Kamanda wa Polisi mkoa wa Singida, SACP Geofrey Kamwela.
JESHI la Polisi Mkoa wa Singida limefanikiwa kumkamata George James (30) mkazi wa kijiji cha Mwamagembe tarafa ya Itigi wilaya ya Manyoni mkoa wa Singida kwa tuhuma ya kumiliki kinyume cha sheria nyara za serikali vipande 21 vya meno ya tembo.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Singida,SACP Geofrey Kamwela amesema wamefanikiwa kumkamata George februari 13 mwaka huu saa 2.30 asubuhi huko katika kizuizi cha mazaoa ya misitu na chakula kilichopo katika kijiji cha Ukimbu kata ya Mgandu,tarafa ya Itigi,wilaya ya Manyoni.
Amesema mtuhumiwa huyo alikuwa akitumia gari aina ya toyota hieze T.797 CQL kusafirisha nyara hizo kutoka kijiji cha Mwamangembe kwenda Itigi mjini.
“Baada ya kufanya upekuzi makini,vijana wangu waliweza kuzikuta nyara hizo zikiwa kwenye