Friday, February 15, 2013

Wakulima watatu wanusurika kuuawa mkoani Singida kufuatia ugomvi wa shamba

Mkulima John Leonard Njiku akiwa amelazwa katika wodi namba tatu katika hospitali ya mkoa mjini Singida baada ya kuvamiwa akiwa shambani na wenzake  wawili. Njiku amedai kuwa uvamizi huo unachangiwa na ugomvi wa kugombe shamba kati yake na Dk. Damas Simbu aishiye Dar-es-salaam.

 Wakulima watatu wakazi wa kijiji cha Ughaugha (b) manispaa ya Singida, wamenusurika kuuawa baada ya kuvamiwa na watu wanaokadiriwa kuwa 12 wakiwa shambani na kushambuliwa kwa majembe kwa kile kilichodaiwa kuwa ni ugomvi wa kugombea shamba.
Wakulima hao waliovamiwa
Februari nane mwaka huu saa tatu asubuhi wakiwa shambani ni John Leonard Njiku (41) na mdogo wake Mateo (37), wakati mkulima mwingine ni Eliasi George (37) na wote hao wamelazwa wodi namba tatu katika hospitali ya mkoa mjini Singida na hali zao zinaendelea vizuri.
Uvamizi huo  unadaiwa kuwa umechangiwa kwa kiasi kikubwa na ugomvi wa kugombea shamba kati ya John na Dk.Damas Simbu, anayefanyia kazi jijini Dar-es-salaam.
Akizungumza kwa taabu kubwa  akiwa kitandani ,John amesema kuwa siku ya tukio wakiwa shambani kwake, ghafla walivamiwa na kundi la watu lililokuwa limebeba hengo na mawe mikono yao yote miwili.
Amesema yeye inaonekena kuwa alikuwa mlengwa kwani watu hao walimuanza kumkata kwa hengo kwenye paji lake la uso na kusababisha aanguke chini na kupoteza fahamu.
Amesema kuwa watu hao vile vile walimpiga kwa jiwe mdomoni na kusababisha meno matatu kulegea na kudai kutokana na kulegea sana,huenda yakatolewa.
“Mdogo wangu Mateo yeye amepigwa na jiwe lenye ncha kali kichwani na ameumizwa vibaya kwa jembe kwenye mbavu za kulia, wakati jirani na rafiki yetu George yeye amejeruhiwa vibaya kichwani na sehemu za mbavu zake kwa kukatwa na jembe na pia kupigwa kwa mawe”,amesema mkulima huyo.
Akifafanua zaidi, John amesema uvamizi huo umechangiwa na ugomvi wa muda mrefu wa kugombea shamaba yeye na Dk.Simbu.
Alisema yeye na Dk.Simbu wamewahi kifikishana mbele ya baraza la ardhi la wilaya na pia kwenye mahakama ya wilaya ya Singida na kote huko alimgaragaza vibaya daktari huyo.
John amesema kuwa pamoja na vyombo vyote hivyo vya sheria kumpa ushindi Dk.Simbu hakuweza kuridhika na hivi sasa faili lipo mahakama kuu Dodoma.

No comments:

Post a Comment