Sunday, December 16, 2012

TFDA yakamata bidhaa zilizomaliza muda wake Mkoani Singida.

 Maafisa TFDA kanda ya kati, Florent Kyombo (kushoto) akishuhudia mmiliki wa duka la Temba, Singida mjini Bw. Temba akisaini fomu yakutekeza bidhaa zilizoisha muda wake na akazitoa dukani, TFDA walimsifu sana.
Kaimu meneja TFDA kanda kati, Florent Kyombo na Joseph Mwasambili wakikagua vinywaji vikali kwenye moja ya duka mjini Singida, katika oparesheni maalumu kusaka bidhaa zilizomaliza muda kwa matumizi ya binadamu.

 Mamlaka ya chakula na dawa nchini (TFDA), imekamata bidhaa mbalimbali ikiwemo vipodozi vilivyopigwa marufuku na vilivyomaliza muda vikiwa na thamani ya zaidi ya Sh. Milioni

Dkt. Kone awataka wakuu wa wilaya Singida kuhakikisha watoto wanapata chanjo mbili mpya za Rotavirus na PCV 13.

 Mkuu wa mkoa wa Singida Dk.Parseko Kone akizungumza kwenye mkutano maalum wa uhabarishaji juu ya umuhimu wa chanjo mpya za Rotavirus inayokinga maradhi ya kuharisha na PCV 13,inayokinga ugonjwa wa Nimonia.Chanjo hizo ambazo ni mpya,zinatarajiwa kuanza kutolewa kuanzia Januari mwakani.
Mkuu wa wilaya ya Iramba.Yahaya Nawanda akichingia mada juu ya chanjo mpya za totavirus na PCV 13 kwenye mkutano maalum kwa lengo la kuhabarisha juu ya chanjo hizo.

 Mkuu wa mkoa wa Singida Dkt. Parseko Kone amewaagiza wakuu wa wilaya kuhakikisha wanawahamasisha wananchi juu ya umuhimu wa watoto wao kupata chanjo mbili mpya, za Rotavirus na PCV 13 ili kujikinga na magonjwa  ya

Wednesday, December 12, 2012

Watu 25 mbaroni mkoani Singida kufuatia tukio la kupora fedha na kisha kuvunja jeneza na kusachi maiti.

Kamanda wa polisi mkoa wa Singida, Linus Sinzumwa akionyesha silaha za jadi zilizokuwa zinatumiwa na majambazi yaliyoteka gari la SUA no.SU 37012 na kuporwa zaidi ya shilingi 19.8 miloni na mali mbali mbali nje kidogo ya mji wa Singida.


Jeshi la polisi mkoani Sngida limefanikiwa kuwakamata watu 25 wanaotuhumiwa kuteka gari la Chuo Kikuu cha Sokoine (SUA) mjini Morogoro na kisha kupora watu waliokuwa wanasindikiza maiti kupeleka mkoani Mara kwa ajili ya mazishi.
Gari lililotekwa ni Land Cruiser SU 37012 lililokuwa likiendeshwa na Kalistus Mapulila.
Katika utekaji huo, inadawa kuwa jeneza lililokuwa limebeba mwili wa marehemu

Tuesday, December 11, 2012

Wahandishi wa habari mkoa wa Singida wagawanyika, mkutano mkuu wautaka uongozi wa zamani kukabidhi ofisi ndani ya wiki mbili.

Katibu wa klabu ya waandishi wa habari (Singpress) mkoa wa Singida Bw. Abby Nkungu akitoa taarifa yake ya utekelezaji kwa kipindi cha mwaka uliopita.


Mkutano Mkuu wa mwaka wa Klabu ya Waandishi wa habari (Singpress) Mkoani Singida, umeagiza uongozi wa zamani wa Klabu hiyo, kukabidhi ofisi katika kipindi cha wiki mbili, vinginevyo uchukuliwe hatua kali zikiwemo za kisheria.
Mkutano huo uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri ya Wilaya ya Manyoni mjini, Umeagiza uongozi huo uandikiwe barua rasmi ya kuupa muda wa wiki mbili kuanzia

Sunday, December 9, 2012

MAITI YASACHIWA NA KUPORWA ZAIDI YA MILIONI 19 NA MAJAMBAZI


 Gari aina ya Land Cruiser mali ya chuo cha SUA cha mjini Morogoro kama linavyoonekana baada ya kupigwa mawe na watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi nje kidogo ya mji wa Singida.
Mhudumu wa chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali ya mkoa mjini Singida ambaye jina lake halikuweza kutambuliwa mara moja, akiliweka sawa jeneza baada ya kufanyiwa ukarabati baada ya kubomolewa na majambazi na kulisachi.


Watu wasiofahamika idadi yao na ambao wanadhaniwa kuwa ni majambazi, wamevamia gari lililokuwa linasafirisha maiti kutoka Morogoro mjini hadi mkoa wa Mara na kupora  zaidi ya shilingi milioni 19.8.
Baada ya kumaliza zoezi la uporaji huo, majambazi hayo yalishusha jeneza na kisha...

Saturday, December 8, 2012

Kampuni ya Tan Discovery yakanusha kutowasaidia wachimbaji wadogo wa madini mkoani Singida.

Afisa msimamizi wa kampuni ya Tan Discovery Akida Sungura akiwa Internet Cafe akitekeleza majukumu yake.


Kampuni ya Tan Discovery inayojishughulisha na kuuza na kukodisha vifaa vya uchimbaji madini kwa wachimbaji wadogo mkoani Singida, imekanusha taarifa zilizotolewa na baadhi ya vyombo vya habari kwamba haijawasaidia wachimbaji kufikia

Madhehebu ya dini jimbo la Singida yamtwisha mgana msindai mzigo wa kutokomeza rushwa ndani ya CCM.

 Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Singida Mgana Izumbe Msindai akizungumza kwenye mkutano wa viongozi wa madhehebu ya dini jimbo la Singida mjini.Kushoto ni mwenyekiti wa CCM jimbo la Singida mjini Hamisi Nguli na wa pili kulia ni katibu wa CCM mkoa wa Singida,Naomi Kapambala.
 Mmoja wa viongozi wa madhahebu ya dini,mzee Omari Hamza akitoa kero alizokuwa nazo kwa mwenyekiti wa CCM mkoa wa Singida Mgana Msindai (hayupo kwenye picha).
Baadhi ya viongozi wa madhehebu ya dini waliohudhuria mkutano ulioitishwa kwa ajili ya mwenyekiti wa CCM mkoa kujitambulisha kwao na wao kutoa kero ushauri ya maoni kwa lengo la kuendeleza manispaa ya Singida.


Viongozi wa madhehebu mbalimbali ya dini jimbo la Singida mjini wamemwomba Mwenyekiti mpya wa CCM  mkoa wa Singida Mgana Izumbe Msindai, kuweka mikakati madhubuti itakayokomesha vitendo vyote vya rushwa ili