania waliohudhuria mafunzo ya usimamizi na uthibiti wa fedha yaliyofanyika kwenye ukumbi wa hotel ya Stanley mjini Singida.

WANACHAMA 40 wa shirika lisilo la kiserikali la Mother and Children of Central Tanzania (MCCT) la mkoa wa Singida wamehudhuria mafunzo ya usimamizi na uthibiti wa fedha kwa lengo wawe na uwezo mpana zaidi wa kuboresha shughuli zao za ujasiriamali.

Akizungumza na waandishi wa habari,  Mwezeshaji wa mafunzo hayo, Elihuruma Hema amesema pia lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo wanachama hasa wanawake, kujua taratibu za fedha kitaalam ili ziwasaidie kuendesha shughuli zao kwa ufanisi.

Amesema katika kuwajengea uwezo wanachama hao,wamefundishwa namna bora ya kuweka kumbu kumbu za fedha kwenye vitabu husika ili mwisho wa siku iwe rahisi kwao kujua wanapata faida au hasara.

 ”Kwa ujumla maisha yanahitaji mahesabu, ukisimamia vizuri mahesabu ikiwemo ya biashara ni lazima faida itapatikana.  Lakini ukifanya tofauti ikiwemo kutokutumia vitabu husika katika kuweka kumbu kumbu ya fedha vizuri utapoteza fedha bila kujijua”,alifafanua Hema.

Mkufunzi huyo amesema kutokana na ukweli huo, kila mtu au mjasiriamali anapaswa kuhakikisha

Tuesday, February 11, 2014

Wawili wapoteza maisha katika ajali ya basi la Zuberi.

WASOMAJI WETU TUNAOMBA RADHI KAMA UTAKWAZIKA NA PICHA ZIFUATAZO.
Mtoto mmoja aliyelalaliwa na kusababisha kifo chake na basi la Zuberi T.119 AZZ lilokuwa likitokea Mwanza kuelekea jijini Dar-es-salaam na kupinduka katika eneo la kijiji cha Tumaini kata ya Issuna wilaya ya Ikungi wakati likimkwepa bibi aliyekuwa akikatisha barabara.
 Mmoja wa majeruhi akiwa amelazwa katika Hosptali ya Mkoa ya Singida.
 Mmoja wa majeruhi akiongea na waandishi wa habari katika Hospitali ya mkoa mjini Singida.

BASI la kampuni ya Zuberi T.119 AZZ lililokuwa linatokea jijini Mwanza likielekea jijini Dar-es-salaam,limepinduka na kusababisha vifo vya abiria  wawili na kujeruhi vibaya wengine arobaini wakati likimkwepa bibi mmoja aliyekuwa anakatisha barabara.

 Ajali hiyo imetokea jana saa 7.30 mchana katika barabara kuu ya Sindida –Dodoma eneo la kijiji cha Tumaini kata ya Issuna wilaya ya Ikungi mkoani Singida.

Afisa wa makosa ya jinai mkoa wa Singida (RCO), Thobias Sedoyeka amesema kuwa basi hilo lililokuwa likiendeshwa na Fadhili Kalembo (35),lilipofika eneo la tukio,bibi mmoja alijitokeza akiwa anavuka barabara.

Amesema dereva wa basi alijitahidi kumkwepa bibi huyo lakini ghafla bibi alirudi tena barabarani kitendo kilichosababisha basi hilo kupinduka na kuserereka hatua zaidi ya 50 wakati likimkwepa kwa mara ya pili.

 “Basi hili lilimlalia mtoto mdogo ambaye

DC akemea posho kwa viongozi wa umma.

Mkuu wa wilaya ya Singida, Mwalimu Queen Mwashinga Mlozi, akizungumza kwenye ufunguzi wa mkutano wa mrejesho wa utafiti wa marejesho ya taarifa ya mradi wa ufuatiliaji na uwajibikaji jamii.Wa kwanza kulia,ni kaimu mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Singida na afisa biashara wa halmashauri hiyo,Shao.Wa kwanza kushoto ni Afisa kutoka shirika la HAPA.
Afisa mwanadamizi wa shirika lisilo la kiserikali la Health Actions Promotion Assocition (HAPA) la mkoa wa Singida, Mnyambi akitoa nasaha zake muda mfupi kabla hajamkaribisha mkuu wa wilaya ya Singida Queen Mlozi, kufungua mkutano wa mrejesho wa utafiti juu ya uwajibikaji.Wa kwanza kulia ni mkuu wa wilaya ya Singida,Queen Mlozi.
Afisa wa shirika la HAPA, Baraka Mwakubali akitoa taarifa yake ya marejesho ya taarifa ya mradi wa ufuatiliaji na uwajibikaji jamii kwenye mkutano uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa kanisa katoliki mjini Singida.
Baadhi wa wajumbe waliohudhuria mkutano wa marejesho ya taarifa ya mradi wa ufuatiliaji na uwajibikaji jamii.Mkutano huo ulifanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa kanisa katoliki mjini Singida

MKUU wa Wilaya ya Singida Queen Mlozi ameonya viongozi wanaoweka tamaa mbele ya malipo ya posho wasithubutu kuchukua fomu za kuomba uongozi wowote kwa madai kwamba katika kuwatumikia wananchi, posho sio kipaumbele.

Mlozi ametoa onyo hilo hivi karibuni wakati akizungumza kwenye mkutano wa  marejesho wa taarifa ya mradi wa ufuatiliaji na uwajibikaji jamii uliofanyika kwenye ukumbi wa mkutano wa Kanisa Katoliki mjini hapa.

Amesema kazi nyingi za kuwatumikia wannchi ni za kujitolea kwa hali hiyo kiongozi anayetaka kulipwa posho, huyo hafai kwa sababu atadumaza maendeleo

“Kama unaona huwezi kufanya kazi za wanachi bila kulipwa posho basi usichukue fomu ya kuomba uongozi kwa sababu utakuwa kikwazo kwa maendeleo ya wananchi”.

Awali afisa wa shirika la uboreshaji afya ya jamii (HAPA) Baraka Mwakubali, amesema lengo la ufuatiliaji na uwajibikaji  jamii, ni kuboresha  mfumo wa