Wanakikundi cha uhamasishaji cha kata ya Mungaa jimbo la Singida mashariki, wakitoa burudani kwenye hafla ya uzinduzi wa shina la wakereketwa wa CCM la Mzambarauni katika kijiji cha Makiungu.
Mjumbe wa Mkutano Mkuu CCM (NEC) taifa wilaya ya Ikungi mkoani Singida, Jonathani Njau ameivunja ngome ya CHADEMA kata ya Mungaa, baada ya wanachama wake 51 kukihama na kurejea CCM.
Wanachama hao ambao karibu wote ni vijana, katika risala yao wamedai wamehama CHADEMA, baada ya kubaini kuwa wanatumiwa vibaya na wanasiasa wa chama hicho.
Wamedai kwamba wanasiasa wa CHADEMA wamejaa uchu wa madaraka, wanatumia uongo mkubwa, hila, kupandikiza chuki na wanatoa ahadi za uongo katika kupata uongozi.
“Kabla na baada ya uchaguzi, tuliahidiwa ahadi nyingi na viongozi wa CHADEMA kumbe ahadi zote hizo ni ahadi hewa.Vijana tumekwisha kuwagundua na hatudanganyiki tena.Kwa sababu sisi ni nguvu kazi ya taifa,tunatakiwa kutumika kwa maslahi ya taifa na si kwa maslahi ya mtu binafsi”,inasema sehemu ya risala yao.
Katika hatua nyingine,vijana hao walishangiliwa kwa nguvu na umati uliohudhuria mkutano huo wa hadahara,wakati wakiimba wimbo maalum ambao ulidai kwamba CHADEMA ni sawa na kitanda cha kamba kilichojaa kunguni na hivyo,hakilaliki.
Akizungumza muda mfupi baada ya kuzindua shina la wakereketwa la Mzambarauni waliorejea CCM, Mnec Njau amesema mlango wa CCM upo
Mkuu wa wilaya ya Singida,Queen Mlozi akizungumza kwenye hafla ya ufungaji wa mafunzo ya ufugaji bora nyuki iliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa SIDO mjini Singida.Kulia ni meneja wa SIDO mkoa wa Singida, Shoma Kibende.
Meneja wa SIDO mkoa wa Singida,Shoma Kibende akitoa taarifa yake kwenye hafla ya ufungaji mafunzo ya ufugaji nyuki iliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa SIDO mjini Singida.Wa pili kulia (aliyeketi) ni mkuu wa wilaya ya Singida,Queen Mlozi.
Mkuu wa wilaya ya Singida,Queen Mlozi akimkabidhi mfugaji wa nyuki cheti cha kumaliza mafunzo ya ufugaji bora nyuki yaliyomalizika mwishoni mwa wiki mjini Singida.
Mkuu wa wilaya ya Singida,Queen Mlozi,(aliyeketi katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na wafugaji Nyuki waliohitimu mafunzo ya ufugaji bora wa Nyuki.Wa kwanza kushoto (walioketi) ni meneja wa SIDO mkoa wa Singida,Shoma Kibende na kulia ni mwenyekiti wa wafugaji Nyuki.
Serikali wilayani Singida, imewahimiza wajasiriamali na wafanyabiashara kujenga utamaduni wa kutangaza bidhaa zao kwenye vyombo vya habari ili pamoja na mambo mengine, waweze kujipatia soko la uhakika.
Wito huo umetolewa mwishoni mwa wiki na Mkuu wa Wilaya hiyo Queen Mlozi,wakati akizungumza kwenye hafla ya ufungaji mafunzo ya ufugaji bora wa nyuki na uchakataji wa asali.
Akifafanua amesema ushindani mkubwa wa biashara uliopo hivi sasa,mfanyabiashara atakayefanikiwa ni yule tu ambaye atatangaza biashara yake kikamilifu.
Mlozi amesema biashara bila matangazo,ni sawa na mtu asiye na biashara kwa sababu bidhaa zake,hazitajulikana.
Amesema pamoja na kujitangaza huko,kwanza wahakikishe bidhaa zao zina kuwa na ubora unaohitajika na pia wahakikishe wanashiriki maonyesho yanayoandaliwa na SIDO kanda ya kati.
Awali meneja wa SIDO mkoa wa Singida,Shoma Kibende, amesema kuwa SIDO inao mpango wa
Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Singida, ACP. Geofrey Kamwela akitoa taarifa kwa waandishi wa habari (hawapo kwenye picha) juu ya kijana mmoja Saidi Hamisi (34) kumbaka Kikongwe mwenye umri wa miaka 80 (jina tunalo).Inadaiwa baada ya mtuhumiwa kumaliza kumbaka kikongwe huyo, alilala fo fofo kutokana na kulewa kupindukia hadi alipokuja kukamatwa akiwa amelala kwenye kitanda cha Kikongwe akiwa hajitambui.
JESHI la Polisi Mkoa wa Singida linamshikilia mkulima mkazi wa kijiji cha Wibia tarafa ya Mungaa wilaya ya Ikungi Saidi Hamisi (34) kwa tuhuma ya kumbaka bibi kizee mwenye umri wa miaka 80 na kumsababishia maumivu makali katika sehemu zake za siri.
Akizungumza na waandishi wa habari jana ofisini kwake, kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Singida, ACP Geofrey Kamwela, alisema tukio hilo la aibu na kusikitisha limetokea Novemba Sita mwaka huu huko katika kijiji cha Matongo kata na wilaya ya Ikungi.
Akifafanua, alisema siku ya tukio mtuhumiwa ambaye alikuwa katika kijiji cha Matongo kuwajulia ndugu zake hali, alikunywa kiwango kikubwa cha Pombe ya kienyeji na kupelekea amfanyie kitendo hicho cha kinyama Kikongwe huyo.
“Mtuhumiwa alitumia mwanya wa nyumba za Tembe kutokuwa na mlango imara na hivyo alivuta taratibu mlango uliotengenezwa kwa fito na
Afisa elimu na huduma kwa mlipa kodi TRA mkoa wa Singida, Zakaria Gwagilo akitoa taarifa kwa waandishi wa habari (hawapo kwenye picha) juu ya maadhimisho ya saba ya siku ya mlipa kodi ambayo yamezinduliwa rasmi juzi. Zakaria alitoa taarifa hiyo kwa niaba ya kaimu meneja TRA mkoa wa Singida Alistides Paulo.
MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Singida imezindua rasmi maadhimisho ya saba ya siku ya mlipa kodi Tanzania kwa kufanya shughuli mbalimbali ikiwemo ya kutoa misaada kwa makundi yenye mahitaji maalumu.
Hayo yamesemwa na Kaimu Meneja wa TRA Mkoa wa Singida, Alistides Paulo wakati akitoa taarifa yake kwa waandishi wa habari kuhusu maadhimisho ya saba ya siku ya mlipa kodi Tanzania kwa Mkoa wa Singida.
Katika taarifa yake hiyo iliyosomwa kwa niaba yake na Afisa Elimu na huduma kwa mlipa kodi Zakaria Gwagilo alitaja baadhi ya shughuli zitakazofanyika katika maadhimisho hayo kuwa ni pamoja na kutoa misaada kwenye wodi ya wazazi katika hospitali ya wilaya ya Manyoni.
Paulo alitaja shughuli zingine kuwa watafanya semina kwa makundi mbalimbali ya walipa kodi na pia kuwatembelea walipa kodi kwenye vituo vya biashara na kuzungumza nao kuweza kufahamu matatizo yao.
“Katika kilele cha siku ya mlipa kodi Novemba nane mwaka huu baadhi ya walipa kodi watazawadiwa vyeti kutokana na
Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Ikungi,Protace Magayane akifafanua jambo mbele ya kikao cha kawaida cha madiwani.Katikati ni mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Seelestin Yunde na wa kwanza kulia ni mwenyekiti CCM wilaya ya Ikungi, Hassan Tati.
Baadhi ya watendaji wa halmashauri ya wilaya ya Ikungi,wakifuatilia kwa makini ajenga zilizokuwa zikizungumzwa kwenye kikao cha kawaida cha baraza la Madini.
Diwani wa viti maalum Perpetua Nkuwi,akichangia ajenda iliyowasilishwa kwenye kikao cha kawaida cha baraza la madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Ikungi.
Mbunge (CHADEMA) wa jimbo la Singida mashariki,Tundu Lissu akichangia ajenda zilizokuwa zikiwasilishwa kwenye kikao cha kawaida cha baraza la madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Ikungi.
Mbunge (CCM) wa jimbo la Singida magharibi, Mohammed Missanga akizungumza kwenye kikao cha kawaida cha baraza la madiwani wa halmashauri ya wilaya Ikungi.
Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Mkoa wa Singida imekusanya mapato ya zaidi ya shilingi 154.9m kutoka vyanzo vyake mbalimbali vya mapato kwa kipindi cha miezi mitatu ya Julai hadi Septemba mwaka huu.
Hayo yamesemwa na Mweka Hazina wa Halmashauri hiyo Celestine Muttashobya wakati akitoa taarifa yake mbele ya kikao cha madiwani wa halmashauri hiyo kilichofanyika mjini Singida.
Amesema makusanyo hayo ni sawa na asilimia moja ya lengo la kukusanya mapato ya zaidi ya shilingi 16.9 bilioni kwa kipindi cha mwaka wa fedha wa 2013/2014.
Akifafanua, Muttashobya amesema kati ya fedha hizo mapato ya ndani ya halmashauri yenyewe wamekusanya shilingi 57,757,484/m
“Serikali kuu imetupa ruzuku ya shilingi 30 milioni kufidia kodi na ushuru uliofutwa Pia serikali kuu imetupatia ruzuku ya zaidi ya shilingi 53 milioni kwa ajili ya matumizi yasiyo ya mishahara na zingine zaidi ya shilingi 14.1m kwa ajili ya kugharamia miradi mbalimbali ya maendeleo ya wananchi”,amesema.
Mweka Hazina huyo amesema katika kipindi hicho cha miezi mitatu wametumia shilingi 59,853,962.26m sawa na asilimia tatu ya lengo la kutumia shilingi 16,106,933,419/m.
Katika hatua nyingine Muttashobya alitaja kata tatu za jimbo la Singida mashariki zilizofanya vizuri katika ukusanyaji wa mapato na asilimia iliyokusanywa kwenye mabano kuwa ni
Wanafunzi wenye Ulemavu wa shule ya msingi Ikungi mchanganyiko wilaya ya Ikungi mkoa wa Singida, wakiwajibika darasani.
Shule ya Msingi Ikungi Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ya upungufu wa vifaa vya kufundishia na kujifunzia kwa wanafunzi wenye ulemavu wa kuona (upofu).
Hayo yamesemwa na Mwalimu Mkuu wa shule hiyo,Olivary Kamilly wakati akitoa taarifa yake kwenye mahafali ya 62 ya wahitimu 176 wa darasa la saba mwaka huu.
Amesema upungufu huo unaweza kuchangia wanafunzi hao wenye ulemavu wa kuona,wasifanye vizuri katika mitihani yao ukiwemo wa kumaliza elimu ya msingi.
Aidha, Kamilly alitaja baadhi ya changamoto zingine kuwa ni pamoja na ushirikiano mdogo wa wazazi wa watoto wenye ulemavu kwa kuwaficha watoto wao wenye ulemavu,ili wasipate fursa ya kupata elimu.
“Pia kuna baadhi ya wazazi wachache ambao huzua mambo ambayo huleta hali ya kutokuwa na maelewano mazuri kiasi kwamba hutumia muda mrefu kutatua mtafaruku huo,badala ya kusimamia utoaji wa taaluma”,alifafanua mwalimu mkuu huyo.
Pamoja na changamoto hizo,mwalimu Kamilly amesema wamejipanga vizuri kukabiliana na changamoto mbalimbali za kielimu na matarajio ni kushika nafasi ya kwanza kimkoa na kitaifa kwa ujumla.
“Mheshimiwa mkuu wa wilaya,tunatambua kipaumbele chako cha kutaka kuona elimu katika wilaya yako inapanda na inakuwa bora zaidi.Tunakuahidi
Makamu mwenyekiti CCM taifa Tanzania bara, Phillipo Mangula (wa kwanza kulia) anayefuata ni waziri mkuu mstaafu Edward Lowassa,Mkuu wa mkoa wa Singida, Dk.Parseko Vicent Kone na pili kushoto ni Waziri wa Afya Dk.Hussein Mwinyi,wakiwa kwenye msiba wa mwenyekiti mstaafu CCM mkoa wa Singida, Abdallah Sumbu Gallawa.
Baadhi ya waombolezaji waliohudhuria mazishi ya mwenyekiti mstaafu CCM mkoa wa Singida, Mzee Abdallah Sumbu Gallawa katika kijiji cha Samumba kata ya Ikungi.
Makamu mwenyekiti wa CCM taifa Tanzania bara, Phillipo Mangula akizungumza kwenye mazishi ya mwenyekiti mstaafu CCM mkoa wa Singida, Mzee Abdallah Sumbu Gallawa.
Waziri wa Afya, Dk.Hussein Mwinyi akizungumza kwenye mazishi ya mwenyekiti mstaafu CCM mkoa wa Singida,Abdallah Sumbu Gallawa.Dk.Mwinyi alileta ubaini wa Rais Jakaya Mrisho Kikwete.
Mwili wa mwenyekiti mstaafu wa CCM mkoa wa Singida, Abdallah Sumbu Gallawa ukiingizwa kaburini.
Waziri wa Afya, Dk.Hussein Mwinyi akiweka mchanga ndani ya kaburi la mwenyekiti mstaafu wa CCM mkoa wa Singida,Abdallah Sumbu Gallawa aliyefariki dunia Oktoba 29 mwaka huu akipatiwa matibabu katika hospitali ya misheni ya kijiji cha Puma wilaya ya Ikungi.
MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Philip Mangula amewaongoza maelfu ya wakazi wa Mkoa wa Singida na baadhi ya viongozi wa ngazi mbalimbali wakiwemo wa ngazi ya kitaifa kwenye mazishi ya Mwenyekiti Mstaafu wa CCM Mkoa wa Singida Mzee Abdallah Sumbu Gallawa (79).
Mazishi hayo yanayodaiwa kuvunja rekodi ya kuhudhuriwa na maelfu ya waombolezaji yalifanyika nyumbani kwa marehemu katika kijiji cha Sambaru kata ya Ikungi wilaya ya Mkoa wa Singida.
Akizungumza muda mfupi kabla ya mazishi,Mangula alitoa salamu za rambi rambi kutoka kutoka kwa mwenyekiti CCM taifa na Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania,Dk.Jakaya Mrisho Kikwete ambazo aliwatakia kila la kheri familia ya marehemu mzee Sumbu katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo.
Amesema Mwenyekiti huyo wa CCM taifa,alitamani angekuwepo kwenye mazishi hayo lakini ameshindwa kutokana na majukumu ya kikazi nje ya nchi.
Akizungumzia juu yamzee Gallawa,Mangula amesema alikuwa kiongozi bora na aliyekuwa karibu zaidi na watu na ndio maana mazishi yake yamehudhuriwa na maelfu ya wananchi.
Awali akisoma wasifu wa marehemu Gallawa,mbunge wa jimbo la Singida mashariki,Tundu Lissu amesema mzee Gallawa ni mzawa wa kwanza wa mkoa wa Singida kuchaguliwa kuwa mkuu wa wilaya na alianzia kazi hiyo wilaya ya Mbulu mkoa wa Manyara kuanzia mwaka 1962-1965.
Mwaka 1965 aligombea ubunge wa wilaya ya Singida na