Wednesday, October 7, 2015

Ajali ya basi la City Boys yaua 3, Singida, mwingine agongwa na Noah.1

Kamanda wa polisI Mkoani Singida (ACP) Thobias Sedoyeka (pichani)akizungumza na waandishi wa habari  juu ya kutokea kwa ajali ya basi la City Boys na kusababisha vifo vya watu watatu Wilayani Iramba  na mwingine kugongwa na Noah Singida vijijini.

WATU wanne wamefariki dunia Mkoani Singida baada ya kupata ajali ya kugongwa na basi la City Boys na mwingine Noah wakati wakivuka barabara eneo la Ulemo barabara kuu ya Singida- Nzega.

Kamanda wa polisi Mkoani Singida (ACP), Thobias Sedoyeka alisema ajaili hiyo imetokea jana majira ya 1:00 usiku katika kijiji cha Kitukutu Kata ya Ulemo, Tarafa ya Kinampanda ,Wilayani Iramba.

Alisema siku ya tukio, basi lenye namba za usajili T 846 CDU aina ya Scania  mali ya kampuni ya City Boys likitokea Jijini Dar es Salaam kwenda Kahama lilikuwa likiendeshwa na dereva Adam George (33) mkazi wa Dar es Salaam.

 Aidha alisema dereva huyo alipofika eneo na Kitukutu kutokana na kile kinachosadikiwa kuwa ni

DORIS MOLLEL FOUNDATION: Yakabidhi vitabu 200 kwa Shule ya Msingi Midamigha Ilongero SINGIDA.

Mwalimu wa taaluma wa shule Msingi Midamigha Ilongero, Singida akipokea vitabu hivyo kutoka taasisi ya Dmf wakati wa kukabidhi vitabu hivyo.
[SINGIDA] Taasisi inayoshughulikia na utetezi wa watoto njiti ya Doris Mollel ‘DORIS MOLLEL FOUNDATION’(Dmf)  mwishoni mwa wiki imekabidhi vitabu 200 kwa ajili ya kujifunzia  katika shule ya msingi Midamigha ilongero, singida.

Vitabu hivyo vitakuwa chachu na changamoto kwa wanafunzi wa shule hiyo ambapo watapata furasa za kujifunza mambo mbalimbali katika elimu yao.

Dmf imetoa vitabu hivyo ni kutokana na ufadhili wa taasisi ya Kituruki iitwayo Rhema Trust.

Taasisi ya Dmf  imekuwa mstari wa mbele katika harakati za kutetea watoto hasa watoto njiti wasipoteze maisha kutokana na kukosa vifaa vya kufanya watoto hao waweze kuishi na kufikia malengo kama watoto wengine ambao hawakuzaliwa na wakiwa njiti.

Msindai awatangazia neema mama ntilie, machinga, waendesha boda boda.

Mgombe Ubunge wa Jimbo la Singida Mjini (CHADEMA) Mgana Msindai, akizungumza na wafanyabiashara wa soko kuu mjini Singida wakati wa Mkutano wa kampeni kuomba ridhaa ya wananchi kumchagua kuwa Mbunge ili kuondoa kero ndogo ndogo za kutozwa ushuru kwa wamachinga na mama ntilie.

MGOMBEA Ubunge wa Jimbo la Singida Mjini (CHADEMA ) Mgana Msindai ameahidi kuondoa kero na kodi ndogondogo wanazotozwa wafanyabiashara wadogo wakiwemo mama ntilie.

Akizungumza jana kwenye  Mkutano wa Kampeni wa chama chake eneo la soko kuu, Msindai alisema mojawapo ya kero hizo ni pamoja na kusumbuliwa kwa kina mama lishe bila kujali ugumu wa maisha unaowakabili hivyo akichaguliwa ataziondoa kodi hizo mara moja.

“Hizi kero za mama ntilie kutozwa shilingi 20,000 kwa mwezi na meza ndogo ndogo za matunda na mboga mboga nitazifuta kwa kushirikiana na madiwani wenzangu wa Ukawa, kwani hii sio sheria kuu, ni sheria ndogo ndogo zinazotungwa na madiwani, sisi tutazifuta mara moja  ili watu hawa waweze kubadilika.”Alisema Msindai maarufu kwa jina la CRDB.

Hata hivyo ili kuendena na hadhi ya Manispaa, Msindai ameahidi kushirikiana na madiwani wenzake kujenga soko jipya la kisasa kwa kuvunja

Nitaondoa njaa, wakulima watatumia helkopta kumwagilia mashamba, nitajenga vituo maalumu vya Albino na wazee – Rungwe

Mgombea Urais wa CHAUMA,Hashim Rungwe katika pozi tofauti akihutubia wananchi wa Singida mjini jana.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha ukombozi wa Umma (CHAUMA) Hashim Rungwe akizungumza kwenye Mkutano wa Kampeni Mkoani  Singida, ambapo aliahidi kuwaondolea wananchi njaa.
Mgombea mwenza wa CHAUMA Issa Abas Husein nae akihutubia wananchi wa Singida mjini.
WANANCHI wakimsikiliza Mgombea Urais wa CHAUMA kwenye kituo cha stendi ya zamani Mjini Singida jana.

Friday, September 18, 2015

Zaidi ya wakazi 5,000 hatarini kukumbwa na magonjwa ya mlipuko.

Kaimu Katibu Tawala wa mkoa wa Singida, Aziza Mumba akikata utepe kuzindua nyota mpya ya kijani.
Baadhi ya wananchi wa kata ya Mang’onyi wakiwa kwenye mkutano wa uzinduzi wa kampeni za uchaguzi mkuu kumnadi mgombea wa ubunge wa jimbo hilo.

ZAIDI ya wakazi 5,000 wa Kijiji cha Sambaru,kata ya Mang’onyi,wilaya ya Ikungi,Mkoani Singida wamo hatarini kupatwa na magonjwa ya mlipuko kutokana na kujisaidia vichakani kwa kutokuwa na vyoo vya kudumu kutokana na idadi kubwa ya wahamiaji wanaoishi kwenye vitongoji saba vilivyopo katika Kijiji hicho.

Ofisa mtendaji wa Kijiji cha Sambaru,Bwana Baraka Njiku amesema wakazi hao wapo kwenye hatari ya kukumbwa na magonjwa ya kuharisha,kuhara damu pamoja na kipindupindu kutokana na kula uchafu wa kinyesi wanachojisaidia kwenye vichaka vilivyopo karibu na nyumba zao za makazi.

Aidha ofisa mtendaji huyo amefafanua kwamba  wakazi hao wapatao 5,870 wanaoishi katika kaya 899 wanahitaji matundu 899,lakini matundu ya vyoo vya muda yaliyopo ni 320 kati ya mahitaji wa wakazi wote wa Kijiji hicho.

Kwa mujibu wa Bwana Njiku katika Kitongoji cha Taru namba saba chenye kaya 99 kinahitaji jumla ya matundu ya vyoo 498 yaliyopo kwa sasa ni matundu ya muda

Uzazi wa mpango utekelezwe na familia kwa vitendo, ili kustawi vyema na kuimarika kiuchumi

Kaimu Katibu Tawala wa mkoa wa Singida, Aziza Mumba akikata utepe kuzindua nyota mpya ya kijani.
Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida Aziza Mumba akizungumza na wananchi wa Mkoa wa Singida wakati wa uzinduzi wa kampeni mpya ya nyota ya kijani kwenye viwanja vya peoples Mjini Singida.
 Kaimu Mganga mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk. Mussa Kimala akizungumza kwenye sherehe hizo.

Thursday, September 17, 2015

Tundu Lissu amshukia Dk.Slaa kwa madai ya kuponzwa na mkewe.

Mwanasheria wa CHADEMA na mgombea ubunge jimbo la Singida mashariki, Tundu Lissu,akizungumza kwenye mkutano wa kampeni ya Ukawa mkoa wa Singida uliofanyika kwenye uwanja wa Peoples mjini hapa.Pamoja na mambo mengine,Tundu amewaomba wakazi wa Singida, kumpa kura ya ndiyo mgombea urais kwa tiketi ya Ukawa, Edward Ngoyai Lowassa, wabunge na madiwani wa Ukawa,ili kuigaragaza CCM kwa madai imechoka na umechuja mbele ya macho ya Watanzania.

Mgombea ubunge jimbo la Singida mjini kupitia ukawa, Mgana Izumbe Msindai, akiomba kura kwenye mkutano wa kampeni wa Ukawa uliofanyika kwenye uwanja wa Peoples mjini hapa. Msindai ambaye amewahi kuwa mbunge wa jimbo la Iramba mashariki kwa vipindi vitatu mfululizo na mwenyekiti wa wenyeviti wa CCM wa mikoa nchini,amewata wakazi wa jimbo la Singida mjini kujitokeza kwa wingi oktoba 25 mwaka huu kuichana chana CCM kwa kadi zao za kupigia kura.