Sunday, September 1, 2013

Halmashauri ya Singida yakusanya mapato ya zaidi ya shilingi bilioni 22 kutoka vyanzo yake mbalimbali.

 Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Singida Jumanne Mnyampanda (katikati) akiongoza kikao cha baraza la madiwani kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa chuo cha maendeleo ya wanancvhi mjini Singida. Wa kwanza kushoto ni makamu mwenyekiti halmashauri ya wilaya ya Singida Hamisi Mumbee na kulia ni Mkurugenzi wa halmashauri ya Singida Illuminata Mwenda.
 Baadhi ya madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Singida wakifuatilia kwa makini hoja zilizokuwa zikijadiliwa kwenye kikao cha baraza la madiwani. Kikao hicho kilifanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa chuo cha maendeleo ya wananchi mjini Singida.
Mwenyekiti wa huduma za jamii katika halmashauri ya wilaya ya Singida na diwani (CCM) wa kata ya Msange Elia Digha, akichangia hoja kwenye kikao cha baraza la madiwani wa halmashauri ya Singida.

Halmashauri ya wilaya ya Singida imekusanya mapato kutoka vyanzo vyake mbalimbali zaidi ya shilingi bilioni 22.9 kati ya Julai mwaka jana na Juni mwaka huu.

Mkurugenzi wa halmashauri hiyo Illuminata Mwenda amesema hayo wakati  akitoa taarifa yake ya mapato na matumizi kwenye kikao cha baraza la madiwani, kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa chuo cha maendeleo ya wananchi mjini Singida.

 Amesema makusanyo hayo ya mapato ni sawa na asilimia 78 ya lengo la kukusanya shilingi 29,583,444,380 kwa mwaka huo wa fedha.

 Mwenda amesema kuwa vyanzo vya ndani vya mapato, walikusanya zaidi ya shilingi..........
419,000,000 sawa na aslimia 42 ya lengo la kukusanya shilingi 1,004,817,000.

Mkurugenzi huyo amesema serikali  kuu imewapa ruzuku ya kulipia mishahara zaidi ya shilingi 13.8 bilioni na ruzuku nyingine ya zaidi ya shilingi 1.5 bilioni kwa ajili ya matumizi yasiyo ya mishahara.

 Katika hatua nyingine, kikao hicho kimeagiza mkaguzi wa mahesabu wa ndani afanye ukaguzi wa vitabu vya kukusanyia mapato ya ndani kwa watendaji wote wa kata.

 Vile vile mkaguzi huyo, amkague kwa makini Afisa mapato wa halmashauri hiyo anayehusika na kutoa vitabu vya kukusanyia mapato.


 Aidha, kikao hicho kimemwagiza mkaguzi huyo kufanya ukaguzi zaidi kwa watendaji wa kata ya Merya, Itaja, Mudida na Ikhanoda ili kubaini tuhuma zinazowakabili.

No comments:

Post a Comment